Monday 27 November 2023

TCRA CCC YAKUTANA NA WATOA HUDUMA ZA MAWASILIANO KUBORESHA HUDUMA KWA MTUMIAJI WA MAWASILIANO

...

Katika kutekeleza majukumu yake ya Kisheria Baraza la washauri la watumiaji huduma za mawasiliano (TCRA CCC), 
chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Hawa Ng'humbi
 imefanya mkutano na Umoja wa Watoa Huduma za Mawasiliano (TAMNOA) kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayomhusu mtumiaji wa huduma za mawasiliano ili kuboresha huduma kwa mtumiaji. 

Mkutano huo uliofanyika leo Jumatatu Novemba 27, 2023 pamoja na mambo mengine umeangazia changamoto za watumiaji na namna ambavyo TCRA CCC, Watoa Huduma na wadau wengine wanaweza kuzishughulikia ili kuondoa kero kwa watumiaji.

#HudumaBoraZaMawasilianoNiHakiYako
#TanzaniaYaKidijitali
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger