Sunday 24 January 2016

magazeti ya leo jumapili january 24,2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY















Share:

Saturday 23 January 2016

AUDIO | JOS MTAMBO Ft. FID Q, Cowboy, Joslin, Adam Mchovu, Rama DEE & Babuu Wakitaa - BATA BOY | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
DOWNLOAD via MKITO
https://mkito.com/song/bata-boy/18436/bwi-1-36202
Share:

Jokate, Kiba wamwagana

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

JOKATE_MWEGELO4
Staa wa Bongo, Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’.
MUSA MATEJA, Risasi Jumamosi
Dar es Salaam: Hii ni habari ya kipekee (Exclusive Story)! Mastaa wawili wenye majina makubwa Bongo ambao walikuwa wachumba walioshibana, Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’ na Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ wanadaiwa kumwagana, Risasi Jumamosi ndilo gazeti pekee linaloweza kuthubutu kukupa mchapo kamili.
JOKATE44
Mastaa wawili wenye majina makubwa Bongo ambao walikuwa wachumba walioshibana, Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’ na Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ wakiwa katika pozi.
Habari ya mjini kwa sasa ni juu ya wawili hao ambao walikuwa gumzo kwa watoto wa mjini, kwa kila mmoja kuchukua hamsini zake na kufanya yake tofauti na walivyokuwa awali huku chanzo cha kutengena kwao kikitajwa kuwa ni wazazi wa sehemu zote mbili kutoridhiana.
King-Kiba
Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni mtu wa karibu wa wawili hao, mbali na ishu ya wazazi, hivi karibuni Jokate na Kiba waliingia kwenye gogoro kubwa la kimapenzi baada ya kufumaniana kwenye simu, jambo ambalo limeendelea kutokea huku jamaa akiongoza kukutwa na meseji kwenye simu yake za mwanamke mmoja anayedaiwa kuishi nje ya Tanzania.
BOFYA HAPA KUSIKIA CHANZO
“Ukisema nikusimulie juu ya kumwagana kwa Jokate na Kiba basi tunaweza kukesha ila mbali na mambo ya wazazi, kwa kifupi tu ni kwamba, hawa watu wameingia kwenye mgogoro na kilichokuwa kikiwagombanisha mara nyingi ni uhusiano wao wa zamani.”
KIBA ANA DEMU?
“Mara kadhaa Jojo (Jokate) amekuwa akimlalamikia jamaa (Kiba) kuwa ana demu nje ya nchi ambaye amekuwa akimtundika katika mitandao ya jamii na kujinadi kuwa ndiye mkewe tofauti na wengi wanavyojua kuwa Jokate ndiye mtu wake.
“Mbali na hilo, sasa kuna suala la familia zao kuonesha hali ya kutokubaliana na wao kuoana hasa upande wa Jokate ambao ulionesha msimamo mkubwa kutomtaka hata kidogo Kiba, mambo hayo yamekuwa ni chagizo kubwa katika kuhatarisha mapenzi yao hivyo kufikia hatua hata ya wao kutoendelea kupendana kwa dhati kama ilivyokuwa mwanzo wa penzi lao.”
VIKAO VYAGONGA MWAMBA
“Tofauti na watu walivyozoea kuwaona pamoja, kwa sasa wametibuana na hapa tunapozungumza tayari kuna vikao kibao huko nyuma vilishakaa ili kunusuru penzi lao lakini imeshindikana maana kila mmoja sasa hivi anajifanyia mambo yake na hakuna dalili za kurudiana.
“Kiba anaonekana ameshajiingiza kwenye penzi la demu wake wa zamani huku Jokate naye akiwa ‘in love’ na mtu wake mwingine.”
MPANGO WA KUZAA WAYEYUKA
“Kitambo tu nimekuwa nikiwaambia kwa staili waliyokuwa nayo hakika wasingeoana hata kama ukiweka pembeni suala la dini zao kutoendana, maana kuna siku niliwasikia wakiambiana hata kama wazazi wakigoma wao wangefanya kila juhudi hata wazae pamoja tu.
“Lakini ukweli ni kwamba ilishindikana baada ya kuanza kugombana mara kwa mara, pamoja na kwamba Jokate alikuwa akikubalika kwa asilimia zote kwa mama Kiba na hata ndugu wengi wa Kiba walionekana kumpenda waziwazi,” kilisema chanzo hicho.
KIBA AFUNGUKA
Baada ya kupenyezewa mchongo huo, gazeti hili liliingia mzigoni kumtafuta Kiba ili atoe la moyoni juu ya madai hayo ya kumwagana na Jokate ambapo alipopatikana alisema kuwa haoni sababu ya kuzungumzia ishu hiyo kwani ni mambo binafsi.
sfud7zknmrs4955def775ef165“Kusema kweli ishu hii mimi sina uwezo wa kuiongelea zaidi kwa sasa kwani ni mambo binafsi sana na sioni faida ya kuzungumzia vitu ambavyo havina maana.
“Kwanza sioni nini cha kuongelea hapa kwani kila jambo lina mipaka yake,” alisema Kiba akikataa kuulizwa zaidi juu ya suala hilo.
JOKATE VIPI?
Kwa upande wa Jokate alipotafutwa kwa siku kadhaa ili azungumzie sakata hilo kwa ufasaha hakupokea simu ya mwandishi wetu hadi gazeti linaingia mitamboni.
PENZI LA JOKATE NA KIBA
Awali zilipovuja habari za penzi la Jokate na Kiba wote walikanusha, kadiri siku zilivyosonga ndivyo walivyozidi kuwa gumzo kwa mashabiki wao waliofurahishwa na ‘kapo’ yao huku wakionekana kwenye viwanja mbalimbali vya starehe wakiwa kimahaba lakini sasa mambo yanaonekana kwenda mrama.
Share:

Ostaz Juma: Miaka 10 na wanamuziki ilitaka kunivunjia ndoa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
_MG_4483
Meneja wa muziki hapa Bongo, Ostaz Juma Namusoma.
Musa mateja
UKIANZA kutaja majina ya mameneja mbalimbali wa muziki hapa Bongo, baadhi ya majina makubwa yasiyoisha miongoni mwao huwezi kulikosa jina la Ostaz Juma Namusoma.
_MG_4486 Kwa mujibu wa kinywa chake mwenyewe Ostaz Juma Namusoma, juzikati nilipata nafasi ya kumbana na kunieleza kiunagaubaga namna alivyoweza kujipenyeza hadi kupata jina kupitia muziki wa Bongo.
Kwa kinywa chake aliniambia kwamba, muziki kwake ni sehemu ya maisha ambayo ameishi kwa kipindi kirefu sana, kwani tangu alipokuwa mdogo alipenda muziki kushinda kitu chochote, msikie mwenyewe.
OSTAZ JUMA: Mimi ni miongoni mwa vijana wa kipindi hicho ninayetokea Musoma mkoani Mara. Nilianza kupenda muziki tangu nasoma shule ya msingi tena mapema kabisa nikiwa darasa la tatu.
Nikiwa shuleni nilikuwa napenda sana kuimba nyimbo mbalimbali za wasanii wa Kongo hadi nikafikia hatua ya kununua redio na kuwarekodi watoto wenzangu wakiimba kisha nazitunza nyimbo walizokuwa wakishindana kuimba hasa za Boringo za Wazaire.
_MG_4506
Nimefanya hivyo hadi nikawa nagombezwa na wazazi wangu lakini sikukoma hadi nilipokuwa mtu mzima na kuanza kujifanyia mambo yangu ambapo wazazi hawakuweza kuniingilia.
Kwa jinsi hii ndiyo utaweza kugundua kuwa nina kipaji cha kusimamia watu ndiyo maana nimeweza kuwasaidia wanamuziki wengi tu kwenye dansi ambapo kabla ya kujiingiza katika Bongo Fleva niliwahi kuwasaidia wanamuziki wa dansi kama Ally Chocky, Super Nyamwela, Jose Mara, Kalala Junior, Nyoshi El-Saadat, Mwinjuma Muumini na Mulemule.
Tabia za wanamuziki kiukweli hazipishani sana hivyo ukiona meneja yeyote analalamika juu ya wanamuziki basi ujue matatizo yao mara kadhaa yamekuwa hayapishani sana, ila wanaopishana tabia na namna ya kuongoza ni mameneja tu.
_MG_4516
Namna ya kuongoza na kummeneji mtu kunategemeana na uwezo wa kifedha na akili pia, nasema hivyo kwa sababu muziki wetu umekuwa ukiyumba mara kadhaa kutokana na baadhi ya mameneja kuwa wasimamizi wabovu na wengine wanasimamia wakiwa hawana fedha ya kuweza kuwaongoza wasanii.
Meneja ninayeweza kumpa saluti hapa Bongo ni Saidi Fella kwani ameonesha njia kubwa ya kuimarisha Muziki wa Dansi na sasa umeanza kuwa juu kiasi cha watu kuanza kuupenda tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ulianza kupoteza dira.
ALIANZAJE KUSIMAMIA BONGO FLEVA?
Ostaz Juma: Kwenye Bongo Fleva niliingia baada ya kuanza kumsimamia shemeji yangu aitwaye Abdallah David aliyekuwa akijiita Fil David, huyu nilijikuta namsimamia baada ya kumuona ana kipaji kizuri na baadaye nikaanzisha rasmi kampuni yangu ya Mtanashati.
Mtanashati ilipoanza tu nikapunguza kuwasaidia wanamuziki wa dansi hivyo nikajikita kwenye Bongo Fleva ambapo nilianza kumsimamia marehemu Sharo Milionea aliyemleta Kitale, lakini kabla sijaingia mkataba na Sharo akafariki dunia.
Baada ya kufariki kwa Sharo Milionea ambaye ndiye msanii naweza kujisifia katika upande wa Bongo Fleva kwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu sana, nilimchukua PNC, Dogo Janja na Happy Balis ambao nilifanyanao project kibao kiasi ilifikia hatua nikawa nakosana hadi na mke wangu kisa muziki huu.
Nimekuwa nikiwasaidia wasanii hawa kwa muda lakini nilichoweza kujifunza ni kwamba wasanii wengi hawana adabu kabisa, kwani kuna siku niliwahi kukosana na mke wangu kwa kushindwa kumpeleka hospitali kisa kumpeleka Dogo Janja kwenye interview jambo ambalo mke wangu amekuwa akinikumbusha kila mara nami huwa halitoki kichwani hadi leo.
Fedha niliyowahi kutumia hadi leo kwa ajili ya Dogo Janja na PNC naweza kujenga hata ghorofa tatu hapa mjini, lakini kwa kuwa nilikuwa naupenda muziki ndiyo maana leo utaona inafikia muda sasa nimeamua kuachana na hawa Bongo Fleva maana hawana nidhamu hata tone ila ukilinganisha na wanamuziki wa dansi utagundua ni bora dansi kuliko Bongo Fleva.
Nasema wanamuziki wa dansi ni bora kuliko wa Bongo Fleva kwa sababu wakati nadili na wanamuziki wa dansi walikuwa wanaonesha nidhamu ya hali ya juu jambo ambalo wanalifanya hadi sasa.
Ujue nilikuwa nikiwapatia fedha za kodi za nyumba, mara nyingine kama Christian Bella na Chocky hawa niliwahi hata kuwalipia studio mara kadhaa kwa ajili ya kurekodi nyimbo zao binafsi.
Christian Bella yeye aliwahi hadi kunitungia wimbo ambao unaitwa Ubinadamu ambao hata yeye ukimuuliza leo anaujua na ninao mimi mwenyewe.
Wasanii wakijua kuwa muziki ni kazi na sehemu ya maisha yao basi hakuna Bongo Fleva atakuja kushindwa kufanya mambo makubwa kama anavyofanya Diamond kwani kinachomfanya kuheshimika na kufanikiwa ni nidhamu yake tu.
Share:

Apiga chini shule, aondoka kwao, aanza harakati za muziki

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


BELAChristian Bella ‘Obama’
Wiki iliyopita ndipo tulianza na Christian Bella ‘Obama’ kwenye kolamu hii akisimulia juu ya maisha yake, aliishia kusimulia pale ambapo hali ya kiuchumi kwenye familia yao ilipobadilika kutoka ya ‘kishua’ na kuwa ya kifukara, akalazimika kuingia mitaani kujitafutia kipato, akajifunza pia kutengeneza mikate kwenye kiwanda-bubu kilichokuwa nyumbani kwao na rafiki yake Junion Kumbukumbu.
Tambaa nayo…
“Enhee, baada ya kuanza kujifunza kutengeneza mikate nini kiliendelea?” nilimuuliza Bella huku nikikaa sawa kwenye kiti, aliendelea kusimulia baada ya kupiga mafunda mawili matatu ya kinywaji chake fulani hivi bariiidi.
Anasema kuwa baada ya kufahamu vizuri kutengeneza mikate na kuanza kuingiza mkwanja wa kueleweka kwa ‘level’ yake kiasi kwamba akawa hategemei tena kupata pesa ndogondogo kutoka nyumbani kwao, alijikuta akipiga chini kwenda shule na kujikita zaidi kwenye masuala ya kutafuta pesa na kuhudhuria kwenye vikundi vya uimbaji pamoja na rafiki zake.
“Nilipoachana na shule baba aliumia sana maana alichoamini urithi wa mtoto ulikuwa ni kwenye elimu tu, aliniita mara kadhaa na kunionya juu ya uamuzi wangu lakini wakati huo sikuhitaji kumsikiliza mtu yeyote zaidi ya sauti niliyokuwa naisikia ndani yangu,” alisema Bella.
“Ni sauti gani hiyo uliyokuwa unaisikia?” nilimuuliza huku nikimtazama kwa makini.
“Niache shule, nitafute pesa na kufanya muziki,” alijibu.
“Mama vipi, yeye aliupokeaje uamuzi wako huo wa kuacha shule?”
“Ulionekana kumshangaza, hakuamini kama ningeweza kufanya hivyo, pia kama mzazi alijaribu kunisihi lakini sikuhitaji kurudi nyuma.”
“Enhee, nini kikaendelea?”
“Basi bwana; baada ya kukacha skuli sikupenda kuishi tena nyumbani maana tayari mimi na wazazi wangu zilikuwa haziungi tena freshi, kwa hiyo nilichoamua kufanya ilikuwa ni kuondoka nyumbani na kwenda kuishi magetoni kwa washkaji zangu.”
“Nikiwa huko mishemishe za muziki ndiyo zikaanza rasmi maana nao walikuwa katika harakati hizohizo, sasa kule kwetu Kongo kipindi cha nyuma kwa vijana wadogo ambao wanafanya ishu za muziki walikuwa wanatunga nyimbo wakishazikariri wanatengeneza bendi na kuanza kufanyia mazoezi kwenye majumba mabovu huku ala za muziki zikiwa madebe.”
“Kwa hiyo na nyie mlifanya hivyo?”
“Ndiyo, tulifanya hivyo na kila jioni tulikuwa kwenye jumba bovu f’lani hivi karibu na nyumbani kwao na mshkaji wangu Bosei Junioh tukifanya yetu, huwezi amini watu walikuwa wanajaa kinoma kila waliposikia tunaimba, baada ya muda tukaanza kuwa vizuri na kuwa kivutio mtaani.”
Bella anaendelea kuwa matumaini na mwanga juu ya kufanikiwa kimuziki alianza kuvipata kutokana na kukubalika huko kwenye mitaa ya kwao, anasema kilichomfurahisha zaidi kwa wakati huo ilikuwa ni wasichana wengi wa mtaani kwao kuanza kuhitaji kuwa naye kimapenzi.
“Kutokana na umri ilikuwa ni vigumu kujizuia kuruka na baadhi yao waliokuwa wananivutia na kunihitaji, hata hivyo nilikuwa na msichana f’lani ambaye nilikuwa nina mpenda sana, huyo alikuwa kila kitu kwangu, lakini tofauti na wengine yeye hakuwa anataka kabisa tufanye mapenzi.”
“Alikuwa ana umri gani?” nilimuuliza.
“Miaka kumi na sita.”
“Wewe?”
“Wakati huo kumi na nane na ndiyo umri nilioanza kufanya mapenzi.”
“Mkh…”
“Siku zikasonga mbele, kila kitu kuhusu masuala yangu na wasichana wengine yalikuwa ni siri kubwa kwa huyo niliyempenda, nikazidi kustrago kwenye ishu zangu za muziki nilipofikisha miaka kumi na tisa ikabidi niende kuomba kujiunga kwenye Bendi ya Chateau du Soleil.”
“Baada ya kupeleka maombi yangu kwenye bendi hiyo ambayo ilikuwa inamilikiwa na tajiri mmoja aitwaye Frank Isekya rafikiye mkubwa na Papa Wemba nikapangiwa siku ya kufanyiwa usaili kabla ya kunikubali au kunibwaga kwenye bendi yao.”
Baada ya maneno hayo Bella anachukua glasi yenye kinywaji akipendacho mezani na kubugia mafunda matatu, kisha anairudisha mezani na kunitazama huku akitabasamu, macho yake yalinifanya nipate swali la haraka la kumuuliza.
“Bila shaka kumbukumbu za usaili ndizo zinakufurahisha?”
“Asikwambie mtu, siku hiyo nakumbuka usiku wake sikupata usingizi kabisa, akili yangu yote ilikuwa kwenye usaili ambao ningeufanya kesho yake, lakini kikubwa nilikuwa nimepania kujikamua sawasawa nipate nafasi na nilimuomba Mungu hilo liwezekane.”
Je, nini kitaendelea? Bella atafanikiwa kupita kwenye usaili huo? Vipi kuhusu mpenzi wake anayempenda sana, wataishia wapi? Usikose wiki
Share:

magazeti ya leo jumamosi tarehe 23/1/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY





Share:

Friday 22 January 2016

New AUDIO | Stamina - Panga Pangua Ft. Mr Blue | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Leo Stamina ameachia album yake aliyokuahidi Mt. Uluguru ikiwa na nyimbo 20!
Licha ya hiyo, Stamina ameongeza nyimbo 6 BONUS kwenye album hiyo ambazo zitakuwa zikipatikana Mkito.
Wimbo wa kwanza kwenye bonus hizo ni huu hapa akimshirikisha Mr Blue, Panga Pangua!
 DOWNLOAD via MKITO
https://mkito.com/song/panga-pangua-ft-mr-blue/18431/bwi-1-36182
Share:

MAGAZETI YA LEO TAREHE 22/1/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger