Tuesday 20 June 2023

KUTANA NA NYANI MDOGO ANAYEISHI KIFAHARI SASA GUMZO MTANDAONI

...

Nyani mdogo na mrembo ambaye anaishi maisha ya kifahari ambayo wengi wangependelea, ndiye anayegonga vichwa vya habari mtandaoni.

Maarufu kama Mojo, mnyama huyo kutoka Marekani anajivunia wafuasi milioni 8.5 ambao huvutiwa na maisha yake ya kifahari.

Kwenye video zake zinazovutia kwenye TikTok, Mojo anaonekana akipata kikao cha kujipamba kwa utulivu, akionyesha nguo nzuri, na akifurahia chakula kizuri pamoja na vitafunio vyake vinavyopendwa kama pilipili tamu.

Wafuasi wake pia wanashiriki katika safari zake za barabarani, wachezaji wenzake ndani na nje ya nyumba, na kuendelea kuuliza kilichotokea tangu video ya mwisho waliyoangalia.

"Kuwa na nyani kama kipenzi ni gharama kubwa sana, anatumia nepi nne kwa siku na pakiti moja inagharimu KSh 6000. Atatumia nepi kwa maisha yake yote," alisema mmiliki wake." "Pia anahitaji unga wa lishe ambao ulikuwa KSh 5000 na tangu azidi kuzihitaji, sasa nampa biskuti za sokwe, matunda, na mboga. Gharama ya haya yote ni KSh 8500 kwa wiki. Pia wanatoka nje na kula nyasi kwa virutubisho vyao," alisema.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger