Sunday 14 July 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 14,2024





















 

Share:

Saturday 13 July 2024

KATAMBI AZINDUA UMOJA WA WAZEE WASTAAFU TARAFA YA OLDSHINYANGA,ALIA NA MMOMONYOKO WA MAADILI

 

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Patrobas Katambi ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu amekutana na kufanya mazungumzo na Wazee kupitia Baraza la Ushauri la Ushauri la Wazee Manispaa ya Shinyanga na 

amezindua umoja wa wazee wastaafu tarafa ya Oldshinyanga,huku akiwaomba wazee kusimamia suala la Mmomonyoko wa maadili.

Uzinduzi huo umefanyika leo Julai 12,2024 katika ya Oldshinyanga.

Katambi akizungumza wakati wa kuzindua umoja huo wa wazee wastaafu, amesema wazee hao wamefanya jambo jema la kizalendo kwa kuanzisha umoja wao ambao utasaidia kutoa ushauri kwa viongozi mbalimbali wakiwamo watumishi wa Serikali pamoja na kuzuia Mmomonyoko wa maadili.

Amesema wazee ni tunu ya taifa,hivyo wanategemewa katika mambo mbalimbali ya ushauri na ndiyo maana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anawathamini na hata kuweka mambo sawa katika masuala ya pensheni.
"Umoja huu wa wazee ambao nimeuzindua leo tunautengemea sana katika masuala ya ushauri,watu kuwa wazalendo na kupenda uraifa wao pamoja na kuzuia tatizo la Mmomonyoko wa maadili," amesema Katambi.

"Tatizo hili la mmonyoko wa maadili ni tishio kwa usalama wa nchi, sababu hata baadhi ya viongozi wa Serikali limewakumba na hata kutumia madaraka vibaya na kufanya ufujaji wa mali za umma na kunyanyasa wananchi,"ameongeza.
Aidha,amewaomba wazee kuchukua hatua za makusudi juu ya kudhibiti tatizo la Mmomonyoko wa maadili sababu kuna uwezekano taifa kuja kukosa viongozi imara kutokana na sasa wanaume kwa wanaume wanaoana na hata wanawake hivyo hivyo.

Naye Katibu wa umoja wa wazee wastaafu tarafa ya Oldshinyanga Stephano Tano,akisoma risala amesema wameanzisha umoja huo katika kusaidiana masuala mbalimbali yakiwamo ya shida na raha na kujikwamua kiuchumi.
Amesema kutokana na ongezeko la wazee wastaafu tarafa ya Oldshinyanga ndipo wakona waanzishe umoja wao mwezi juni mwaka huu na sasa wapo wazee 100.

"Umoja wetu ambao unazinduliwa leo una shabaha ya kuwaunganisha wastaafu wote,kusaidiana katika shida na raha,kujikwamua kiuchumi pamoja na kusimamia maadili mema kwa jamii,"amesema Tano.
Amesema pia wazee hao wanampongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kazi zake na uongozo wenye dira nzuri kwa taifa.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Share:

KATAMBI AENDELEA NA ZIARA KUELEZEA MIRADI YA MAENDELEO ALIYOITEKELEZA KWA WANANCHI

 





Na Marco Maduhu,SHINYANGA

MBUNGE wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi,ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu kazi,vijana,ajira na watu wenye ulemavu,ameeleza kutekeleza miradi mingi ya maendeleo kwa wananchi jimboni kwake.

Amebainisha hayo leo Julai 12,2024 kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Kata Nne, ambazo ni Mwawaza, Masekelo,Ndala pamoja na Kambarage.
Amesema mwaka 2020 kwenye uchaguzi mkuu,wananchi walimpatia ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini ili akawatumikie na kuwaletea maendeleo,na hadi sasa ametekeleza ahadi zake kwa asilimia 99.5,huku akimshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan,kwa kumpatia fedha na kutekeleza miradi mingi kwa wananchi.

"Mwaka 2020 kwenye uchaguzi mkuu wananchi mlinipatia ridhaa ya kuwa Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini, na kazi yangu ni moja tu kuwatumikia na kuwaletea maendeleo," amesema Katambi.
"Maendeleo yetu ni faida yetu, ili tupate maendeleo lazima tuwe wa moja,na nimetekeleza ilani ya CCM kwa asilimia 99.5"ameongeza Katambi.

Nao viongozi mbalimbali wa CCM wilaya ya Shinyanga mjini wakiongozwa na Mwenyekiti Anorld Makombe, wamempongeza Mbunge Katambi kwa kazi kubwa ambayo anaifanya ya kuwaletea maendeleo wananchi na kuitendea haki ilani ya uchaguzi ya CCM.
Nao Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga,kwa nyakati tofauti wakizungumza kwenye mkutano huo wakiongozwa na Meya Elias Masumbuko,wamesema miradi mingi ya maendeleo imetekelezwa kwa wananchi, kwa kushirikiana na Mbunge chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Wametaja miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa ikiwamo sekta ya elimu,afya,kilimo,mifugo,maji, nishati,miundombinu ya barabara,ujenzi wa uwanja wa ndege,masoko,stendi ya mabasi na jengo la utawala manispaa ya Shinyanga.
Naye Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko,amempongeza Katambi kwa uboreshaji wa miundombinu mbalimbali ikiwamo ya ujenzi wa masoko,na hata kusababisha ukusanyaji mapato kuongezeka kutoka bilioni 2 hadi bilioni 6.
TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi, ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, kazi,vijana,ajira na watu wenye ulemavu akizungumza kwenye Mkutano huo.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anorld Makombe akizungumza kwenye mkutano huo.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza kwenye mkutano huo
Katibu wa siasa na uenezi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Said Bwanga akizungumza kwenye mkutano huo.


Share:

WATAALAM 30 WA TEHAMA WALIOFADHILIWA NA MRADI WA KIDIGITALI WATUNUKIWA VYETI




Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Serikali imewataka Wanufaika wa ufadhili wa Mafunzo ya muda mrefu awamu ya pili kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali wanaokwenda kusoma Ughaibuni kuwa mabalozi kwa Watumishi wengine ili kuleta tija katika kuongeza ubunifu,kueleimisha na kusukuma gurudumu la mabadiliko ya Kidijitali nchini.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla ameeleza hayo Julai 12,2024 Jijini Dodoma katika hafla ya kutoa vyeti na kutia saini Mkataba wa kutumikia Serikali baada ya kumaliza Masomo kwa Watalaam wa Tehama waliopata ufadhili kupitia kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali.

Amesema kuwa wao kama Wizara tayari wamekamilisha masuala ya maboresho kwa kuendelea kufanyia baadhi ya mifumo ikiwa ni pamoja na kukamilisha mkakati wa miaka 10 wa uchumi wa Kidijitali unaolenga ujuzi wa jamii ya Kidijitali.
"Ujuzi mtakaopata utusaidia taaluma yenu na kuwasaidia Watumishi wenzenu kubuni,kuelimisha na kusukuma gurudumu la mabadiliko ya Kidijitali,sisi kama Wizara tumekamilisha baadhi ya masuala mbalimbali tunaendelea kuyafanya, " amesema

Mbali na hayo ameeleza kuwa kama Wizara wamekamilisha mkakati wa miaka 10 wa uchumi wa Kidijitali, unaolenga ujuzi wa jamii ya Kidijitali ambayo ni kuwa na jamii inayojua Teknolojia katika biashara na mambo mengine ya biashara mtandao.

Kutokana na hayo Salvatory Mbilinyi ambaye ni Mkurugenzi Diaspora kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ameewaasa wanufaika hao kutokubeza tamaduni za watu pale watakapokwenda masomoni hasa tamaduni za mavazi japo inategema na nchini husika,ili kutojiingiza katika malumbano yasiyo ya lazima.

"Sisi Watanzania tuna tamaduni tofauti na wenzetu msiende kubeza tamaduni za watu,mfano katika mavazi maana unaweza kukutana na mtu kavaa ambavyo huwezi kuelewa usioneshe kuchukizwa na Utamaduni wake,we muangalie kama alivyo kwasababu anaweza kuchukia pia,lakini hiyo inategemea umeenda nchi gani".
Naye Mwakilishi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Raisi Menejimenti ya Utumishi na utawala bora Ibrahim Mahumi amewataka wakafuate Sheria,Taratibu na Kanuni na kuongeza kuwa ni mategemeo ya Ofisi ya Raisi na Utumishi na Serikali kwa ujumla kuwa wanufaika hao watakapo kwenda masomoni watafanya kile ambacho kinakusudiwa kufanyika na sio Mambo mengine.

Akitoa Shukurani kwa niaba ya wanufaika wote Mhandisi Mwandamizi kutoka mfuko wa mawasiliano kwa wote Brian Kasuma amesema kuwa watatumia fursa hii adhimu kwa kujibiidisha katika masomo ili kuweza kuchangia katika maendeleo ya nchi na hasa katika uchumi wa Kidijitali na kuahidi kuwa mabalozi wa kuitangaza Tanna vivutuo vyake.

"Tunaahidi kutumikia vyema fursa hii adhimu kwa kujibidiisha katika masomo ili kuweza kuchangia katika maendeleo ya nchi yetu hasa katika uchumi wa Kidijitali. Pia tunaahidi kuwa wazalenndo wa nchi yetu na mabalozi wazuri wa jamii ya nchi yetu kwa kutii sheria na taratibu nchi husika tunazoenda kusoma na kuvitangaza vivutio vyetu vya utalii kila tutakapopata nafasi".

Pamoja na mambo mengine Wanufaika waliosaini Mkataba huo na kupokea vyeti kwa ni 30 ambapo ni awamu ya pili na awamu ya kwanza walikuwa 20 hivyo jumla wamefikia 50 ambapo ndio idadi iliyokuwa ikihitajika.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger