Wednesday 26 February 2020

IGP Sirro Ataka Wazazi Waimarishe Malezi Kwa Watoto Ili Kuwa na Jamii Inayochukia Uhalifu

...
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro ametoa wito kwa jamii hasa wazazi nchini kuhakikisha wanaimarisha malezi ya watoto wao, jambo litalalosaidia kuwa na jamii itakayochukia uhalifu.

IGP Sirro ametoa wito huo mkoani Dodoma wakati akizungumza na baadhi ya Wakazi wa eneo la Mbande, baada ya kukagua ujenzi wa kituo cha polisi katika eneo hilo.

Amewashauri wazazi wote nchini kuendelea kuwasomesha watoto wao na kutowaacha wajiingize kwenye vitendo vya uhalifu.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger