Saturday 7 October 2023

NSSF TANGA WAMSHUKURU RAIS DKT SAMIA ANAVYOPAMBANIA NCHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

...

 

MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akizungumza wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
AFISA Mkuu wa Idara ya Matekelezo wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakari Mshangama akifuatilia kwa umakini matukio mbalimbali wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya wateja 
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga katikati akikata keki na waajiri wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akimlisha cheki mmoja wa waajiri wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akimlisha keki mwandishi wa habari wa Chanel Ten Raya Kipingu wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa mfuko huo wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja



Na Oscar Assenga,TANGA.

MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoa wa Tanga Nuhu Ramadhani Mbaga amshukukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa jinsi anavyopambania nchi katika kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini na hivyo kuongeza chachu kwao kutokana na  kuongeza wigo wa waajiriwa wapya

Mbaga aliyasema hayo wakati wa kilele cha kuhitimisha wiki ya huduma kwa wateja iliyokwenda sambamba na kuwakabidhi vyeti waajiri wakubwa katika mkoa huo Pepee ,Tanga Cement ,Maweni kwa kutambua mchango wao katika uchangiaji katika mfuko huo

Alisema utekelezaji wa miradi hiyo imewawezesha kuongeza wigo wa makusanyo kwa mkoa wa Tanga na hivyo kupanua wigo mpana wa kuongeza makusanyo katika mfuko huo kutokana na waajiri kuongezeka.

“Leo tupo kwenye kilele cha Kufunga siku ya huduma kwa wateja tunawashukuru bodi ya wadhamani ya NSSF Mkurugenzi mkuu na watumishi katika kuadhimisha wiki ya wateja lakini pia tunamshukukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa jinsi anavyopambania nchi katika kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati nchini na hivyo kuongeza chachu kwao kwa kuongeza waajiriwa wapya

Meneja huyo alisema ili kutoa huduma nzuri kwa wanachama lazima waajiri wawe wamelipa michango yao kwa wakati huku akitoa wito kwa waajiri wanaodaiwa michango na mfuko huo ikiwemo waliongia makubaliano nao kulipa michango yao kwa wakati kwa mujibu wa sheria.

Ambapo alisema michango hiyo inatakiwa kuwasilishwa mwezi moja baada ya kulipa mishahara ya wafanyakazi wao ili nao kama mfuko waweza kusimamia na kutoa huduma nzuri kwa wanachama huku akieleza kwa sasa wanaweza kulipa ndani ya siku moja wanachama wao na hivyo kupelekea furaha kwa wanachama kwa sababu wanafanyaa kazi kutoka na miongozi na sheria na taratibu.

Akizungumzia suala la rushwa ,Meneja huyo alisema jambo hilo ni adaui wa haki mtu hatakiwa kupokea rushwa wala kudai rushwa ikiwemo kutoa wito kwa wafanyakazi wenzake kufanya kazi kwa waledi pasipo kudai mtu chochote.

Alisema rushwa ina madhara makubwa kwa mfuko na ni adui wa haki na inaharibu sifa nzuri ya mfuko huo ambao umejengeka kwa muda mrefu halikadhalika serikali chini ya Rais Dkt Samia Suluhu inapinga rushwa kwa vitendo.

Alisema nao wanaunga mkono juhudi hizo za Serikali kwa kupinga na kukemea masuala ya rushwa kwenye mfuko huo huku akitoa wito kwa wananchi kutumia mifumo yao iliyopo katika kuandikisha wanachama wengi zaidi pamoja na akuchangia kwa hiari ili kuweza kuongeza wigo wa kinga ya hifadhi ya jamii kwa wananchi.

Kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja kwa mwaka huu kimebeba kauli mbiu isemavyo “Ushirikiano kwa huduma Bora”



Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger