Friday 28 February 2020

Makamu wa rais wa Iran athibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona

...
Makamu wa Rais wa Iran anayeshughulikia mambo ya wanawake na familia Bibi Masoumeh Ebtekar jana amethibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona.

Mapema jana mwenyekiti wa kamati ya usalama wa taifa na sera za kidiplomasia wa Iran Bw. Mojtaba Zonnour, ambaye pia amethibitishwa kuambukizwa virusi, ametoa wito kwa raia wa Iran wawe watulivu na kusema, nchi yao ina uwezo wa kushinda mapambano dhidi ya virusi hivyo.

Habari zinasema, ibada ya sala ya ijumaa mjini Tehran imefutwa kutokana na mlipuko wa virusi hivyo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger