Tuesday 29 September 2020

Mbaroni Kwa Kumbaka Mwanae Wa Kumzaa Shinyanga

SALVATORY NTANDU, SHINYANGA
Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Kambarage Manspaa ya Shinyanga Petro Maro (43) kwa tuhuma ya Kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 13 Mwanafunzi wa Darasa la Saba.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Leo Septemba 29,2020 na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema kuwa Petro alitekeleza tukio hilo Septemba 27 majira ya usiku nyumbani kwake.

Alisema kuwa Mama Msamaria mwema anayeishi jirani na Petro aligundua  binti huyo kubakwa na baba yake Mzazi na kisha kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika na kisha kumkamata.

"Binti huyu alibakwa na baba yake usiku akiwa amelala na chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kingono baada ya kutengana na Mke wake hali iyosababisha kuendelea kuishi na mwanae wa kike nyumba mmoja," alisema Magiligimba.

Kamanda Magiligimba alitoa wito wananchi mkoani humo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili kukomesha matukio na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.

Aliongeza kuwa hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtuhumiwa huyo na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.

Mwisho.


Share:

Watumishi Wizara Ya Kilimo Wapatiwa Mafunzo Ya Uadilifu


Watumishi wa Wizara ya Kilimo wametakiwa kufanya kazi kwa uadilifu na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuongeza tija katika kuwahudumia wananchi.


Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya ametoa wito huo leo (29.09.2020) mjini Morogoro wakati alipofungua mafunzo ya siku nne kwa wakuu wa taasisi, bodi na wakala chini ya wizara kuhusu kamati za kudhibiti uadilifu.


Kusaya amewataka watumishi wote kuwa waadilifu ndani ya mioyo yao ili watende kazi walizokabidhiwa kama dhamana ya kuhudumia umma bila upendeleo na kujiepusha na vitendo vya rushwa.


“Lengo la wizara ya kilimo ni kuwa na watumishi wenye udilifu na maadili mema ndio maana nimetoa kibali mafunzo haya yafanyike na kuwezesha kutimiza malengo ya kazi .Mtumishi mwadilifu atatumikia watanzania muda wote “alisema Kusaya


Mafunzo haya yanawakutanisha wakuu wa taasisi, bodi za mazao na wakala pamoja na kamati za uadilifu toka taasisi zote 23 chini ya wizara ya kilimo ambapo lengo  ni kujifunza namna ya kuishi uadilifu katika kuhakikisha shughuli za serikali zinafikia malengo yaliyowekwa huku watumishi wakizingatia misingi ya uadilifu na maadili .

Katibu Mkuu huyo wa wizara ya kilimo amewaambia watumishi hao kuwa katika utendaji kazi wao wanapimwa kwa matokeo hivyo wajibidiishe kutenda haki kwa wananchi pindi wawapo sehemu za kazi kwa kuepuka vitendo vinavyokiuka misingi ya maadili ikiwemo rushwa, kauli mbaya na matumizi mabaya ya madaraka.


“Tujione tunawiwa kuwahudumia watanzania kwani tumepewa dhamana ya kuwatumikia wenzetu kwa uaminifu na uadilifu “Kusaya alisema


Katika hatua nyingine Kusaya amesema atachukua hatua kali kwa baadhi ya watumishi kwenye taasisi chini ya wizara ambapo amebaini kuwa wanajihusisha na vitendo vibaya vya kuwajibu wananchi kwa kauli mbaya.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala Udhibiti wa Viuatilifu (TPRI) Dkt. Magret Mollel amemshukuru Katibu Mkuu kwa kutoa kibali cha kufanyika mafunzo hayo yenye kulenga kuongeza tija na utendaji kazi wa wizara ya kilimo.


Dkt. Mollel alisema kwa siku nne wajumbe wa kamati za uadilifu toka taasisi zote za wizara watashiriki mafunzo ya uadilifu na maadili toka kwa wawezeshaji kutoka Ofisi ya Rais-Ikulu, Ofisi ya Rais Utumishi pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Wizara ya Kilimo Filbert Lutare alisema mafunzo hayo yanahusisha washiriki 130 toka taasisi 23 chini ya wizara na kuwa wizara itahakikisha baada ya mafunzo haya watumishi kwenye taasisi zote wanaishi uadilifu na kuongeza kiwango cha maadili mema katika kuhudumia umma.


Aliongeza kusema kuwa Kamati za Kudhibiti Uadilifu zinaundwa kwa mujibu wa Waraka  wa Katibu Mkuu Kiongozi  wa mwaka 2017 ukilenga kutekeleza Mkakati wa Taifa Dhidi ya Rushwa Awamu ya Tatu ili watumishi wa umma washiriki kikamilifu na kwa vitendo kupambana na vitendo vya rushwa.

Mwisho
Imeandaliwa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Kilimo
MOROGORO
29.09.2020







Share:

PICHA: Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr Magufuli azungumza na Wananchi wa Makambako mkoani Njombe

 









Share:

Busega Yapambana na Uvuvi Haram


 Jumla ya Nyavu 60, Timber 30 na kokoro 3 zimekamatwa na kuteketezwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega. Zana hizo haram za uvuvi zimekamatwa katika kata za Nyashimo na Kabita mnamo tarehe 22 na 25 Septemba, 2020.

Zana hizo zilizokuwa zinatumika katika uvuvi haram zimekamatwa wakati wa operesheni za kawaida za kudhibiti uvuvi haram Wilayani Busega na kubaini uvunjifu mkubwa wa sheria na taratibu za uvuvi unaofanywa na baadhi ya wavuvi, alisema Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Busega Bw. Mwita Mokeha.

Licha ya kuteketeza zana haram za uvuvi pia baadhi ya wavuvi wanaofanya uvuvi haram wameweza kupigwa faini na kupewa onyo kali kufanya shughuli za uvuvi haram ili iwe fundisho kwa wavuvi wengine wasiofata sheria na taratibu za uvuvi. Zana hizo haram zimeteketezwa baada ya kupata idhini ya mahakama, aliongeza Afisa Uvuvi wa Wilaya ya Busega, Bw. Mokeha.

Uvuvi haram katika Ziwa Viktoria umekuwa ukifanywa na baadhi ya wavuvi na kusababisha upunguaji wa samaki katika ziwa hilo, na kupelekea upotevu mkubwa wa mapato ya halmashauri yatokanayo na shughuli za uvuvi. Kwa upande mwingine imebainika kwamba baadhi ya wavuvi wamekuwa na uelewa mdogo kuhusu shughuli za uvuvi hivyo hupelekea kufanya uvuvi haram.

MWISHO


Share:

Picha : MVUA YA UPEPO YAANGUSHA MNARA WA MATANGAZO RADIO FARAJA NA KUPONDA KANISA LA MAMA MWENYE HURUMA NGOKOLO


Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha jana Jumatatu Septemba 28,2020. 

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Mnara wa Kurushia Matangazo wa Kituo cha Redio Faraja Fm Stereo umeanguka kisha kuponda Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Ngokolo Mjini Shinyanga na kusababisha uharibifu wa mali kufuatia mvua kubwa iliyoambatana na upepo kunyesha jana Jumatatu Septemba 28, 2020 kuanzia saa 12 jioni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga, Padre Anatoly Salawa amesema mvua iliyoambatana na upepo iliyonyesha jana jioni imeleta madhara katika Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo sambamba na upande wa Radio Faraja na Radio Kwizera ambayo pia inatumia mnara huo kurusha matangazo yake Mjini Shinyanga.

“Mnara wetu wa Matangazo wa Radio Faraja wenye urefu mita 60 kwenda juu umeanguka na kuvunja paa la Kanisa upande wa nyuma. Tunashukuru kutokana na uimara wa kanisa hakuna madhara makubwa sana yaliyotokea na wakati tukio linatokea hapakuwa na watu kanisani”,amesema Padre Salawa.

“Tangu madhara yatokee hatupo hewani,Mpaka sasa tumezima matangazo na tutarejesha mara baada ya kupokea mitambo kutoka Mgodi wa Mwadui kwa ajili ya kuondoa mnara ulioanguka na tutarejesha matangazo tukitumia sehemu ya mnara wa msalaba/kengere uliobakia lakini kule Kahama na kwenye mitandao ya kijamii tunaendelea na matangazo yetu”,ameeleza Padre Salawa.

Aidha Mkurugenzi huyo wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga amesema tayari viongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga wakiongozwa na Askofu Liberatus Sangu ambapo amewaomba waumini na wadau mbalimbali kuchangia ukarabati wa Kanisa ili lirudi kwenye hali ya kawaida.

Padre Salawa amewaomba wadau walioguswa na madhara yaliyotokea katika Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo na Radio Faraja kuwasilisha michango yao kupitia M-PESA namba 0762444746 (BISHOP) au kupitia Benki ya CRDB namba 01J1058390001 (Diocese of Shinyanga).

Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga, Padre Anatoly Salawa akielezea kuhusu madhara yaliyojitokeza baada ya Mnara wa Matangazo ya Redio Faraja kuangukia Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo kufuatia mvua kubwa iliyoambata na upepo kunyesha jana jioni Septemba 28,2020. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga, Padre Anatoly Salawa akionesha Mnara wa Matangazo ya Redio Faraja ulioangukia Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo.
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa  mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Taarifa Kwa Umma Toka Jeshi la Polisi Makao Makuu







Share:

DK. MZEE : FANYENI MAZOEZI KUJIKINGA NA MAGONJWA YASIYO YA KUAMBUKIZA


Mratibu wa Malaria Mkoa wa Shinyanga Dkt. Daniel Mzee akimvisha Medali Mshindi upande wa watoto aliyeshiriki mashindano hayo. Picha na  Neema Sawaka
Mkurugenzi wa Shidepha+ Venance Mzuka akiongea na Washiriki wa mbio za Malaria Marathon.
Meneja wa T- Marc Hamid Al Alawy akiwahutubia washiriki wa mbio za Malaria Marathoni katika uwanja wa Halmashauri mjini Kahama.
***
Na Raymond Mihayo Kahama
Wananchi Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga wametakiwa kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi kila siku kwa ili kuufanya mwili kuwa na kinga imara na kuepukana na magonjwa hatari ambayo siyo ya kuambukiza.

Hayo yalisemwa jana Mratibu wa Malaria Mkoa wa Shinyanga Dkt. Daniel Mzee wakati akifunga mashindano ya riadha yenye lengo kuhamasisha kubadilisha tabia na kutokomeza Malaria (malaria Marathon) yaliyoandaliwa na shirika lisilokuwa la kiserikali la Comic Rerief la Uingereza kwa kushiana na Shirika la SHDEPHA+ Kahama.

"Ukifanya mazoezi kila siku ni rahisi kwa mwili kutumia kinga ya asili kupambana na magonjwa yasiyoambukiza kama vile Shikizo la Moyo, Kisukari na Mgonjwa mengine yasiyo ya kuambukiza kwa binadamu",alisema Dkt. Mzee.

Dkt. Mzee alisema kuwa mbio hizo zimeambatana na ujumbe wa kutokomeza Malaria Mkoa wa Shinyanga huku zikiwashirikisha wakimbiaji kutoka Wilaya ya Kahama na nje ya Kahama yaani Mkoani Manyara na Arusha wa jinsi ya kike na Kiume huku wakikimbia umbali wa kilometa 21.

Kwa upande wake Afisa Michezo kutoka Halmashauri ya Mji wa Kahama Lupola Mkomwa alisema kuwa lengo la mbio hizo ni kutokomeza ugonjwa wa Malaria katika Halmashauri sita zilipo katika Mkoa wa Shinyanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SHDEPHA+ Tanzania Venance Mzuka alisema kuwa shirika lake litaendelea kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria na kuhimiza michezo na maagizo mbalimbali yanayotolewa na Serikali.

Alisema kuwa njia mojawapo iliyotumika katika kutokomeza ugonjwa huo ni pamoja na kutumia mashindano kama hayo ngoma za asili kutoa elimu kwa jamii iliyopo maeneo yenye maambukizo makubwa vijijini hali ambayo imechangia kuleta mabadiliko chanya kwa ugonjwa kupungua kiasi kikubwa.

Mbio hizo za Malaria Marathon zilimalizika huku washindi kwa upande wa Wanaume akiwa ni Elisante Elibariki aliyemaliza mbio hizo kwa kutumia muda wa dakika 43, mshindi wa pili alikuwa ni Halipha Atanas aliyetumia muda wa dakika 44.28 huku mshindi wa tatu akiwa Adam Neta akitumia dakika 45 kumaliza mbio hizo.

Kwa upande wa Wanawake aliyeongoza katika mbio hizo zlikuwa Hamida Nassoro aliyetumia dakika 49 huku aliyemfuata alikuwa Nyamizi Ngasa aliyetumia saa moja huku Esta Njingu aliyetumia saa 2.

Kwa upande wa watoto walioshiriki mbio hizo aliyeongoza alikuwa Seleman Salehe (16) Mwanafunzi wa shule ya sekondari Busoka, wa pili alikuwa Jeronimo Solomoni (10) na hivyo kutoa upinzani mkubwa kwa washiriki wengine wakubwa walioshiriki mbio hizo.

Mradi huo wa Malaria ambao ulikuwa wa miaka miwili utekelezaji wake umemalizika mwaka huu kwani ulianza mwaka 2018 huku Kauli mbiu wananchi kubadilisha tabia na kutokomeza Malaria ulifadhiliwa na Shirika la Comic Relief kutoka Nchini Uingereza kwa kushirikina na Shirika la SHDEPHA+ ambapo utekelezaji wake ulikuwa katika Halmashauri za Ushetu, Kahama Mji. Pamoja na Msalala zilizopo Wilayani Kahama pamoja na Halmashauri ya Kishapu, Shinyanga Mji pamoja na ile Shinyanga Vijijini.

Share:

Financial Crime Lead at Absa Bank

We are a diversified standalone African financial services group, delivering an integrated set of products and services across personal and business banking, corporate and investment banking, wealth, investment management and insurance. Absa Group Limited is listed on the JSE and is one of Africa’s largest diversified financial services groups with a presence in 12 countries […]

The post Financial Crime Lead at Absa Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Supervisor: Fleet & Facilities at Vodacom

Joining Vodacom is more than a job, what we do matters. We don’t just carry minutes, texts and data – we carry people’s lives. And that’s a huge responsibility. If you think for a minute about the people you rely on…the likelihood is they rely on us. Customers are at the heart of everything we […]

The post Supervisor: Fleet & Facilities at Vodacom appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Photographer (No Experience or Camera Required) at TransPerfect

Photographer (No Experience or Camera Required) Trans Perfect We are looking for participants to join our new Photo/Video Collection Project. The task consists of collecting photos and videos with your smartphone device of several daily objects to improve the design and development of AI products, technologies, and services. The content WILL NOT be used for […]

The post Photographer (No Experience or Camera Required) at TransPerfect appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Managing Director at Jobortunity

Managing Director Jobortunity Arusha, Tanzania Managing Director, Arusha – Tanzania Jobortunity seeks a Managing Director to help build, manage, and most of all add value to a portfolio of innovative programs empowering youth and companies in Tanzania. The managing director oversees Jobortunity’s operations, liaises with stakeholders, drives strategic organisational growth, and is responsible for the […]

The post Managing Director at Jobortunity appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Customer Service Representative at Greenlight Planet

Customer Service Representative Greenlight Planet Arusha, Tanzania Job description The Customer Service Executive will work closely with the Operations and Sales teams to serve existing and potential customers by providing product and service information while resolving product issues effectively. Key Responsibilities Managing large amounts of inbound and outbound calls in a timely manner while following […]

The post Customer Service Representative at Greenlight Planet appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Chemicals, Sales Engineer at REDA

Sales Engineer REDA Chemicals Dar es Salaam, Tanzania Sales Engineer in Specialty Chemicals Job Ref: JB574 – Dar es Salaam, Tanzania REDA Chemicals Are you looking for a new challenge? At REDA Chemicals, we passionately market and distribute a unique and innovative portfolio of specialty raw materials and industrial chemicals. We are the largest distribution […]

The post Chemicals, Sales Engineer at REDA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Monitoring, Evaluation, and Learning Manager at PATH

Senior Monitoring, Evaluation, and Learning Manager – C3HP HIV/TB Project Tracking Code 10233 Job Description Location: Arusha, Tanzania Division: Global Health Programs PATH is a global organization that works to accelerate health equity by bringing together public institutions, businesses, social enterprises, and investors to solve the world’s most pressing health challenges. With expertise in science, health, […]

The post Senior Monitoring, Evaluation, and Learning Manager at PATH appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Community Engagement Officers (4 Positions) at TAHEA

Community Engagement Officers (4 Positions) The Community Engagement Officer under TAHEA will work in collaboration with Biomedical technical officer at regional levels and community in respective Council to implement HIV prevention program targeting population at risk, Vulnerable Adolescent Girls and Young women, female sex workers and MSM, s/he will monitor the implementation of the SBCC, […]

The post Community Engagement Officers (4 Positions) at TAHEA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Assistant Project Accountant (1 Position) at TAHEA

Assistant Project Accountant (1 Position) Position Description: The assistant accountant will be supporting an accountant and finance department to coordinate and supervise financial activities of the project. This shall include the timely preparation and submission of financial and accounting reports and documents including cash books, payment vouchers, bank reconciliation statements, budget compliance reports and any […]

The post Assistant Project Accountant (1 Position) at TAHEA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DREAMS Program Officer (1 Position) at TAHEA

DREAMS Program Officer (1 Position) Main Accountabilities and Responsibilities • Oversee the design and roll-out of a DREAMS package of services for AGYW (may include Stepping Stones Curriculum, health service demand creation activities including HIV testing and counseling and linkage to care, creation of safe spaces, GBV screening, scale-up of adolescent-friendly health services, support for […]

The post DREAMS Program Officer (1 Position) at TAHEA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger