Thursday 27 February 2020

Misri Yamzika Hosni Mubarak kwa heshima za kijeshi....Alikuwa Rais wa Nchi Hiyo Kwa Miongo Mitatu Kabla ya Kupinduliwa

...
Misri imefanya mazishi ya heshima za kijeshi ya aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak, ambaye aliitawala nchi hiyo kwa miongo mitatu kabla ya kuondolewa katika mwaka wa 2011 kupitia wimbi la vuguvugu la mageuzi katika ulimwengu wa Kiarabu. 

Hafla hiyo ya mazishi, ilihusisha kufyatuliwa mizinga na jeneza lake kubebwa kwenye msafara wa farasi kuashiria mafanikio ya Mubarak ya enzi ya vita. 

Rais wa sasa wa Misri Abdel Fatah al-Sissi, alihudhuria kwa muda mfupi, na kutoa salamu zake ra rambirambi kwa kupeana mkono na watoto wawili wa Mubarak, Alaa na Gamal na mkewe Suzanne. 

Soma na hii: Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak Afariki Dunia
Mwili wa Mubarak umezikwa kwenye eneo la makaburi ya familia yake la Heliopolis viungani mwa mji mkuu wa Cairo


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger