Wednesday 19 October 2016

MH.ANTONY MTAKA ATEKELEZA AHADI YA MH.MAGUFULI YA VIWANDA KWA VITENDO MKOANI SIMIYU

...



File Photo
Baada ya Mkoa wa Simiyu kukamilisha uanzishwaji wa viwanda vidogovidogo kwenye wilaya za Meatu na Maswa, hivi sasa umeanza kazi hiyo  kwa Itilima, Bariadi na Busega ili kwenda sambamba na uamuzi wa Rais John Magufuli.
Wilaya ya Meatu imeanzisha Kiwanda cha Kusindika Maziwa, huku Maswa ikianzisha Kiwanda cha Uzalishaji Chaki vyote vikishirikisha makundi ya vijana.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,  Anthony Mtaka alisema Bariadi inatarajiwa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza sabuni; Busega kitajengwa kiwanda cha maji wakati mipango zaidi ikiendelea kuangalia kiwanda kinachofaa  wilayani Itilima.
Mtaka alisema katika kutekeleza azma ya Tanzania ya viwanda, mkoa umekuwa ukifanya jitihada za kuwaunganisha vijana kwa kuwajengea uwezo wa kujitegemea.
“Ni fedheha kuona hata bandeji za hospitalini zinatoka nje huku malighafi zake inapatikana nchini. Ni vyema kuzitumia fursa zilizopo  na mikakati ya kuanzisha kiwanda cha bandeji na maji,” alisema Mtaka.
Katika kutekeleza kaulimbiu ya mkoa huo ya ‘One district one product’, wanatarajia kuwashirikisha vijana na kuwajengea uwezo ili wafanye kazi za kujiletea maendeleo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Jenista Mhagama alisema wizara yake itaendelea kuwaunga mkono vijana wanaothubutu kwa kuwapa mikopo ili waazishe miradi.
Mhagama alisema vijana wa Simiyu wameonyesha njia kwa wenzao nchini na kuwaahidi  kuwapa mkopo wa Sh30 kwa kuanzisha kiwanda cha chaki na maziwa.
Aliwataka vijana kuchangamkia fursa badala ya kukaa vijiweni na kulalamika kuwa hawana kazi.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger