Friday 28 February 2020

NATO Kukutana Kwa Dharura Leo Baada ya Wanajeshi 33 wa Uturuki Kuuawa Syria

...
Baraza la kiutawala la Jumuia ya Kujihami ya NATO linakutana leo katika kikao cha dharura kuhusu mzozo wa Syria, baada ya wanajeshi wapatao 33 wa Uturuki kuuawa katika shambulizi la anga huku wengine wengi wakijeruhiwa vibaya..

Baraza hilo ambalo linawajumuisha mabalozi wa nchi zote 29 za NATO wanakutana baada ya Uturuki kuomba mazungumzo yafanyike chini ya kifungu cha 4 cha Mkataba wa NATO, kuhusu hali ya Syria. 

Kulingana na kifungu hicho, mwanachama yeyote wa NATO anaweza kuomba mazungumzo yafanyike iwapo ataamini kuwa kuna kitisho katika uhuru wake wa kisiasa au usalama. 

Katibu Mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg ametoa wito wa mapigano kusitishwa na amelaani mashambulizi ya anga katika mazungumzo yake kwa njia ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mevlut Cavusoglu.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger