Sunday 1 March 2020

Nafasi za Kazi 21 Benjamin William Mkapa Foundation (BMF)

Overview
The Benjamin William Mkapa Foundation (BMF) is a non- profit Trust, established in 2006 with the vision towards healthy lives and well-being for all, in Tanzania and the rest of Africa. Its strategic focused results areas include to combat HIV and AIDS, TB, Malaria and Reproductive, Maternal New Born, Child and Adolescent Health coupled with Health Systems Strengthening including Human Resource for Health. The Foundation addresses the above health challenges through innovative design and implementation of sustainable programs such as the Mkapa Fellows Program.

Achievement of the BMF’s vision can be achieved through empowered workforce, which is self-motivated, committed to growth and integrity, and seeks excellence in execution. BMF seeks for innovative, self-driven, dynamic and competent qualified candidates to fill various vacancies as described in PDF file:

BMF is an equal opportunity employer and we value diversity.
For more information please Download attached PDF file to get full details of all jobs requirements.

The deadline for application is on Monday, 09th March 2020



Share:

Majeshi Ya Uturuki Yadungua Ndege Mbili za Kivita za Syria

Vikosi vya Uturuki vimedungua ndege mbili za kivita za serikali ya Syria katika mkoa wa kaskazini-maghribi wa Idlib siku ya Jumapili, baada ya Ankara kutangaza operesheni ya kijeshi ndani ya mipaka ya Syria.

Shirika la uangalizi wa haki za binadamu la Syria lenye makao yake nchini Uingereza, lilisema ndege hizo mbili chapa ya Sukhoi zilianguka katika maeneo yanayodhibitiwa na vikosi vya utawala, baada ya kushambuliwa na ndege za Uturuki aina ya F-16.

Shirika la habari la serikali ya Syria SANA, lilisema vikosi vya Uturuki "vimelenga" mbili kati ya ndege zake kaskazini-magharibi mwa Syria. T

angu Desemba, vikosi vya utawala vikiungwa mkono na Urusi vimeongoza operesheni ya kijeshi dhidi ya ngome ya mwisho ya waasi ya Idlib, ambako Uturuki inayaunga mkono baadhi ya makundi ya waasi.

Wizara ya ulinzi ya Uturuki pia iliripoti kudunguliwa kwa ndege hizo siku ya Jumapili, lakini haikuthibitisha juu ya nani alihusika. "Ndege mbili za utawala za SU-24 zilizokuwa zinashambulia ndege zetu zimeangushwa," ilisema.
 
Hatua hiyo ilikuja baada ya Uturuki kutangaza operesheni ya kijeshi kaskazini-magharibi mwa Syria baada ya mashambulizi ya ndege za utawala wa Syria kuuwa wanajeshi  zaidi ya 30 wa Uturuki siku ya Alhamisi.

Mashambulizi ya kisasi ya ndege zisizo na rubani na mizinga yameuwa wanajeshi 74 wa Syria na wapingaji 14 washirika tangu siku ya Ijumaa, limesema shirika la uangalizi wa haki za binadamu. Pia Jumapili jeshi la Syria lilianguisha ndege ya Uturuki isiyo na rubani kaskazini-magharibi mwa Syria.

Shirika la SANA lilisema ndege isiyo n rubani ilidunguliwa karibu na mji wa Saraqeb, na kuchapicha picha za ndege ikiporomoka kutoka angani ikiwaka moto. 

Shirika la haki za binadamu pia lilithibitisha tukio hilo. Jeshi la Syria lilikuwa limeonya kwamba lingedungua ndege yoyote inayokiuka anga yake kaskazini-magharibi mwa Syria.

-DW


Share:

Tanzania Yatajwa kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki na ya nne Afrika kwa kuweka mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara ndogondogo.

Na Mwandishi Wetu
Tanzania imetajwa kuwa nchi ya kwanza Afrika Mashariki na ya nne Afrika kwa kuweka mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara ndogondogo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dodoma, Msemaji mkuu wa Serikali  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa kidunia Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika Nyanja mbalimbali ambapo katika suala hilo anasema kidunia imekuwa ya 21.

“Taasisi za Kimataifa zinatambua juhudi za Serikali yetu katika kuwaletea wananchi maendeleo, Baadhi ya masuala yaliyofanyika  kwa wajasiriamali wadogo ni  kupewa vitambulisho maalum vya kuwatambulisha, tozo mbalimbali zimefutwa ili kuwesesha ukuaji wa  sekta ya biashara hapa nchini”,Alisistiza Dkt. Abbasi

Akifafanua  Dkt. Abbasi amesema kuwa Kituo cha Kimataifa cha Televisheni cha CNBC Africa kimerusha makala maalum inayoonesha mafanikio ya Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na kuoneshwa na zaidi ya nchi 100 Duniani.

Katika makala hiyo iliyoakisi sekta za utalii, miundombinu, nishati, madini, kilimo na uzalishaji, Dkt. Abbasi amesema kuwa hatua hiyo ni moja ya ishara kuwa Taasisi za Kimataifa zinaendelea kutambua hatua zinazochukiliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika hatua nyingine Dkt. Abbasi amesema kuwa Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki Prof. Palamagamba Kabudi aliwasilisha ripoti ya Tanzania katika Baraza la Dunia la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu  na kusisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuheshimu na kulinda haki za binadamu kama ilivyokawaida yake.

“ Haki za Binadamu sio siasa, kama nchi tumeendelea kusisitiza na tutaendelea kuzienzi haki zote za Binadamu kwa maslahi ya watu wote” , alisisitiza Dkt. Abbasi

Tanzania imetajwa kwa nyakati tofauti na Taasisi mbalimbali za Kimataifa kuwa Taifa la kupigiwa mfano kwa namna inavyochukua hatua za kuwaletea wananchi maendeleo, kupiga vita rushwa, kujenga uchumi na ustawi wa wananchi.


Share:

Ujenzi wa SGR Waendelea kwa Kasi, Trilioni 2.957Zatumika hadi Sasa

Na Frank Mvungi- MAELEZO
Serikali imetumia kiasi cha Shilingi Trilioni 2.957 kutekeleza mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) huku kasi ya utekelezaji ikiongezeka.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma , Msemaji Mkuu wa Serikali  na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo na Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo unaendelea kama ulivyopangwa.

“Mradi  wa SGR kwa kipande cha Dar es Salaam na Morogoro umefikia asilimia asilimia 75 wakati kipande cha Morogoro Makutopora Singida kimefikia takribani asilimia 28”, Alisisitiza Dkt. Abbasi

Akifafanua Dkt. Abbasi amesema kuwa watanzania wataanza kutumia usafiri huo wa kisasa kwa kipande cha Dar es Salaam hadi Morogoro mwaka huu wa 2020 hivyo ile ahadi ya Serikali kwa wananchi itatimia kama ilivyopangwa na kwa wakati.

Kwa upande wa kipande cha Mwanza-Isaka  Dkt.Abbasi amesema kuwa wakati wowote tenda itatangazwa ili kumpata mkandarasi atakayejenga reli hiyo kwa kipande hicho ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Dkt. John Pombe Magufuli alilolitoa mwezi Desemba 2019 Jijini Mwanza kwa Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano.

Akizungumzia baadhi ya wanasiasa wanaobeza juhudi za Serikali kuwaletea wananchi maendeleo kupitia miradi kama SGR Dkt. Abbasi amesema kuwa Serikali haitarudi nyuma katika kuwaletea wananchi maendeleo kwa kuwa hata wanaobeza watanufaika na miradi hiyo ikiwemo ndege na umeme.

Kwa upande wa utekelezaji wa mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere(JNHPP) , ujenzi wa eneo la kuchepusha maji ya mto Rufiji ili ujenzi wa ukuta wa bwawa uanze limekamilika kwa asilimia mia moja,  Aidha bwawa hilo linatajwa kuwa kati ya mabwawa makubwa 70 ya kuzalisha umeme wa maji Duniani na kwa Afrika litakuwa la nne kwa ukubwa.

Kwa upande wa kiwango cha fedha kilicholipwa hadi hasa Dkt. Abbasi amesema kuwa Shilingi Trilioni 1.275 kati ya Trilioni 6.5 zimeshalipwa ambapo kazi zote zinaendelea kama ilivyopangwa.

Katika hatua nyingine Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu wa Wizara zote kesho Machi 2, 2020 na watatembelea mradi wa SGR  ili kujionea utekelezaji wake.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi wa Chelezo katika Ziwa Victoria Dkt. Abbasi  amesema kuwa umekamilika kwa asilimia 100 na Shilingi Bilioni 32.8 zimeshalipwa na katikati ya mwezi Machi Itaanza kufanya kazi , huku ukarabati wa MV Victoria umefikia asilimia 89 na Bilioni 14 zimeshalipwa, Wakati MV Butiama ukarabati wake umefikia asilimia 86 na Bilioni 3 zimeshalipwa kati ya Bilioni 4 zilizotengwa kwa ajili ya mradi huo.

“ Ujenzi wa meli mpya  na ya kisasa katika Ziwa Victoria itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria 1200 na Tani 400 za mizigo umefikia asilimia 52 hadi sasa na unaendelea kutekelezwa kwa kasi kama ilivyopangwa.

Utaratibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali kukutana na vyombo vya habari unalenga kuileta Serikali kwa pamoja na wananchi kwa kueleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa maslahi yao katika maeneo mbalimbali hapa nchini


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa Apokea Taarifa Ya Kmati Aliyoiunda Ya Kuchunguza Zo La Katani

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea taarifa ya uchunguzi wa tuhuma mbalimbali katika tasnia ya kilimo cha mkonge mkoani Tangana kuagiza mapendekezo yaliyotolewa na timu hiyo yakiwemo ya kurejeshwa Serikalini kwa nyumba na. 176 eneo la Bombo ambayo ilimilikishwa kwa Bw. Salum Shamte yafanyiwe kazi.

Nyumba nyingine zilizopendekezwa kurejeshwa Serikalini ni pamoja na nyumba kumi zilizoko ndani ya Jiji la Tanga katika maeneo ya Raskazone, Bombo, Nguvumali na Market street ambazo zilinunuliwa na watumishi hao kwa udanganyifu.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumapili, Machi 1, 2020) wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri za mkoa wa Tanga, viongozi wa taasisi mbalimbali, wadau wa zao la mkonge pamoja na viongozi wa dini kwenye ukumbi wa hoteli ya Naivera.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wawekezaji ambao wanamiliki mashamba ya mkonge yenye ukubwa wa zaidi ya ekari 2,000 ambao hawajayaendeleza wayaendeleze wakishindwa yatachukuliwa na kugawiwa kwa wananchi.

Timu hiyo maalum ya uchunguzi iliundwa na Waziri Mkuu na ilifanya uchunguzi mkoani Tanga kuanzia tarehe 29/11/2019 hadi tarehe 07/02/2020. Timu hiyo iliyokuwa na  wajumbe 13 ilihusisha maafisa kutoka ofisi mbalimbali za Serikali.

Uchunguzi huo maalum ulihusu masuala mbalimbali katika tasnia ya zao la mkonge mkoani Tanga ambayo ni pamoja na uzalishaji wa mkonge, bei ya zao la mkonge katika soko la ndani na nje ya nchi.

Pia, ilichunguza kuhusu mali za iliyokuwa Mamlaka ya mkonge nchini, ubia kati ya Kampuni ya Katani Limited na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Utendaji kazi wa Kampuni ya Katani Ltd na pia Utendaji kazi wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB).

Awali,Mwenyekiti wa timu hiyo Bw. Gerald Kusaya alisema timu ilibaini kuwa Kampuni ya Katani Ltd tokea mwanzo ilikuwa na mgongano wa kimaslahi na kupelekea kuhujumu uchumi kwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wake Bw. Salum Shamte alikuwa mtumishi wa umma na alishiriki vikao vyote vya ubinafsishaji wa Mamlaka ya Mkonge ilhali akijua kuwa ana maslahi kwenye Kampuni inayonunua.

“Kwa kuwa uchunguzi umebaini viongozi na wanahisa wa Katani Ltd waliohusika kuingia mikataba walikuwa watumishi wa Mamlaka ya Mkonge wakati wa mchakato wote wa ubinafsishaji hivyo walitumia vibaya madaraka yao kwa kuishawishi Serikali kuingia mkataba huo usiokuwa na tija kwa Serikali bali kwa manufaa yao binafsi. Hivyo, Timu imeandaa taratibu kwa ajili ya wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.”

Bw. Kusaya amesema timu hiyo inapendekeza kuwa Serikali itoe fedha kwa ajili ya kazi ya kuyapima upya mashamba matano ya Mwelya, Ngombezi, Hale, Magunga na Magoma ili wananchi wanaoendelea kutumia mashamba hayo kwa kukodishwa na Bodi ya Mkonge kama ilivyokubalika kwenye Baraza la Mawaziri mwaka 2005 ili waweze kupewa Hati ndogo (leasehold tittle);

Alisema timu inapendekeza nyumba 30 zilizopo eneo la Muheza, ambazo baadhi zilitolewa kwa wananchi waliokuwa watumishi wa Mamlaka ya Mkonge na baadhi kuachwa kwa ajili ya makazi ziendelee kuwa mali ya wananchi hao kwa kuwa eneo hilo kwa sasa lipo chini ya Halmashauri ya Wilaya ya Muheza.

“Nyumba 22 zilizoko ndani ya mashamba ya mkonge na maeneo ya kiwanda cha TANCORD ziendelee kubaki mali ya Serikali na nyumba iliyoko katika kiwanja Na. 176 eneo la Bombo iliyohamishwa kwenda kwa Ndg. Salum Shamte irejeshwe Serikalini kwa njia ya urekebishaji wa daftari la Msajili wa Hati.”

Kwa upande wao, viongozi wa mkoa wa Tanga wakiwemo wabunge wamemshukuru Waziri Mkuu kwa kuunda timu hiyo ya uchunguzi wa zao la mkonge kwa kuwa mapendekezo yake yamejibu changamoto zilizokuwa zinalikabili zao hilo.

Wamesema mapendekezo yaliyotolewa na timu hiyo yanakwenda kufufua kilimo cha zao la mkonge hivyo kuongeza tija kwa wakulima wa mkonge mkoani Tanga.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Mawaziri Wa SADC Sekta Ya Kazi Na Ajira Kukutana Jijini Dar Es Salaam

Na: Mwandishi Wetu
Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) sekta ya Kazi na Ajira unatarajiwa kufanyika hapa nchini kuanzia tarehe 2 hadi 6 Machi, 2020 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) uliopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari alieleza kuwa Mkutano huo utafunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Kauli mbiu ya Mkutano huo ikiwa ni “Kukuza Soko la Ajira na Mahusiano Mema Sehemu za Kazi kwa Maendeleo Endelevu”.

Waziri Mhagama amesema kuwa katika Mkutano huo ambao kwa kiasi kikukubwa utawakutanisha Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Kazi na Ajira, Wataalam na Vyama vya Waajiri na Vyama vya Wafanyakazi kutoka Nchi Wanachama wa SADC na utakuwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali ya sekta ya Kazi na Ajira katika Ukanda huo wa Afrika.

“Mkutano huu wa Mawaziri, Wataalamu na Wadau wa Utatu wa Sekta ya Kazi na Ajira utatoa fursa ya majadiliano ya pamoja  kwa nchi wanachama wa SADC kuangalia utekelezaji wa maazimio mbalimbali kuhusu masuala ya Kazi, Ajira, Vijana, Uhamaji wa Nguvukazi na Hifadhi ya Jamii”, Alisema Waziri Mhagama.

Alieleza kuwa katika Mkutano huo itazindua rasmi Programu ya Mafunzo ya Uzoefu kwa Wahitimu Mahala pa Kazi (Intership) kwa vijana inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Alieleza kuwa Programu hiyo ni Mahususi kwa vijana wa Kitanzania waliohitimu vyuo mbalimbali hapa nchini na inagharamiwa na Serikali kwa kushirikiana na Waajiri.

“Serikali iliamua kuanzisha Programu hii kwa lengo la kuwapatia fursa vijana ya kupata uzoefu, ujuzi, maadili ya kazi na namna bora ya kuhudumia wateja katika sehemu zao za kazi,” alieleza Mhagama

“Vijana 5,000 wameweza kunufaika na programu hiyo na kati yao vijana wapatao 1,000 waliomaliza muda wao wa mafunzo hayo wameweza kupata ajira katika maeneo mbalimbali,” alisema Mhagama   

Akitaja manufaa ya Programu hiyo ya Mafunzo kwa Vitendo Mahala pa Kazi kwa Vijana kuwa ni pamoja na Kuwawezesha vijana wanaoshiriki kuoanisha ujuzi waliopata kwenye taasisi za elimu na mafunzo pamoja na mahitaji halisi ya ujuzi kwa waajiri; Kuwezesha vijana kujifunza maadili, mtazamo chanya kuhusu kazi pamoja na tamaduni za kuishi mahali pa kazi na Kuwapatia uzoefu wa kazi unaohitajika na waajiri.

Aliongeza kuwa Programu hiyo imeongeza ushirikiano mzuri kati ya waajiri, Serikali na Vijana na imewapa hamasa waajiri kushiriki katika kuwajengea Ujuzi vijana, maadili na weledi unaohitajika katika soko la Ajira.

Aidha, Waziri Mhagama alitoa wito kwa Wananchi ikiwemo wamiliki na Wafanyakazi wa Mahoteli, Migahawa, Vyombo vya Usafiri na sehemu mbalimbali watakazotembelea wageni kuwakarimu na kutoa ushirikiano na ukaribisho unaostahili ili sifa ya nchi iendelee kuwa kielelezo kwa wageni.

MWISHO


Share:

Serikali Yatoa siku tatu kwa mikoa yote nchini kuainisha maeneo maalumu yaliyotengwa kuhudumia washukiwa wa Virusi Vya Corona

Serikali  imetoa siku tatu kwa mikoa yote nchini, kuainisha maeneo maalumu yaliyotengwa kuhudumia washukiwa au wagonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na kirusi cha corona.

Hadi kufikia Alhamisi iliyopita, watu 83,652 wamethibitika kuugua corona, huku wengine 2,858 wakifariki dunia na nchi 51 zikiwa zimeshakumbwa na ugonjwa huo.

Kwa upande wa nchi za Afrika, ugonjwa huo umeshaingia Algeria, Nigeria na Misri.

Akizungumza jana, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema hadi sasa Tanzania haina mgonjwa wala mshukiwa.

“Tunahitaji kuendelea kuchukua tahadhari kubwa ya kujikinga, hospitali zote za umma na binafsi zihakikishe zina eneo la muda la kumshikilia mshukiwa.

“Mikoa ihakikishe uwepo wa vitakasa mikono katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu, zikiwemo hoteli, nyumba za wageni, sehemu za ibada, shule, ofisi, sehemu za kazi na biashara,” alisema Ummy.

Alisema kati ya Januari 30 hadi Februari 27, mwaka huu, wasafiri 11,048 wamechunguzwa katika mipaka mbalimbali nchini ambao walitoka katika nchi zilizo na ugonjwa huo, ikiwamo China.

Alisema pia wana vipimo vya joto 140 na kati ya hivyo, 125 ni vya mkono na 15 ni vya kupima watu wengi kwa mpigo, ambavyo vimefungwa na vinatumika maeneo ya mipakani, viwanja vya ndege na bandari.

Ummy alisema wameongeza idadi ya wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kuajiri watumishi 100 ili kuimarisha ufuatiliaji wa wasafiri wanaoingia nchini kupitia mipakani.

“Tumeandaa dawa, vifaa kinga na vitakasa mikono ambavyo tayari vipo kwenye bohari za dawa za kanda na maeneo maalumu katika mikoa yenye uwezekano mkubwa wa kupata wagonjwa kwa ajili ya kuwaweka washukiwa na kuwapatia matibabu,” alisema Ummy.

Alisema pia wameimarisha uwezo wa kupima sampuli kupitia maabara ya taifa ya jamii iliyopo kwa watu wote wanaohisiwa kuwa na viashiria au dalili za ugonjwa huo na kwamba ndani ya saa 4 – 6 wanaweza kutoa majibu ya vipimo.


Share:

Serikali Yaagiza Wakimbizi 1000 Waliotoroka Makambini na Kwenda Kufanya Uhalifu Waondolewe na Wafunguliwe Mashitaka

Na Mwandishi Wetu,Kibondo
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameviagiza Vyombo vya Ulinzi na Usalama mkoani Kigoma kuwaondosha na kuwafungulia mashtaka wakimbizi zaidi ya Elfu Moja waliotoroka kutoka katika Kambi mbalimbali za wakimbizi  na kwenda kufanya uhalifu nje ya makambi.

Naibu Waziri Masauni ameyasema hayo leo  wakati akiongea na wakimbizi kutoka nchini Burundi waliohifadhiwa katika Kambi ya Nduta iliyoko wilayani Kibondo, mkoani Kigoma huku ikihifadhi jumla ya wakimbizi na waomba hifadhi 75,055.

“Tanzania na Burundi zimekua zikishirikiana kwa muda mrefu,Tanzania si nchi ya kubembeleza watu waovu na haijawahi kufuga wahalifu , kuna watu zaidi ya Elfu Moja  wamevunja sheria za ukimbizi kwa kutoroka kwenye makambi na kwenda kufanya uhalifu huko nje, sasa naviagiza vyombo vya usalama kuhakikisha wanawaondosha hao watu kwa mujibu wa sheria na itakua fundisho kwa watu wote wenye tabia ya kutoroka makambini na kwenda nje  kufanya uhalifu, ” alisema Masauni

Masauni pia aliwataka wakimbizi hao kuendelea kujiandikisha  kwa hiari ili waweze kurudi nchini kwao Burundi ambako hali ya amani sasa imerejea na tayari pande tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania, Serikali ya Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) washatiliana saini mkataba utakaofanikisha zoezi hilo kwa wanaotaka kurejea Burundi

“Serikali ya Burundi imetuthibitishia kurejea kwa amani katika nchi yenu, nendeni mkaijenge na kuitumikia  nchi  yenu, nchi yoyote ili iweze kuendelea  inahitaji  watu na hapa naona kuna vijana wengi tu ambao ndio msingi wa maendeleo wa nchi yoyote ile duniani”aliongeza Masauni

Akizungumza katika Mkutano huo Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibondo,  Kanali Hosea Ndagala aliwataka wakimbizi hao kufuata sheria za nchi na wao kama Kamati ya Ulinzi na Usalama watahakikisha kila atakaethibitika kufanya uhalifu sheria itachukua mkondo wake ikiwemo kufutiwa ukimbizi na kufunguliwa mashtaka.

“Hatutoruhusu mtu yoyote kuingiza vitu visivyoruhusiwa katika makambi ambavyo vinaweza kuhatarisha usalama katika makambi yenu na tunaomba mkiona kitu chochote kisicho cha kawaida mtoe taarifa kwa viongozi ili mbakie katika mazingira salama” alisema Kanali Ndagala

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano huo wakimbizi hao waliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuwahifadhi na kuwapa huduma ya ulinzi huku wakiomba kuwahishiwa huduma mbalimbali ikiwemo nguo,chakula na huduma za afya.


Share:

Hali Ya Dharura Yatangazwa Marekani Baada Ya Virusi Vya Corona Kuua Mtu Mmoja

Gavana wa jimbo la Washington nchini Marekani ametangaza hali ya dharura ya kiafya baada ya mtu mmoja kuaga dunia kutokana na virusi vya Corona katika jimbo hilo, hii ikiwa ni kesi ya kwanza virusi hivyo kuua nchini Marekani.

Gavana Jay Inslee ameziagiza idara zote za serikali ya jimbo hilo kutumia rasilimali zote kupambana na mripuko na maambukizi ya Corona baada ya kifo hicho kuripotiwa jimboni hapo.

Maafisa wa majimbo ya Marekani ya California, Oregon na Washington wana wasiwasi mkubwa wa kuenea kwa virusi hivyo baada ya kesi nyingi kuthibitishwa miongoni mwa watu wa jamii za West Coast nchini humo.

Rais Donald Trump ambaye siku ya Ijumaa aliwashambulia viongozi wa chama cha Democratic ambao wametilia shaka uwezo na utayarifu wa serikali yake katika kukabiliana na maambukizi ya virusi hatari vya Corona nchini humo ametaka Wamarekani kutokuwa na hofu baada ya kifo hicho kuripotiwa, akidai kuwa virusi hivyo vitatoweka vyenyewe kimiujiza.


Share:

RC Ole Sendeka awapa mwezi mmoja viongozi kuwatafuta wanafunzi 708

Na Amiri kilagalila,Njombe
Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka ametoa muda wa mwezi mmoja kwa watendaji,maafisa elimu kata pamoja na viongozi wa mitaa na vijiji kuhakikisha wanawasaka wanafunzi 708 ambao hawajajiunga na masomo ya kidato cha kwanza,vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Sendeka ameonyesha Kukasirishwa na kitendo cha wanafunzi hao 708 waliofaulu kidato cha kwanza na kushindwa kujiunga na masomo.

Ametoa agizo hilo katika kikao cha tathimini ya elimu kilichowakutanisha halmashauri zote za mkoa huo na wadau wa elimu ambapo amesema ni jambo la kushangaza kuona wanafunzi wanagoma kuendelea na masomo wakati serikali imekuwa ikifanya jitihada kubwa kuboresha miundombinu ya elimu hivyo zoezi la kuwatafuta na kuwapeleka shule wanafunzi ambao hawajajiunga na kidato cha kwanza.

"Nichukue nafasi hii kuwaelekeza wakuu wangu wa wilaya,wakurugenzi watoto wote ambao hawajaripoti kidato cha kwanza,natoa mwezi mmoja kutoka leo,yeyote ambaye atakuwa hajaripoti baada ya hapo watendaji wa kata husika,maafisa elimu,viongozi wa vijiji husika wachukulieni hatua,simamieni ninyi wenyewe na maafisa elimu wenu"alisema Ole Sendeka

Akiweka bayana kuhusu idadi ya wanafunzi waliofaulu kidato cha kwanza, walioripoti na ambao hawajaripoti tangu januari 6 shule zilipofungua ,afisa elimu mkoa wa Njombe Gift Kyando anasema takribani wafunzi 15,711 walifauru lakini asilimia 84.7 pekee ndiyo walioripoti shule na kuitaja wilaya ya Ludewa kuwa na wanafunzi 200 ambao hawajaripoti.

"Kwanza lengo kubwa kwenye mkutano huu ilikuwa ni kuangalia wapi tumetoka na tukaolekea pamoja na mstakabali mzima wa elimu,hali ya kuripoti wananfunzi katika shule zetu waliomaliza mwaka 2019 na kujiunga kidato cha kwanza 2020 si mbaya sana lakini bado kuna wanafunzi ambao hawajaripoti na mpaka sasa ambao hawajaripoti ni 708"alisema Gift Kyando

Nao baadhi ya wadau wa elimu wakitoa mapendekezo ya kuboresha sekta ya elimu akiwemo Flaten Kwahison, Ewdin Mwanzinga na Joram Hongoli mbunge wa Lupembe wanasema ili mkoa uweze kupiga hatua inapaswa kuboresha mazingira ya kupokea na kutoa elimu ,nidhamu na umoja ambayo utekelezaji wake utafanyika kimkakati wa mda mfupi na mrefu.

Katika kikao hicho tuzo za fedha na vyeti zimetolewa kwa halmashauri na shule ambazo zimefanya vizuri kitaaluma. 


Share:

Raia wawili wa Afrika Kusini Nchini Japan wapata Corona

Watu wawili raia wa Afrika Kusini, wafanyakazi katika meli ya ‘Diamond Princess Cruise Ship’ wamekutwa na virusi vya Corona nchini Japan.

Hii ni kesi ya kwanza ya virusi vya Corona kwa wananchi wa Afrika Kusini ndani na nje ya nchi.

Alhamis Februari 27, rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa, alitangaza kuwarudisha nyumbani wananchi wote wa Afrika Kusini waliopo Wuhan, China, eneo mlipuko wa virusi hivyo ulipoanzia.

Huku virusi vya Corona vikiendelea kutapakaa sehemu mbalimbali duniani, kwa Afrika Nigeria wiki hii, imerekodi muathirika wa virusi vya Corona ambaye ni raia wa Italia.


Share:

43 Wafariki Kwa Virusi Vya CORONA Iran....Wananchi Watakiwa Kusalia Majumbani

Idadi ya waliokufa kutokana na maambukizi ya virusi vya Corona nchini Iran imefikia watu 43 na kuwa taifa la pili lenye idadi kubwa ya vifo nje ya China. 

Msemaji wa wizara ya Afya ya Iran amearifu kuwa watu 9 wamekufa kutokana na virusi hivyo katika muda wa saa 24 zilizopita na visa maambukizi vimepanda na kufikia watu 593. 

Serikali mjini Tehran imeamuru kufungwa kwa shule zote hadi siku ya Jumanne na kurefusha likizo ya vyuo vikuu pamoja na kupiga marufuku matamasha na shughuli za michezo kwa wiki moja. 

Maafisa kadhaa wa ngazi ya juu akiwamo makamu wa rais, naibu waziri wa afya na wabunge 5 wamethibitika kuambukizwa virusi hivyo na kuilazimisha serikali kulifunga bunge pamoja na kuweka marufuku ya kusafiri.


Share:

Askari wa Zimamoto Watakiwa Kuwa na Upendo Kwa Wananchi Wanaowahudumia

Na Bahati Mollel, TAA
Askari wa Zimamoto wa Kiwanja cha Ndege cha Mafia na cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) wametakiwa kuwa na upendo kwa wananchi wanaowahudumia wakati wa kufanya shughuli za kuzima moto na uokoaji katika majanga mbalimbali yanayoweza kutokea kwenye viwanja vya ndege.

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Kamishna wa Zimamoto na Uokoaji, ambaye pia ni Mkuu wa Chuo cha Jeshi hilo Kampasi ya Dar es Salaam na Chogo kilichopo Handeni Tanga, DCF Kennedy Komba wakati akifunga mafunzo ya siku tano ya kujengeana uwezo kwa Wazimamoto hao yaliyokuwa yakifanyika kwenye Jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TB3).

DCF Komba amesema anatarajia wahitimu hao wapatao 54 watatoa huduma bora katika vituo vyao vya kazi kutokana na kujengewa uwezo mkubwa, ambapo anatarajia siku moja jeshi hilo kupitia vituo vya viwanja vya ndege Tanzania, watatunukiwa cheti au tuzo ya heshima kutokana na kufanya kazi iliyotukuka.

“Kazi yenu ni ya wito mnatakiwa kuwa na upendo na watu mnaokwenda kuwahudumia wakati wa majanga, msitumie lugha mbaya na ni aibu kwa askari wakati wa maokozi wewe unaanza kumpekua mhanga na kuanza kumuibia labda simu au fedha alizokuwa nazo mifukoni, mnachotakiwa ni kuonesha upendo wa hali ya juu kuanzia mwanzo hadi mwisho wa zoezi la uokoaji,” amesema DCF Komba.

Pia aliwataka wahitimu hao kutunza afya zao kutokana na kazi yao inahitaji wawe askari hodari na shupavu, kwani akiwa mgonjwa hataweza kazi ya uokoaji wakati wa
majanga kwani inahitaji nguvu na akili nyingi.

“Hapa naona wahitimu wote ni vijana nawaambia wazi ukimwi unaua na ukimwi unadhoofisha mwili, hivyo mjitunze kwani ukiwa na afya mgogoro hautaweza kuhimili mikikimikiki ya kazi yetu, na wakuu wenzangu mnapokuwa na nafasi ya kukutana na askari msichoke kuwaeleza juu ya kutunza afya zao,” amesisitiza DCF Komba.

Halikadhalika amewataka wahitimu kuwa mabalozi wazuri maeneo wanayoishi kwa kuwa na vifaa vya zimamoto majumbani mwao ukiwemo mchanga mkavu unaowekwa kwenye ndoo na ‘Fire extinguisher’ pia kutoa maelekezo mbalimbali kwa wanaowazunguka endapo kutatokea janga la moto au uokoaji wa majanga mengine, ili kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na moto.

DCF Komba ameishukuru Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwa kufanikisha mafunzo hayo, na ameiomba isichoke kuwajengea uwezo askari hao ili
waweze kufanya kazi bora zaidi kwa manufaa ya taifa nzima la Tanzania.

Katika hatua nyingine DCF, amemshukuru Kamishna Msaidizi (Mstaafu), Christom Manyologa kwa kuwanoa askari hao na kumuomba kuendelea kufanya hivyo pindi
atakapohitajika wakati mwingine, pamoja na wastaafu wengine.

Kwa upande wake, Kamishna Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji kwa upande wa Viwanja vya Ndege Tanzania, ACP Bakari Mrisho alisisitiza askari kuwa na upendo na kuthamini kazi yao kwa kuwa viwanja vya ndege vinawategemea.

“Tuwe tayari kwa matukio na tuangalie mafunzo yanayolenga kazi yetu na sio kulazimisha mafunzo ambayo hayaendani na kazi yetu hii,” amesema ACP Mrisho.

Naye Mkufunzi ACP Manyologa amewataka washiriki kujiandaa wakati wote tayari kwa matukio, ambao alitoa mfano mwaka juzi katika kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) ilitua ndege kubwa ya A380 ya shirika la Emirates kwa dharura ambayo ina abiria zaidi ya 500 na inakiasi kikubwa cha mafuta na waliweza kuwa tayari kwa lolote ambalo lingeweza kutokea na ndege ilitua na kuondoka salama.


Share:

RAIS SHEIN : UCHAGUZI WA ZANZIBAR UTAKUWA HURU NA WA HAKI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein amewahakikishia Wazanzibar kuwa uchaguzi mkuu utakuwa huru na wa haki huku akithibitisha kuwa hakuna Mzanzibar atakayekosa haki yake ya kupiga kura.


Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Ikulu ya Zanzibar, Dk. Shein aliyasema hayo katika mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya kuhakiki taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpigakura katika kituo cha kupigia kura cha skuli ya Msingi Bungi, Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema pia kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ni huru ambayo imekuwepo muda mrefu tokea kuanzishwa uchaguzi Zanzibar.

Dk. Shein alisema tume hiyo imekuwa ikifanya vizuri  kutokana na kuendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ikiwa ni pamoja na kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.

Alisema licha ya kuwapo kwa mabadiliko ya uongozi kwa kila ufikapo muda uliowekwa, lakini bado tume hiyo ipo vizuri na haijatetereka.

Dk. Shein alisema anaamini tume hiyo itafanya vizuri sana katika Uchaguzi Mkuu ujao kwani tokea alipoingia madarakani mwaka 2010, imekuwa ikifanya vizuri.

Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi waliokuwa hawajapatiwa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi kuwa na subira kwani ni haki ya kila mwananchi wa Zanzibar.

Akiwa amefuatana na mkewe  Mwanamwema Shein, alisema kitambulisho cha Mzanzibari mkaazi kina umuhimu kwa mwananchi wa Zanzibar kutokana na kusaidia katika shughuli mbalimbali na si kutumia kwa uchaguzi pekee.

Aliwataka wananchi wasiwe na wasiwasi kwani Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar itachukua jukumu lake la kuhakikisha kila mwenye sifa ya kupata kitambulisho hicho anakipata kwa taratibu na sheria zilizopo.

Aidha alieleza kuwa uhakiki unakwenda vizuri kutokana na muda na taratibu zilizowekwa ambazo zimekuwa zikiwasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi kuweza kuhakiki taarifa zao kwa ufanisi mkubwa pale wanapofika vituoni.

Alieleza kuwa kazi zote zina changamoto na hasa zile zinazowahusu watu wengi sambamba na kuwepo kwa utaalamu mpya, hivyo aliwataka wananchi waendelee kuwa wastahamilivu na bila ya kukiuka sheria na kuwahakikishia kuwa kila mwenye haki yake ya kupata Kitambulisho cha Mzanzibari mkaazi atakipata.

“Zoezi linakwenda vizuri, nimetumia muda mfupi na wasimamizi na waandishi wanafanya kazi zao vizuri,” alisema Dk. Shein.


Share:

MBWANA SAMATTA APANIA KUWEKA HISTORIA LEO UWANJA WA WEMBLEY


Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Mbwana Samatta, ambaye anakipiga katika klabu ya Aston Villa inayoshiriki Ligi Kuu nchini England, leo atakuwa kwenye Uwanja wa Wembley kukipiga dhidi ya Manchester City.

Samatta ataongoza safu ya ushambuliaji ya Aston Villa kwenye mchezo wa fainali ya Kombe la Carabao dhidi ya mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu nchini England.

Hii ni mara ya kwanza kwa mchezaji wa kitanzania kucheza michuano hiyo ya Carabao pamoja na kucheza fainali kwenye uwanja huo wenye historia kubwa nchini England.

Samatta alijiunga na Aston Villa wakati wa uhamisho wa dirisha dogo la usajili la Januari mwaka huu akitokea katika klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji baada ya kuonesha kiwango cha hali ya juu kwa kipindi cha misimu minne.

Hadi sasa tangu asajiliwe, amefanikiwa kucheza jumla ya michezo mitatu ya Ligi Kuu nchini Uingereza na kufanikiwa kupachika bao moja kwenye mchezo dhidi ya Bournemouth, huku Aston Villa wakipigwa mabao 2-1.

Samatta amedai kucheza kwenye Uwanja wa Wembley dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England kwake ni kama ndoto, hivyo lazima apambane ili kuiandikia historia klabu yake na yeye mwenyewe kwa ujumla.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili March 1















Share:

Saturday 29 February 2020

Mamlaka Ya Udhibiti Na Usimamizi Wa Bima Nchini[TIRA ] Yatoa Mafunzo Kwa Wanahabari Umuhimu Wa Bima Katika Jamii


Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa bima nchini [TIRA]imetoa Mafunzoya kuwajengea uwezo Wanahabari umuhimu wa bima katika jamii  kwani ni moja ya suluhisho kwa Majanga  .


Akiwasilisha mada mbalimbali katika Mafunzo hayo jijini Dodoma,Mkurugenzi wa kuendeleza soko la bima na utafiti ,mamlaka ya Usimamizi wa bima Tanzania,Bi,Adelande  Muganyizi amesema bima husaidia kupunguza maumivu ya majanga mbalimbali ikiwa  ni pamoja na majanga ya moto,ajali,ukame,na mafuriko hivyo wanahabari wanatakiwa kuwa mabalozi wazuri  katika kuelimisha jamii umuhimu wa bima kwani huondoa umasikini.


“Majanga hayabigi hodi lakini bima inasaidia kupunguza sana maumivu yaliyotokana na majanga ,hivyo  tunatakiwa tuelewe sana haki ya usalama katika mali zetu pindi tunapokumbwa na majanga kwa hiyo tunapoongelea suala la bima ni usalama wa afya,Usalama wa mali zetu”amesema.


Aidha,Bi.Muganyizi ameanisha kanuni za msingi za  mkataba wa bima ni pamoja na kuwepo na uhusiano unaotambulika kisheria[Insurable interest],uaminifu wa hali ya juu[ultmost  faith], kumrejeshea mkata bima thamani halisi kabla ya janga kutokea pamoja na kuchangia hasara endapo mali moja imechangiwa na makampuni ya bima zaidi ya moja.


Akizungumzia kuhusu bima ya lazima,Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa bima[TIRA]kanda ya kati Stella Rutaguza amesema kwenye magari ya usafiri wa umma kila abiria aliyebebwa anatakiwa awe amekatiwa bima.


“Tukija kwenye suala hili naona kama kuna changamoto kidogo ,lakini kuhusu bima ya lazima inatakiwa kila abiria aliyebebwa kwenye gari la usafiri wa umma awe amekatiwa bima na mwenye jukumu hilo ni mmiliki wa gari husika,kama gari lako lina uwezo wa kibeba abiria 55 na sheria inataka hivyo hivyo ukate bima ya watu wa idadi kama hiyo”amesema .
Pia,Rutaguza amesema moja ya kanuni kubwa  ya bima ni kuwa hairuhusiwi kuikatia bima mali isiyokuwa ya kwako hata kama ni ya ndugu  huku akitaja aina mbalimbali za bima zikiwa ni pamoja na bima za kilimo,bima za ndoa,bima za dhima za umma ,bima za makosa ya kitaaluma ,bima za wizi ,bima za waajiriwa  ,bima za maisha,bima za elimu  na bima za vifo.


Meneja usimamizi wa Maendeleo ya Masoko ,Kutoka Mamlaka ya Usimamizi na udhibiti wa bima Tanzania[TIRA]Bw.Edgar Shao amesema TIRA ina jukumu la kusajili kampuni za bima pamoja na kutoa elimu kwa wananchi


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger