Monday 1 May 2023

MTOTO ALIYEDAIWA KUFARIKI NA KUZIKWA AKUTWA AKIWA HAI

...

Wakazi wa Kijiji cha Salong’we kilichopo wilayani Magu mkoani Mwanza wamekumbwa na taharuki baada ya mtoto aitwaye Mabilika Wilson aliyefariki na kuzikwa tarehe 17 mwezi huu kupatikana akiwa hai katika Kijiji cha Mwangika wilayani Kwimba mkoani humo.

Wilson Bulabo ni baba mzazi wa mtoto huyo amesema ni kweli mtoto wake huyo aliumwa kwa siku mbili na kufariki hatimaye wakamzika lakini alipoenda kumuangalia huyo mtoto aliyeonekana Kijiji cha Mwangika alimgundua kuwa ndiye mtoto wake aliyezikwa wiki chache zilizopita.

Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amefika katika Kijiji hicho na kushuhudia kaburi likifukuliwa kwa ajili ya taratibu za uchunguzi wa tukio hilo ambapo amewataka wakazi wa Kijiji hicho na vijiji vya Jirani, kuwa watulivu kipindi ambacho uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

Via EATV
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger