Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Saturday 27 April 2024

Video Mpya : KISIMA - SUZANA

 

Share:

KATAMBI AKABIDHI AMBULANCE NYINGINE KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA MANISPAA YA SHINYANGA

Na Kadama Malunde & Marco Maduhu - Shinyanga

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu amekabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  ambalo litatumika kutoa huduma Kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga.


Katambi amekabidhi Ambulance hiyo leo Jumamosi Aprili 27,2024 katika Stendi ya Magari Soko Kuu Manispaa ya Shinyanga  na kushuhudiwa na wananchi,viongozi wa Serikali pamoja na Chama Cha Mapinduzi.

Amesema hiyo ni Ambulance ya pili ambayo ameitoa katika ahadi zake, ambapo ya kwanza aliitoa February 8 Mwaka huu na leo pia amekabidhi Ambulance nyingine ili kuendelea kuboresha huduma za Afya.

"Nimekuja kwa awamu nyingine kukabidhi gari hili ‘Ambulance’ niliyopewa na Mama, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ili lisaidie kuboresha huduma za afya katika Manispaa ya Shinyanga. Mimi nikiahidi natekeleza, Ambulance ambayo naikabidhi leo itatumika kutoa huduma Kituo cha Afya Kambarage na ile ilikuwa ya Kambarage kwa sababu ni ndogo itakwenda Ihapa,"amesema Katambi.

Katambi amemshukuru  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi na kuboresha huduma za afya kwa wananchi pamoja na kutoa ajira za afya pamoja na upatikanaji wa vifaa tiba.

Katika hatua nyingine amemshukuru Rais Samia, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa miongozo yao na kumwezesha kufanya kazi za Serikali pamoja na kuhudumia wananchi wa Jimbo lake.

Kwa upande, Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga (DMO) Dkt. Elisha Robert, ameshukuru kupata Ambulance hiyo na kwamba sasa zimefika nne katika Manispaa hiyo ambazo zitasaidia kubeba wagonjwa na kuwawahisha kupata huduma za matibabu.

Amesema ndani ya miaka mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Manispaa ya Shinyanga zimeshajengwa zahanati mpya sita na zingine mbili zinaendelea kukamilishwa ikiwamo ya Mwamagunguli pamoja na kutoa ajira 93 za watumishi wa afya.

Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Zamda Shaban, amemshukuru Mbunge Katambi kwa kuendelea kupambania Wananchi katika suala zima la Maendeleo na sasa ameendelea kutekeleza Ahadi yake ya kuleta magari ya wagonjwa.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anord Makombe, ametoa wito kwamba Magari hayo ya Wagonjwa ambayo yamekabidhiwa na Mbunge kwamba wayatunze pamoja na Madereva kuyaendesha vizuri na kutosababisha ajali.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga leo Jumamosi Aprili 27,2024 - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akikata utepe wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akikata utepe wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akikata utepe wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu (kushoto) akikata utepe wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akiendesha gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’ katika Manispaa ya Shinyanga
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga (DMO) Dkt. Elisha Robert akionesha vifaa vilivyomo ndani ya gari jipya la wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga (DMO) Dkt. Elisha Robert akionesha vifaa vilivyomo ndani ya gari jipya la wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  lililokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu  kwa ajili ya kutoa huduma za afya Manispaa ya Shinyanga
Gari maalumu la kubebea wagonjwa lililokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu  kwa ajili ya kutoa huduma za afya Manispaa ya Shinyanga
Gari maalumu la kubebea wagonjwa lililokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu  kwa ajili ya kutoa huduma za afya Manispaa ya Shinyanga
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga (DMO) Dkt. Elisha Robert na watumishi wa afya wakionesha furaha baada ya kukabidhiwa gari jipya la wagonjwa 
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu akizungumza wakati akikabidhi gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anord Makombe akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Shinyanga (DMO) Dkt. Elisha Robert akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Zamda Shaban akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Naibu Katalambula akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa ‘ Ambulance’  katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga

Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga
Viongozi na wananchi wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya gari maalumu la kubebea wagonjwa katika Manispaa ya Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Friday 26 April 2024

WAKULIMA VIJANA WAELEZA FAIDA ZA MATUMIZI YA MBEGU BORA

 
Mkulima kijana kutoka jijini Arusha anayefahamika kwa jina la Edward Jacob anayejihusisha na kilimo cha Mbogamboga na Matunda ameeleza faida za matumizi ya Mbegu bora na matarajio yake kuelekea Bajeti ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 itakayosomwa Bungeni jijini Dodoma mnamo Mei 02 na Mei 03, 2024.

Miongoni mwa faida nyingi alizoeleza ni pamoja na kupata mazao yenye ubora, yasiyoharibiwa kirahisi na wadudu pamoja na kupata mavuno ndani ya muda mfupi.


Sambamba na faida hizo Edward pia ameeleza matarajio yake kwa Bajeti ya kilimo kwa Mwaka 2024/2025 kuwa ni kuendelea kupata mbegu hizo zinazozalishwa na taasisi zinazotambulika nchini pamoja na kupata pembejeo kwa urahisi zaidi ili kuendelea kupata mazao bora.


Kwa upande wake, Agnes Sachi ambaye pia ni kijana anayejihusisha na Kilimo cha Mbogamboga jijini Arusha ameeleza namna kulima kwa kutumia mbegu na miche bora kulivyomnufaisha na matarajio yake kuelekea bajeti ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2024/2025.

Share:

Video Mpya : NELEMI MBASANDO - MAFURIKO

 

Share:

VIJANA 58 WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UTENGENEZAJI VIHENGE KUPITIA MRADI WA TANIPAC KUZUIA SUMUKUVU


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jumla ya Vijana 58 kutoka mikoa ya Tabora, Mwanza, Geita na Simiyu wamehitimu mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.


Akizungumza leo Ijumaa Aprili 26,2024 wakati wa kufunga Mafunzo ya kutengeneza Vihenge awamu ya tatu, Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban amesema mafunzo hayo yamehitimishwa rasmi baada ya kutolewa katika awamu tatu yakinufaisha vijana 58.

“Mafunzo ya kutengeneza vihenge yalianza tarehe 26,2024 kwa awamu ya kwanza ambapo washiriki walikuwa 19, ikafuatia awamu ya pili ikiwa na washiriki 23 na leo washiriki 16 wamehitimu. Wamefundishwa masuala ya ujasiriamali, utengenezaji wa vihenge kwa nadharia na vitendo, nadharia ya masoko, usimamizi wa fedha na urasimishaji wa biashara”,amesema Taban ambaye ni Afisa Uendelezaji Biashara SIDO Mkoa wa Shinyanga.


“Serikali kupitia mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii. Mradi wa TANIPAC unalenga kuwezesha jamii kutumia njia sahihi na za kisasa za uhifadhi wa nafaka hususani mahindi kutokana na sumukuvu”,ameongeza Taban.

Amefafanua kuwa, Serikali imeingia gharama kuhakikisha kuwa vijana wanapatiwa ujuzi wa kutengeneza vifaa vya kisasa na vinavyodumu kwa muda mrefu (vihenge) ili kutimiza adhima ya kupunguza sumukuvu.

Taban amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuhakikisha wanayatumia kwa vitendo kuhakikisha kuwa lengo la mafunzo linatimia ambapo pia yatawezesha kuongeza kipato cha mmoja mmoja, kaya na taifa kwa ujumla.

“Mafunzo haya yametolewa kwa vijana wachache lakini wengi wangependa kupata mafunzo haya,hivyo nitumie nafasi hii kuwaomba mkawe waalimu wa kufundisha vijana wenzenu kwenye maeneo yenu ya kazi ili kwa pamoja tuweze kupambana kwa vitendo kupunguza kama siyo kuondoa kabisa sumukuvu”,amesema Taban.

Akisoma risala kwa niaba ya Washiriki wenzake wa mafunzo, Wanjala Daudi amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji kazi na kuzalisha bidhaa za vihenge (Silos) na nyinginezo kwa tija ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

“Tunaushukuru uongozi wa SIDO na Wizara ya Kilimo kwa kutoa fursa ya mafunzo haya. Hakika mafunzo haya yametujengea uwezo wa kujiamini na kuamsha ari ndani yetu ya kujiajiri na kuachana na kasumba ya kusubiri ajira”,amesema Daudi.

“Pamoja na ari na motisha ya kujiajiri iliyojengeka ndani yetu, tunakabiliwa na changamoto ya mitaji kwa ajili ya kununua vifaa/vitendea kazi vya kuanzisha shughuli mbalimbali kutokana na fani tulizojifunza”,ameongeza Daudi.

Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa vijana wakati akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa ‘Tanzania Initiative For Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo - Picha na Kadama Malunde 1 blog
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kushoto) akikagua Vihenge vilivyotengenezwa na Vijana walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (wa nne mbele kushoto) , viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (wa nne mbele kushoto) , viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo wenye lengo la kuimarisha usalama wa chakula kwa wananchi na kuimarisha afya ya jamii.
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban akizungumza wakati wa akifunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu (TANIPAC) ulio chini ya Wizara ya Kilimo


Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mratibu wa Mafunzo ya Kutengeneza Vihenge Mkoa wa Shinyanga, Misuka Makwaya ambaye ni Mhasibu wa SIDO Mkoa wa Shinyanga akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Wanjala Daudi akisoma risala ya washiriki wa mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Afisa Mipango SIDO Shinyanga , Frank Nguyu akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mwenyekiti wa Mafunzo, Charles Kulwa akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge
Mratibu wa Mafunzo SIDO Mkoa wa Shinyanga, Mhandisi Manyama Lububi akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya kutengeneza Vihenge


Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban (kulia), akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge 
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo
Kaimu Meneja wa SIDO Mkoa wa Shinyanga bw. Joseph Taban, viongozi wa SIDO Shinyanga wakipiga picha ya kumbukumbu walioshiriki mafunzo ya kutengeneza Vihenge yaliyotolewa na SIDO Mkoa wa Shinyanga kupitia Mradi wa Kuzuia Sumukuvu wa TANIPAC ulio chini ya Wizara ya Kilimo

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger