Friday 29 November 2019

Strategic Information Specialist Job at ICAP Tanzania

Strategic Information Specialist Job Opportunity at ICAP Tanzania, Deadline 15 December 2019 Strategic Information (SI) Specialist, Tanzania Job no: 492301 Work type: Regular Full-Time Location: Tanzania – Dar es Salam, Tanzania – Kagera, Tanzania – Kigoma, Tanzania – Mara, Tanzania – Mwanza, Tanzania – Pwani, Tanzania – Tanga Categories: Strategic Information/Surveillance/Monitoring & Evaluation ICAP at Columbia University, a… Read More »

The post Strategic Information Specialist Job at ICAP Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Clinical Officer Jobs at Médecins Sans Frontières

Clinical Officer Job Opportunity at Médecins Sans Frontières, Deadline 6 December 2019 Position: CLINICAL OFFICER (Nduta Camp) Job Summary Médecins Sans Frontières (MSF) is an international, independent, medical humanitarian organisation that delivers emergency aid to people affected by armed conflict, epidemics, natural disasters and exclusion from healthcare. MSF offers assistance to people based on need, irrespective of race,… Read More »

The post Clinical Officer Jobs at Médecins Sans Frontières appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DPP Afuta Kesi 59 Zaidi Jijini Mbeya

Katika mwendelezo wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Balozi Dkt Augustine Mahiga (Mb) kwenye mikoa ya kusini, Mkurugenzi Mkuu wa Mashitaka Tanzania (DPP) Biswalo Mganga amefuta jumla ya kesi 59 katika mahakama za Mkoa wa Mbeya.

Mkurugenzi Biswalo ameyafanya hayo katika gereza la Ruanda mjini Mbeya na gereza la Tukuyu Wilaya ya Rungwe alipoambatana na Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Mahiga ili kujionea hali halisi ya mazingira ya utoaji haki jinai katika magereza hayo na taasisi mbalimbali za haki jinai ikiwemo Ofisi ya Taifa ya Mashitaka, Polisi, Mahakama na Magereza yenyewe.

“Niliowafutia Kesi nendeni mkawe raia wema, msirudie makosa, badala yake mkawe mabalozi wema mtakaofanya kazi kwa bidii ili kumuunga mkono Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Joseph Maguli katika kauli yake ya hapa kazi tu.”

Kwa upande wake Waziri mwenye dhamana ya Katiba na Sheria Balozi Dkt Augustine Mahiga (Mb) aliwataka wote waliofutiwa mashitaka kwenda kufurahi na familia zao huku wakimshukuru Mungu na kujutia makosa yaliyosababisha kushitakiwa kwao. Aidha, aliwaonya kutokurudia makosa hayo badala yake watumie nguvu na akili walizonazo kuzalisha mali kwa maendeleo yao na familia zao pamoja na kukuza uchumi wa Taifa.

“Mliosamehewa leo nendeni mkafurahi na familia zenu sambamba na kuwa watu wema katika jamii inayowazunguka kwani ni matumaini yangu kuwa mmejifunza mengi na mmebadilika. Kuna watu hapa nikiwatizama misuli yao, walipaswa wakaitumie kufanya kazi na kuzalisha mali kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla badala ya kuitumia kufanya uhalifu.”

Kwa mujibu wa kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, sura ya 20 kama ilivyofanyiwa marejeo 2002, Mkurugenzi Mkuu wa Mashitaka anayo mamlaka ya kuwafutia mashitaka watuhumiwa wa makosa ya jinai katika magereza mbalimbali nchini. Mpaka sasa katika ziara hii ya kikazi ya Waziri wa Katiba na Sheria katika mikoa mitatu DPP Biswalo ameshafuta  jumla ya kesi 120 na bado ziara inaendelea katika Wilaya ya Kyela na baadae mkoa wa Njombe.


Share:

KAIMU DC MUHEZA KIJAZI ATOA WIKI MOJA KWA MAAFISA KILIMO KUSHUGHULIKIA JANGA LINALOATHIRI PILIPILI MANGA MUHEZA

 KAIMU Mkuu wa wilaya ya Muheza Ally Kijazi ambaye pia ni Afisa Tarafa ya Bwembwera wilayani humo akizungumza mara baada ya kufungua Jukwaa hilo la viungo
 Afisa Kilimo wilaya ya Muheza Hayange Mbwambo  akizungumza wakati wa Jukwaa hilo 
 MENEJA wa Benki ya CRDB wilayani Muheza Shija akizungumza wakati wa Jukwaa hilo
 Mkulima wa Iliki Kata ya Zirai Ally Zubeya akichangia jambo kwenye Jukwaa hilo


 AFISA Kilimo Idrisa Kijazi akieleza jambo wakati wa Jukwaa hilo 
 MDAU wa  mazao ya viungo wilayani Muheza kutoka Baraza la Biashara za Uholanzi na Afrik akielezea uzoefu wao kwenye Jukwaa hilo
 Sehemu ya wakulima wa mazao ya viungo wilayani Muheza wakiwa kwenye kikao hicho
 Sehemu ya wakulima wa mazao ya viungo wilayani Muheza wakiwa kwenye kikao hicho


KAIMU Mkuu wa wilaya ya Muheza Ally Kijazi amewaagiza maafisa kilimo na watendaji wa Kata wilayani humo kuhakikisha ndani ya wiki moja washughulikia janga ambalo linaendelea kuathiri zao la pilipili manga ndani ya wiki moja.

Pia alimtaka Afisa Kilimo wa wilaya hiyo Hayange Mbwambo kushirikiana na maafisa hao kuhakikisha wanapata suluhu ya tatizo hilo ambalo linaleta athari kwa wakulima hao wa pilipili manga. 

Kijazi ambaye ni Afisa Tarafa ya Bwembwera wilayani Muheza alitoa agizo hilo wakati wa Jukwaa la wadau wa mazao ya viungo wilayani humo ambapo pia walitumika kuweka mikakati mbalimbali. 

Alisema baada ya muda huo waweze kutoa ripoti ya tatizo linalopelekea kukausha zao hilo la pilipili Manga huku likiufanya mti wa zao hilo kukauka na kuleta athari kubwa kwa wakulima. 

“Tunaweza kujaribu kufanya tathimini kukuta janga hili ni kubwa hasa kwa wakulima lakini pia mkishindwa kulitatua tupeleke ombi tuweze kusaidiwa kwenye ngazi za juu akiwemo Mkuu wa wilaya hata Mkuu wa Mkoa kuweza kuona namna ya kulitatua kwa pamoja”Alisema

Kaimu Mkuu huyo wa wilaya alisema ufunguzi rasmi ya kuvuna zao pilipili Manga wilayani humo litakuwa ni Januari 3 mwakani huku akiwaonya watakaojaribu kuvuna kabla ya muda huo watawachukulia hatua.

“Tunawafahamu njia ambazo mnatumia kusafirisha mazao hayo hivyo hakikisheni mnazingatia muda wa kuvuna msije kuingia matatani kwani watakaokamatwa kabla ya wakati watawashughulikia kwa mujibu wa sheria kukomesha vitendo hivyo “Alisema

Awali akizungumza wakati wa Jukwaa hilo Afisa Kilimo wilaya ya Muheza Hayange Mbwambo alisema kwamba walipokubaliana wawe na muda wa kuvuna iliwasaidia sana kuhakikisha kwenye masoko wanapata pilipili manga iliyokomaa na yenye ubora.

Alisema kwamba licha ya kuwepo kwa kasoro ndogo ndogo zinazungumzika na wamefikia hatua nzuri ya mahali wanapotaka kufika huku akieleza kwamba wameanza kuaminika kwamba asilimia 70 ya pilipili zinazovunwa zinasifa ya ukomavu na kuleta ubora na hivyo kupunguza malalamiko sokoni.

“Lakini pia wiki mbili zilizopita tulitembelewa na wageni kutoka kwenye makampuni ya nje moja ya mambo ambayo walitupongeza ni kuweka utaratibu mzuri wa kufungua msimu”Alisema

Naye kwa upande wake Mkulima wa Iliki Kata ya Zirai Ally Zubeya alisema visababishi vya iliki kuwa changa ni wakulima kuwekeza shamba lake kwa mtu kwamba ukifika muda Fulani atavuna mazao na anapokwenda kuvuna anavuna zote. 

Alisema mwarobaini wa suala hilo ni vyama vya ushirika kuhakikisha wanakagua mazao husika yanapokuwa shambani kabla ya kuvunwa kutokana na kwamba nyengine zinavunwa kabla ya kukomaa na kupelekea kukosekana kwa ubora.

Mwisho.

Share:

Senior Officer Sales Job at Oman Air

Job Opportunity at Oman Air, Senior Officer Sales Senior Officer Sales  Reference No AL-19-062/ Job Title: Senior Officer.Zanzibar – Sales Category COMMERCIAL Educational Qualifications Bachelor degree in a related discipline with 04 years of relevant experience in the sales function preferably with an Airline industry OR Two years college Diploma in a related discipline preferably in IATA /… Read More »

The post Senior Officer Sales Job at Oman Air appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa November 229




Share:

Thursday 28 November 2019

Sumaye Apigwa Chini Uchaguzi CHADEMA

Aliyekuwa mgombea pekee wa nafasi ya uenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye ameshindwa kutetea nafasi hiyo baada ya kupigiwa kura ya hapana.

Katika uchaguzi huo uliofanyika leo Alhamisi Novemba 28, 2019 mjini Kibaha Mkoa wa Pwani, Sumaye aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania mwaka 1995 hadi 2005 amepigiwa kura 28 za ndio na 48 za hapana na kura moja imeharibika.

Matokeo hayo yametangazwa na msimamizi wa uchaguzi, Patrick Ole Sosopi ambaye ni mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha).

Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo, Sumaye amesema lililofanyika ni demokrasia japo hana uhakika kama kutoa adhabu kwa mtu aliyekuwa anatumia haki yake kufanya demokrasia ni sahihi.

Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo baadhi ya wajumbe na wanachama waliokuwepo walilipuka kwa shangwe huku wakiimba nyimbo mbalimbali za chama.


Share:

Msanii Bi Cheka Afariki Dunia

Msanii wa Muziki Nchini Tanzania Cheka Hija Mzee Maarufu zaidi Bi Cheka amefariki dunia mchana wa Leo Novemba 28,2019 katika Hospitali ya Mloganzila.

Kifo cha msanii huyo mkongwe kimethibitishwa na mtoto wake wa kiume, Adam Juma, ambaye amesema kuwa mama yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo.

Familia ya marehemu inaendelea na mipango ya mazishi ambayo itaitangaza.


Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi


Share:

Waziri Mkuu: Nchi Yetu Inahitaji Wataalamu Wa Sekta Ya Uvuvi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania inahitaji kupata watendaji wa sekta ya uvuvi kuanzia ngazi ya vitongoji kwani kuna vijiji vina mito, maziwa na baadhi vimepakana na bahari na hivyo kutoa fursa za uvuvi.

“Nchi yetu inahitaji kupata watendaji kuanzia ngazi ya vitongoji kwani vipo vijiji vyenye fursa za uvuvi hivyo vinahitaji maofisa ugani ili waweze kufanya kazi vijijini na katika vitongoji, lengo likiwa ni kuwasaidia wavuvi wadogowadogo wajue namna bora ya kuvua na kuhifadhi samaki,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa kauli leo jioni (Alhamisi, Novemba 28, 2019), wakati akizungungumza na wahadhiri na wanafunzi mara baada ya ziara yake ya kutembelea Kampasi ya Kunduchi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Amesema hivi sasa Serikali inaandaa mazingira mazuri ya kuendesha sekta ya uvuvi kwa kupata watalaamu wa ngazi mbalimbali watakaoisimamia sekta hiyo.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli ambayo imejikita katika ujenzi wa uchumi wa viwanda inasisitiza uwepo wa vyuo vya ngazi mbalimbali ili tuweze kupata watalaamu wa kuendesha viwanda vinavyojengwa nchini,” amesema.

Amesema Serikali inawatambua na inawahitaji sana wasomi wanaopata taaluma zao katika vyuo mbalimbali hapa nchini ikiwemo  kampasi ya Kunduchi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam  ambayo kwa sasa inatumika kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa vitendo ya shahada ya awali, kufundishia na kufanya utafiti kwa wanafunzi wa Shahada ya Uzamili pamoja na wafanyakazi watafiti.

Waziri Mkuu amesema angependa kuona watafiti na watalaam wanapewa fursa ya kuongoza na kusimamia maeneo mbalimbali yanayohusiana na utafiti walioufanya ili kupata matokeo sahihi na chanya ya utafiti wao.

Amesisitiza kuwa Dkt. John Pombe Magufuli alitoa maelekezo thabiti ambayo amemkabidhi Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Bw. Luhaga Mpina ambaye ameyafanyia kazi  na yameleta mafanikio makubwa katika sekta ya uvuvi nchini.

“Hatua ya kwanza ya kuboresha sekta ya uvuvi ilikuwa ni kuwaondoa watumishi wabovu na wasio waamifu  na nafasi zao kuwapa watumishi  wazuri, wenye taaluma ya uvuvi, waaminifu  na wanaojali zaidi maslahi ya Taifa, kazi ambayo imefanywa na Waziri na watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,” amesema.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,  Ajira, Kazi ,Vijana na Wenye Ulemavu, Bibi Jenista Mhagama amesema Serikali inaitegemea sana Kampasi ya Kunduchi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam  kwa vile watalaam wanaopata taaluma zao katika kampasi hiyo wanahitajika sana katika maendeleo ya uvuvi nchini.

 Amesema Serikali ya Awamu ya Tano imeamua kujenga uchumi wa viwanda ambavyo vitatumia malighafi inayopatikana nchini ikizalishwa na Watanzania wenyewe na bidhaa zake kuuzwa ndani na nje ya nchi ili kupata fedha za kigeni.

Naye Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewahakikishia Watanzania kuwa hivi sasa idadi ya samaki na mapato ya Serikali yanayotokana na uvuvi yameongezeka.

Amesema kabla ya Serikali ya Awamu ya Tano kuanza kazi ya usimamizi wa  na udhibiti wa uvuvi nchini, mauzo ya bidhaa za uvuvi nje ya nchi yalikuwa ni sh. bilioni  371 kwa mwaka na hivi sasa Serikali inajipatia sh. biloni 691 kwa mwaka.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, NOVEMBA 28, 2019.


Share:

KIGOGO WA TACAIDS ATAKA KONDOMU KUGAWIWA BURE BAA , GESTI

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dk Leonard Maboko ameeleza anavyotamani kushuhudia Serikali ikigawa kondomu bure hasa katika maeneo hatarishi ikiwemo nyumba zote wageni na kwenye baa.

Akizungumza leo Alhamisi Novemba 28, 2019 katika kongamano la kitaifa la maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani jijini Mwanza,Dkt. Maboko amesema ifike mahali hali ya kuzuia maambukizi isichukuliwe kama mzaha.


Amesema anatamani mwaka 2020 nyumba zote wageni, baa na maeneo mengine kondomu kugawiwa bure.

"Natamani mwakani tuweze kusambaza kondomu kila mahali ili tuweze kudhibiti ugonjwa huu, najua huko ndiko watu wanakutana na kufanya wanavyofanya lakini kama Serikali tuone namna gani tunawasaidia wale wanaoshindwa kununua," amesema Dk. Maboko

Amesema lengo ni kuzuia maambukizi mapya ya Ukimwi kwa vijana kwa maelezo kuwa kwa sasa ndio kundi linaloongoza kwa kupata maambukizi mapya.

Share:

Picha : AGAPE YAENDESHA KIKAO KUJADILI KUTENGENEZA MUONGOZO WA KUPAMBANA NA UKATILI SOKONI SHINYANGA



Shirika lisilo la kiserikali Agape Aids Control Programme limeendesha kikao cha kujadili namna ya kutengeneza muongozo ambao utatumika kwenye masoko ya Shinyanga Mjini, kwa ajili ya kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia kwenye Masoko.

Kikao hicho kimefanyika leo Novemba 28, 2019, kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Liga, ambacho kimeshirikisha viongozi wa masoko sita ya Shinyanga mjini, maofisa ustawi, maendeleo ya jamii, wanasheria, dawati la jinsia, pamoja na wajumbe wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto Mtakuwwa.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao hicho, Mwansheria kutoka Shirika la Agape Felix Ngaiza, akimwakilisha mkurugenzi wa Shirika hilo John Myola, amesema, utengenezaji wa muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili kwenye masoko, utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni.

Amesema Shirika hilo limekuwa likitekeleza mradi wa kupambana na matukio ya ukatili wa kijinisa sokoni, uitwao Mpe Riziki Si Matusi, ambapo sasa wameamua watengeneze muongozo ambao utatumika kuzuia na kupambana na matukio hayo ya ukatili wa kijinsia sokoni, ili pawe mahali salama pa kufanyia biashara.

“Muongozo huu ni muhimu sana ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni, na ndio maana leo tumeamua kufanya kikao na viongozi wa masoko, maofisa ustawi jamii, maendeleo, dawati la jinsia, wanasheria, na wajumbe wa Mtakuwwa, ili tupate kuutengeneza na kuanza kutumika,”amesema Ngaiza.

Aidha amesema muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia kwenye Masoko, utakuwa ukitoa faini na adhabu mbalimbali kwa watu ambao watakuwa wakifanya matukio hayo ya ukatili kwenye masoko.

Naye Afisa mradi wa kutokomeza ukatili sokoni wa ‘Mpe Riziki Si Matusi’ Helena Daudi, amesema mradi huo umeanza kutekelezwa tangu mwaka Novemba 2018 ambao unakoma mwaka huu 2019, ambapo mpaka sasa wamefanikiwa kupunguza ukatili huo kwa kiwango kikubwa.

Amesema mradi huo unafadhiliwa na Shirika la UN WOMEN kupitia shirika la Equality for Growth (EFG), ambao umedhamiria kutokomeza ukatili kwenye masoko sita ya manispaa ya Shinyanga dhidi ya wanawake na wasichana, ambayo ni Kambarage, Soko kuu, Nguzonane, Ngokolo, Majengo mapya, na Ibinzamata.

Nao baadhi ya wenyeviti wa masoko akiwemo Alex Stephen kutoka soko kuu la Shinyanga, wamebainisha matukio ya ukatili ambayo yamekuwa yakitendeka ikiwamo kutolewa kwa lugha chafu za matusi ya nguoni, kushikwa maumbile kwa wanawake bila ya ridhaa yao, kutakwa kimapenzi kwa nguvu, kudhulumiwa pamoja na vipigo.


TAZAMA PICHA HAPA CHINI

Mwanasheria wa Shirila la Agape Felix Ngaiza akizungumza wakati wa kufungua kikao cha kujadili namna ya kutengeneza muongozo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Afisa mradi wa kutokomeza ukatili sokoni wa ‘Mpe Riziki Si Matusi’ kutoka Shirika la Agape Helena Daudi, akielezea umuhimu wa masoko kuwa na muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni, ambapo utasaidia kutokomeza ukatili huo.

Afisa mradi wa kutokomeza ukatili sokoni wa ‘Mpe Riziki Si Matusi’ kutoka Shirika la Agape Helena Daudi, akielezea umuhimu wa masoko kuwa na muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni, ambapo utasaidia kutokomeza ukatili huo.

Mwanasheria kutoka Shirika la Agape Emmanuel Nyalada akiwasilisha mada kuhusu muongozo wa kuzuia na kupambana na ukatili kijinsia sokoni.

Meneja miradi kutoka Shirika la Agape Peter Amani, akizungumza kwenye kikao hicho.

Mwanasheria wa manispaa ya Shinyanga Mushi Josephat akieleza kuwa muongozo huo wa kuzuia na kupambana na ukatili wa kijinsia sokoni utasaidia kumalizana kesi wao kwa wao zinazohusu ukatili, kuliko kupelekana kwenye vyombo vya Sheria ambapo matukio yote ya ukatili ni Makosa ya Jinai.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadili utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia sokoni.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadili utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni.

Wajumbe wakiwa kwenye kikao cha kujadiri utengenezaji wa muongozo ambao utasaidia kuzuia na kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia masokoni.

Wajumbe wakiendelea na kikao.

Wajumbe wakiendelea na kikao.

Wajumbe wakiendelea na kikao.

Mwenyekiti wa Soko kuu la Shinyanga Alex Stephen akichangia mada kwenye kikao hicho.

Mhasibu wa Soko la Ibinzamata Juliana Francis akichangia mada kwenye kikao hicho.

Msaidizi wa kisheria kutoka Soko kuu la Shinyanga Zera Semuguruka, akichangia mada kwenye kikao hicho.

Mwakilishi wa Soko la Nguzo Nane Hilda Athanas, akichangia mada kwenye kikao.

Mchungaji wa kanisa la KKKT Makedonia Harold Mkaro, ambaye pia ni mjumbe wa MTAKUWWA, akichangia mada kwenye kikao.

Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi.

Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi.

Wajumbe wakiwa kwenye kazi ya makundi.

Mwenyekiti wa Soko la Kambarage Seif Mtete akiwasilisha kazi ya kikundi.

Wajumbe wakiendelea kuwasilisha kazi ya kikundi.

Wajumbe wakiwasilisha kazi ya kikundi.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger