Sunday, 30 December 2018

VIGOGO WACHANGA FEDHA KUIPONGEZA YANGA,WAFUNGA MWAKA BILA KUFUNGWA

Baada ya kufanikiwa kuibuka na ushindi dhidi ya Mbeya City jumla ya mabao 2-1 hapo jana katika uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, wadau wa klabu ya Yanga wamechanga kiasi cha Sh. 960,000 kuwapongeza wachezaji kwa ushindi.

Mashabiki hao kutoka Wilaya ya Mbozi wakiongozwa na waziri wa kilimo Japhet Hasunga pamoja na mkuu wa mkoa wa Lindi Erasto Zambi wamechangia kiasi hicho cha pesa kama motisha kwa wachezaji pamoja na benchi la ufundi kutokana na kushinda mchezo huo.

Wadau hao wachache waliamua kuchangishana fedha kutoka mifukoni mwao ambazo waliwagawia kiasi cha Sh 35,000 kila mchezaji na Sh 30,000 kwa kila mmoja katika benchi la ufundi la klabu hiyo kama shukurani zao kwa kuwafanya mashabiki wao kufunga mwaka kwa furaha.

Yanga inaongoza ligi mpaka sasa ikiwa na jumla ya pointi 50 baada ya kushuka dimbani michezo 18, ikimuacha mpinzani wake Azam FC aliye katika nafasi ya pili kwa tofauti ya pointi 10.

Pia imeweka rekodi ya kutopoteza mchezo wowote mpaka sasa, ikiwa imeshinda michezo 15 na kwenda sare michezo miwili, huku ikiondoka na ushindi mfululizo katika mechi zake saba za mwisho.
Share:

MBUNGE NACHINGWEA ALIA NA KASI NDOGO MALIPO YA KOROSHO

Na Bakari Chijumba, Mtwara Mbunge wa jimbo la Nachingwea Mkoani Lindi, Hassani Massala amefika mjini Mtwara ambapo ni kituo kikuu cha malipo kwa wakulima wote wa korosho kwa kipindi hiki, Lengo likiwa ni kufuatilia kuhusu Hoja za wakulima wa Korosho kwenye jimboni lake, kwa madai licha ya takwimu mbalimbali anazozipata lakini bado kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wakulima, hivyo kumlazimu kama mwakilishi afuatilie. Akizungumza na mtandao wa DarMpya hii Leo, katika eneo la uwanja wa ndege mjini Mtwara, Masala amesema kwenye jimbo lake la Nachingwea, bado kumekuwa na malalamiko kutoka…

Source

Share:

MABAKI YA MWILI WA MSTAAFU ALIYEPOTEA BAADA KUPOKEA MAFAO YAPATIKANA MAKABURINI



 Inawezekana likawa ni moja ya tukio la nadra kutokea nchini. Alison Mcharo aliyepotea mwaka 2006 imebainika kuwa aliuawa na kuzikwa katika makaburi ya familia yake.

Mcharo aliyekuwa mkazi wa Kijiji cha Mpinji, Kata ya Mamba Myamba wilayani Same, alipotea baada ya kupokea mafao yake ya kustaafu kazi ya ualimu.

Inadaiwa kuwa Mcharo alitoweka baada ya kufika nyumbani na hakuonekana tena.

Jana, Polisi Mkoa wa Kilimanjaro walisema kuwa wamewatia mbaroni mkewe, Nasemba Alison (80) na mtoto wake, Orgenes Alison (45) wakiwatuhumu kwa mauaji hayo.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Hamis Issah alisema mabaki ya mwili wa Mcharo yaligunduliwa Jumapili iliyopita, jirani na kaburi la baba yake mzazi.

Kamanda Issah alidai kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na polisi unaonyesha kuwapo kwa ushiriki wa mkewe katika kupanga na kutekeleza mauaji hayo kwa kile alichodai ni tamaa ya fedha.

Haikufahamika mara moja kiasi cha fedha ambacho marehemu alilipwa baada ya kustaafu.

“Uchunguzi wetu wa awali umebaini marehemu aliuawa baada ya kukabidhiwa mafao yake na waliohusika waliingia tamaa baada ya kuona fedha nyingi alizokuwa amekabidhiwa.

“Baada ya kupokea mafao yake na kurudi nyumbani, ndipo aliuawa lakini taarifa ikatolewa kuwa amepotea. Mkewe baada ya kuhojiwa amejieleza vizuri...,” alidai kamanda huyo.

Alisema ripoti ya kupotea kwake ilitolewa polisi mwaka 2006 na kipindi chote cha miaka 12, alitafutwa bila mafanikio hadi Jumapili iliyopita mabaki ya mwili wake yalipoonekana.

Mwili wake uligundulikaje?

Kugundulika kwa mabaki ya mtu anayedaiwa kuwa ni Mcharo kulianzia kwenye kifo cha mama yake mzazi ambaye alikuwa ameacha wosia kuwa azikwe jirani na alipozikwa mumewe.

Kamanda Issah alisema ndugu na jamaa walikwenda kuchimba kaburi eneo ambalo marehemu aliacha wosia, lakini walishtuka kukuta mabaki ya mwili wa mtu mwingine katika eneo hilo.

“Kulikuwa hakuna alama yoyote kama kuna kaburi, lakini cha ajabu walikuta mabaki ya mtu, hapo waliacha kuchimba kaburi na kutoa taarifa Polisi kwa sababu ukikuta kaburi huwezi kuendelea kuchimba.

“Baada ya polisi kupata taarifa hizo tuliomba kibali cha Mahakama na tulipochimba eneo lile, kweli yalionekana mabaki ya mwanadamu na kulionekana kuna tai na shati.

“Hizo nguo zilitambuliwa kuwa ni za mwalimu Mcharo ambaye alidaiwa kupotea na alikuwa hajulikani alipo tangu mwaka, 2006.

“Jambo lingine lililotushangaza tulipofukua kaburi, tulikuta mabaki yale yamekaa mkao ambao si wa maiti inavyozikwa. Ilikuwa kwenye mkao ambao si wenyewe kama taratibu za maziko zilivyo,” alidai Kamanda Issah.

Alisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa kisayansi ikiwamo kuchukua sampuli za mifupa ili kuthibitisha kisayansi kuwa ni ndiye.
Na  Florah Temba, Mwananchi 
Share:

MANAIBU WAZIRI BITEKO NA MAVUNDE WAWACHARUKIA WAZALISHA KOKOTO MKOANI DODOMA

Naibu Waziri wa Madini Mh Dotto Biteko na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde  leo wametembelea kwa kushtukiza katika migodi ya machimbo ya kokoto katika eneo la Chigongwe Jiji la Dodoma ili kujionea shughuli za uchimbaji na usagaji mawe kufuatia agizo la Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Majaliwa la kutaka wazalishaji wa kokoto waliopata tenda ya kusambaza kokoto katika ujenzi wa mji wa serikali kuongeza kasi ya uzalishaji ili iendane sambamba na kasi ya ujenzi ambapo mahitaji ya kokoto yamekuwa makubwa sana. Baada ya…

Source

Share:

DKT.BASHIRU ALLY ATOA SIKU TATU KWA UONGOZI WA KCU, WAWE WAMEWALIPA WAKULIMA WA KAHAWA FEDHA ZAO.

  Na, Mwandishi wetu, Kagera. Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi taifa Dkt Bashiru Ally amewapa muda wa siku tatu viongozi wa chama kikuu cha ushirika KCU (T)199 LTD Mkoani Kagera, kuhakikisha kinawalipa wakulima wa zao la kahawa fedha za awali kabla hawajachukuliwa hatua. Dkt Bashiru Ally ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wajumbe wa halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi kwenye kikao utendaji kazi kilichowahusisha wajumbe kutoka halmashauri za Biharamulo na Muleba. Amesema kuwa wapo baadhi ya wakulima wanadai fedha zao tangu msimu uanze Mwezi Mei mwaka huu hadi…

Source

Share:

MTOTO AFICHWA KABATINI KWA MIEZI MITANO DODOMA

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa miezi mitano, jijini Dodoma amefungiwa kabatini na mwajiri wa mama mzazi wa mtoto huyo ambaye alikuwa akifanya kazi za ndani.

Akithibitisha kupokelewa kwa mtoto huyo katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Ibenzi amesema kuwa mtoto amefikishwa hospitali siku tatu zilizopita na kwamba atatibiwa kwanza tatizo la ukosefu wa lishe (utapiamlo).

Dkt. Ibenzi amesema kuwa mama wa mtoto huyo alifikishwa hospitalini hapo akiwa hajitambui kwa kile kilichodaiwa kupigwa na mwajiri wake hadi kupoteza fahamu.

"Mtoto anaendelea na matibabu kwakuwa bado tunamfanyia uchunguzi zaidi ikiwemo kufuatilia kama alipotiwa chanjo zote stahiki, na sisi tunatibu wagonjwa tu, mambo mengine watayafuatilia wahusika", amesema Dkt. Ibenzi.

Taarifa za awali zinadai kuwa binti huyo alipata ujauzito akiwa nyumbani kwa mwajiri wake anayedaiwa kuwa ni mwalimu wa shule ya msingi jijini humo ambaye alimtaka kufanya siri ili majirani wasifahamu kama yeye ni mjamzito.

Baadaye alifanikiwa kujifungua na kuendelea kufanya siri na mtoto kuhifadhiwa kabatini, hadi hapo juzi ambapo inadaiwa alimpiga binti huyo hadi kupoteza fahamu ndipo majirani walipofika eneo la tukio na kugundua kulikuwa na mtoto mchanga ndani ya kabati.
Chanzo:Eatv


Share:

OLE WAO WANAOHUJUMU MIUNDOMBINU YA UMEME – WAZIRI KALEMANI

  Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani jana (Desemba 29, 2018) amefanya ziara wilayani Kwimba, Mkoa wa Mwanza na kutoa onyo kali kwa watu wenye tabia ya kuhujumu miundombinu ya umeme pamoja na vishoka. Akizungumza kwa nyakati tofauti katika vijiji vya Ngulla na Ibindo, akiwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme, kuwasha umeme na kuzungumza na wananchi; Waziri Kalemani alitahadharisha kuwa serikali haitamvumilia yeyote atakayebainika kufanya hayo. “Mtu atakayebainika akikata nguzo, akiiba nyaya, akichezea transfoma kiasi cha kukosesha umeme wananchi, Mkuu wa Wilaya wa eneo husika…

Source

Share:

KAYA MASKINI WAELEZA WALIVYONUFAIKA NA FEDHA ZA TASAF, WABORESHA MAKAZI.

  Na Dinna Maningo,Tarime. Baadhi ya kaya maskini Wilayani Tarime mkoani Mara wameeleza kunufaika na fedha zitolewazo na mfuko wa maendeleo ya Jamii(TASAF) lengo likiwa kuwasaidia ili wajikwamue kimaisha katika kujiongezea kipato. Wakizungumza wakati wakipokea fedha za miezi miwili ya Novemba na Desemba katika viunga vya shule ya msingi Buhemba kata Bomani wamesema kuwa tangu waingizwe kwenye mpango wakunusuru kaya maskini wameweza kununua mifugo na fedha zingine zimewasaidia kujikimu kimaisha. Alex Muhagama miaka (73) mkazi wa mtaa wa Buhemba ambaye upokea sh.20,000 alisema kuwa kulingana na umri wake hana uwezo…

Source

Share:

BIDHAA ZENYE KILEVI KUTOZWA USHURU KIELEKTRONIKI


Bidhaa zinazostahili kutozwa ushuru wa bidhaa kama vile sigara, mvinyo, pombe kali pamoja na bia zitaanza kutumia rasmi stempu za kielektroniki Januari, 2019 katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga na Mbeya ambapo mfumo wa stempu hizo umeshafungwa kwenye mitambo ya uzalishaji.
Akizungumza mara baada ya kumaliza kukagua ufungaji wa mfumo huo katika Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) na Kiwanda cha kutengeneza vinywaji vikali cha Nyati Spirit Tanzania jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Charles Kichere alisema kuwa mfumo huo mpya unaondoa mfumo wa zamani wa stempu za karatasi.

“Nimekuja kufanya ziara katika viwanda hivi ili kujiridhisha kama kweli mfumo huu wa stepu za kielektroniki umefungwa na nimejionea mwenyewe mfumo tayari umefungwa katika viwanda vyote nilivyotembelea. Hivyo, tunaachana na mfumo wa zamani wa stempu za karatasi na kwa sasa tunaendelea kufunga mfumo huu mpya wa stempu za kielektroniki kwenye mikoa mingine ambayo haitaanza katika awamu hii”, alisema Kichere.

Kichere alisema kuwa lengo la kuweka stempu za kielektroniki kwenye bidhaa hizo ni kupata idadi halisi ya uzalishaji wa bidhaa ili kutoza kodi stahiki na kuondoa dhana ya kusema kwamba TRA inawaonea wafanyabiashara wanaozalisha bidhaa hizo kwa kutoza kodi isiyoendana na uzalishaji.

“Lengo la kuweka stempu hizi za kielektroniki ni kupata kiasi halisi cha uzalishaji wa bidhaa hizi ili kila upande uridhike yaani mzalishaji alipe kodi sahihi na sisi TRA tutoze kodi stahiki bila kupingana wala kugombana na wateja wetu”, alisema Kichere.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa kiwanda cha kutengeneza vinywaji vikali cha Nyati Spirit Tanzania Rupa Suchak amesema kuwa amefurahishwa na kitendo cha serikali kufunga mfumo huo wa stempu za kielektroniki kwa sababu serikali itaongeza mapato na wafanyabiashara wataongeza uhiari wa kulipa kodi.

“Ninaishukuru sana serikali yetu kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kuleta mfumo huu mpya ambao utaongeza mapato na kupanua wigo wa kodi lakini pia kwetu sisi wafanyabiashara tutaongeza uhiari wa kulipa kodi”, alisema Rupa.

Uwekwaji wa stempu za kielektroniki katika bidhaa nyingine kama vile juisi, maji ya chupa, bidhaa za muziki na filamu (CD\DVD\Tape) zitafuata kwa tarehe ambayo itatangazwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania hapo badae.
Share:

SERIKALI KUSAJILI WAKULIMA WOTE NCHINI

Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga (Mb) amewaagiza Wakurugenzi wa Bodi za Mazao kuanza mara moja zoezi la kuwatambua na kuwasajili wakulima wa mazao yote nchini lengo likiwa kuwatambua ili kupanga mipango sahihi yenye kuongeza tija na uzalishaji katika mazao yote.


Mhe Hasunga amesema hayo Jumamosi 29 Disemba 2018 wakati akizungumza na Wenyeviti wa Bodi za Mazao pamoja na Wakurugenzi wa Bodi hizo za Mazao Jijini Dodoma ambapo amesisitiza kuwa ili kuongeza tija na uzalishaji katika Sekta ya kilimo na kuandaa mipango madhubuti ya kuendeleza mazao yote ni vyema kuwatambua Wakulima wote nchini.

Agizo hilo limekuja baada ya takribani wiki tatu kupita tangu Waziri Hasunga alipotoa agizo kwa Bodi ya Korosho kuandaa daftali maalumu la kuwatambua wakulima wa korosho nchi nzima, ambapo moja ya taarifa ambazo zitajumuishwa katika daftali hilo ni pamoja na jina kamili la Mkulima, Mkoa, Wilaya, Kata na Tarafa anayotoka.

Mambo mengine yanayojumuishwa ni pamoja na Kitongoji, Mtaa au Jina la Kijijini anapotoka, mahali lilipo shamba pamoja na ukubwa wa shamba lake.

“Tumepata changamoto kadhaa wakati wa kuwahakiki wakulima wa korosho katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Ruvuma na kama Bodi ya Korosho ingekuwa makini kuandaa daftari la Wakulima zoezi la uhakiki lingekuwa rahisi, kwa ajili hiyo niliwaagiza Bodi ya Korosho kukamilisha zoezi hili mpaka Mwezi Machi, 2019 na Bodi za Mazao zilizobaki ukiacha Bodi ya Tumbaku ambao wao tayari walishafanya hivyo, kukamilisha Mwezi June, 2019,” amesema Mhe Hasunga.

Waziri Hasunga ameongeza kuwa mipango sahihi ya kuwaendeleza Wakulima kuanzia kwenye kilimo chenyewe hadi kufikia katika hatua ya kuvuna, kuhifadhi na kulifikia soko ni vyema kuwa na mfumo maalumu wa kanzi data (Database) ya kuwafahamu ili kushughulikia mahitaji yao kisasa na kwa haraka zaidi.

Bodi za Mazao zilizoshiriki mkutano huo ni pamoja na Bodi ya Korosho, Bodi ya Pamba, Bodi ya Mkonge, Bodi ya Pareto, Bodi ya Chai, Bodi ya Kahawa, Bodi ya Tumbaku, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko na Bodi ya Sukari.

Wakala zilizoshiriki ni pamoja na Wakala wa Taifa wa Mbolea (ASA) Wakala wa Wakulima Wadogo wa Chai (TSHTDA).

Taasisi nyingine za Wizara ya Kilimo zilizoshiriki ni pamoja na Taasisi ya Udhibiti wa Mbegu (TOSCI), Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO), Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu vya Ukanda wa Kitropiki (TPRI), Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (AGITF), Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA), Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI), Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Kampuni ya Taifa ya Mbolea (TFC) na Bodi ya Leseni za Maghala.

Chanzo:Eatv
Share:

Picha:RAIS MAGUFULI AMTEMBELEA MAMA YAKE MZAZI ANAYETIBIWA JIJIN DAR ES SALAAM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Wasaidizi wake wakimuombea Mama yake Mzazi Bibi. Suzana Magufuli anayepatiwa Matibabu Jijini Dar es Salaam Desemba 30, 2018. Bibi Suzana Magufuli anasumbuliwa na ugonjwa wa Kiharusi ambapo amekuwa akipatiwa matibabu kwa takribani miezi mitatu sasa.




Picha na Ikulu
Share:

POLISI WAUA MAGAIDI 40 WALIOPANGA KULIPUA MAKANISA


Jeshi la polisi nchini Misri limesema kuwa limeua wapiganaji 40 wa makundi ya kigaidi waliokuwa wanapanga mashambulizi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani, polisi waliwavamia magaidi hao katika maficho yao yaliyokuwa Giza na Sinai Kaskazini, jana alfajiri.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa magaidi hao walikuwa wamepanga kushambulia makanisa, askari pamoja na maeneo yenye watalii wengi.

Juzi, wapiganaji wa makundi ya kigaidi walitekeleza shambulizi la bomu katika eneo la Giza kwenye basi la watalii. Hakuna kundi lolote lililojitokeza kudai kutekeleza tukio hilo ambalo lilisababisha vifo vya watalii kutoka Vietnam pamoja na waongozaji wa watalii hao

Imeelezwa kuwa polisi waliwaua watu 30 katika mashambulizi mawili ya kushtukiza kwenye eneo la Giza, na wengine 10 waliuawa katika eneo la El-Arish ambao ni makao makuu ya jimbo la Sinai Kaskazin

“Makundi ya magaidi yalikuwa yanapanga kutekeleza mashambulizi katika maeneo ya makanisa na sehemu ambazo wakristo walikuwa wanaabudia. Pia, walipanga kulenga maeneo ya utalii pamoja maeneo mengine ya kiuchumi,” imeeleza taarifa ya Wizara.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, polisi wamekamata vifaa vya kutengenezea mabomu pamoja na idadi kubwa ya silaha.
Share:

TAKUKURU KUINGILIA KATI SAKATA LA RUSHWA YA NGONO VYUO VIKUU

Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) imeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuongeza jitihada zaidi za kuwajengea uwezo 
wanafunzi na wahadhiri juu ya masuala ya rushwa hasa ya ngono kwa lengo la kupunguza au kumaliza kabisa tatizo hilo vyuoni.

TSNP umesema kuwa rushwa ya ngono kwa sasa imeshamiri katika vyuo mbalimbali nchini hivyo inapaswa kukemea kwani inaharibu maisha ya wanafunzi ambao wanategemewa kuwa viongozi wa baadae.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Katibu wa TSNP, Joseph Marekela alisema rushwa ya ngono vyuoni ni changamoto kubwa hasa kwa wanafunzi wa kike hivyo jitihada za makusudi zinahitajika ili kuhakikisha kuwa 
hakuna mtu anayepoteza haki yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa hiyo ambayo si tu inapoteza utu wa mtu bali ni kinyume na haki za binadamu.

Alisema mfumo wa upimaji uwezo uliyopo sasa umempa mamlaka makubwa mhadhiri ya kuamua hatma ya mwanafunzi kitaaluma jambo ambalo lina
sababisha uwepo wa mianya ya rushwa ya ngono kwa wahadhiri wasio na maadili ambao wanatumia nafasi yao kuminya haki ya mwanafunzi.

“Kwakuwa tatizo hili ni kubwa na limeathiri wanafunzi wengi chuoni tunatoa wito kwa Takukuru waongoze jitihada zaidi kwa kuwajengea uwezo taasisi za 
Takukuru vyuoni ili kupambana na tatizo hili kikamilifu, pia vituo vya jinsia na Serikali za wanafunzi ziwajibike ipasavyo ili kuhakikisha kuwa hakuna anaepoteza haki yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa hiyo ya ngono,” alisema.

Hata hivyo mtandao huo umesema kuwa ukosefu wa taulo za kujisitiri wanafunzi wa kike hasa wa vijijini kipindi cha hedhi inaathiri maendeleo ya wanafunzi 
hao kitaaluma.

Kutokana na hali hiyo, Marekela alisema wanatoa wito kwa Serikali kupitiaWizara yenye dhamana kulitazama upya suala kwa kugawa bure taulo hizo kwa 
wanafunzi wa kike hasa waliopo maeneo ya vijijini ili kunusuru ndoto zao walizojiwekea.

Aidha alisema suala la mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu bado ni changamoto kwani wengi wao wameshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa mikopo hiyo
Share:

CHADEMA WAZUIWA KUFANYA MKUTANO JIMBONI KWA MBOWE

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimezuiwa kufanya mkutano pamoja na ziara ya viongozi wa chama hicho kitaifa, wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.

Hayo yamebainishwa kupitia barua iliyotumwa kwa Katibu wa CHADEMA wilayani Hai, ambayo imesainiwa na Katibu tawala wa wilaya hiyo, Said Omary iliyoelekeza kusitisha kibali cha kufanya mkutano wilayani humo.

"Nimeagizwa na Mkuu wa Wilaya ambae ni mwenyekiti wa kamati ya usalama ya Hai. Nikuandikie kukutaka kusitisha mkutano na ziara ya viongozi wako kitaifa, tarehe 29/12/2018 na kuendelea", imesema barua hiyo.

Baada ya zuio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amethibitisha kukamatwa kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji pamoja na viongozi wengine watatu kwa makosa ya kufanya kusanyiko bila kibali.

Share:

Good News : Pakua Upya App ya Malunde 1 blog ...Imeboreshwa Kukupa Raha zaidi ...Bonyeza HAPA SASA

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.

Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog

NB: App uliyokuwa unatumia mwanzo tumeifuta na kuleta mpya ya kisasa zaidi..Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Share:

DC MBONEKO AWAONYA POLISI WANAOTUMIWA NA VIONGOZI KUONEA WANANCHI,CHUKI ZA DIWANI ZATAJWA

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko amewaonya baadhi ya askari wa Kituo cha Polisi Kata ya Salawe kutumiwa na viongozi kwenda kuvuruga amani kwa wananchi, kinyume cha maadili ya kazi yao inayowataka kulinda usalama wa raia na mali zao.


Inadaiwa diwani wa kata hiyo, Joseph Buyugu anawatumia baadhi ya askari kuonea wananchi hasa wanaofichua maovu kwenye mikutano ya hadhara ya viongozi wakuu kwa kuwapiga na kisha kuwatia mbaroni.

DC Mboneko ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama alitoa onyo hilo juzi wakati alipofanya mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua kwenye kata hiyo, ambapo hivi karibuni kulitaka kutokea machafuko ya amani kwenye eneo hilo.

 Alisema amesikitishwa na viongozi wa maeneo hayo kulitumia Jeshi la Polisi vibaya kutaka kuvuruga amani ya nchi na kujichukulia mamlaka ambayo yapo nje ya utawala wao kwa kuwapiga wale ambao wamekuwa wakifichukua maovu yao pamoja na kuwavunjia nyumba wananchi na kuharibu mali zao.

“Jeshi la Polisi nawaonya msitumiwe na viongozi kuvuruga amani ya nchi ninyi kazi yenu ni kudumisha amani na kulinda usalama wa raia na mali zao na si vinginevyo, acheni kutumika kuonea wananchi pamoja na kuwaomba rushwa, kama mnaona mishahara yenu haitoshi acheni kazi,” alisema Mboneko. 

“Na nyie viongozi msiwe chanzo cha machafuko ya kuvuruga amani kwa wananchi, kazi yenu ni kuwatumikia na kutatua kero zao pamoja na kuwa hamasisha kwenye masuala ya maendeleo, na siyo kugeuka miungu watu na kuanza kuwaonea huku mkiwapiga, kuwavunjia nyumba zao, na kisha kuwasweka rumande,” aliongeza.

Awali baadhi ya wananchi wa kata hiyo ya Salawe wakiwakilisha kero zao kwa mkuu huyo wa wilaya akiwamo Seke Nyeke na Dumila Hamis, alisema malalamiko yao mengi yalikuwa ni viongozi wa maeneo hayo akiwamo na diwani wamekuwa wakishirikiana na askari Polisi kuwaonea na ili kutoka rumande, lazima watoe kitu kidogo.

Kwa upande wake, diwani Buyugu alikana tuhuma hizo za kulitumia Jeshi la Polisi kuvuruga amani huku Kamanda wa Polisi Wilaya ya Shinyanga, Claud Kanyolota akiwaonya askari hao kutorudia tabia hiyo na kubainisha malalamiko hayo atayafanyia kazi ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Ngassa Mboje alisikitishwa na kitendo cha diwani wa Salawe aliyechaguliwa na wananchi na matokeo yake kuwakandamiza huku tatizo hilo limeonekana analifanya kwa wale ambao ana chuki nao, jambo ambalo halifai na ni hatari alimuomba aache tabia hiyo ili wananchi waishi kwa amani.



Share:

Serikali Yakaribisha Wafanyabishara Wanaotaka Kubangua Korosho

SERIKALI  kupitia kwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda imewakaribisha wafanyabiashara kununua korosho na kuzibangua.
 
Mbali na uamuzi huo, Waziri Kakunda amesema Serikali  bado inaendelea kuingia mikataba na wabanguaji ili kupunguza mzigo wa korosho.

Kakunda ametoa kauli hiyo wakati taarifa ya timu ya pamoja ya wataalamu kuhusu hali ya utekelezaji wa operesheni korosho iliyotolewa Novemba 27 ikionyesha kuwa itachukua muda mrefu  kubangua korosho za msimu huu.
 
Novemba 12, Rais John Magufuli alitangaza Serikali kununua korosho yote kutoka kwa wakulima msimu huu kwa bei ya Sh3,300 kwa kilo.
 
Licha ya Waziri Kakunda kusema haina shida kwa ubanguaji kuchukua muda mrefu, amewataka wafanyabiashara wanaoweza kubangua wenyewe wakae meza moja na Serikali ili wauziwe korosho.
 
“Kama mtu anatokea popote iwe ndani au nje akasema mimi nataka ninunue korosho nikabangue mwenyewe, labda ana bei nzuri aje tuzungumze. Ije mvua, lije jua korosho ziko kwenye maghala, kuna tatizo hapo? Zitabanguliwa tu muda wowote,” alisema.
 
Alisema ubanguaji unaendelea baada ya Serikali kuingia mkataba na baadhi ya kampuni.
 
“Leo (juzi) ilikuwa niende kuzindua ubanguaji wa kule Mtwara, kwa hiyo siyo tumekaa tunasubiri wateja, tunaendelea kubangua.
 
“Sido (Shirika la Viwanda Vidogo) ambao ni wabanguaji wadogo, wameshabangua tani sita. Bado kuna viwanda tulikuwa tunaingia navyo mkataba, hadi jana (juzi) tumeingia mikataba minne na bado tutaingia mingine zaidi ya 12,” alisema.
 
Inaelezwa kuwa kuna jumla ya viwanda 23 vya kubangua korosho na ambavyo uwezo wake uliosimikwa sasa ni kubangua jumla ya tani 42,200. Hata hivyo, uwezo wa mashine kwa kiwanda kimoja ni tani 11,142 kwa mwaka sawa na asilimia 26 tu ya uwezo uliosimikwa wa viwanda hivyo.
 
Taarifa hiyo ya timu ya pamoja ya wataalamu inaonyesha matarajio ya uvunaji wa korosho kwa msimu wa mwaka 2018/19 kufikia jumla ya tani 275,191 na kama viwanda vinane vinavyofanyakazi vingebangua korosho kwa kiwango kinachotakiwa cha tani 127,200 kwa mwaka, kazi hiyo itafanyika kwa miaka miwili.
 


from MPEKUZI http://bit.ly/2LHBEZl
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger