Saturday, 7 October 2023

DKT. RWEZIMULA ATOA MAELEKEZO KWA MENEJIMENTI YA DIT- MWANZA KATIKA USIMAMIZI WA MRADI WA EASTRIP


Na Mwandishi wetu - Mwanza

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia anayehusika na Elimu, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula Leo tarehe 7/10/2023 ametembelea Taasisi ya Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza kuona Maendeleo ya Shughuli za ujenzi wa kituo Cha Umahiri wa Teknolojia ya Ngozi (Center of Excellence).


Ujenzi huo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa ujuzi kwa maendeleo na uingiliano wa kikanda katika ukanda wa Afrika Mashariki(EASTRIP),unaotekelezwa na serikali kwa Ufadhili wa Benki ya Dunia.


Dkt. Franklin amesema kituo hiki Cha Umahiri wa Teknolojia ya Ngozi kitakapokamilika kitakuwa msaada mkubwa ndani na nje yaTanzania kwa kuwa kitaongeza wataalam wa masuala ya Ngozi, kufundisha wakulima na wafugaji pamoja na kuchakata mazao ya ngozi (Leather Product Processing).

Kwa upande wake, Mhandisi Mshauri na msimamizi wa mradi upande wa serikali 
Silvester Francis  amesema hadi sasa mradi huu umekamilika kwa asilimia 60% na amebainisha maeneo hayo ambayo ni jengo la taaluma, utawala, mabweni ya kiume na kike, jengo la ngozi ( Leather Building) na uzio.


Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa DIT-Mwanza ambaye pia ni Kaimu Mratibu wa mradi wa EASTRIP Mhandisi Issa Mwangosi amefurahia ujio huu.

"Tumepokea maelekezo na ushauri wa Naibu Katibu Mkuu (Elimu) na tupo tayari kutekeleza ili kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita katika kuleta mapinduzi ya Elimu ya Teknolojia kwa maslahi mapana ya nchi",amesema Mhandisi Mwangosi.

Mradi Huu ulianza kutekelezwa Mwaka 2019 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2024 ambapo utagharimu kiasi cha shillingi za kitanzania Billioni 37.

Share:

TBS KANDA YA MASHARIKI YATEKETEZA VIPODOZI TANI NANE VYENYE VIAMBATA SUMU


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) Kanda ya Mashariki limeteketeza tani nane ya bidhaa za vipodozi vyenye viambata sumu zenye thamani ya shilingi Milioni 80 ambazo zilikamatwa katika Mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro.

Akizungumza na waandishi wa habari hapo Jana Oktoba 6,2023 Mkuranga mkoani Pwani, Kaimu Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Bw.Francis Mapunda amesema zoezi la kukamata bidhaa za vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku ni endelevu hivyo amewataka wafanyabiashara kuacha kuuza bidhaa hizo.

Aidha alitoa wito kwa wafanyabiashara wa vipodozi kufanya usajili wa vipodozi na kufuata orodha ya bidhaa za vipodozi ambavyo vimesajiliwa na kuruhusiwa kuuzwa.

Pamoja na hayo amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanajiepusha na biashara ya bidhaa za vipodozi zenye viambata sumu vilivyopigwa marufuku kuepusha usumbufu na gharama zisizo za lazima.


Share:

Video Mpya : SUPER KINYAMBE ft NG'WANA TELI - POMBE


Hii hapa ngoma mpya ya Msanii Super Kinyambe amemshirikisha Ng'wana Teli inaitwa Pombe

Share:

MREMBO AOLEWA NA WANAUME WAWILI......WANALALA KITANDA KIMOJA

Mwanamke mmoja raia wa Congo ambaye ameolewa na waume wawili, amewaduwaza wengi ikizingatiwa kwamba ndoa ya waume wengi ni nadra barani Afrika.

Francine Jisele anaishi na waume wawili, mume wa kwanza Remi Murula na wa pili Albert Jarlace katika nyumba moja pamoja na wanao.

Jisele alifunga ndoa miaka sita iliyopita na Murula na walijaliwa watoto wawili. Murula aliondoka kwenda kutafuta kazi ya kukimu familia yake na kukata mawasiliano na mke wake.

"Kwa sababu maisha hayakuwa rahisi, mwanaume huyo alifunga safari na hakurudi tena. Nilijikuta pekee yangu, nilikaa miaka mitatu na nusu bila mume wangu," aliiambia Afrimax English katika mahojiano.

 "Baada ya miaka hiyo yote nilimpoteza na kupendana na mwanaume huyu mwingine. Baada ya mwaka mmoja na mume wa pili, wa kwanza alirudi," alifichua. 

Jisele hakutarajia mume wake angerudi baada ya kuwa mbali kwa miaka yote hiyo. Nilikutana na mwanamke huyu nikiwa nafanya kazi kwenye sekta ya madini na akaniambia kuwa ana mume mwingine na jinsi mwanaume huyo alivyomuacha akisema anaenda kutafuta maisha,”

“Nilihisi sina la kufanya kwa sababu tayari tulikuwa pamoja tangu nilipoishi naye bila kujua ana mwanaume mwingine,” alieleza Albert Jarlace. 

“Mwanamke huyo aliniomba nisimuache hivyo nikaona ni lazima nibaki naye na kwa sasa tuna mtoto mmoja pamoja,” alisema Jarlace.

 Murula aliporudi alipigana na Jarlace akibishana kuwa Jisele ni mke wake.

"Tuko wanaume watatu hapa na tunaelewana, huyu mwanamke ni mke wetu. Tangu niondoke sikuzungumza na mke wangu hata siku moja. Niliporudi nilimkuta mke wangu na mwanaume mwingine," aliongeza Murula.

Murula alikuwa amemwomba mpenzi wake amtimue Jarlace lakini alisisitiza kuwa hana mahali pengine pa kwenda. 

"Mwanzoni nilipiga kelele lakini niligundua ikiwa ningezungumza na mke wangu hangefanya jambo kama hilo. Sikuwa na mahali pa kwenda na nilikuwa na makosa," alisema Murula. 

“Tunakula meza moja, tunalala chumba kimoja na kitanda kimoja, nawapenda wote wawili, tunaishi kwa amani nyumbani,” alisema Jisele. 

Wanaume hao hugawana kazi na kuleta mkate nyumbani huku mwanamke akiwaheshimu wote wawili. 

Wasiwasi walio nao ni kutoweza kuwatofautisha watoto wao.


Mwanamke ndiye anayetambua baba wa watoto. Linapokuja suala la kusoma uroda, mmoja wetu humwacha mwingine ili afurahie. 

“Familia yangu inafahamu hali yangu na kunishauri nitulie kwa sababu nilimtelekeza mke wangu,” alisema Murula. 

Jisele anasema ni ngumu kwake; anatamani kila mwanaume angekuwa na nyumba na angeenda kwao.


Hataki wote wawili waendelee kukutana katika chumba kimoja cha kulala kwa wakati mmoja. 

"Nataka kuondoka na kumpa nafasi 'hubby wa mwanamke huyo kwani ni mume wake anajulikana. Ningepata msaada wa tiketi ningeondoka na kumwacha mume mwenzangu abaki nyumbani kwake. Mwanamke asingekubali kuhama mbali," alisema Jarlace.


"Sifurahii kuona sisi wanaume wawili tukigawana mwanamke; ardhi na nyumba ni yangu na mwanamke ni wangu," aliongeza.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 7,2023

 



























      

 



    Share:

    NSSF TANGA WAMSHUKURU RAIS DKT SAMIA ANAVYOPAMBANIA NCHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

     

    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
    AFISA Mkuu wa Idara ya Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakari Mshangama akifuatilia kwa umakini matukio mbalimbali wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya wateja 
    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga katikati akikata keki na waajiri wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akimlisha cheki mmoja wa waajiri wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akimlisha keki mwandishi wa habari wa Chanel Ten Raya Kipingu wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa mfuko huo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja



    Na Oscar Assenga,TANGA.

    MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga amshukukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa jinsi anavyopambania nchi katika kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini na hivyo kuongeza chachu kwao kutokana na  kuongeza wigo wa waajiriwa wapya

    Mbaga aliyasema hayo wakati wa kilele cha kuhitimisha wiki ya huduma kwa wateja iliyokwenda sambamba na kuwakabidhi vyeti waajiri wakubwa katika mkoa huo Pepee ,Tanga Cement ,Maweni kwa kutambua mchango wao katika uchangiaji katika mfuko huo

    Alisema utekelezaji wa miradi hiyo imewawezesha kuongeza wigo wa makusanyo kwa mkoa wa Tanga na hivyo kupanua wigo mpana wa kuongeza makusanyo katika mfuko huo kutokana na waajiri kuongezeka.

    “Leo tupo kwenye kilele cha Kufunga siku ya huduma kwa wateja tunawashukuru bodi ya wadhamani ya NSSF Mkurugenzi mkuu na watumishi katika kuadhimisha wiki ya wateja lakini pia tunamshukukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa jinsi anavyopambania nchi katika kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini na hivyo kuongeza chachu kwao kwa kuongeza waajiriwa wapya

    Meneja huyo alisema ili kutoa huduma nzuri kwa wanachama lazima waajiri wawe wamelipa michango yao kwa wakati huku akitoa wito kwa waajiri wanaodaiwa michango na mfuko huo ikiwemo waliongia makubaliano nao kulipa michango yao kwa wakati kwa mujibu wa sheria.

    Ambapo alisema michango hiyo inatakiwa kuwasilishwa mwezi moja baada ya kulipa mishahara ya wafanyakazi wao ili nao kama mfuko waweza kusimamia na kutoa huduma nzuri kwa wanachama huku akieleza kwa sasa wanaweza kulipa ndani ya siku moja wanachama wao na hivyo kupelekea furaha kwa wanachama kwa sababu wanafanyaa kazi kutoka na miongozi na sheria na taratibu.

    Akizungumzia suala la rushwa ,Meneja huyo alisema jambo hilo ni adaui wa haki mtu hatakiwa kupokea rushwa wala kudai rushwa ikiwemo kutoa wito kwa wafanyakazi wenzake kufanya kazi kwa waledi pasipo kudai mtu chochote.

    Alisema rushwa ina madhara makubwa kwa mfuko na ni adui wa haki na inaharibu sifa nzuri ya mfuko huo ambao umejengeka kwa muda mrefu halikadhalika serikali chini ya Rais Dkt Samia Suluhu inapinga rushwa kwa vitendo.

    Alisema nao wanaunga mkono juhudi hizo za Serikali kwa kupinga na kukemea masuala ya rushwa kwenye mfuko huo huku akitoa wito kwa wananchi kutumia mifumo yao iliyopo katika kuandikisha wanachama wengi zaidi pamoja na akuchangia kwa hiari ili kuweza kuongeza wigo wa kinga ya hifadhi ya jamii kwa wananchi.

    Kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja kwa mwaka huu kimebeba kauli mbiu isemavyo “Ushirikiano kwa huduma Bora”



    Share:

    Friday, 6 October 2023

    DK.MPANGO AYAONYA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI


    Na Dotto Kwilasa, Dodoma

    MAKAMU wa Rais Dk Philip Mpango amezindua ramani ya kidigitali ya utambuzi wa mashirika yasiyo ya kiserikali huku akiyataka mashirika hayo kulinda na kutunza  maadili ya kitanzania kwa kutokubali kutumiwa na baadhi ya watu wasioitakia mema nchi.

    Katika hilo ametoa maelekezo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Ustawi na Maendeleo ya Jamii kufanya uchambuzi wa mchango wa mashirika hayo na kuishauri serikali juu ya mwenendo na ufanisi wake.

    Dokta Mpango ametoa msisitizo huo jana Jijini Dodoma wakati akifunga Jukwaa la Mwaka la Mashirika yasiyo ya kiserikali na kuyashauri mashirika hayo kupeleka changamoto zote za kikodi zilizopo wizara ya fedha nayeye apewe taarifa.

    Aidha amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili NGOs ziendelee kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi wa hali ya juu.

    "Serikali inaahidi kuendelea na jitihada za kuondoa baadhi ya  changamoto zinazoathiri ufanisi wa NGOs nchini lakini NGOs zinapaswa kuwa na uwazi  jinsi ya uendeshaji wa shughuli zake, " alisema na kuongeza, "amesema na kuongeza;

    Nazipongeza NGOs zote kwa kazi zinazofanya kwani zinawagusa wananchi katika nyanja mbalimbali za maisha na kuiunga Serikali mkono katika kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla, " Amesema Dk. Mpango

    Kuhusu mabadiliko ya tabia nchi,Dk.Mpango amesema Serikali inaendelea na kuhimiza kupanda miti na shughuli za maendeleo katika kukabiliana na athari hiyo na kuzipongeza NGOs ambazo zinapambana na suala hilo .

    "Natoa wito kwa mashirika yote kuendelea kutoa elimu kwa wanachi kuhusu kutunza mazingira,nimeridhia pia ombi la Mwenyekiti wa Bodi ya NaCoNGO kwa kuelekeza mamlaka za mikoa na wilaya kufanya kazi kwa karibu na NGOs kwa kufuatilia kazi zao na kuziwekea mazingira mazuri ili ziendelee kufanya kazi vema, "alisema

    Pamoja na hayo Makamu huyo wa Rais ametaka NGOs zote  kuimarisha ushirikiano na NGOs za nchi zingine ili kuweza kujenga ufanisi katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali na kuwasisitiza wendaji wa Serikali kujibu haraka wanapoandikiwa barua na NGOs,  ili wapate majibu kwa lengo husika.

    Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Dokta Dorothy Gwajima amesema wizara yake kupitia ofisi ya msajili wa NGOs ina jukumu la kuratibu shughuli za mashirika hayo kwa upande wa Tanznaia Bara ili kuhakikisha yanaleta tija kwa jamii.

    Awali,Mwenyekiti wa Uratibu wa Mashirika yasiyo ya kiserikali Mwantumu Mahiza ameziomba mamlaka za mikoa na wilaya kufanya kazi kwa karibu na mashirika yasiyo ya kiserikali huku Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO),Lilian ametaja changamoto zilizopo ikiwemo mfumo wa mamlaka ya kodi kutokuwa rafiki.

    Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO), Dkt. Lilian Badi amesema sekta ya mashirika yasiyo ya Kiserikali inaendelea kukua mwaka hadi mwaka siyo tu kwa idadi inavyoongezeka bali utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

    Ameitaja baadhi ya miradi inayotekelezwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo afya, mazingira, ulinzi wa jamii, uwezeshaji wa wananchi, elimu, kilimo, jinsia, maji, utawala bora na haki za binadamu.

    "Tunaahidi kuendelea kushirikiana na Wizara yenye dhamana ya mashirika yasiyo ya Kiserikali ili kutekeleza majukumu yetu kwa ajili ya maslahi ya Watanzania na Taifa kwa ujumla, " Amesema


    Share:

    DKT. TULIA ASHIRIKI MKUTANO WA JUMUIYA YA MADOLA GHANA

     

    Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 5 Oktoba, 2023 ameshiriki Mkutano wa 66 wa Kibunge wa Jumuiya ya Madola (CPC) unaoendelea katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Accra nchini Ghana wenye dhima isemayo “The Commonwealth Charter 10 years on: Values and Principles for Parliaments to Uphold”

    Katika Mkutano huo, Dkt. Tulia ameambatana na baadhi ya Wabunge akiwemo Mhe. Dkt. Alice Kaijage, Mhe. Abdallah Mwinyi, Mhe. Dkt. Pius Chaya, Mhe. Dkt. Joseph Mhagama, Mhe. Elibariki Kingu pamoja na Katibu wa Bunge Bi. Nenelwa Mwihambi ndc

    Share:

    Thursday, 5 October 2023

    TANZANIA YATAKIWA KUJIANDAA KWA TIBA UTALII


    MRATIBU wa Tiba Utalii Dkt.Asha Mahita amesema kuwa kuna umuhimu Tanzania tukajiandaa kwa tiba Utalii na ili iweze kufanikiwa tunahitaji ubora wa huduma kwenye maeneo mbalimbali husika kwa kuzingatia mahitaji maalumu.

    Ameyasema hayo jana katika Mkutano wa Afya uliofanyika kwenye ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa Tanzania imeanza kupokea wageni wengi wanaokuja kufuata matibabu, hii inaonyesha kuwa tayari nchi za Afrika zimeanza kutuamini katika huduma za Afya.

    "Ni muhimu sasa hospitali na watoa huduma za Afya waanze kufikiria nje ya box. mwananchi au mgeni apate huduma katika mazingira bora, kwa wakati, yenye utaalamu wa hali ya juu na kuhudumiwa kwa lugha nzuri yenye kumpa matumaini". Amesema

    Aidha Dr. Mahita amepongeza jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu akisema kampeni ya Royal Tour imefungua milango kwa watalii wengi kuja nchini, lakini wakati huo.

    "Rais amekuwa chachu ya maendeleo katika sekta ya afya kwani kupitia yeye Tanzania sasa imeanza kupokea sifa katika Tiba Utalii". Amesema Dkt.Mahita.

    Naye ,Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Afya Dkt.Caroline Damiani aliwasilisha mada ya Ubora wa Huduma za Afya katika Ngazi ya Msingi wa utoaji huduma za Afya na Muelekeo wa Wizara kuhakikisha huduma bora za Afya zinapatikana nchini

    Mkutano wa Afya Tanzania (Tanzania Health Summit) ndio mkutano mkubwa zaidi wa kila mwaka wa huduma ya afya nchini Tanzania, unaovutia mamia ya washiriki wa kibinafsi na wa mtandao kutoka kwa mfumo wa huduma ya afya nchini ili kuzingatia maendeleo kuelekea Malengo ya Maendeleo Endelevu.

    Mada nyingine zilizotawala.katika Mkutano huo ni kuhusu “Kushughulikia Ukosefu wa Usawa wa Afya ya Mtoto kupitia Ufadhili Endelevu.” Wasilisho lake litachunguza vikwazo nchini Tanzania vinavyozuia upatikanaji sawa wa matibabu ya nimonia ya kuokoa maisha na kuchunguza masuluhisho yanayoweza kusaidia kupanua wigo pia Mkutano huo ulitoa taarifa mpya kuhusu ahadi zilizotolewa na Serikali ya Tanzania katika kuongeza uwekezaji katika ufadhili wa afya endelevu ambao unapaswa kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa Watanzania na kuwezesha nchi kukabiliana na majanga yasiyotarajiwa kama vile janga la Covid-19.



    Share:

    RAIS SAMIA AMWAGA MABILIONI YA FEDHA KILIMANJARO KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO; MBUNGE MALEKO AFUNGUKA





    Na Mwandishi Wetu, KILIMANJARO

    MBUNGE wa Vitimaalum Mkoa wa Kilimanjaro Ester Malleko, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuendelea kuwa kinara wa maendeleo, Mama mlezi, Mzazi, na Mfariji wa wasio matumaini, kwa kutoa mabilioni ya fedha katika Mkoa huo na kutekelezwa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi.

    Amebainisha hayo leo Oktoba 5, 2023 wakati akizungumza katika Mikutano mbalimbali na kukutana na makundi ya Wanakilimanjaro akielezea namna alivyokoshwa na Rais SAMIA katika kuwatumikia Watanzania na kuwaletea maendeleo.

    Amesema katika Mkoa huo wa Kilimanjaro ndani ya Utawala wake Rais Samia, ametoa fedha nyingi ambazo zimetekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo, jambo ambalo wanajivunia kuwa na Rais mpenda maendeleo hapa nchini.

    Aidha, amesema mbali na mambo mengi aliyofanya Mhe. Rais kukuza Utalii, Ujenzi Uwanja wa Ndege moshi, UjenI Barabara kwa viwango mbalimbali ikiwemo Lami, katika Sekta ya Afya Rais Samia ametoa kiasi cha fedha Sh.bilioni 2.59 ambazo zimetumika kuboresha huduma za Afya katika Zahanati 35, na Vituo vya Afya katika Mkoa huo wa Kilimanjaro.

    Pia, amesema Rais Samia hakuishia hapo akatoa tena Sh.bilioni 4 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya katika Halmashauri za Moshi Mjini, Mwanga, Hai, Siha na Rombo.

    Amesema pia Rais Samia ametoa fedha Sh. Bilioni 7.9 kwa ajili ya ujenzi wa Majengo ya Hospitali katika wilaya zote saba mkoani Kilimanjaro.

    “Mkoa wa Kilimanjaro tunampongeza Rais Samia kwa kutoa mabilioni ya fedha na kutekelezwa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi, kwa kweli Rais Samia ni Kinara wa Maendeleo na sisi tutaendelea kumuunga mkono katika utawala wake ili awatumikie Watanzania,”amesema Malleko.

     

    Akizungumzia Sekta ya Elimu, amesema katika Mkoa huo wa Kilimanjaro ametoa Sh.bilioni 21 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya elimu na uhifadhi wa mazingira, kwa shule zote za Msingi na Sekondari, pamoja na kutoa Bilioni 6.3 fedha za mpango wa elimu bila malipo.

    Amesema kwa upande wa Sekta ya Maji, ametoa Sh.bilioni 6.29 ambao zimetumika kukarabati miundombinu ya Maji, na kuongeza mtandao wa upatikanaji Majisafi na Salama hadi maeneo ya vijijini.

    Pia amesema katika kupambana na umaskini na kuwezesha wananchi kiuchumi kupitia mpango wa TASAF, kwamba Jumla ya Kaya 41,108 wamepata Ruzuku huku walengwa 27,472 wamenufaika na Ajira za muda za mpango huo katika miradi 604 ambayo inaendelea kutekelezwa katika Halmashauri zote Saba mkoani humo.

    Mbunge huyo pia amewashukuru Viongozi wa Serikali na Chama pamoja na Wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro, kwa namna wanavyompatia ushirikiano katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku kama Mbunge, na kuahidi kuendelea kushirikiana nao ili kusukuma guruduma la maendeleo mkoani humo na kwamba Watanzania wamuunge Mkono Mhe. Rais Samia wasimvunje moyo kwakuwa ana mapenzi, dhamira na nia njema ya kuipaisha Tanzania kimaendeleo na kutoa Rai kwa wanasiasa kuacha nongwa na fitina za kisiasa za kugombania madaraka badala yake wachape kazi, wajenge utu, uzalendo na uadilifu na kumuunga mkono Rais Samia na Serikali yake.

    Share:
    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    Popular Posts

    Unordered List

    Pages

    Blog Archive


    Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger