Tuesday 1 June 2021

TAWA YATOA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MAENEO YAKE

Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania -TAWA imetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji wa kitalii ili kuongeza uwezo wa kifedha katika kusimamia maeneo yaliyo chini ya Mamlaka hiyo, ikiwa ni moja ya mkakati wa ukuzaji na uendelezaji wa Mamlaka pamoja na kuongeza pato la Taifa.

Hayo yameelezwa na Kaimu Kamishina wa Uhifadhi wa Wanyamapori nchini Bw. Mabula Misungwi Nyanda wakati akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo amesema moja ya mkakati wa kuboresha uhifadhi na mapato ya serikali ni kutenga maneo ya uwekezaji wa kitalii ambayo yatatoa fursa kwa wawekezaji kuja kuwekeza nchini katika Sekta ya Utalii.

Maeneo hayo ya hifadhi ni pamoja na Mapori ya Akiba Mpanga-Kipengere, Pande, Mkungunero, Kijershi,Swangaswanga na eneo la urithi wa dunia la Kilwa ambalo pia limetenga maeneo maeneo matatu kwa ajili ya uwekezaji ambayo ni Kilwa Kisiwani, Songo Mnara na Sanje Kati.

Aidha kutokana na jitihada zinazofanywa na Mamlaka hiyo katika uhifadhi wa mapori ya akiba zimezidi kuwavutia watalii wengi kuweza kutembelea vivutio vya utalii katika mapori ya akiba,kutoka watalii 35,479 katika kipindi cha mwaka 2015-2016 na kufika watalii 129,428 katika kipindi cha 2018-2019.

Katika hatua nyingine Bwana Misungwi amewataka watanzania kuwekeza katika ufugaji wa wanyamapori kupitia bustani za wanyamapori(wildlife zoos),mashamba (wildlife farms) na ranchi za wanyamapori (wildlife ranches),ambapo mwekezaji anatakiwa kumiliki eneo lake ambalo atafanyia uwekezaji.

Aidha ameongeza kuwa mpaka sasa jumla ya vitalu 28 vimetengwa kwa ajili ya uwekezaji kupitia biashara ya uwindaji wa kitalii,ambapo mwekezaji hupewa kitalu kwa ajili ya kukitumia katika shughuli ya uwindaji kikiwemo kitalu cha Selous GR MT kilichopo hifadhi ya Selous.

Sambamba na hayo Mamlaka imetenga jumla ya maeneo kumi na mbili kwa ajili ya uwekezaji mahiri (Special Wildlife investment concession Areas- SWICA) yakiwemo Grumeti,Ikorongo,Maswa Mbono,Maswa Kimali,Mkungumero,Rungwa Inyonga,Selous LL1, Selous MT2, Selous MHJ1, Selous MHJ2, Selous ML1 na Lake Natron East,ambayo yana jumla ya km2 15,149.
Share:

Breaking : HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, UFUNDI 2021

Share:

Waziri wa Uganda ajeruhiwa na mwanae kufa baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana

Watu wenye silaha wamemshambulia na kumjeruhi Waziri na Kamanda wa zamani wa jeshi la Uganda, na kumuua binti yake na dereva.

Walioshuhudia tukio hilo wanasema washambuliaji ambao hawajafahamika walliokuwa kwenye pikipiki walifyatua risasi kadhaa kwenye gari alimokuwa Jenerali Katumba Wamala.

Shambulio hilo limeonekana kama jaribio la kumuua kamanda huyo wa zamani wa jeshi na Mkuu wa zamani wa polisi ambaye kwa sasa ni Waziri wa Ujenzi na Uchuku na limemewashtua wengi nchini Uganda.

Kuna takriban mashimo saba ya risasi kwenye dirisha la gari la Jenerali Katumba Wamala. Binti yake na dereva wote wameuawa.

Washambuliaji walitoroka kwa pikipiki zao baada ya kutekeleza shambulio hilo.

Picha ya video kutoka kwenye eneo la tukio inamuonesha Jenerali Wamala huku nguo zake zikiwa zimejaa damu –akibebwa kwenye pikipiki na kukimbizwa hospitalini.

Shambulio hili dhidi ya mmoja wa wanasiasa na wanajeshi wanaoheshimika zaidi nchini Uganda pia linawakumbusha wengi mauaji ya watu maarufu waliouawa miaka ya nyuma kwa risasi.

Katika miaka ya hivi karibuni mashambulio sawa na shambulio hili ni pamoja na hakimu, viongozi wa Kiislamu , mshirika maarufu wa kisasa wa Rais Yoweri Museveni na Mkuu wa ngazi ya juu wa polisi.

Wahusika wa mauaji hayo hawajawahi kushitakiwa.

 Source:BBC



Share:

TAMISEMI Form Five Selection 2021 | Waliochaguliwa Kidato Cha Tano 2021

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

How to see TAMISEMI Form Five Selection 2021/2022. You can ask yourself how to check students selected to join form five 2021 (Majina waliochaguliwa kidato cha Tano 2021/2022). The following below are steps to see all names of students with their school and combination he or she will go to study in advanced level:- View […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

VIDEO: Zoezi la Uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano na vyuo vya elimu na mafunzo ya ufundi 2021

p style="text-align: justify;"> VIDEO: Zoezi la Uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha tano na vyuo vya elimu na mafunzo ya ufundi 2021

Share:

PICHA: Ndugai amtimua mbunge aliyevaa suruali ya kubana bungeni

 Spika wa Bunge,  Job Ndugai leo Jumanne Juni Mosi,  2021  amemtoa katika ukumbi wa Bunge  mbunge wa Momba (CCM),  Condester Sichwale kutokana na kuvaa suruali iliyombana.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge,  wabunge wanawake hawaruhusiwi kuvaa suruali za kubana.

Mara baada ya kipindi cha maswali na majibu, alisimama mbunge wa Nyang'wale (CCM),  Hussein Amar na kuomba mwongozo wa Spika.

"Spika nasimama kwa kanuni ya  70 inayohusu mavazi ya staha kwa wabunge, kanuni imeeleza  wazi kuhusu mavazi hayo na kwa akina dada lakini humu ndani kuna wabunge wamevaa nguo ambazo hazina staha," amesema Amar.

Spika Ndugai alimpa nafasi mbunge huyo kumtaja mwenzake  aliyevaa mavazi ambayo hayakuwa na staha ili iwe mfano.

"Mbunge huyo yuko hapo katika mkono wangu wa kulia, amevalia tisheti  lakini naomba umuite mbele uone suruali aliyovaa namna ilivyobana, amevaa miwani," amesema Ameir bila kumtaja jina.

Spika alisimama na kumtaka mbunge aliyevaa mavazi hayo asimame na aondoke ndani ya ukumbi ili akavae mavazi yenye staha ndipo atarejea tena bungeni.

Sichwale alisimama  akabeba mkoba wake na  kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.

Spika Ndugai ameagiza askari wote katika milango ya kuingia bungeni wawe makini wasiruhusu wabunge kuingia wakiwa wamevaa mavazi yaliyokatazwa.



Share:

Rais Samia awasimamisha kazi viongozi soko la Kariakoo


Rais Samia Suluhu Hassan ameusimamisha kwa muda  uongozi wa soko la Kariakoo lililopo jijini Dar es salaam, na kuagiza uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma mbalimbali zinazoukabili uongozi huo.

Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza hatua hiyo wakati wa ziara yake ya kushtukiza katika soko hilo, ambapo pia amesikiliza kero za Wafanyabiashara mbalimbali wa soko hilo.

Amesema hali ya soko hilo la Kariakoo hairidhishi, na kwamba Serikali kwa sasa inaenda kufanya tahmini ya kina kuona namna ya kuliendesha soko hilo.

Rais Samia Suluhu Hassan amesema lengo la kuanzishwa kwa soko hilo ni kuwasadia Wafanyabiashara wadogo, lakini kwa sasa jambo hilo halipo na kinachofanyika ni kuwanufaisha viongozi wa soko hilo pekee.

Ameongeza kuwa mpangilio wa bidhaa ndani ya soko hilo ni mbaya, jambo ambalo linahitaji kufanyiwa marekebisho ya haraka.


Share:

International Individual Consultant – COVAX communication at UNICEF June 2021

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job no: 540837 Contract type: Consultancy Level: Consultancy Location: Tanzania,Uni.Re Categories: Communication for Development (C4D), Consultancy UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged children. To save their lives,To defend their rights and to help them fulfill their potential. Across 190 countries and territories, we work for every child, everywhere, every day, to […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Relationship Manager; Mass Affluent (2 year contract) at NMB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Purpose To create new and manage existing relationships effectively in order to facilitate the growth of Affluent and Mass Affluent Liability and Asset portfolio as well as income within Private Banking. To make effective sales activation – Account opening and enrolment to digital channels to all clients new and existing from Private schemes. Main […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Head of Retail Credit at NBC Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Job Summary To develop tactical strategy and delivery plans, formulate associated practice/s and to ensure operational implementation and adoption i.t.o. credit risk management methodology, practice, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Head, Corporate Affairs, Brand & Marketing at Standard Chartered Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

About Standard Chartered  We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit.  It’s about showing how you embody our valued behaviours – do the right thing, better together and never settle – […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MRADI WA ADGG WAWANUFAISHA WAFUGAJI WA MIKOA 7

 

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Prof. Erick Komba akisikiliza mada iliyokuwa ikiwasilishwa kuhusu mradi wa Uboreshaji na Uendelezaji wa Mbari za Ng'ombe wa Maziwa katika kikao kilichofanyika katika Makao Makuu ya Taasisi hiyo Jijini Dodoma.

Msimamizi Mkuu wa Mradi Uboreshaji na Uendelezaji wa Mbari za Ng'ombe wa Maziwa (ADGG), Dkt. Daniel Komwihangilo akifafanua jambo kuhusu mradi huo katika kikao cha tathmini kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Jijini Dodoma. Kulia ni Mshauri wa Mradi huo, Dkt. Maria Mashingo ambaye pia alishawahi kuwa Katibu Mkuu Mifugo.

Mratibu wa mradi wa ADGG, Dkt. Eliamoni Lyatuu akiwasilisha mada kuhusu mradi wa Uboreshaji na Uendelezaji wa Mbari za Ng'ombe wa Maziwa katika kikao kilichofanyika katika Makao Makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania Jijini Dodoma.

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Prof. Erick Komba (aliyevaa suti nyeusi) na wajumbe wa kikao kilichofanya tathmini ya maendeleo ya mradi wa Uboreshaji na Uendelezaji wa Mbari za Ng'ombe wa Maziwa mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika katika Makao Makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania Jijini Dodoma.

***

Mradi wa uboreshaji na uendelezaji mbari za ng’ombe wa maziwa (ADGG) ambao umefanyika katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Iringa, Mbeya Njombe, na Songwe wawanufaisha wafugaji katika maeneo hayo.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Prof. Erick Komba (31.05.2021) baada ya kumalizika kwa kikao cha tathmini ya maendeleo ya mradi huo ambao kwa hapa Tanzania unafanyika katika mikoa saba (7) na Halmashauri ishirini nan ne (24).

Prof. Komba amesema mradi huo ulikuwa ni wa miaka sita na unatarajiwa kumalizika mwaka 2022 mwezi wa nne. Lengo la kikao hicho cha tathmini ilikuwa ni kuangalia mazuri yaliyofanyika kupitia mradi na namna gani yanaweza kuendelezwa ili wafugaji waendelee kupata tija na kukuza kipato ufugaji.

“Wafugaji wamenufaika sana kutokana na uwepo wa mradi huu kutokana na ushauri mbalimbali waliokuwa wakiupata kutoka kwa wataalamu juu ya nini cha kufanya pale mifugo yao inapopata matatizo na aina gani ya mbegu bora za ng’ombe wa maziwa wanatakiwa kufuga,” alisema Prof. Kombe.

Katika kikao hicho pia wamejadili namna ya kuwashirikisha wadau mbalimbali ambao watasaidia kuendeleza kazi zilizofanywa na mradi ili ziwe kuwa endelevu ikiwepo serikali, wadau wa maziwa na wadau wa mawasiliano.

Lengo ni kuhakikisha uzalishaji wa maziwa unaongezeka hapa nchini na hivyo kupunguza uagizaji wa maziwa kutoka nje ya nchi na hivyo kumnufaisha mfugaji wa hapa nchini kwa kukuza kipato chake.

Naye Mshauri wa Mradi wa kuendeleza mbari za ng’ombe wa maziwa, Dkt. Maria Mashingo ambaye pia alishawahi kuwa Katibu Mkuu Mifugo amesema mradi huu ni muhimu sana katika kuleta mageuzi kwenye sekta ya maziwa kwa kuhakikisha kuna kuwa na mbegu au vizazi bora vya ng’ombe ambao wanauwezo mkubwa wa kutoa maziwa mengi.

Dkt. Mashingo amesema mradi huu umetekelezwa kwa kutumia mbinu kubwa ambayo katika Sekta ya Mifugo haijawahi kufanyika kwani kinachofanyika ni pamoja na utambuzi wa ng’ombe kwa kujua uzazi na ubora wake.

Hivyo ameshauri itafutwe njia ya kuhakikisha matokeo ya mradi huu yanaendelezwa kwani watafiti wamefanya kazi kubwa ambayo imeleta tija kwa wafugaji kwa kuongeza uzalishaji wa maziwa na kuongeza kipato chao.

Msimamizi Mkuu wa Mradi wa ADGG, Dkt. Daniel Mwakihangilo amesema wamekuwa wakiwashauri wafugaji juu ya matumizi ya mbegu bora za ng’ombe wa maziwa ikiwa ni pamoja na matumizi ya madume bora ambayo yanapatikana katika maeneo wanayoishi na kwa kutumia njia ya uhimilishaji ili wapate ng’ombe wenye uwezo wa kutoa maziwa mengi.

Mratibu wa mradi wa ADGG na Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Duniani, Dkt. Eliamoni Lyatuu amesema kwanza walikuwa na lengo la kuwa na mfumo wa ukusanyaji wa taarifa za mifugo, pili kuweza kurejesha mrejesho kwa wafugaji pale wanapokuwa na maswali au maoni na tatu ni kuipanga mifugo kulingana na ubora wake ili kuwasaidia wafugaji kupata mifugo sahihi yenye uwezo wa kutoa maziwa mengi.

Akizungumzia kuhusu mradi huu, Bi. Yusta Elisha ambaye ni mfugaji wa ng’ombe wa maziwa amesema kupitia mradi wa ADGG wameweza kupata maelekezo juu ya ufugaji bora, wamekuwa wakipata ujembe kupitia simu juu ya namna ya kuendeleza shughuli zao za ufugaji ambazo zimewasaidi kuongeza uzalishaji wa maziwa tofauti na kiwango cha maziwa walichokuwa wakikipata kipindi cha nyuma ambapo kwa sasa wanapata lita 20 kwa siku tofauti na lita kumi walizokuwa wakipata kabla ya mradi.

Share:

ASKARI POLISI AMUUA KWA KUMPIGA RISASI JAMAA WAKIGOMBANIA MWANAMKE

Maafisa wa polisi kaunti ya Nairobi nchini Kenya wanachunguza kisa kimoja ambapo afisa wa polisi anadaiwa kumuua jamaa wa umri wa makamo kwa kumpiga risasi baada ya wawili hao kugombana kuhusu mwanamke.

Afisa huyo Titus Kipchirchiri Kirui anasemekana kumpiga risasi Charles Karugu Kikuyu mwenye umri wa miaka 32 kwa madai kwamba alikuwa akimnyemelea mpenzi wake.

 Kulingana na ripoti ya polisi, Maafisa wenzake wa polisi kutoka Embakasi waliofika katika eneo la tukio waliupata mwili wa Kikuyu ukielea kwenye damu sakafuni katika buchari moja mtaani Embakasi. 

Kikuyu alikimbizwa katika hospitali ya Mama Lucy lakini alifariki dunia kabla ya kuhudumiwa, upasuaji wa maiti unatarajiwa kufanywa wakati wowote. Kirui alikamatwa baadaye na yuko kizuizini huku uchunguzi zaidi ukiendelea. 

Maafisa wa polisi walipata risasi moja ambayo itatumika kama ushahidi katika kesi dhidi ya Kirui. 

 Chanzo - Tuko news


Share:

MKURUGENZI MKUU TBS DKT NGENYA ATOA WITO KWA WATANZANIA WASINUNUE BIDHAA BILA KUHAKIKISHA INA ALAMA YA UBORA

 

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS)  Dkt Yusuph Ngenya akizungumza na waandishi wa habari

NA OSCAR ASSENGA, TANGA

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS)  Dkt Yusuph Ngenya ametoa wito kwa  watanzania wasinunue bidhaa yoyote bila kuhakikisha kwamba ina alama ya ubora kwa bidhaa zinazozalishwa nchini.

Ngenya aliyasema hayo eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya nane ya Biashara ambapo alisema hatua hiyo itasaidia kuwaondolea hasara ambazo wamekuwa wakikumbana nazo kutokana na bidhaa wanazonunua kutokuwa na ubora unaotakiwa.

Alisema kwani bidhaa zimekuwa na athari nyingi katika matumizi ya binadamu hiyo ni muhimu watanzania kutambua kwamba wanaponunua bidhaa wanapaswa kuzikagua na kuona kama zina ubora unaotakiwa ili kuweza kuepukana na majanga ambayo yanaweza kuwakuta kutokana na bidhaa  feki.

“Lakini hata katika operesheni zetu ambazo tumekuwa tukizifanya tunagundua  bidhaa gani ambazo zinaingizwa kwenye masoko na hazina ubora ikiwemo bidhaa za ujenzi ,vifaa vya umeme vingi vinakuja feki hivyo tujitahidi kuvitambua na kuviondoa kwenye soko kwani mfano vifaa vya umeme madhara yake vinaweza kushika moto na kuweza kuharibu mali”Alisema Mkurugenzi huyo wa TBS

Akizungumzia lengo la uwepo wao kwenye maonyesho hayo ya nane ya biashara alisema wapo kwa ajili ya kuwaelimisha wananchi kuhusu shughuli za TBS na namna ya kupata huduma zao

“TBS pamoja na mambo megine kwenye maonyesho kama haya tunawakaribisha wananchi kuweza kuwaelimisha kwa mfano wale wanaotaka kupata huduma za TBS ikiwemo  bidhaa zao ziweze kupata alama ya ubora lakini pia tunashughulikia uuzaji wa bidhaa za chakula na vipodozi kuweza kupata usajili wa shughuli zao”Alisema Mkurugenzi huyo mkuu wa TBS.

Hata hivyo aliwataka wajasiriamali watengenezaji  wa bidhaa ndogo ndogo ni rahisi kwanza kwenda sido kupata mafunzo ambayo yatawasaidia kupata cheti  kitachowawezesha kupata barua kutoka sido na baadae waende   TBS kuweza kutambulika na wao watafanya kazi iliyobakia mpaka kuhakikisha bidhaa yao inapata ubora.

Mwisho.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 1,2021










ABBAS TARIMBA BUNGENI ALIA NA TFF

 


Share:

SERIKALI KUENDELEA KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI NA WAFANYABIASHARA WADOGO WADOGO NCHINI

 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma alipokuwaa akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akisisitiza jambo kwa washiri wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma alipokuwaa akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka ,akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akifurahia jambo na Mlezi wa umoja wa Mafundi Cherehani Dodoma ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Anthony Mavunde (katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka wakati wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma alipokuwaa akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo

Baadhi ya washiriki wakifatilia hotuba ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,(hayupo pichani) wakati akizungumza kwenye Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma alipokuwaa akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah,akifatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma alipokuwaa akimuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Prof.Kitila Mkumbo.

Mlezi wa umoja wa Mafundi Cherehani Dodoma ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Anthony Mavunde akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma

Mwenyekiti wa umoja wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) Bw.Sadoki Kasuka,akielezea umuhimu wa umoja huo wakati wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma

Mlezi wa umoja wa Mafundi Cherehani Dodoma ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Anthony Mavunde akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka wakati wa Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna,Dodoma

NAIBU Katibu Mkuu wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah,amesema kuwa Serikali itaendelea kuwezesha wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo kupata mafunzo ya kuendesha shughuli zao pamoja na kuwapatia mitaji ili kutimiza azma ya serikali ya viwanda.

Dkt.Abdallah ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mafundi Cherehani Dodoma (UMACHEDO) uliofanyika jijini Dodoma.

Dk. Abdallah amesema kuwa serikali ipo tayari kuwezesha wajasiriamali kufanya shughuli zao bila ya kuwepo na kikwazo chochote kwa mujibu wa sheria ili waweze kufikia malengo yao.

“Wajasiriamali wamekuwa wakilalamika kuwa moja kati ya changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na elimu ya biashara pamoja na mitaji, hili sisi kama serikali tutahakikisha tunalifanyia kazi kupitia taasisi yetu ya Sido kwa kuendesha mafunzo na kutoa mitaji kwa kuzingitia vigezo”amesema Dk. Abdallah

Pia amesema kuwa pamoja na kutoa mitaji na elimu pia kupitia Sido wataendelea kuwezesha wajasiriamali nyenzo zenye ubora ili kuzalisha bidhaa zenye ubora.

“Mfuko wetu wa kuwezesha wajasiriamali unaouwezo kwa kila mtu ambaye atakidhi vigezo kukopeshwa kiasi cha Sh. milioni tano lakini pia serikali kupitia shirika la NSSF na Sido wameingia makubalinaoa na benki ya Azania ili kukopesha mtaji wajasiriamali kiasi cha Sh. miliini 50 hadi 100”amesisitiza

Hata hivyo amesema kuwa serikali inaendelea kuwasilina na mamlaka husika katika maeneo mbalimbali nchini ili kupata maeneo rasmi ambayo yatatengwa kwa ajili ya wajasiriamali kufanya kushughuli zao.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka amewataka wajasiriamali wa mkoa wa Dodoma, kuwa wabunifu katika shughuli zao za kila siku ili kulikamata soko la bidhaa zao.

“Msipokuwa makini ujio wa makao makuu ya serikali nyinyi manaweza kuwa waangaliaji tu na fursa zote wakachukua wageni hivyo basi mnapaswa kuvaa sura za kazi ili mfikie malengo yenu kwa kubani zaidi bidhaa”amesema Mtaka

Awali Mlezi wa umoja wa mafundi cherehani ambaye ni mbunge wa Dodoma mjini, Antony Mavunde amesema kuwa tayari jiji la Dodoma limetenga ekari 8 kwa ajili ya wajasiriamali ili waweze kukidhi mahitaji yao.

“Tumetenga kiasi hicho cha eneo lakini pia na fedha ya kuanzia kiasi cha Sh. milioni 600 kwa ajili ya kuandaa eneo hili kwa ajili ya wajasirimali katika maeneo ya Nzunguni jijini Dodoma”amesema Mavunde

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger