Monday, 14 January 2019

TRUMP AIONYA UTURUKI DHIDI YA WAKURDI

Vikosi vinavyoungwa mkono na Uturuki wako tayari kushambulia wapiganaji wa Kikurdi kaskazini mwa Syria.

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia 'kuiangamiza Uturuki kiuchumi' iwapo taifa hilo litavishambulia vikosi vya wakurdi nchini Syria baada ya wanajeshi wa Marekani kuondoka Syria.

Katika ujumbe wake alioutuma kwenye mtandao wa kijamii Twitter, Trump amesema hakutaka Wakurdi kwa upande wao nao pia waichokoza Uturuki.

Vikosi vya Marekani vimepambana kwa ushirikiano na wanamgambo wa Kikurdi kaskazini mwa Syria dhidi ya kundi la Islamic State (IS).

Uturuki hatahivyo inatazama wapiganaji hao wa vitengo vya YPG kama magaidi.

Rais Recep Tayyip Erdogan amezungumza kwa hasira kuhusu Marekani kuliunga mkono kundi hilo, na kuapa kuliangamiza.

Chanzo:Bbc
Share:

SADC YATOA WITO WA SERIKALI YA MUUNGANO DRC

Muungano wa maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SADC, umetoa wito wa kuundwa kwa serikali ya muungano nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia mzozo uliokumba matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika mwezi uliyopita.

Tangazo hilo limetolewa kupitia taarifa ya rais wa Zambia Edgar Lungu.

Afrika Kusini pia inaunga mkono wazo la kubuniwa kwa serikali ya muungano.

Hatua hii ya SADC inakuja siku moja baada ya mgombea wa upinzani katika uchaguzi mkuu uliyofanyika nchini Jamhuri ya kidemocrasia ya Congo kuwasilisha kesi katika mahakama ya katiba kupinga matokeo ya uchaguzi huo.

Martin Fayulu amesisitiza kuwa alishinda uchaguzi huo lakini tume ya uchaguzi ikamtangaza mshindani wake Felix Tshisekedi kuwa mshindi.


Chanzo:Bbc
Share:

FAHAMU KIKOSI BORA ZAIDI BARANI ULAYA 2018

England walifika nusu fainali katika Kombe la Dunia nchini Urusi mwaka 2018, lakini hakuna mchezaji hata mmoja wa timu hiyo ya taifa aliyejumuishwa kwenye kikosi bora cha wachezaji 11 Ulaya, chaguo la mashabiki kwa mwaka huo.


Ingawa kuna wachezaji watatu wanaocheza Ligi ya Premia kwenye kikosi hicho, hata nahodha wa England Harry Kane aliyeshinda tuzo ya mfungaji bora zaidi Urusi, hajajumuishwa.

Kiungo wa Liverpool Virgil van Dijk na wachezaji wawili wa Chelsea N'Golo Kante na Eden Hazard wamo kwenye kikosi hicho cha wachezaji XI.

Cristiano Ronaldo ni miongoni mwao, ambapo amejumuishwa kwa mara ya 13 sasa, na kuwa mchezaji aliyejumuishwa mara nyingi zaidi.

Mshambuliaji huyo wa Ureno ambaye sasa huchezea Juventus ya Italia, aliisaidia klabu yake ya zamani Real Madrid kushinda Kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya tatu mtawalia mjini Kiev, Ukraine mwezi Mei ambapo waliwalaza Liverpool.

Chanzo:Bbc
Share:

DE GEA KUWA KIPA BORA ZAIDI MAN UNITED??

David de Gea huenda akajijengea hadhi ya kuwa mlinda lango bora zaidi kuwahi kuichezea klabu ya Manchester United hasa baada ya ustadi wake Jumapili, kwa mujibu wa kaimu meneja wao Ole Gunnar Solskjaer.

Mhispania huyo mwenye miaka, 28, aliokoa mipira 11 na kuwawezesha United kuwalaza Tottenham 1-0 katika mechi iliyochezewa uwnaja wa Wembley.

Kwa mujibu wa BBC, katika miaka 11 aliyokuwa Old Trafford akiwa mshambuliaji, Solskjaer alicheza na magolikipa stadi kama vile Edwin van der Sar na Peter Schmeichel.

"Tumekuwa na magolikipa wazuri sana katika klabu hii na nafikiri kwa sasa anawatishia wote wawili Edwin na Peter katika nafasi hiyo ya kipa bora zaidi [kuwahi kuchezea United] katika historia," Solskjaer alisema.

De Gea aliokoa mipira 11 langoni katika mechi hiyo ya Ligi Kuu ya England na pia akawawezesha kumaliza mechi hiyo bila kufungwa.

Ushindi wao uliwawezesha United sasa kukamilisha ushindi wa mechi sita kati ya sita walizocheza chini ya Solskjaer.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alijiunga na United kutoka Atletico Madrid mwaka 2011 na ameshinda tuzo ya mchezaji bora klabu wa mwaka katika misimu minne kati ya mitano ya karibuni zaidi.

"Alifaa kudaka mipira kadha," Solskjaer alitania.

"Tulikuwa na mabeki wazuri na David nyuma yao mambo yalikwenda vyema ajabu. Unaruhusiwa kuwa na kipa mzuri.

"Nimecheza na magolikipa kadha wazuri sana. Tumekuwa na utamaduni wa kuwa nao na amekomaa na kukomaa hata zaidi. Alistahiki tuzo hiyo ya mchezaji bora wa mechi ya leo (jana)."

Solskjaer ameshinda mechi tano za ligi mfululizo akiwa na United matokeo ambayo sasa yamewawezesha kutua nafasi ya sita wakiwa sawa kwa alama na Arsneal walio nafasi ya tano, wakiwa mbele kwa wingi wa mabao.

United wamo alama sita pekee kutoka nafasi ya nne inayowezesha klabu kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

"Bado tunaamini kwamba tunaweza kumaliza katika nne bora," alisema De Gea.

"Sisi ni United, tuna wachezaji wazuri na tunang'ang'ania kumaliza katika nne bora.

"Ilikuwa mechi nzuri sana, hata zaidi ukizingatia tulikuwa uwanja wa Wembley. Zilikuwa alama tatu muhimu sana. Ninafurahia sana uchezaji wangu na timu inacheza vyema sana pia, na kuunda nafasi na kucheza soka ya kushambulia zaidi.

"Tumecheza mechi tatu sasa mtawalia bila kufungwa, jambo ambalo ni zuri sana. Wachezaji wana furaha, na unaweza kuliona hilo uwanjani, wanachezaji wa kujituma sana, kama Manchester United."
Share:

TIMU 9 ZILIZOTOA VIPIGO VIKUBWA ZAIDI ENGLAND

Katika mchezo wa soka timu kufunga mabao ni jambo muhimu zaidi. Ukifanya hivyo ndio unashinda. Bila shaka kwamba kama unataka kuwa na uhakika wa kushinda kwenye kila mchezo wa soka, ukifunga mabao mengi zaidi ndiyo yanayokuwezesha kukufanya uwe mshindi. 

Baada ya Manchester City kuonyesha kiwango cha juu na kufunga mabao 9-0 dhidi ya Burton Albion kwenye mchezo wa Carabao, hapa tunakuchambulia timu zilizowahi kupata ushindi mkubwa zaidi katika historia ya mchezo wa soka nchini England.

9. Manchester United 9-0 Ipswich (Machi 4, 1995)

Mashetani Wekundi hao waliibuka na ushindi wa mabao 9-0 dhidi ya Ipswich na hadi sasa imebakia kuwa rekodi kwenye zama za Ligi Kuu ya England.

Andy Cole alifunga mabao matano – akiweka rekodi ya kufunga mabao mengi kwenye mchezo mmoja wa Ligi Kuu, huku Roy Keane akifunga, Mark Hughes (mawili) pamoja na Paul Ince akifunga moja.

Kichapo hicho kilikuwa cha kushangaza kwa kuwa Ipswich iliichapa United 3-2 kwenye mchezo wa mwanzoni mwa msimu huo.

8. West Ham United 10-0 Bury (Oktoba 25, 1983)

Ushindi mwingine wa kushangaza ni kwenye mchezo wa Kombe la Ligi, wagonga nyundo hawa wa London walipata ushindi mkubwa zaidi katika historia yao. 

Tony Cottee ambaye alikuwa na umri wa miaka 19 peke yake alitikisa nyavu mara nne, huku Trevor Brooking aliyekuwa na miaka 36 alifunga mawili dhidi ya Bury, ambao walikuwa vinara wa ligi daraja la kwanza na walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo.

7. Liverpool 10-0 Fulham (Septemba 23, 1986)

Huu ulikuwa ni mchezo wa Kombe la Ligi na wekundu hawa wa Anfield walitoa kichapo cha kihistoria. 

Uwanja ukiwa na watazamaji 13,498 pale Anfield ulishuhudia Steve McMahon na Ian Rush wakiiangamiza Fulham. McMahon alifunga mabao manne, lakini alikosa penalti kwenye mchezo huo. Liverpool walitinga fainali ya Kombe la Ligi lakini wakaja kufungwa na Arsenal magoli 2-1.

6. West Brom 12-0 Darwen (Aprili 4, 1982)

Darwen FC ilikuwa ni timu kutoka pale mitaa ya Lancashire, ambayo ilionekana kuwa na matarajio makubwa kwenye soka la England.

Lakini walipokutana na West Brom kwenye Ligi Daraja la Kwanza wakajikuta wakikumbana na kipigo cha mabao 12-0.

5. Nottingham Forest 12-0 Leicester City (Aprili 21, 1909)

Nottingham Forest ilikuwa ni timu tishio wakati huo na walipokutana na Leicester waliitandika bila huruma mabao 12. Gwiji wa Forest na ambaye ndiye mfungaji wa wakati wote wa timu hiyo, Grenville Morris, alifunga mabao mawili kwenye mchezo huo. 

4. Newcastle United 13-0 Newport County (Oktoba 5, 1946)

Wakati huo wakiwa wanacheza Ligi Daraja la pili, Newcastle walitoa kipigo cha aina yake, huku kipindi cha kwanza wakiongoza kwa mabao saba.

Mchezaji, Len Shackleton ambaye ndio alikuwa ametoka tu kujiunga na klabu hiyo kwa ada ya pauni 13,000, alifunga mabao sita peke yake na kuwafanya vijana hao kuondoka uwanjani wakiwa na shangwe kubwa.

3. Stockport County 13-0 Halifax Town (Januari 6, 1934)

Miaka 85 iliyopita Stockport waliweka historia kwenye soka la England ambao hawajawahi kuifikia tena hadi leo.

Stan Milton alikuwa akicheza mchezo wake wa kwanza kwenye Ligi Daraja la Tatu na hadi kipindi cha kwanza kinamalizika ubao ulikuwa unasomekana 2-0 Stockport wakiwa wanaongoza. Lakini kipindi cha pili Milton alifunga mabao 11 peke yake na kuweka historia yake kwenye mchezo huo hadi leo. 

2. Clapton 0-14 Nottingham Forest (Januari 17 January 1891)

Forest waliweka tena historia nyingine. Huu ulikuwa mchezo wa raundi ya nne ya Kombe la FA wakaifunga Clapton mabao 14-0 na kujiandikia historia yao. 

1. Preston North End 26-0 Hyde FC (Oktoba 15, 1887)

Hii ndio historia iliyoshindwa kuvunjwa hadi leo kwenye soka huko England na itachukua miaka mingi kuweza kuivunja. 

Ni miaka 131 iliyopita, Preston wakiwa kwenye dimba la nyumbani waliifumua Hyde FC mabao 26-0 kwenye uwanja wa Deepdale ukiwa ni mchezo wa raundi ya kwanza ya Kombe la FA. 

North End kwenye mchezo huo iliweka rekodi ya aina yake katika historia ya soka la Uingereza: Kufunga mabao mengi kwenye mchezo mmoja, kupata ushindi mkubwa zaidi nyumbani ambao ni rekodi hadi leo. 

Cha kuchangaza licha ya ushindi huo mnono na kuweza kutinga fainali, lakini wakaja kufungwa na West Brom 2-1.
Share:

MATATANI KWA KUGAWA SARE ZA JESHI



Vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Kigoma vimemtia mbaroni kiongozi wa Shirika la Danish Refugees Services linalotoa usaidizi wa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa kwenye kambi za Nduta wilayani Kibondo na Mtendeli wilayani Kakonko.

Kiongozi huyo anatuhumiwa kuhusika na uingizwaji na uwagawaji wa nguo zinazofanana na sare za jeshi ndani ya kambi hizo za wakimbizi.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Samson Anga akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Emmanuel Maganga wakati wa uchomaji wa nguo uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Kawawa mjini Kigoma, ambapo alisema kuwa kiongozi huyo anashikiliwa na vyombo vya ulinzi na usalama kwa uchunguzi zaidi.

Bila kumtaja jina kiongozi huyo, Anga amesema kukamatwa kwake kunatokana na Mkuu wa Makazi katika kambi ya Wakimbizi ya Nduta wilaya Kibondo kutilia shaka uwepo wa nguo hizo na mgawanyo wake.

Ndipo baada ya kufuatilia kwa kina akagundua kuwa nguo hizo zinafanana na sare za jeshi hivyo kuarifu kamati za ulinzi na usalama na nguo hizo kukamatwa kabla hazijaanza kugawanywa.

“Katika hatua ya awali tunamshikilia kiongozi wa Taasisi ya Danish Refugees Services ambaye kwa namna moja au nyingine anahusika na uingizwaji wa nguo 1,947 kwenye hizo kambi za wakimbizi na uchunguzi zaidi unaendelea, taarifa itatolewa baadaye kuhusiana na yale yanayoendelea kwenye suala hilo,” alisema.

Na Fadhili Abdallah - Habarileo Kigoma 

Share:

KAULI YA KANGI LUGOLA KUHUSU VIDEO YA TRAFIKI KUMSHAMBULIA 'KUMNG'ATA MENO' DEREVA WA LORI


Wakati video inayoonyesha askari watatu wa Kikosi cha Usalama Barabarani wakimshambulia dereva wa lori ikizua mjadala mitandaoni, Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limesema litatoa tamko la tukio hilo haraka iwezekanavyo.

Katika video hiyo, askari hao wanaonekana wakimshambulia dereva huyo kabla ya kundi la wananchi waliokuwa wakiwashangaa awali, kuamua ugomvi huo.

Alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola alisema, “Nimemtumia kipande hicho cha video Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Muslimu ili afuatilie kujua undani wake na taarifa itatolewa.”

Hata hivyo, alipotafutwa kwa simu jana, Kamanda Muslimu hakupatikana kwani simu yake iliita bila kupokewa.

Lakini akizungumza na Mwananchi jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange alisema tayari wameshapewa maelezo na watatoa ufafanuzi kuhusu jambo hilo.

“Mimi mambo yote huwa yanatolewa ofisini kwa njia ya ‘Press’ (mkutano na waandishi wa habari) sio kwa njia ya simu hivyo mtafahamu ni kitu gani,” alisema.

Tukio hilo limeibua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii kutokana na jinsi askari hao walivyotumia nguvu kubwa kumkamata dereva huyo ambaye haikufahamika mara kosa alilotendana alikokuwa akitokea au kuelekea.

Katika video hiyo, askari wanaonekana wakimshambulia dereva huyu katika jitihada za kutaka kumkamata na kumdhibiti lakini alionekana kufanikiwa kujinasua katika mikono yao.

Katika patashika hiyo, dereva huyo anasikika akipiga kelele kuomba msaada akilalamika kung’atwa shingoni na mmoja wa askari.

Baada ya kufanikiwa kutoka katika mikono ya askari dereva wa lori alionekana kukimbilia katika gari na kuchukua panga jambo ambalo liliwafanya watu kutimua mbio.

Na Aurea Simtowe, Mwananchi
Angalia video hapa chini

Share:

WAKAZI WA MADALE NA VITONGOJI VYAKE KUFURAHIA HUDUMA YA MAJI DAWASA


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo akizungumza na wananchi wakati alipotembelea Tenki la maji la Wazo na kuwahakikishia Watapata maji kama walivyoahidiwa na Afisa Mtendaji wa DAWASA. Picha zote na Cathbert Kajunason/MMG.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza mbele ya wananchi wa Tegeta Wazo na kuwahakikishia maji safi na salama kufikia leo usiku.
Mmoja ya wananchi akitoa shukrani mara baada ya kumaliza mkutano.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja (wa pili toka kushoto) akiw ana wananchi wakikagua maji yaliyokuwa yakitolewa katika tanki la maji ili kuweza maji safi tayari kuwasambazia wananchi.
Pampu za maji zilizofungwa ili kuweza kuwasambazia wananchi maji.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja wakishuka kutoka katika tanki la maji.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja wakikagua umaliziaji wa bomba ili kuweza kuwapatia maji wakazi wa Kata ya Madale na vitongoji vyake.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Daniel Chongolo akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati alipotembelea tenki la maji la Wazo.


Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.

Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA) imewahakikishia wananchi wa Kata ya Wazo kupata maji kwa kipindi chote kwa mwaka mzima bila kukatika. 

DAWASA imewekeza zaidi kwa kujenga tanki kubwa litakalokuwa likizalisha lita milioni sita tofauti na mwanzo ilipokuwa ikizalisha lita elfu sitini tu kwa mwaka.

Hayo yamezungumzwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja mbele ya wananchi akiwemo Mkuu wa Wilaya Kinondoni Daniel Chongolo, wakati akifafanua jinsi ya kutatua changamoto ya maji iliyokuwa ikiwakabili wakazi wa Kata ya Wazo na vitongoji vyake.

Amesema kuwa kulikuwa na changamoto kidogo ila kwa sasa wananchi wote waliokuwa kwenye mtandao wa maji wa zamani wataanza kupata maji kuanzia saa 2 usiku.

"Naomba niwatoe wasiwasi wananchi maana mradi huu wa sasa una uwezo wa kuzalisha maji lita milioni sita kwa sasa tofauti na ule wa zamani uliokuwa na uwezo wa kuzalisha maji lita elfu sitini na kupelekea mgao wa maji kwenye maeneo mengi," amesema Luhemeja.

Ameonheza kuwa kuanzia sasa hakutakuwa na mgao wa maji kwenye maeneo yote yaliyo na mtandao wa maji wamejipanga kuwahudumia ipasavyo wakazi hao.

Akielezea maeneo ambayo hayajafika mradi kutokana na kutokuwepo kwa mtandao wa 

maji, Mhandisi Luhemeja amesema kuna fedha takribani Bilioni 115 zimeshapatikana kwa ajili ya kusambaza mabomba yenye urefu wa Kilometa zaidi ya 1000 katika maeneo yote ya Mkoa wa Dar es Salaam.

“Kuna shilingi bilioni 115 zimeshatengwa tayari na zipo kwenye mchakato wa mwisho ili ziweze kutoka tuweze kuwahudumia wale wote ambao hawajafikiwa na mtandao wa maji kwa jiji la Dar es Salaam na Pwani,”amesema Luhemeja.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya Mh.Daniel Chongolo amesema katika serikali ya awamu ya tano chini ya Dkt John Pombe Magufuli miradi mingi imekuwa ikitekelezwa na wananchi wawe na subira na wameshaahidiwa maji kutoka kuanzia usiku wa leo.

Chongolo amesema, yeye binafsi anaamini kuwa Mtendaji Mkuu wa DAWASA sio mwanasiasa hawezi kudanganya kazi imefanyika na inaonekana ya kutoka uzalishaji wa maji lita elfu sita hadi milioni sita kwa lisaa.

"Kiukweli siwezi kuwasema vibaya DAWASA maana wamekuwa wakitoa huduma nzuri na hawa ni watendaji wala si wanasiasa hawawezi kuwaongopea, niwaombe tu wananchi muendelee kuwa wapole na wavumilivu wakati wanaendelea kuwatatulia matatizo yenu ya maji, binafsi nitakuja kujionea kwa macho kama maji yameanza kutoka kuanzia Jumannee Januari 15, 2019," amesema Chongolo. 

DAWASA wamedhamiria kufika asilimia 95 ya upatikanaji wa maji kwa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani kufikia Desemba mwaka huu.
Share:

ALLIANCE FC, BIASHARA UNITED ZAGOMA KUWA DARAJA


Kikosi cha Biashara United

Tukiachana na namna Simba wanavyoendelea kunoga katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika na Azam FC kuchukua Kombe la Mapinduzi kwa mara ya tatu mfululizo, mitanange ya Ligi Kuu soka Tanzania Bara inaendelea kila siku.

Kumekuwa na maendeleo makubwa kwa timu za Aliance FC na Biashara United tangu zilipofanya maamuzi mazito ya kutimua makocha wake mwishoni mwa mwaka uliopita kutokana na hali mbaya katika matokeo ya michezo yao.

Biashara United ilimtimua kocha wake Thiery Hitimana, Desemba 27 baada ya kuiongoza timu hiyo takribani mechi 16 na kuambulia mechi 11 pekee zilizoifanya timu hiyo kuburuza mkia katika msimamo wa ligi.

Lakini baada ya kuajiri kocha mpya Amri Said ambaye aliondoka Mbao FC, timu hiyo imefanikiwa kushinda michezo miwili na kwenda sare mechi moja, michezo ambayo imeifanya klabu hiyo kuondoka mkiani mwa ligi hadi katika nafasi ya 18 ikiwa na pointi 17.

Alliance FC ambayo imesifika kwa kusheheni vijana, ilianza vema katika mechi za awali za ligi kabla ya kupotea kabisa katikati ya mzunguko wa kwanza, hali iliyopelekea timu hiyo kuwa katika nafasi tatu za mwisho za msimamo wa ligi.

Baada ya kumtimua kocha wake na kumsajili kocha mpya, Malale Hamsini, Alliance FC ikaanza kubadilika na kuwa klabu shindani katika ligi. Katika michezo mitano ya mwisho, Alliance imefanikiwa kushinda michezo mitatu na kutoka sare mechi mbili na kusogea hadi nafasi ya 12 ya msimamo wa ligi.

Hali hii inaonesha kuwa timu hizi zimebadilika kwa kiasi kikubwa na kuleta matumaini mapya kuwa huenda zikamaliza katika nafasi nzuri zaidi za ligi.
Share:

HAWA NDIYO MAKOCHA 7 WENYE NAFASI YA KUTUA MAN UNITED


OLE Gunnar Solskjaer amepewa nafasi kama kocha wa muda wa Manchester United baada ya kufukuzwa kwa Jose Mourinho hapo kwenye dimba la Old Trafford.

Pamoja na kwamba Solskjaer ameanza vizuri kwenye kikosi hicho kwa kushinda mechi zake zote tano za mwanzo, lakini bado kuna majina yanayotajwa kuwa yanafaa kupewa nafasi ya ukocha hapo United.

Hapa tunawachambua makocha saba wanaopewa nafasi ya kuchukua mikoba ya kuiongoza klabu hiyo.

7. Antonio Conte

Ni mmoja wa majina yanayotajwa zaidi, hasa baada ya kuwa tayari ameshawahi kushinda taji la Ligi Kuu England. Tangu alipochukua nafasi ya kuinoa Juventus mwaka 2011, Conte ameshinda mataji sita katika miaka saba. Kama United wakitaka mtu ambaye atawarudisha kwenye utamaduni wao wa kushinda, basi Conte ana nafasi.

6. Eddie Howe

Howe amekuwa mmoja wa makocha wenye sifa nzuri zaidi katika historia ya soka la Uingereza kwa miaka ya hivi karibuni, kwa kuwa ameweza kuiongoza Bournemouth kutoka ligi daraja la chini na kuipandisha hadi Ligi Kuu, huku pia amewahi kuitumikia kwa muda mfupi.

Anaweza asiwe na gharama kubwa kumpata, kwa sababu anaijua vizuri ligi hiyo na haiba yake ni nzuri zaidi kwa wachezaji. Kikubwa zaidi ni kwamba bado kijana, katika umri wake wa miaka 41, anaweza kuwa chaguo sahihi zaidi kwa United kwa sasa.

5. Laurent Blanc

Blanc ana uzoefu wa kutosha kwenye kufundisha soka katika ngazi ya juu zaidi, na inasemwa kwamba yeye ndio sababu ya PSG kutawala soka la Ufaransa na Ligi Kuu ya nchi hiyo. Kwa kuwa alifanya makubwa kuijenga timu hiyo baada ya kurithi mikoba kutoka kwa Carlo Ancelotti. Kwa sasa yupo huru na anaweza kurudi kwenye nafasi ya ukocha kwa kuifikisha mbali United. 

4. Massimilliano Allegri

Ameshinda kila kitu kwenye ardhi ya nyumbani kwake Italia akiwa na Juventus, hivyo kama United wanataka kuendeleza utamaduni wao wa kushinda kila kitu, Massimilliano ndio anafaa kubebeshwa mikoba ya hapo Old Trafford. Taji pekee ambalo hajashinda na Juventus ni la Ligi ya Mabingwa Ulaya, hivyo iwapo atatua hapo Man United anaweza kupata changamoto nzuri na pengine hata kulibeba taji hilo. 

3. Zinedine Zidane

Zidane amechukua likizo kwenye kazi ya ukocha baada ya kuondoka pale Real Madrid wakati wa kipindi cha majira ya joto na alitarajiwa kwamba angerudi haraka. Man United anaweza kuwafaa, kwa kuwa Zidane nae ana molari ya kushinda na kama atatua hapo anaweza kuwa msaada mkubwa kwao.

Tayari mafanikio yake ya muda mfupi pale Real Madrid yanaweza kuwa chachu nzuri zaidi ya kuisaidia Man United. 

2. Ole Gunnar Solskjaer

Tayari anapendwa na mashabiki wa Man United na hasa kutoka na historia yake wakati akiichezea klabu hiyo kwa miaka 11. Tangu amechukua mikoba ya kuinoa timu hiyo kwa muda hadi mwishoni mwa msimu, tayari ameshinda mechi zote tano (kabla ya mechi ya jana wikendi). Anaonekana kama kocha anayeelewana zaidi na wachezaji na kwa uhakika anaweza kuifikisha United mahali panapotakiwa.

1. Mauricio Pochettino

Mashabiki wa Tottenham Hotspurs wana kila sababu ya kuchukizwa na habari kwamba kocha wao anawaniwa na klabu kadhaa kubwa Ulaya na hii ni kutokana na mafanikio aliyonayo kwenye klabu yao. Tangu ametua hapo Spurs kocha huyu raia wa Argentina ameiongoza timu hiyo kutokuwa nje ya tano bora kwenye msimamo wa Ligi Kuu na hayo ni mafanikio makubwa zaidi kwa kikosi hicho.

Kwa vyovyote vile, Pochettino ana nafasi nzuri zaidi ya kusaidia Man United kuweza kurudi kwenye enzi zake za gwiji Sir Alex Ferguson katika kutawala soka la Uingereza na hata Ulaya. 

Pochettino ana nafasi ya kuifanya tena United kuwa fahari ya soka la Uingereza, ambapo kwa miaka ya hivi karibuni imeonekana kama kiwango chake kimeporomoka.

Hivyo kama kocha huyo atapewa nafasi hapo Old Trafford kuna uwezekano mkubwa kuifanya timu hiyo kurudi kwenye kiwango chake kilichozoeleka.
Share:

TUNDU LISSU AANZA ZIARA...ATUA UINGEREZA

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ameanza ziara barani Ulaya na leo atakuwa London, Uingereza ambako amesema ataeleza kwa kina kile alichoandika katika waraka aliotoa kwa ajili ya mwaka huu.

Ziara ya Lissu inaanza baada ya Desemba 31, mwaka jana kuhitimisha safari ya matibabu aliyoanza Septemba 7, 2017 baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana kwa zaidi ya risasi 30 mjini Dodoma muda mfupi baada ya kutoka kuhudhuria kikao cha mchana cha Bunge.

Akizungumza na Mwananchi jana, Lissu ambaye hivi karibuni ameeleza nia yake ya kugombea urais kupitia Chadema, alisema leo ataitikia mwaliko wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).

Lissu alikwenda Ubelgiji Januari 6 mwaka jana kuendelea na matibabu akitokea Hospitali ya Nairobi, Kenya na katika kipindi chote cha matibabu, amefanyiwa upasuaji mara 22.

Alisema baada ya kutoka Uingereza, amepata mwaliko mwingine wa kwenda katika ofisi za Umoja wa Ulaya (EU) zilizopo Brussels, Ubelgiji na baadaye ataelekea Marekani na katika ziara hizo amesema ataelezea kile kilichomtokea Septemba 7, 2017, hali ya kisiasa nchini na mambo mengine.

Katika waraka wake huo alioutoa Januari 5, Lissu alitaja matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu huku pia akihoji sababu ya Bunge kutogharamia matibabu yake, mambo ambayo pia amesema kwamba atayaeleza katika ziara yake hiyo.

Waraka huo wenye kichwa cha habari ‘Mwaka mpya 2019, Mwaka wa kurudisha demokrasia, haki za binadamu na utu wetu Tanzania’ umegusia pia masuala ya haki za binadamu yakiwamo matukio ya utekaji, mauaji na mashambulio ya kudhuru mwili.

Mbali na kudai gharama za matibabu, Lissu amelalamika kutotembelewa na Spika Job Ndugai wala watumishi wa Bunge tangu alipolazwa hospitali licha ya kuwapo kwa ahadi hiyo.

“Kabla sijahamishiwa nchini Ubelgiji kutoka Kenya, Spika Ndugai aliahidi hadharani, kwenye mahojiano na Azam TV, kwamba atafika kunitembelea, mahali popote nitakapokuwa nimelazwa hospitalini.

“Hadi ninapoandika maneno haya, bado Spika Ndugai hajatimiza ahadi yake hiyo. Na hadi sasa, hakuna mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge, au afisa yeyote wa Bunge, aliyefika hospitalini kuniona na kunijulia hali,” ameandika Lissu katika waraka wake.

Hata hivyo, Spika Ndugai alijibu madai hayo ya Lissu akimtaka arejee nchini waweke mambo mezani kisha Watanzania wapime nani asiye na shukrani.

Alisema alipanga kwenda kumtembelea Nairobi lakini, “tarehe zangu nilizokuwa nimezipanga, akawa amehamishiwa kwenda Ubeligiji, kwa hiyo safari yote ikawa imevurugika.”

Kuhusu Bunge kugharamia matibabu yake, alisema ni kwa sababu hakufuata utaratibu unaotakiwa kwa mbunge kutibiwa nje.

“Mbunge hatibiwi katika nchi anayotaka mwenyewe kama yeye anavyofanya, unatibiwa nje pale inapobidi, pale unapokuwa na recommendations (ushauri) ya madaktari bingwa watatu wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” alisema.
Chanzo - Mwananchi
Share:

VYAMA VYA SIASA VYAALIKWA KUTOA MAONI MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA

Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria inatarajia kukutana na wawakilishi wa vyama vya siasa Januari 19 na 20, 2019 kuwasikiliza na kupokea maoni yao kuhusu muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa wa mwaka 2018.


Kamati hiyo itapokea maoni yao baada ya kumaliza vikao vyake na wadau wengine vitakavyofanyika Januari 17 na 18, 2019 mjini Dodoma kuhusu muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa mwaka 2018 na kufuatiwa na mkutano wake na wawakilishi wa kila chama cha siasa chenye usajili wa kudumu hapa nchini ambao wanapinga muswada huo.


Bunge litapokea maoni hayo wakati leo kesi iliyofunguliwa kupinga Bunge kujadili muswada huo ikiwa inatolewa uamuzi mahakamani.


Kesi hiyo ilifunguliwa Mahakama Kuu na wanasiasa watatu ambao ni kiongozi wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, Joram Bashange na Salim Bimani kutoka Chama cha Wananchi (CUF) kwa niaba ya wanachama wa vyama 10 vya siasa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Share:

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO JANUARI 14,2019.

Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 14, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.

Source

Share:

BATCH 7A LOAN ALLOCATION FOR FIRST YEAR AND CONTINUING STUDENTS WHO SECURED SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB

BATCH 7A LOAN ALLOCATION FOR FIRST YEAR AND CONTINUING STUDENTS WHO SECURED SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB

Click here to view batch 7a loan allocation for Sokoine University Of Agriculture first year and continuing students who secured sponsorship offered by HESLB in the academic year 2018/2019

The post BATCH 7A LOAN ALLOCATION FOR FIRST YEAR AND CONTINUING STUDENTS WHO SECURED SPONSORSHIP OFFERED BY HESLB appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Sunday, 13 January 2019

WAZIRI KIGWANGALLA NA WAKILI KARUME WAWEKA HISTORIA

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Hamis Kigwangalla amekutana na kufanya kikao chake cha chakula cha mchana na Wakili Fatuma Karume kujadili jinsi ya kuboresha uhusiano baina ya viongozi wanapowasiliana kutumia mitandao ya jamii na kuwa mfano bora kwa vijana wanaochipukia kwenye uongozi. Kupitia ukurasa wake wa twitter, Waziri Kigwangalla ameandika kuwa, “ Tuache utani pembeni, Siasa pembeni. Kuna la kujifunza katika hadithi hii; Shangazi ni mtu poa sana, mnyenyekevu, mvumilivu, msikivu, mwenye uelewa mpana wa mambo, na anasababu zake katika kila anachokifanya. Aidha Kigwangalla amesema, mkutano huo unatoa funzo kwa…

Source

Share:

KANGI LUGOLA ATUMBUA VIGOGO WATANO


Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewasimamisha kazi maofisa 5 wa idara ya wakimbizi wakituhumiwa kutoripoti uwepo wa nguo 1,947 zinazodaiwa ni za jeshi la Burundi, kwenye kambi za Nduta na Mtendeli zilizopo Mkoani Kigoma.


Waziri Lugola ametoa uamuzi huo leo, katika mkutano wake wa dharura na wanahabari katika ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es salaam.

Amewataja aliowasimamishwa kazi kuwa ni, Harrison Mseke (Mkurugenzi wa Huduma kwa Wakimbizi), Deusdedit Masusu (Mkurugenzai msaidizi), seleman Mzirai (Mkurugenzi msaidizi akishugulikia usalama na oparesheni), Peter Bulugu (Mkuu wa Kambi ya Nduta), na John Mwita (Mkuu wa kambi ya Mtendeli.

Aidha amesema kuwa misaada inapoingia nchini inatakiwa kukaguliwa, kwani kwa kitendo kilichofanywa ni kuhatarisha uhusiano kati ya Tanzania na Burundi.

"Leo tumekuta sare za Jeshi, kesho na keshokutwa tutakuta silaha za kivita na tunazipokea tuu bila kukagua eti ni misaada", amesema Waziri Lugola.

Disemba 31, 2018 vyombo vya dola mkoani Kigoma vilikamata nguo 1,947 zinazofanana na sare za jeshi zikiwa katika kambi za wakimbizi za Nduta na Mtendeli zilizopo mkoa wa Kigoma.
Share:

KILICHOTOKEA BAADA YA FATMA KARUME KUKUTANA NA KIGWANGALLA

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger