Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Sunday 18 August 2019

Waasi wa Kihouthi washambulia kiwanda cha mafuta nchini Saudia Arabia

Waasi wa kihouthi nchini Yemen hapo jana walifanya Shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani dhidi ya kisima cha mafuta cha Shaybah nchini Saudi Arabia kinachotoa takriban mapipa milioni moja ya mafuta ghafi kwa siku. 

Hilo ni shambulizi la pili la aina hiyo katika sekta hiyo muhimu ya mafuta nchini humo katika siku za hivi karibuni.

Vyombo vya habari nchini humo viliwanukuu maafisa wa serikali ya Saudi Arabia wakisema kuwa uzalishaji mafuta katika kisima hicho haukuathirika Kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali ya Saudia Aramco, imetoa taarifa inayokiri kutokea moto kiasi katika kituo hicho kinachotoa mafuta huko Shaybah.

Waasi wa kihouthi wamefanya misururu ya mashambulizi ya angani yanayolenga maeneo tofauti tofauti ya Saudi Arabia katika miezi ya hivi karibuni. 

Mzozo huo nchini Yemen kwa kiasi kikubwa unaonekana kuwa ni vita baina ya Saudi Arabia yenye Waislamu wa dhehebu la Kisunni na Iran yenye Waislamu wa madhehebu ya Kishia.


Share:

LIVE -- MWENYEKITI WA SADC RAIS DKT JOHN MAGUFULI AKIHITIMISHA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI WA JUMUIYA YA SADC

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 18 August




Share:

Saturday 17 August 2019

MWINYI, MKAPA, KIKWETE, KARUME WAHUDHURIA MKUTANO KUSHUHUDIA RAIS MAGUFULI ATAKAVYOKABIDHIWA UENYEKITI WA JUMUIYA YA NCHI ZA SADC

 Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii

MARAISI wastaafu wa Serikali ya Tanzania wamehudhuria Mkutano Mkuu wa 39 unaofanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  kushuhudia Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk.John Magufuli akikabidhiwa Uenyekiti wa jumuiya hiyo.

Katika mitandao ya kijamii baadhi ya watu wasiokuwa na njema walikiwa wakizusha kuwa Dk.Magufuli amesusiwa mkutano huo na watangulizi wake.Hata hivyo uzushi wao umekosa mashiko kwani viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwamo marais hao wote wastaafu wamehudhuria mkutano huo wa kihistoria.

Marais wastaafu ambao wamehudhuria ni Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni Rais ww Serikali ya Awamu ya Pili,Benjamin Mkapa ambaye ni Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu,Jakaka Kikwete aliyekuwa Rais wa Awamu ya Nne na kwa upande wa Zanziabar Rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Amani Karume.

Mbali ya wastaafu hao kuwemo kwenye mkutano huo ambao pia wametambulishwa kwa wageni mbalimbali kutoka nchi 15 za jumuiya hiyo,pia viongozi wengine wa Serikali ya Tanzania waliohudhuria ni Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Mama Samia Suluh Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Wengine ni Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu Balozi John Kijazi,mawaziri, viongozi wa ngazi mbalimbali wastaafu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Poul Makonda.Pia wamehudhuria watu mashuri wa ndani na nje ya Tanzania.

Pamoja na shughuli mbalimbali ambazo zinaendelea kwenye mkutano wa jumuiya hiyo ambao utafanyika kwa siku mbili,tukio ambalo linasubiriwa na Watanzania wengi ni kuona Rais Dk.Magufuli anakabidhiwa Uenyekiti wa SADC.
Nafasi hiyo ya Uenyekiti wa SADC kwa Tanzania mara ya mwisho ilishikiliwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa miaka 16 iliyopita na sasa anakwenda kukabidhiwa Rais mchakazi Dk.Magufuli.

Hata hivyo nchi mbalimbali za jumuiya hiyo zimeonesha matumaini na imani kubwa kwa Rais Magufuli hasa kutokana na utendaji wake tangu akiwa Rais ambaye anaamini katika wananchi kufanya kazi na nchi kujitegemea.

Pia amekuwa na kauli mbiu ya Tanzania ya viwanda ambayo itaipeleka nchi uchumi wa kati.Kwa nchi za SADC moja ya mkakati wao ni kuhamasisha viwanda kwa nchi wanachama kazi ambayo Rais Magufuli ameianza kabla ya kukabidhiwa uenyekiti,hivyo nchi za jumuiya hiyo zinaamini akiwa Rais Magufuli atawafikisha kwenye nchi ambazo uchumi wake utatokana na viwanda.
Share:

Wananchi Bahi Watakiwa Kutowaficha Na Kuwanyanyapaa Walemavu

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wananchi wa kata ya ibihwa wilayani bahi wametakiwa kutowaficha watoto wao ndani kwa kigezo cha ulemavu ,Kama  sheria ya mtoto kifungu cha 8  inavyotoa katazo la jamii kumnyima mtoto haki ya kusoma kwa kigezo cha ulemavu.
 
Akizungumza katika mkutano wa wanachi uliyoratibiwa na shirika la International Aids service jana mkoani Dodoma meneja wa shirika hilo Alan Kamnde alisema ukosefu wa elimu  kwa wanachi kuhusu umuhimu wa kumthamini mtoto mwenye ulemavu bado ni kikwazo kikubwa katika jamii.
 
“Lengo la shirika hili ni kuhakikisha  jamii inafikiwa na kupewa uwelewa kuweza kuwaruhusu watoto kupata haki ya kielimu na Zaidi kuweza kuwajumisha watoto wenye ulemavu na wasiyo na ulemavu kujumika na kupata elimu pamoja kwasabau watoto  wote ni sawa”Alisema kamnde. 
 
Naye afisa mradi wa shirika hilo Jane Mjidange amesema ni vyema wazazi wakawapenda watoto ,samabmba na kuomba mamlaka zinazohusika kuyashughulikia matukio ya watoto wenye ulemvu kuyachukulia uzito matukio yao.
 
“Jamani mama zangu hakuna mtoto aliyeomba mungu amuumbe akiwa mlemavu hivyo msiwatenge na ni vizuri hata zile mamlaka zinazohusika zikachukulia uzito kesi za watoto”alisema jenipha.
 
 Diwani wa kata ya Ibihwa, Daudi lesaka alisema  katika kata yake kumekuwa na mimba za mara kwa mara kesi zimefikishwa mahakani na zinafanyiwa kazi  kwa mujibu wa sharia
 
Aliongeza  kwenye kata yake atachukua hatua kwa familia zote aambazo zimezuia kuwapeleka watoto shule
 
“Kuhusu swala la mimba tumechukua hatua za kuzipeleka kesi zote mahakamani na zinzshughulikiwa na kwa upande wa familia ambazo zimeshindwa kuwapeleka watoto shule nao tutawachukulia hatua haraka sana” alisema lesaka.


Share:

AFISA UVUVI MULEBA AWAONYA WAVUVI HARAMU



Kaimu Afisa uvuvi wilayani Muleba mkoani Kagera Maengo Nchimani 
Na Lydia Lugakila -Malunde1 blog
Kaimu Afisa Uvuvi wilayani Muleba mkoani Kagera Maengo Nchimani ametoa onyo kali kwa wananchi wanaojihusisha na vitendo vya uvuvi haramu vinavyosababisha kipato cha mkoa wa Kagera kushuka.

Nchimani ametoa onyo hilo wakati akiongea na baadhi ya wafanyabiashara waliojitokeza katika uwanja wa Gymkana katika Manispaa ya Bukoba ambako imefanyika wiki ya uwekezaji Kagera yenye lengo la kutangaza fursa mbalimbali zilizopo mkoani Kagera.

Afisa huyo amesema vitendo vya uvuvi haramu vinavyoendelea katika baadhi ya maeneo wilayani Muleba mkoani hapa vinakwamisha maendeleo na jitihada za mkuu wa mkoa wa kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti za kuutangaza mkoa wa kagera kama sehemu ya uwekezaji ambapo wahitaji wa mazao hayo ya samaki kutohitaji samaki waliokosa ubora na thamani.

Amesema kuwa sheria kali zitachukuliwa dhidi ya wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo huku akitaja kuanzisha doria za usiku ili kuwabania wale wote wanaofanya vitendo hivyo .

Akielezea wilaya hiyo amesema kuwa wilaya ya Muleba ina zaidi ya mitumbwi zaidi ya 400 na inavua dagaa kwa wingi na uzalishaji wake ni kwa asilimia kubwa hivyo amewataka wananchi hao kuacha tabia hiyo mara moja ili kupata wawekezaji wengi toka nje ya nchi.

Amesema kuwa wilayani hiyo ina changamoto ya kutokuwa na kiwanda cha kuongeza thamani ya zao hilo hivyo kuwataka wawekezaji kujitokeze kwa wingi ili kuinua uchumi wa Kagera .

Amesema juhudi kubwa za utoaji elimu juu ya uvuvi haramu zinafanyika ili kunusuru kizazi cha samaki kwa pato la kagera na taifa zima.


Share:

RAIS MAGUFULI AIOMBA JUMUIYA YA KIMATIAFA KUIONDOLEA VIKWAZO ZIMBABWE


Rais  Magufuli ameiomba Jumuiya ya Kimataifa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi nchi ya Zimbabwe ambapo amesema kuwa vikwazo hivyo vimelemaza uchumi wa taifa hilo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 17, alipokuwa akihutubia wakuu wa nchi Wanachama Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo na Rais wa Namibia, Dk Hage Geingob ambapo ataingoza kwa kipindi cha mwaka mmoja.

"Zimbabwe wamekuwa kwenye vikwazo kwa muda mrefu, hiki kifungo tunaathirika sisi wote, napenda kupendekeza kupitia mkutano huu kuziomba Jumuiya za Kimataifa ziiondolee vikwazo Zimbabwe, na nawaomba wanachama wote tulisemee hili." amesema Rais Magufuli

Zimbabwe iliwekewa vikwazo na mataifa ya Magharibi kutokana na hatua ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe, kuchukua kwa lazima ardhi ya wahamiaji wenye asili ya kizungu.


Share:

Rais Magufuli Akabidhiwa Uenyekiti Wa SADC Na Kuitaka Sekretarieti Ya SADC Kuchukua Hatua Kukuza GDP Ndani Ya Jumuiya

Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt John Magufuli amekabidhiwa rasmi nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) huku akiitaka Sekretarieti ya Jumuiya hiyo kuchukua hatua za makusudi ili kuharakisha ukuaji wa Pato la Uchumi la Taifa ndani ya Jumuiya hiyo ambalo limekuwa likishuka mwaka hadi mwaka.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo leo Jumamosi (Agosti 17, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ukuaji wa Pato la Taifa katika jumuiya hiyo umekuwa si wa kuridhisha, pamoja na nchi nyingi za Jumuiya hiyo kuwa na wingi wa utajiri wa raslimali.

Rais Magufuli alisema Sekretarieti ya Jumuiya hiyo haina budi kuweka mikakati na mipango madhubuti kwa Nchi wanachama ndani ya jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinaweka na kuandaa mazingira bora na wezeshi yenye uwezo wa kutoa fursa za ukuaji wa uchumi ikiwemo ukuzaji wa sekta ya biashara ndani ya jumuiya hiyo.

“Mwaka 2005, 2006 na 2007 ukuaji wa Pato la Taifa ndani ya Jumuiya lilikuwa kwa asilimia 6.6 (2005), 7.3 (2006) na 8.0 (2007) lakini mara baada ya hapo ukuaji wake haukuwa wa kuridhisha ambapo mwaka 2012 ilikuwa (4.4), 2013 (4.3), 2014 (3.4), 2015 (2.2), 2016 (1.4), 2017 (3.0) na 2018 (3.1)” alisema Rais Magufuli.

Alisema ili kuweza kukuza uchumi Nchi za SADC, Viongozi wa Mataifa hayo hayana budi kuwa na viwango, sera, sheria na kanuni za pamoja zinazotoa fursa kwa nchi hizo kuwa na mfumo wa pamoja utakaowezesha jumuiya hiyo kuweza kubadilishana ujuzi, uwezo na kuuziana bidhaa na kuondoa masharti mepesi yatakayorahisha ukuaji wa uchumi.

Akifafanua zaidi, Rais Magufuli alisema pamoja na Jumuiya hiyo kujiwekea malengo kwa kila Nchi za jumuiya hiyo kukuza uchumi wake angalau kufikia kiwango cha asilimia 7 mwaka 2018 kwa kila Nchi, lakini ni nchi chache zilizofanikiwa kufikia kiwango hicho, hivyo juhudi za pamoja zinahitajika katika kuhakikisha kuwa kiwango hicho kinafikiwa kwa nchi zote.

Aliongeza kuwa malengo ya pamoja yanapaswa kuwekwa na Nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa taarifa za biashara ambazo Mataifa mengi ya Asia yamekuwa yakitumia fursa hiyo pamoja na kuimarisha na kujenga viwanda vyenye uwezo wa kuzalisha bidhaa vitavyowezesha kupunguza gharama za ununuzi wa bidhaa kutoka nje ya Jumuiya hiyo.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema pamoja na mafanikio mbalimbali ambayo tayari yamepatikana, zipo baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikiikabili jumuiya hiyo ikiwemo majanga ya binadamu, njaa na ukame ambazo zimefanya ukuaji wa uchumi katika baadhi ya nchi wanachama kuweza kuathirika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti aliyemaliza muda ambaye pia ni Rais wa Namibia Dkt. Hage Geingob alisema Jumuiya hiyo ina imani na Uongozi mpya wa Rais Dkt. John Magufuli kutokana na utendaji kazi na msisitizo alionao katika kusimamia malengo ya uanzishaji wa jumuiya hiyo katika kuleta maslahi na maendeleo ya wananchi waliopo ndani ya jumuiya hiyo.

Anaongeza kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Uongozi wake, Jumuiya hiyo imeweza kutekeleza miradi na programu mbalimbali kupitia Mpango kazi wa miaka mitano wa Jumuiya hiyo (2015-2020) ikiwemo kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana ambalo limekuwa likiongezeka siku hadi siku.

Aidha aliongeza kuwa ili kufikia Malengo mapana ya Jumuiya hiyo, Nchi wanachama hazina budi kuweka mkazo katika  kujenga ushirikiano baina ya sekta binafsi na ile ya umma kwa kutekeleza miradi na programu mbalimbali pamoja na usimamizi wa rasilimali muhimu zilizopo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo nishati, madini na viwanda.

Awali Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stegomena Tax aliisifu Tanzania kutokana na kiwango kizuri cha ukuaji wa uchumi wake uliofikia asilimia 7.0 na kuwa Nchi ya mfano katika Jumuiya hiyo, hatua iliyotokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha Dkt. Tax pia aliusifu utekelezaji wa  mradi wa kufua umeme wa maji wa Nyerere katika Maporomoko ya Mto Rufiji kwa kuwa ni miongoni mwa miradi ya kimkakati ambayo inatarajia kumaliza changamoto ya ukosefu wa nishati ya uhakika katika Nchi za SADC.

MWISHO


Share:

Soko La DSE Laendelea Kushika Nafasi Ya Tatu Barani Afrika Kwa Ubora

Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Soko la Hisa la Dar es Salaam- DSE limetakiwa kuendelea kujiimarisha kwa kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuwekeza zaidi katika soko hilo lengo likiwa kukuza kipato chao na uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Soko hilo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt. Kazungu alisema kuwa, idadi ya watu takribani laki tano ambao wamewekeza katika Soko hilo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 50, hivyo ni vema DSE ikatumia majukwaa mbalimbali kuhamasisha wananchi kushiriki katika Soko hilo ili kukuza kipato chao kutokana na faida zake.

Alisema ushiriki wa watu wengi katika Soko hilo hususani walio katika sekta ya uvuvi, mifugo na kilimo, kutaongeza chachu ya maendeleo yao na Taifa kwa ujumla hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati uliojikita katika viwanda.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE, Bw. Moremi Marwa, amesema kuwa Soko la DSE lipo kwa ajili ya kuwezesha wawekezaji kuwekeza katika maeneneo mbalimbali kulingana na bidhaa zilizopo sokoni.

Alisema ili kuleta bidhaa zaidi katika Soko la Mitaji, DSE imekuwa ikifanya juhudi kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuziwezesha Serikali za Mitaa na Halmashauri za Miji na Majiji kuweza kupata fedha kupitia mifumo ya Masoko ya Mitaji ili kuweza kuwekeza katika miradi ya Maendeleo ya Uchumi na Kijamii.

Alieleza kuwa mifumo ya masoko ya Mitaji katika Halmashauri inataleta wigo mwingine wa upatikaji wa fedha kwa ajili ya kujenga miradi ya miundombinu na viwanda katika miji na majiji nchini.

Bw. Marwa alibainisha kuwa DSE huwapa wajasiriamali, wafanyabiashara, wawekezaji pamoja na Serikali kutumia soko kwa ajili ya masuala ya upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu na wa kati katika kusaidia wafanyabiashara kuboresha biashara zao pia kwa Serikali Kuu kuendesha miradi mbalimbali ya Serikali hasa iliyo katika Bajeti.

“Soko la DSE limekua kutoka Sh. trilioni 16 hadi trilioni 20 katika kipindi cha miaka minne,  hati fungani Sh. trilioni 3.5 hadi trilioni 9.5. na kwa wawekezaji kutoka  220,000 na sasa 550,000; ukwasi na miamala sokoni imeongezeka kutoka wastani wa  takribani Shilingi bilioni 50 kwa mwaka hadi zaidi Shilingi bilioni 500  kwa mwaka na katika miamala na ukwasi wa hati fungani kutoka wastani wa Shilingi bilioni 300 hadi kufikia wastani wa takribani Shilingi bilioni 900 kwa mwaka”, alieleza Bw. Marwa

Bw. Marwa alisema kuwa kumekuwa na maendeleo mazuri katika vigezo hivyo ambavyo hutumika katika kupima maendeleo ya Soko, pia DSE imeongeza tija na ufanisi kwa kuwa kampuni inayojiendesha kwa faida na kulipa faida hiyo kama gawio kwa wanahisa wake, ikiwemo Serikali.

Alisema kuwa DSE ilipata uanachama wa kidumu katika Chombo cha Kimataifa kinachosimamia masoko ya Hisa (World Federation of Exchanges) mwanzoni mwa mwaka huu, ikiwa ni soko la saba kufikia hatua hiyo barani Afrika.

Afisa huyo Mtendaji Mkuu wa DSE alisema Soko hilo limewekwa kwenye uangalizi “Watch-List” na Shirika la Kimataifa la Kupima viwango na ubora vya Uchumi na Masoko ya Mitaji “Country and Market Classification” kwa nia ya kuifanya DSE kuwa “Frontier Market Status” ifikapo Septemba Mwaka huu.

Hatua hiyo inatoa fursa ya kulitangaza zaidi soko kwa wawekezaji wa nje lakini pia kupata mitaji kutoka kwa wawekezaji wanaotoka nje wanaokuja kuwekeza katika kampuni na biashara nchini na kwenye miradi mbalimbali.



Soko la DSE limekuwa la tatu katika masoko 30 yaliyopo barani Afrika kufikia hatua hiyo, masoko mengine ni Soko la Hisa ni Johannesburg la Afrika Kusini ambalo lina miaka zaidi ya 100, na pia Soko la Hisa la Nairobi (Nairobi Securities Exchange) ambalo lina miaka takribani 70 tangu uanzishwaji wake, lakini DSE likiwa na miaka 20 tu na  linafanya vizuri katika medani za kimataifa.

Alisema kuwa DSE ina bidhaa kuu tatu zilizopo Sokoni ambazo mwananchi yeyote anaweza kuwekeza, bidhaa hizo ni Hisa, ambapo kuna Kampuni 28 zilizoorodheshwa Sokoni zenye ukubwa wa thamani ya takribani Shilingi bilioni 19.2. Bidhaa nyingine ni Hati Fungani za Serikali zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 9.5 na pia Hati fungani za makampuni binafsi zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 250.

Mwisho


Share:

Breaking : LORI LA MAFUTA LAANGUKA ISAKA - KAHAMA


lori la Mafuta Kampuni ya Interpetrol likitokea Jijini Dar  es salaam kuelekea Burundi limeanguka katika Mji Mdogo wa Isaka wilayani Kahama Mkoani Shinyanga  leo Jumamosi Agosti 17,2019 majira ya saa nane na nusu mchana.



Lori hilo limesababisha mafuta aina ya diesel kumwagika ambapo tayari vyombo vya Ulinzi na usalama vya Wilaya ya Kahama vikiongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Anamringi Macha vimewasili eneo la tukio.
Share:

Nafasi za kazi Mzumbe University August 2019

Nafasi za kazi Mzumbe University. Mzumbe Jobs. Find a latest Lecturers Jobs in Mzumbe University. Nafasi za kazi chuo kikuu cha mzumbe: ajira mpya Mzumbe University. MZUMBE UNIVERSITY (CHUO KIKUU MZUMBE)  VACANCIES The Mzumbe University invites applications from suitably qualified and competent Tanzanians to fill the following vacant posts: ASSISTANT LECTURER – (5 Posts) (a) Qualification and Experience… Read More »

The post Nafasi za kazi Mzumbe University August 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MANYANYA AWAONYA WANAOENEZA PROPAGANDA CHAFU NA KUKIMBIZA WAWEKEZAJI TANZANIA


Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog
Serikali imesema haikuwafumbia macho watanzania watakaojaribu kuikashfu nchi kwa maneno ya propaganda zinazosababisha kuwakatisha tamaa wawekezaji kutoka nje na ndani ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 16 2019, na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Eng.Stella Manyanya akiwa mkoani Kagera katika hitimisho la wiki ya Uwekezaji Kagera iliyofanyika katika uwanja wa Gyamkana uliopo Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.


Manyanya alisema kuna baadhi ya watu wenye tabia ya kutoa maneno ya propaganda ya kuikashfu nchi ya Tanzania jambo linalokatisha tamaa wawekezaji mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuwekeza hapa nchini.

"Hatutokuwa tayari kuwakumbatia wanaokwamisha maendeleo, propaganda na maneno havina nafasi, serikali imejipanga kikamilifu na hatutamuonea huruma mtu yeyote anayetaka kujaribu kuichafua nchi hii iliyojawa amani na upendo",alisema.

"Watanzania tuache kuiuza nchi yetu kwa maneno ya Propaganda. Huu sio muda wa maneno maneno badala yake watu wajitathmini na kuona ni wapi wamefanikiwa na ni wapi wanakwama kibiashara kwa kukaa kwa pamoja na kujadiliana na kuinua uchumi wa mkoa wa Kagera na taifa kwa ujumla",aliongeza Manyanya.

Aliwataka wafanya biashara kuzingatia bidhaa bora huku akimpongeza Rais Magufuli kwa kuondoa utitiri wa kodi zilizokuwa zikikwamisha biashara nchini.

Aidha aliahidi ushirikiano na wana Kagera katika suala la kibiashara na kumpongeza mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti katika kubuni wiki ya uwekezaji Kagera kwani hadi sasa Kagera imenoga kwa kuwa na fursa nyingi za uwekezaji.





Share:

Maombi ya kujiunga na veta 2019- VETA Call for application 2019

VETA CALL FOR APPLICATION: FURSA ZA KUJIUNGA NA MAFUNZO KATIKA VYUO VIPYA VYA VETA 2019, veta certificate, veta long courses,TANGAZO NAFASI ZA KUJIUNGA NA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI KATIKA VYUO VYA VETA 2019, veta application form, veta courses 2019,  veta courses 2019, , fomu za kujiunga na veta 2019, sifa za kujiunga na veta 2019, sifa… Read More »

The post Maombi ya kujiunga na veta 2019- VETA Call for application 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

SERIKALI YAPONGEZWA KUTIMIZA AHADI YA UMEME BUSINDE - KIGOMA

Na Rhoda Ezekiel -Malunde1 blog Kigoma
Wananchi wa kata ya Businde Manispaa ya Kigoma Ujiji,mkoani Kigoma wameishukuru serikali kwa kuwatatulia kero ya muda mrefu ya umeme na kuomba shirika la umeme kuongeza nguzo ili waweze wananchi wote wanaohitaji huduma hiyo nao wapate umeme.

Wakizungumza jana wakati wa zoezi la ufunguzi wa Umeme wa REA  katika kata hiyo uliyozinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga, Mwenyekiti wa mtaa wa Businde Husein Yaga alisema kwa muda mrefu wananchi walingoja kufikishiwa huduma hiyo na sasa serikali imetimiza ahadi yake ya kuwapatia umeme. 

Hata hivyo alisema  eneo lililopata umeme ni dogo,   hivyo kuliomba  Shirika la umeme kuongeza maeneo ya kuunganisha umeme ili wananchi wote wapate kuunganishiwa umeme  hasa katika maeneo ya taasisi za dini na sokoni.

Naye Diwani wa kata ya Businde Masoud Masoud aliomba  Shirika la Umeme (TANESCO) kuwaongezea nguzo 76 ili waweze kuunganisha umeme kwa asilima 80% katika eneo hilo kwani wananchi wengi wanahitaji wa umeme.

Meneja  wa TANESCO Mkoa wa Kigoma  Masangija Lugata, aliwataka wananchi ambao nyumba zao sio kubwa kutumia kifaa cha Umeta  ambacho gharama yake ni shilingi elfu 27 pamoja na elfu 32 ya vifaa vingine ili kuepuka gharama na usumbufu wa wakandarasi katika uvutaji wa umeme.

Alisema Serikali ilitoa maelekezo Businde ipatewe umeme, kiasi cha shilingi  Milioni  122  zilitolewa kwaajili ya kukamilisha zoezi la umeme wa  kilovoti 21 na kuunganishia  wateja waawali 156  ambao wamefungiwa umeme katika kata ya Businde. 

Alisema baadhi  ya wananchi wamefanyiwa mchakato wa kupatiwa umeme na utaratibu wa kuunganisha umeme unaendelea.

Mkuu wa wilaya ya Kigoma Samson Anga, alisema aliahidi kutatua kero ya umeme katika kata hiyo na alizingumza na viongozi wanaohusika na kero hiyo na tayari imetatuliwa, hivyo Tanesco wanatakiwa kuongeza nguzo ili wananchi wote waweze kunufaika na huduma hiyo.

Alisema kitu kikubwa kinachochochea maendeleo ni umeme hivyo ana uhakika baada ya wananchi kupata umeme huo, wataanzisha shughuli mbalimbali ili waweze kujikwamua na umaskini.

Aidha kuhusu changamoto ya maji ambayo ni kero nyingine, aliahidi serikali itatauta kero hiyo kabla ya mwezi wa kumi na moja maji yataaanza kutoka katika kata ya Businde na kuepukana na changamoto ya ukosefu wa maji.
Meneja wa TANESCO Kigoma Masangija Lugata akionyesha Wananchi kifaa cha Umeta kinachotumia gharama kidogo katika kuunganisha umeme.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Samson Anga  akiwa na Meneja wa TANESCO Kigoma Masangija Lugata  na Diwani wa Kata ya Businde  wakati wa uzinduzi wa Umeme Businde
Share:

PICHA: Marais 12 kati ya 16 Wahudhuri Mkutano wa SADC Tanzania

Marais wa nchi 12 wamehudhuria mkutano wa kilele wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) unaofanyika jijini Dar es Salaam leo Jumamosi Agosti 17, 2019 na kesho.

Mkutano huo umeanza saa 3:49 asubuhi na kuhudhuriwa na marais na mawaziri kutoka nchi wanachama, marais wastaafu, viongozi na washiriki mbalimbali.

Marais hao ni John Magufuli (Tanzania),  Cyril Ramaphosa (Afrika Kusini), Azali Assoumani (Comoro),  Danny Faure (Shelisheli),  Joao Manuel Goncalves (Angola).

Wengine ni Edgar Lungu (Zambia), Felix Tshisekedi (DRC),  Andry Rajoelina (Madagascar), Emerson Mnangagwa (Zimbabwe), Filipe Nyusi (Msumbiji) na Dk Hage Geingob (Namibia).

Nchi  ya Eswatin imewakilishwa na waziri mkuu,  Ambrose Dlamini;  Lesotho pia imewakilishwa na waziri mkuu, Motsahai Thabane  huku Malawi ikiwakilishwa na makamu wa rais sambamba na Botswana na Mauritius zilizotuma wawakilishi.


Share:

Tanzania Yamwagiwa SIFA Kwa Kuwa Nchi Pekee ya SADC Ambayo Uchumi Wake Unakua Kwa Asilimia 7

Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya SADC  Dr. Stergomena Lawrence Tax ameipongeza Tanzania kuwa nchi pekee ambayo imeongoza kwa kukidhi vigezo vya ukuaji wa uchumi, kwa kufikia asilimia 7, ikiwa ni tofauti na nchi nyingine.

Kauli hiyo ametoa wakati wa mkutano wa kwanza wa SADC uliofanyika jijini Dar es salaam, ambapo viongozi mbalimbali wa jumuiya hiyo wakiwemo viongozi wastaafu na Mawaziri wamehudhuria.

Dk.Tax amesema kwa nchi za jumuiya hiyo pamoja na mambo mengine kwenye eneo la uchumi kuna malengo ambayo yamewekwa kwa nchi wanachama na Tanzania ni nchi pekee ambayo uchumi wake unakuwa kwa asilimia saba na hivyo wanastahili kupongezwa.

 "Uhimilivu wa uchumi ni nyenzo muhimu katika maendeleo, nchi wanachama zimekidhi vigezo vya SADC kiuchumi, takwimu zimeonesha Tanzania inafanya vizuri, na kwa vigezo pekee Tanzania ndiyo nchi pekee ambayo imefikia ukuaji wa asilimia 7, mjipongeze." Amesema Dr Tax na kuongeza;
 

"Katika kufikia uchumi wa Viwanda nchi wanachama hawana budi kukuza uzalishaji wa umeme, kwa kuwa ni kitu muhimu kwenye ujenzi wa viwanda, nashukuru katika wiki ya Viwanda  hata Tanzania ,  tumeona mradi mkubwa wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji ambao ujenzi wake unaendelea"


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger