Sunday 23 February 2020

Mwanajeshi Mwingine wa Uturuki Auawa Kwa Bomu Na Vikosi Vya Syria Vinavyoungwa Mkono na Urusi

Askari mwingine wa Uturuki ameuawa kwenye shambulio la bomu katika mkoa wa Idlib. 

Huyo ni askari wa 16 kuuawa kwenye mashambulio yanayofanywa na vikosi vya Syria vinavyoungwa mkono na Urusi. 

Wizara ya ulinzi ya Uturuki imesema mauaji hayo yametokea wakati ambapo mazungumzo ya kusitisha mapigano baina ya Ankara na Moscow yamekwama. 

Kuongezeka kwa vifo vya wanajeshi wa Uturuki, kunaweza kuondoa uwezekano wa kupatikana suluhu ya kusitisha mapigano katika eneo la Kaskazini magharibi mwa Syria. 

Tangu mapema mwezi Desemba, raia karibu milioni moja wa Syria wengi wao ni wanawake na watoto hawana makaazi na hasa katika kipindi hiki cha baridi kutokana na mapigano. 

Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan anatarajia kukutana na viongozi wenzake wa Urusi, Ujerumani na Ufaransa Machi 5 kwa ajili ya kuuzungumzia mkoa wa Idlib.

Baada ya syria kukumbwa na vita kwa miaka tisa sasa, vikosi vya serikali ya Syria vinapambana kulidhibiti eneo hilo la mwisho linaloshikiliwa na waasi.


Share:

Kigwangalla Amuomba Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo Awasamehe Waliosambaza Picha za Uharibifu wa Barabara Hifadhi ya Ngorongoro

Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania, Dk Hamis Kigwangalla amewaombea msamaha waongoza utalii ambao walisambaza video kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha uharibifu wa barabara kwenye Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.

Kupitia akaunti yake ya twitter, Dk Kigwangalla ameandika kuwa amemuomba Mkuu wa mkoa wa Arusha Nchini Tanzania, Mrisho Gambo na kamati ya ulinzi kuwasamehe na kuchukulia hilo kama onyo.

Kigwangalla amesema kwa kuwa ni tukio la kwanza, amempongeza Gambo kuingilia kati suala hilo ambalo ameeleza linalinda hadhi ya nchi.
 
Amesema ni vema taarifa kama hizo wawe wanazifikisha mahala husika ili zipatiwe ufumbuzi na ikishindikana afikishiwe Waziri moja kwa moja.

“Ni vema taarifa za changamoto zikafikishwa kwetu kwa njia sahihi. Kama mtu hawapati watu wetu wa huko chini, mimi napatikana kila kona, sijajifungia kwenye selo na sijabadili namba zangu! Nipe taarifa zako na nakuhakikishia nitachukua hatua stahiki na kwa wakati,” ameandika Kigwangalla.

“Huwa sipuuzi taarifa wala ushauri na siangalii umetoka kwa nani. Nafanyia kazi kila kitu. Na ndiyo maana hata majangili tunawakamata kila siku. Kweli tuna uhuru wa kusema na kufanya lolote, lakini tuutumie vizuri kwa maslahi mapana ya Taifa letu. Hii ni nchi yetu sote, tuilinde, tuipende, tuijenge, tuifaidi,” ameandika.


Share:

Serikali Yajipanga Kutokomeza Magonjwa Ya Mifugo Nchini.

Na. Edward Kondela
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema serikali itahakikisha inaendelea kutoa dawa za ruzuku za kuogeshea mifugo nchini ikiwa na lengo la kutokomeza kabisa magonjwa ya mifugo.

Naibu Waziri Ulega amesema hayo (22.02.2020) wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika mnada wa mifugo wa Ndelema uliopo katika Halmashauri ya Mji wa Handeni Mkoani Tanga ambapo amewataka wafugaji kutoacha kuosha mifugo yao kwani kwa kufanya hivyo mifugo itakuwa na afya njema na hatimaye kupata bei nzuri ya soko.

“Mwaka jana tulipata pesa kutoka kwa mheshimiwa rais zaidi ya Shilingi Milioni 300 kwa ajili ya kununua dawa na kugawa kwa majosho 1,400 nchi nzima, mwaka huu wametuongeza tumepata zaidi ya Shilingi Milioni 400 kwa ajili ya kununua dawa na kusambaza katika majosho 1,700 tutaendelea na zoezi hilo la kutoa dawa za ruzuku bila kuacha ili kuhakikisha tunapiga kabisa vita magonjwa ya mifugo.” Amesema Mhe. Ulega

Aidha kuhusu wafugaji wa Wilaya ya Handeni kuingiza mifugo yao katika misitu ya serikali Naibu Waziri Ulega akizungumza moja kwa moja kwa njia ya simu katika mkutano huo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo amemtaka kuweka alama katika misitu hiyo ili wafugaji waweze kutambua misitu ya serikali na kutoingiza mifugo yao kwa bila kukusudia.

Prof. Silayo amemuahidi Naibu Waziri Ulega katika mkutano huo kuwa atawatuma wataalamu siku ya Jumatatu ili kuanza utekelezaji huo mara moja na kuondoa migogoro ya wafugaji kuingiza mifugo yao katika misitu ya serikali.

Katika mkutano huo pia naibu waziri huyo ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Handeni kuhakikisha unatua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wafugaji na wafanyabiashara wa mifugo ikiwemo ya miundombinu katika mnada huo pamoja na barabara ili waweze kusafirisha mifugo yao kwa urahisi zaidi.

Nao baadhi ya wafugaji waliopatiwa nafasi kuuliza maswali na kutoa maoni yao juu ya sekta ya mifugo, wameipongeza serikali kwa namna ambavyo imekuwa ikihakikisha inawaboreshea mazingira ya shughuli zao huku wakiomba wazidi kupatiwa elimu zaidi ya masuala mbalimbali ili wafanye shughuli zao bila kukiuka sheria za nchi.

Awali akitembelea bwawa la asili katika Kijiji cha Kweingoma kilichopo Wilaya ya Handeni Vijijini Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewataka wananchi wanaofanya shughuli za uvuvi katika bwawa hilo lenye urefu wa Kilometa Nne kujiunga katika ushirika ili serikali iweze kuwasaidia katika maeneo mbalimbali huku akiahidi kutoa mashine kwa ajili ya mtumbwi utakaotengenezwa na uongozi wa wilaya hiyo ili kurahisisha shughuli za uvuvi.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amemaliza ziara ya kikazi ya siku tatu Mkoani Tanga ambapo amepita pia katika Wilaya za Muheza, Pangani, Mkinga na Halmashauri ya Jiji la Tanga na kuzungumza na wafugaji na wavuvi ili kufahamu changamoto wanazokabiliana nazo.


Share:

Utatuzi Migogoro Ya Ardhi Dar Es Salaam Wamfikisha Lukuvi Saa Nne Usiku

Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amepongezwa na wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kwa uamuzi wake wa kukutana nao na kutatua migogoro ya ardhi 628 katika mkoa huo katika kipindi cha siku tano kupitia progaramu ya Funguka kwa Waziri hadi saa nne usiku.

Lukuvi alihitimisha programu ya Funguka kwa Waziri kwa kukutana na wananchi wa Manispaa ya Kinondoni jana tarehe 22 Februari kwa kusikiliza na kutatua kero, malalamiko na migogoro mia tatu (300) iliyomfikisha saa 4:22 usiku.

Awali, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alikutana na wananchi wa Manispaa za Ilala ambapo alishughulikia migogoro 122, Ubungo 75, Kigamboni migogoro 65 na Manispaa ya Temeke migogoro 66 na kufanya jumla ya migogoro aliyoishughulikia kwa siku zote tano kufikia 628.

Kati ya Wananchi aliokutana nao tangu kuanza kwa program hiyo siku ya jumanne tarehe 18 Februari 2020, Manispaa ya Kinondoni ilioonekana kuwa na idadi kubwa ya wananchi wenye malalamiko ya ardhi ukilinganisha na Manispaa nyingine za mkoa wa Dar es Salaam.

Baadhi ya Wananchi waliokutana na Waziri Lukuvi walionesha kufurahishwa na utaratibu wa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kukutana na wananchi kwa nia ya kupata suluhu ya migogoro ya ardhi iliyoelezwa kuwa imekuwa ikiwahangaisha kwa muda mrefu bila mafanikio.

Raphael Ngowi mkazi wa Kinondoni ambaye malalamiko yake ni kuhusiana na kiwanja chake kumilikishwa kwa watu wawili alisema, utaratibu wa Waziri wa Ardhi kukutana moja kwa moja na wananchi unamsaidia kupata mambo mengi kutoka kwa mhusika badala ya kusikia kutoka kwa watendaji.

Alisema, utaratibu huo siyo tu unasaidia wananchi wenye matatizo ama kudhulumiwa haki zao katika sekta ya ardhi bali unatoa pia fursa kwa Waziri mwenye dhamana ya ardhi kubainia uzembe wa baadhi ya watendaji wake katika maeneo yenye migogoro.

Kwa mujibu wa Ngowi, kati ya Mawaziri wa Serikali ya awamu ya tano, Lukuvi amevunja rekodi kwa kuweza kutatua matatizo ya wananchi kwa kukutana nao ana kwa ana jambo alilolieleza kuwa limeasisiwa na Mwl. Nyerere kwa kuweka uwazi wa kushugulikia kero.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya wenye Mashamba eneo la Mabwepande katika manispaa ya Kinondoni Seif Maungu anayewakilisha wananchi 258 walio katika mgogoro wa kuvamiwa eneo lao alisema, baada ya kuonana na Waziri Lukuvi sasa wamepata faraja kubwa baada ya mateso ya takriban miaka 13.

‘’Kwa muda mrefu tulikuwa hatupati majibu kuhusiana na mgogoro wa maeneo yetu lakini sasa baada ya kukutana na mhe. Lukuvi tumepata faraja na Rais Magufuli amepata jembe’’ alisema Maungu.

Mkazi mwingine wa Magomeni aliyejitambulisha kwa jina la Rashid Maulid Kinyogoli aliyewasilisha tatizo lake la kutopata Hati ya Ardhi, aliilezea program ya Funguka kwa Waziri kuwa ni mwarobaini wa matatizo ya ardhi yanayosababishwa na watendaji wa sekta ya ardhi wasiokuwa waaminifu.

‘’Utaratibu wa Funguka kwa Waziri uliaonzishwa na Lukuvi kwa kusikiliza kero na malalamiko ya wananchi ungekuwa ukifanywa na viongozi wengine kupitia sekta zao basi matatizo yangepungua na hivyo kumrahisishia kazi Rais John Pombe Magufuli ya kuleta maendeleo’’ Alisema Kinyogoli.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amekuwa na utaratibu wa kukutana na wananchi wenye malalamiko na kero za ardhi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi kwa nia ya kutafuta suluhu ya migogoro ya ardhi ambapo tayari program hiyo imeshafanyika mikoa mbalimbali ikiwemo Kilimanjaro, Tanga, Rukwa, Mbeya, Iringa, Tabora, Kigoma, Kagera, Katavi na Lindi na kuleta mafanikio makubwa.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili February 23













Share:

Saturday 22 February 2020

Picha : HOTELI YA KISASA 'SAM COMFORT' YAFUNGULIWA RASMI SHINYANGA MJINI



Hoteli ya Kisasa iitwayo ‘Sam Comfort’ iliyopo katika Mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga imefunguliwa rasmi leo Jumamosi Februari 22,2020.



Uzinduzi wa Hoteli hiyo ya Kisasa umehudhuriwa na wadau mbalimbali mjini Shinyanga.

Akizungumza kwa niaba ya Mmiliki wa Hoteli 'Sam Comfort' Samwel Mabala, Humphrey Godfrey Katege amesema Samwel ni mzawa wa Shinyanga amethubutu kuwekeza mkoani Shinyanga na anawaomba wadau wa ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kumuunga mkono.

“Nawashukuru wote mliofika hapa kutuunga mkono,naamini kuanzishwa kwa Hoteli hii ya kisasa ni sehemu ya kuchangia shughuli za maendeleo katika mkoa wetu wa Shinyanga na taifa kwa ujumla”,amesema Katege.

Naye Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe amesema miongoni mwa huduma zinazopatikani hotelini hapo ni vyumba vya kulala, chakula na vinywaji mbalimbali.

“Leo tumezindua rasmi Hoteli hii ambayo inapatikana katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi. Tunawakaribisha wateja wote kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga,huduma zetu ni nzuri kwa gharama nafuu ambayo ni rafiki kwa kila mtu”,amesema Chief Ng’ombe.

“Sam Comfort imejengwa na ndugu Samwel Mabala mkazi wa Shinyanga,Kijana huyu kwa muda mrefu amekuwa akipanga kujenga Hoteli na amejisikia faraja kubwa kuwekeza katika mkoa wa Shinyanga. Tunawakaribisha kwa moyo mkunjufu kabisa,naomba mjisikie mpo nyumbani”,ameongeza Chief Ng’ombe.

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa mtaa wa Dome,Solomoni Nalinga Najulwa amempongeza mmiliki wa hoteli ya Sam Comfort kujenga hoteli ya Kisasa katika mtaa wake kwani ameonesha uzalendo wa hali ya juu na ameahidi kumuunga mkono.

Wasiliana na wahusika wa Hoteli ya ‘Sam Comfort’ kwa simu namba 0747874636
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mwenyekiti wa mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Solomoni Nalinga Najulwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Hoteli ya ‘Sam Comfort’  usiku wa Jumamosi Februari 22,2020 ambapo amempongeza mmiliki wa hoteli ya Sam Comfort kujenga hoteli ya Kisasa katika mtaa wake. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe akiwakaribisha wateja wote kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kufika katika hoteli ya Sam Comfort kupata huduma ya vyumba vya kulala,vyakula na vinywaji kwa gharama nafuu ambayo ni rafiki kwa kila mtu.
 Humphrey Godfrey Katege akizungumza kwa niaba ya Mmiliki wa Hoteli ya Sam Comfort Samwel Mabala ambapo amesema Samwel amethubutu kuwekeza mkoani Shinyanga na kuomba wadau ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kumuunga mkono.
Wadau mbalimbali waliohudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Wadau mbalimbali waliohudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Meneja wa Sam Comfort, Jackson Wilson akielezea huduma zinazopatikana katika hoteli yao ambazo ni pamoja na vinywaji,vyakula na vyumba vya kulala vyenye, Tv, maji ya moto na ya baridi.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Bango linaloelekeza ilipo Hoteli ‘ Sam Comfort’.
Muonekano wa sehemu ya mapokezi Sam Comfort.
Muokano wa sehemu ya chumba katika hoteli 'Sam Comfort'
Muonekano wa sehemu ya choo/bafu katika hoteli 'Sam Comfort'.
Muonekano wa sehemu ya chumba katika hoteli ya Sam Comfort.
Muonekano wa sehemu ya Vinywaji katika hoteli 'Sam Comfort'.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Sam Comfort.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala na Mkurugenzi wa La Prince, Athanas William wakijiandaa kufungua Shampen wakati wa ufunguzi wa Sam Comfort'.
Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala akigonga Cheers na viongozi wa Sam Comfort na wadau waliojitokeza kwenye uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala akigawa vinywaji.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Kulia ni Mmiliki wa Sam Comfort, Samwel Mabala akiwa ameshikilia kinywaji wakati wa zoezi la kugonga Cheers.
Wadau na viongozi wa Sam Comfort wakifurahia jambo.
Zoezi la kugonga cheers likiendelea.
Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa mtaa wa Mageuzi Derick Elias akifuatiwa na Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe na Mmiliki wa Sam Comfort, Samwel Mabala (kulia) wakicheza muziki wakati wa ufunguzi wa Sam Comfort.
Kulia ni MC Seki akieleza jambo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lulekia, Ansila Benedict akizungumza wakati wa uzinduzi wa Sam Comfort.
Mkurugenzi wa Hoteli ya Liga, Moris akizungumza wakati wa uzinduzi wa Sam Comfort.
MC Seki akitoa maelekezo mbalimbali wakati wa Uzinduzi wa Hoteli ‘Sam Comfort’.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Sam Comfort.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger