Saturday 22 February 2020

Picha : HOTELI YA KISASA 'SAM COMFORT' YAFUNGULIWA RASMI SHINYANGA MJINI

...


Hoteli ya Kisasa iitwayo ‘Sam Comfort’ iliyopo katika Mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga imefunguliwa rasmi leo Jumamosi Februari 22,2020.



Uzinduzi wa Hoteli hiyo ya Kisasa umehudhuriwa na wadau mbalimbali mjini Shinyanga.

Akizungumza kwa niaba ya Mmiliki wa Hoteli 'Sam Comfort' Samwel Mabala, Humphrey Godfrey Katege amesema Samwel ni mzawa wa Shinyanga amethubutu kuwekeza mkoani Shinyanga na anawaomba wadau wa ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kumuunga mkono.

“Nawashukuru wote mliofika hapa kutuunga mkono,naamini kuanzishwa kwa Hoteli hii ya kisasa ni sehemu ya kuchangia shughuli za maendeleo katika mkoa wetu wa Shinyanga na taifa kwa ujumla”,amesema Katege.

Naye Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe amesema miongoni mwa huduma zinazopatikani hotelini hapo ni vyumba vya kulala, chakula na vinywaji mbalimbali.

“Leo tumezindua rasmi Hoteli hii ambayo inapatikana katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi. Tunawakaribisha wateja wote kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga,huduma zetu ni nzuri kwa gharama nafuu ambayo ni rafiki kwa kila mtu”,amesema Chief Ng’ombe.

“Sam Comfort imejengwa na ndugu Samwel Mabala mkazi wa Shinyanga,Kijana huyu kwa muda mrefu amekuwa akipanga kujenga Hoteli na amejisikia faraja kubwa kuwekeza katika mkoa wa Shinyanga. Tunawakaribisha kwa moyo mkunjufu kabisa,naomba mjisikie mpo nyumbani”,ameongeza Chief Ng’ombe.

Kwa upande wake,Mwenyekiti wa mtaa wa Dome,Solomoni Nalinga Najulwa amempongeza mmiliki wa hoteli ya Sam Comfort kujenga hoteli ya Kisasa katika mtaa wake kwani ameonesha uzalendo wa hali ya juu na ameahidi kumuunga mkono.

Wasiliana na wahusika wa Hoteli ya ‘Sam Comfort’ kwa simu namba 0747874636
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mwenyekiti wa mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Solomoni Nalinga Najulwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Hoteli ya ‘Sam Comfort’  usiku wa Jumamosi Februari 22,2020 ambapo amempongeza mmiliki wa hoteli ya Sam Comfort kujenga hoteli ya Kisasa katika mtaa wake. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe akiwakaribisha wateja wote kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kufika katika hoteli ya Sam Comfort kupata huduma ya vyumba vya kulala,vyakula na vinywaji kwa gharama nafuu ambayo ni rafiki kwa kila mtu.
 Humphrey Godfrey Katege akizungumza kwa niaba ya Mmiliki wa Hoteli ya Sam Comfort Samwel Mabala ambapo amesema Samwel amethubutu kuwekeza mkoani Shinyanga na kuomba wadau ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga kumuunga mkono.
Wadau mbalimbali waliohudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Wadau mbalimbali waliohudhuria hafla fupi ya uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Meneja wa Sam Comfort, Jackson Wilson akielezea huduma zinazopatikana katika hoteli yao ambazo ni pamoja na vinywaji,vyakula na vyumba vya kulala vyenye, Tv, maji ya moto na ya baridi.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya Hoteli ‘ Sam Comfort’ iliyopo katika mtaa wa Dome kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Bango linaloelekeza ilipo Hoteli ‘ Sam Comfort’.
Muonekano wa sehemu ya mapokezi Sam Comfort.
Muokano wa sehemu ya chumba katika hoteli 'Sam Comfort'
Muonekano wa sehemu ya choo/bafu katika hoteli 'Sam Comfort'.
Muonekano wa sehemu ya chumba katika hoteli ya Sam Comfort.
Muonekano wa sehemu ya Vinywaji katika hoteli 'Sam Comfort'.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Sam Comfort.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala na Mkurugenzi wa La Prince, Athanas William wakijiandaa kufungua Shampen wakati wa ufunguzi wa Sam Comfort'.
Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala akigonga Cheers na viongozi wa Sam Comfort na wadau waliojitokeza kwenye uzinduzi wa Hoteli 'Sam Comfort'.
Mkurugenzi wa Crown Pub,Musa Jonas Ngangala akigawa vinywaji.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Zoezi la kugonga Cheers likiendelea.
Kulia ni Mmiliki wa Sam Comfort, Samwel Mabala akiwa ameshikilia kinywaji wakati wa zoezi la kugonga Cheers.
Wadau na viongozi wa Sam Comfort wakifurahia jambo.
Zoezi la kugonga cheers likiendelea.
Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa mtaa wa Mageuzi Derick Elias akifuatiwa na Mjomba wa mmiliki wa Hoteli, Chief Thomas Ng’ombe na Mmiliki wa Sam Comfort, Samwel Mabala (kulia) wakicheza muziki wakati wa ufunguzi wa Sam Comfort.
Kulia ni MC Seki akieleza jambo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lulekia, Ansila Benedict akizungumza wakati wa uzinduzi wa Sam Comfort.
Mkurugenzi wa Hoteli ya Liga, Moris akizungumza wakati wa uzinduzi wa Sam Comfort.
MC Seki akitoa maelekezo mbalimbali wakati wa Uzinduzi wa Hoteli ‘Sam Comfort’.
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Sam Comfort.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger