Monday, 26 August 2019

Kundi la waasi la Houthi la Yemen larusha makombora 10 dhidi ya uwanja wa ndege wa Saudi Arabia

Kundi la waasi la Houthi la Yemen limesema lilirusha makombora 10 dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan nchini Saudi Arabia jana usiku.

Taarifa iliyotolewa na mtandao wa kituo cha televisheni cha al-Masirah kinachomilikiwa na kundi hilo imemnukuu msemaji wa jeshi la waasi hao Yahya Sarea akisema, makombora 10 aina ya Badr-1 yamerushwa kwa pamoja dhidi ya uwanja wa ndege wa Jizan, na yamelenga ndege za kijeshi na helikopta za kivita aina ya Apache ndani ya uwanja huo, na kwamba askari kadhaa wa Saudia wameuawa kwenye shambulizi hilo.

Pia amesema, jeshi la Houthi litafanya mashambulizi mengi zaidi katika kipindi kijacho.


Share:

Serikali Yataja sababu ya ndege ya Tanzania kuzuiliwa Afrika Kusini

Msemaji wa Serikali, Dk Hassan Abbas amesema sababu ya kushikiliwa ndege ya Air Tanzania aina ya Airbus A200-300 ni kesi kati ya Serikali ya Tanzania na mkulima Hermanus raia wa Afrika Kusini ambaye mali zake zilitaifishwa

Dk  Abbas amesema hukumu iliyotolewa na mahakama nchini Afrika Kusini inaruhusu kupinga hatua ya mahakama hiyo kuzuia ndege ya Air Tanzania, kwamba wanasheria watachambua kuona hatua za kuchukua.

Ameyasema hayo Jumapili Agosti 25, 2019 wakati akihojiwa na Shirika la Utangazaji nchini (TBC). 

“Niwakikishie Watanzania kuwa ndege zetu zipo salama ambazo zinaendeshwa na ATCL isipokuwa ndege hii moja iliyozuiliwa Afrika Kusini”

"Kesi hii ni madai ya muda mrefu ya fidia ya ardhi iliyotwaliwa tangu miaka ya 1980 huko, sio kesi kwamba ni ATCL ndiyo inadaiwa, tunaipambania ndege hii kwa maslahi ya Taifa letu na tunaamini siku moja itarudi kuendelea na shughuli zake za kawaida”

“Ni kesi ya fidia inayomuhusu Bwana Hermanus Steyn na Serikali ya Tanzania, kesi hii haina uhusiano wowote na Shirika letu la Ndege (ATCL), sisi tunaheshimu Sheria, Wanasheria wetu wanafuatilia na Sheria itafuata mkondo wake”

“Ukisoma hukumu inaturuhusu hata sisi kupinga, Wanasheria wetu wataichambua na kuona hatua gani za Kuchukua, tunawahakikishia Watanzania tutasimamia maslahi ya Taifa na ndege yetu itarudi na kuendelea na shughuli zake"

“Kesi ya msingi haijasikilizwa, kwa sababu ametumia Sheria za Afrika Kusini kuomba kutekeleza hukumu ya Nchi nyingine, ana hukumu ambayo ilishapatikana Nchini lakini akaomba itekelezwe Afrika Kusini kwa maana ya kiasi cha fedha kilichobaki”

“Kwenye awamu zote kulikuwa na makubaliano lakini ukifuatilia hatua za Kimahakama wanakubaliana lakini malipo hayafanyiki, kiasi kikubwa cha malipo kilifanyika katika awamu ya nne kikabaki kiasi kidogo ambacho ndio unaona amekwenda Afrika Kusini" amesema Dkt. Ababas.


Share:

Hatima Ya Ubunge wa Tundu Lissu Kujulikana Leo

Mahakama  Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo inatarajia kutoa uamuzi  endapo maombi yaliyowasilishwa na aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu  yanasifa ya kusikilizwa na mahakama hiyo na kama aliyefungua kwa niaba yake anayo mamlaka ya kufanya hivyo.


Uamuzi unatarajia kutolewa leo mbele ya Jaji Sirilius Matupa,baada ya kusikiliza sababu nane za kupinga maombi hayo ambayo wanadai hayajakizi vigezo vitano kati ya sita.

Kiongozi wa jopo la mawakili wa Lissu, Peter Kibatala katika kupinga hoja za kutaka maombi ya mteja wake kutupwa  anadai  hoja za wajibu madai hazina mashiko na akaiomba mahakama izitupilie mbali.

Anadai hoja ya kutoambatanisha uamuzi wa Spika uliomvua ubunge Lissu, hilo si hitaji la lazima la kisheria.

Kibatala anadai kwa mujibu wa Kanuni ya  5 ya Mwenendo wa Mashauri ya Mapitio ya Maamuzi ya Mamlaka za Kiserikali, hakuna mahali ambapo panataja kuwa lazima kuambatanisha uamuzi unaolalamikiwa katika maombi ya marejeo ya uamuzi wa mamlaka za kiserikali.

Alisema kwa mujibu wa Kanuni ya 4 hata waliozitunga hawakuweka hilo kama hitaji la lazima kwa kuwa wakati mwingine uamuzi wa mamlaka za kiserikali hufanyika kwa maneno tu na kutekelezwa.

Kuhusu hoja alichokifanya Spika halikuwa tangazo, bali taarifa tu kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi kuwa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kiko wazi, Kibatala anasema alichokifanya kina uamuzi ndani yake.

Anadai Mwenyekiti wa NEC  hawezi kwenda bungeni kungalia nani hayuko bungeni, bila ruhusa ya Spika na kwa upande wa mamlaka ya kisheria kwa kaka wa Lissu, Alute Mughwai kufungua shauri hilo, Wakili Kibatala anadai  hoja hiyo si ya kisheria kwa kuwa ni hoja inayohitaji ushahidi.

Mawakili wa Serikali kwa upande wao kwa kuongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Clement Mashamba waliwasilisha hoja nane za kupinga maombi hayo wakidai hayajakidhi  vigezo vitano kati ya sita na aliyemwakilisha kufungua hana mamlaka ya kufanya hivyo, wanaomba yatupwe


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu 26 August

























Share:

Sunday, 25 August 2019

UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA KUANZA KESHO SHINYANGA...NI SIKU 7 TU

Share:

SERIKALI YAWATAKA WACHAWI KUSITISHA SHUGHULI ZAO USIKU ILI WAHESABIWE


Wachawi wa kukimbia usiku Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya wametakiwa kufunga biashara yao kwa siku mbili ili kuruhusu zoezi la sensa kufanyika bila ya kutatizwa.

 Serikali imewataka kukaa ndani usiku hadi zoezi hilo lililoanza Jumamosi, Agosti 24 litakapokamilika asubuhi ya Jumatatu, Agosti 26,2019. 

Harman Shambi ambaye ni Kamishna wa Kaunti ya Homa Bay, aliwataka wachawi kujizuia kutoka usiku ili nao pia wahesabiwe 

Shughuli za wachawi katika maeneo mengi ya humu nchini hufanywa usiku, na sarakasi zao huwa ni za kutisha mno; miongoni mwazo ni kutimka mbio na kuparamia miti katika maboma ya watu, kurusha mawe na mchanga kwenye paa na ndani ya nyumba, kuacha vinyesi katika maboma ya walengwa wao miongoni mwa nyinginezo nyingi. 

“Ni Wakenya na hivyo ni lazima kuhesabiwa. Kwa hivyo ni lazima kujizuia kutoka usiku ili wahesabiwe,” alisema na kunukuliwa na Nation, Jumamosi, Agosti 24,2019.

 Kauli yake ilifuatia ujumbe wa Twitter uliotamba sana wiki hii uliodai Waziri wa Usalama wa Ndani Dk Fred Matiangi amepiga marufuku shughuli za wachawi wote wa usiku kaunti za Homa Bay na Kisii wakati wa sensa.

“Matiangi awaonya wachawi wote kaunti za Kisii na Homa Bay awataka waheshimu serikali na wasitoke nje kwa siku kadhaa. Wachawi wote sharti kuhesabiwa ,” ujumbe huo ulisema. 

Shambi pia aliwaonya watu wanaopanga kujifanya ni maafisa wa sensa ili kuwahangaisha watu kwamba, watachukuliwa hatua kali za kisheria, aliwataka raia kuwa makini na kuchukua tahadhari za mapema. 

“Maafisa wa sensa watajitambulisha na watachomoa baji zao ma jaketi zao za kumwe kwenye mwangaza. Wataandamana na machifu na wazee wa vijiji ili kuifanya kazi hiyo kuwa rahisi,” alisema. Hata hivyo zoezi hilo linatazamiwa kuendelea kwa siku saba baada ya kufungwa rasmi usiku wa kuamkia Jumatatu.
Chanzo - Tuko
Share:

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo

SUPER MORISIS; nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-85)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wala kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-45

SUNUPER;   Hurefusha na kunenepesha maumbire madogo ya uume uliosinyaa ,  matatizo haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguruma na kujaa gesi hatimae kinyesi kuwa km cha mbuzi, ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia nidawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

ONDOA MATATIZOYAKO YOTE  ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,  kurudisha mali iliyopotea au kuibiwa 

Kwahuduma na msaada wasiliana na DR. GALIMBO  0759208637   /  0620510598


Share:

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AENDA JAPAN KWA ZIARA YA KIKAZI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2019 ameondoka nchini kwenda Japan kwa ziara ya kikazi ya siku saba. Pichani, Mhe. Majaliwa akizungumza na Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Avemaria Semakafu (wapili kushoto) kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kabla ya kuondoka.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Share:

MABINGWA WA TANZANIA SIMBA SC WATEMBEZEWA KICHAPO NYUMBANI


MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wametolewa nje ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na UD Songo ya Msumbiji katika mchezo wa marudiano Raundi ya Kwanza jioni ya leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.

Matokeo hayo yanamaanisha UD Songo inasonga mbele kwa faida ya mabao ya ugenini, kufuatia kulazimishwa sare ya 0-0 mjini Beira wiki mbili zilizopita.

Na sasa watamenyana na FC Platinum ya Zimbabwe iliyowatoa jirani zao, Big Bullets ya Malawi kwa mabao 3-2 ushindi wa ugenini jana kufuatia sare ya 0-0 nyumbani wiki mbili zilizopita. 

Uwanja wa Taifa leo UD Songo waliwatangulia Simba SC kwa bao la dakika ya 14 lililofungwa na Luis Miquissone kwa shuti la mpira wa adhabu, akiutmia mwanya wa mshambuliaji Mnyarwanda Meddie Kagere kutoka kwenye kupenyeza mpira na kufunga kiulaini.

Baada ya kupambana kwa muda mrefu, hatimaye Simba SC ilifanikiwa kusawazisha hilo dakika ya 87 kwa mkwaju wa penalti wa Nahodha wa leo, Erasto Edward Nyoni kufuatia Miraj Athumani ‘Madenge’ kuchezewa rafu kwenye boksi.

Simba SC ilijitahidi kutumia dakika zilizosalia – pamoja na tatu za kufidia kusaka bao la pili, lakini wachezaji wa UD Songo walikuwa makini mno kujilinda na kufanikiwa kusonga mbele.

Simba SC inaungana na KMKM ya Zanzibar kutolewa mapema kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa jumla ya mabao 4-0, ikichapwa 2-0 kila upande nyumbani na ugenini na Primiero de Agosto ya Angola.

Yanga pekee imesonga mbele katika Ligi ya Mabingwa baada ya ushindi wa jumla wa 2-1, ikishinda 1-0 ugenini jana dhidi ya Township Rollers kufuatia sare ya 1-1 nyumbani wiki mbili zilizopita na itamenyana na Zesco United ya Zambia iliyoitoa Green Mamba ya Eswatini kwa jumla ya mabao 5-0, ikishinda 2-0 ugenini na 3-0 nyumbani.

Katika Kombe la Shirikisho Azam FC imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 3-2 dhidi ya Fasil Kenema ya Ethiopia ikifungwa 1-0 ugenini na kushinda 3-1 nyumbani na itamenyana na itamenyana na Triangle United ya Zimbabwe iliyoitoa Rukinzo ya Burundi kwa mabao 5-0, ushindi wa nyumbani kabla ya sare ya 0-0 ugenini.

Malindi SC ya Zanzibar pia imefanikiwa kwenda Raundi ya Pili ya Kombe la Shirikisho baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Mogadishu City na sasa watamenyana na Al-Masry ya Misri katika hatua inayofuata.
Timju zote za Tanzania zilizosonga mbele zitaanzia nyumbani tena kati ya Septemba 13 na 15, kabla ya kusafiri kuwafuata waponzani wao Zambia, Zimbabwe na Misri kwa mchezo wa marudiano kati ya Septemba 27 na 29.

Kikosi cha Simba SC kilikuwa: Aishi Manula, Gardiel Michael/Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ dk77, Pascal Wawa, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Deo Kanda, Jonas Mkude, Sharaf Eldin Shiboub/Miraj Athumani ‘Madenge’dk62, Clatous Chama, Francis Kahata/Hassan Dilunga dk24 na Meddie Kagere.

UD Songo: Leonel Mario, Frank Banda/Cremildo Khantumbo dk57, Amade Momade/Micupel Tembe dk83, John Banda, Infren Matola, Luis Miquissone, Pachoio King, Hermenegildo Mutambe, Pascoal Amorim, Stelio Ernesto/Mario Sebastian dk69 na Antonio Chirinda.

Share:

Tanzania, Burundi Wasaini Makubalinao Kuwarejesha Wakimbizi 2000 Nchini Mwao Kila Wiki

Na Felix Mwagara, Kigoma (MOHA).
TANZANIA na Burundi wamesaini makubaliano ya kuwarejesha Wakimbizi 2000 kwa kila wiki nchini mwao kuanzia Oktoba Mosi, 2019.

Wakimbizi hao waliopo katika Kambi ya Nduta na Mtendeli wanatarajiwa kusafirishwa kuelekea katika nchi yao ya asili kutokana na amani iliyopo katika nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, na Waziri wa Mambo ya Ndani wa nchini Burundi, Pascal Barandagiye tayari wamesaini makubaliano hayo ambayo watahakikisha wakimbizi wote waliopo katika kambi hizo wanartejeshwa nchini mwao bila kukwamishwa na mtu au shirika lolote.

Akizungumza na waandishi wa habari, mjini Kigoma jana, Waziri Lugola alisema makubaliano hayo yataanza rasmi Oktoba mosi na wakimbizi hao watakuwa wanarejeshwa nchini mwao na kupata mapokezi makubwa na Serikali ya Burundi.

“Tunataarifa wapo baadhi ya watu, mashirika ya kimataifa wanawarubani wakimbizi wakiowatangazia kuwa Burundi haina amani, jambo ambalo si la kweli, nchi hiyo ina amani na wakimbizi wanapaswa kurejea nchini mwao,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, atawachukulia hatua kwa watakaokwamisha zoezi hilo la kuwasafirisha wakimbizi hao, kwa kuwa Serikali ya Wakimbizi inataka watu wao na Tanzania imeamua kuwapa watu wao ili waende wakaijenge nchi.

“Natoa kauli hii sio kuwatisha au kutishia nyau, bali nasema, Serikali ya Magufuli haiwezi kuchezewa na mtu yeyote, hivyo tutawakamata wanaowarubani, wanaowashawishi wakimbizi wasiende nchini mwao,” alisema Lugola.

Wiki iliyopita, katika mkutano wa hadhara katika Kambi ya Nduta, baadhi ya Wakimbizi walisema wanawekewa vikwazo na kucheleweshwa na baadhi ya watendaji wa mashirika ya wakimbizi kambini humo wakati wanapoomba kujiandikisha kurejeshwa kwao.

Mkimbizi wa kambi hiyo, Nzoisa Bhainoje, alisema yupo tayari kurejea nchini Burundi lakini amefanya juhudi za kwenda eneo la kujiandikisha kambini hapo lakini hakufanikiwa kutokana na kusumbuliwa akiambiwa kuwa idadi wanaotakiwa kuondoka imekamilika.

“Nakumbuka nilifika eneo la kuondoka siku ya Jumanne lakini ilishindikana kujiandikisha kutokana na kukwamishwa, wengi tunataka kuondoka lakini tunashindwa kuondoka kwasababu tunakwamishwa,” alisema Bhainoje.

Bhainoje aliongeza kuwa, wanaomba watendaji hao wawaruhusu kwa wale wanaotaka kurejea nchini mwao kwa hiari, lakini kwa wale ambao hawataki kuondoka wanaweza kubaki kwa mipango yao.

Baada ya wakimbizi hao kutoa kero zao kwa Waziri Lugola na Waziri Barandagiye, ndipo Lugola aliagiza kufanyika uchunguzi katika kambi hiyo kuwakamata wale wote ambao wanakwamisha wakimbizi hao kurejea nchini kwao kwa hiari.

“Naagiza uchunguzi ufanyike haraka iwezekanavyo kwa yeyote atakayehusika anakwamisha zoezi hili la kuwarejesha wakimbizi hawa ambao wapo tayari kuondoka nchini kwao kutokana na amani iliyopo, awe Afisa kutoka Wizarani, awe afisa wa shirika lolote, awe yupo hapa kambini, lazima tutamkamata na kumpeleka mahakamani,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, muda umefika kwa wakimbizi wa Burundi kurudi nchini mwao, kwasababu zile sababu ambazo zilikuwa zinazuia zoezi la kuwarudisha kwao wakimbizi hao kwa sasa havipo tena kwasababu nchi hiyo ina amani.

Alisema Serikali ya Tanzania chini ya Rais John Magufuli imejiridhisha sababu kubwa iliyowaleta wakimbizi hao wa Burundi nchini ya kutowepo kwa amani haipo tena na kwamba kwa sasa Burundi ipo salama kiulinzi na kiusalama pia kisiasa hivyo wakimbizi hao wanapaswa kurudi nchi mwao wote bila kuwepo kikwazo chochote.

"Wanaosema Burundi haina amani wanaipaka matope nchi hiyo kwani jambo hilo halina ukweli wowote na Tanzania imefanya uchunguzi wa kutosha na kujiridhisha kuwa amani ya kudumu ipo nchini humo, Oktoba Mosi tutaanza kutekeleza mkataba wa pande tatu wa kurudishwa kwa wakimbizi 2000 kila wiki wa Burundi kwenda nchini mwao," alisema Lugola.

Naye Waziri Barandagiye, kwa upande wake alisema Burundi iko tayari kutekelezwa kwa makubaliano ya pande tatu ya kuhakikisha wakimbizi wote wa Burundi wanaohifadhiwa kwenye makambi mbalimbali ya wakimbizi mkoani nchini wanarudi Burundi lakini wanashangazwa na namna Shirika la Kuhudumia Wakimbizi linavyoendesha zoezi hilo kwa kasi ndogo.

Waziri Lugola na Barandagiye walitembelea Kambi ya Nduta, Wiliyani Kibondo na Mtendeli iliyopo Wilayani Kakonko mkoani humo, kwa lengo la kuhamasisha wakimbizi katika kambi hizo kurejea nchini kwao kwa hiari.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na  0714006521


Share:

Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Mabula Aagiza Kaya 13 Kuondoka Eneo La Wafugaji Tabora

Na Munir Shemweta, WANMM IGUNGA
Serikali imeagiza kaya 13 zilizopo eneo la wafugaji katika hifadhi ya Wembele kijiji cha Makomelo kitongoji cha Kitulo wilayani Igunga mkoani Tabora kuondoka katika eneo hilo kwenda eneo ililopangiwa la wakulima ili kuondoa mgogoro wa muda mrefu kati ya wafugaji na wakulima.

Kauli hiyo ya serikali inafuatia wakulima kuvamia eneo la wafugaji katika kijiji hicho na kuzuia wafugaji kulisha mifugo yao jambo lililokiuka makubaliano ya awali ya kila upande kubaki katika eneo lake kwa ajili ya shughuli zake.

Akizungumza na pande mbili za wafugaji na wakulima katika kijiji cha Makomelo akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi na kukagua Masijala ya Ardhi katika mkoa wa Tabora jana tarehe 24 Agosti 2019, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alisema serikali haiwezi kuendelea kuona watu wanapigana na kuuana wakati mipaka ya eneo hilo ilishawekwa.

Alisema, eneo linalogombaniwa na pande hizo mbili linajulikana kama eneo la hifadhi ya Wembele chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii lakini kwa busara serikali iliamua kutoa matumizi kwa ajili ya wakulima na wafugaji na kuweka mipaka lakini wakulima wameamua kukiuka utaratibu na kuvamia eneo la wafugaji kitu alichokieleza kuwa hakikubaliki.

‘’Waliokiuka utaratibu wa awali waondoke, ziko kaya 13 hatuwezi kuendelea na vifo katika haya, serikali ishaweka mipaka kinachotakiwa ni kuheshimu maamuzi’’ alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, kinachotakiwa kwa pande mbili zinazogombana ni kuheshimu makubaliano hadi hapo Wizara ya Maliasili na Utalii itakalichukua eneo lake.

Aliwataka wafugaji na wakulima wasiendelee kufanya vurugu na kuheshimu makubaliano waliyokubaliana awali ambapo alimuagiza Mkuu wa wilaya ya Igunga mkoani Tabora John Mwaipopo kuhakikisha anasimamia zoezi la kuondoka kwa kaya 13 katika eneo la wakulima.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitulo katika Kata ya Igunga Zephania Ndassa alimueleza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa, eneo hilo limekuwa na mgogoro mkubwa kati ya wakulima na wafugaji pamoja na kuwepo makubaliano yaliyofikiwa mwaka 2004 wakati wa uongozi wa Mkuu wa mkoa wa Tabora wakati huo Marehemu Abbas Kandoro.

Kwa mujibu wa Ndassa pande zinazopingana zinatambua kabisa kama eneo hilo ni hifadhi ya Wembele tangu mwaka 2002 na wao wanalitumia eneo hilo wakifahamu pindi litakapohitajika litachukuliwa na Maliasili lakini mgogoro huo umekuwa ukuwasumbua.

Naye Mkazi wa kijiji cha Makomelo Christopher Shigela alimuomba Dkt Mabula kunusuru mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu hasa baada ya juhudi za wilaya na mkoa kugonga mwamba na kubainisha kuwa, pamoja na uwepo alama zilizoainisha maeneo ya wakulima na wafugaji lakini wakulima wameendelea kufanya uvamizi jambo lililozusha mgogoro uliosababisha watu kuumia na wengine kupoteza maisha.


Share:

Omar al-Bashir kuomba kuachiwa kwa dhamana katika kesi ya rushwa

Wakili wa rais wa zamani wa Sudan Omar al-Bashir amesema kuwa atawasilisha ombi la kutaka Bashir aachiliwe kwa dhamana wakati kesi yake ya mashitaka ya rushwa ikiendelea. 

Ahmed Ibrahim amewaambia wanahabari nje ya mahakama kuwa wataiomba mahakama kumuwachia kwa dhamana kwa sababu hiyo ni kesi ya kawaida. 

Bashir anashitakiwa kwa kumiliki kinyume cha sheria fedha za kigeni na kupokea zawadi katika njia isiyo rasmi. Wakati wa kusikilizwa kesi yake, jaji alitaka kupewa ombi la dhamana kupitia maandishi, akisema ofisi yake iko tayari kulipokea wakati wowote. 

Afisa wa polisi aliiambia mahakama Jumatatu kuwa Bashir alikiri kupokea mamilioni ya dola kutoka kwa Saudi Arabia.


Share:

WAHUNI WAIBA NG'OMBE KWA KUTUMIA PIKIPIKI


Baadhi ya Madiwani katika Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamelalamikia kuwepo kwa matukio ya wizi wa mifugo, kunakofanywa na baadhi ya wananchi katika Wilaya hiyo, hali inayopelekea baadhi ya wananchi kutojikita zaidi kwenye shughuli za maendeleo, badala yake wanakesha kulinda mifugo yao.

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani, baadhi ya Madiwani hao wamesema watu hao wamekuwa wakiwabeba ng'ombe kwenye bodaboda na kukimbia nao vijiji vya jirani.

"Hatuwezi kujadili maendeleo wakati kuna vitendo vya kihalifu vya wizi wa mifugo na haipiti siku hujasikia mifugo haijaibiwa kwenye eneo hili, kinachoshangaza zaidi ni wezi wanaiba ng'ombe na wanawabeba kwenye pikipiki, lazima tufanye kitu kwa niaba ya wananchi wetu." amesema Mwenyekiti wa Halmashauri Juma Porini

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurudin Babu, ameagiza Kijiji kitakachobainika, kuiba ng'ombe basi wananchi wake hawana budi kuingia gharama ya kulipa ngombe hao.

"Nimeshaagiza tayari endapo Ng'ombe wataibiwa kwenye Kijiji fulani, wafuatilie nyayo na endapo watabaini hadi Kijiji alipoelekea huyo ng'ombe basi hicho Kijiji kitalazimika kulipa." amesema Nurudin Babu
Share:

COMOROS’ MOVE TO SADC - FRANCOPHONES SEEKING ALTERNATIVES TO ‘FRANçAFRIQUE’

By Victor Mlunde
Economic pan-Africanism

Political pan-Africanism has been an important pillar in achieving political independence of the continent in the last 50 years but this will be given a full meaning if Africa will be able to achieve economic pan-Africanism, through expansion and amalgamation of free trade areas across the continent as well as harmonization of trade, customs and fiscal policies, amongst each other.


To effect economic pan-Africanism, ‘independent’ African states will have to think beyond the traditional ‘comfort’ of political sovereignty by enhancing trade amongst each other and review their approach towards bilateral and multilateral engagement in the global economic environment.

In the recent past, many French-speaking African countries (African francophones) have started breaking the taboo by evaluating their partnership with France, operating under the auspices of ‘Françafrique’, the post-colonial French foreign policy towards Africa, accused by many for economic impoverishment and political instability in its former colonies, allegedly through protection of autocratic regimes in exchange for business deals.

                                 
In August 2019, the Union of Comoros participated in SADC summit in Tanzania for the first time, following successful admission in 2018, following the footsteps of Madagascar, Mauritius and Seychelles.

Earlier in the year, two other francophones Burundi and the DRC sought to join the SADC and EAC regional economic blocs respectively.

In the same spirit, many francophones in West Africa have recently started engaging in open discussions about giving up the CFA franc currency union for own ECOWAS currency, the ‘ECO’ at least from 2020.

Back in France, a movement to reform ‘Françafrique’ has gained enough political correctness that former presidents Nicolas Sarkozy and Francois Hollande were once reported to vowed to end the ‘old-fashioned’ Françafrique policy during their campaigns for office.

Looming demise of CFA franc currency

In 1945, France reportedly agreed to eventually grant independence to its African colonies, provided they accept to use the CFA franc currency, pegged into French franc while France retained a monopoly on their raw materials. In 1999, the CFA franc was pegged into euro, with the financial backing of the French treasury which prints and regulates the currency.   

           
                                                                     
Italian deputy prime minister once blamed France for impoverishing Africa and encouraging migration to Europe, by printing money for 14 African states and pegging their currencies to the French franc. 

CFA franc requires countries to store up to 50% of foreign exchange reserves with the French treasury, in something called an “operational account” – In doing so, African countries reportedly channel more money to France than they receive in aid.

Proponents of CFA Franc argue the currency helps stabilize national currencies of the currency community and greatly facilitates the flow of exports and imports between France and member countries.

Francophones in the EAC

The Democratic Republic of Congo (DRC), a former strategic partner of France during Zaire days, eventually applied to join the EAC in 2019 to enjoy economies of scale, doing away with the traditional lopsided partnership with France, that Mobutu helped supervise. 

With its only chief sea port Matadi located further away to the Atlantic side of the continent, the East African Indian ocean coast obviously provides an alternative shorter sea route for imports to the Eastern, central and Southern parts of the vast central African country.

Rising from the bottom of ethnic and civil strife partly blamed on France, landlocked-Rwanda and Burundi resolved to join the East African Community a decade ago, to enhance stability, reconstruction and development. 

In 2008, Rwanda abandoned French as a medium of instruction in all public schools at all levels for English, Kinyarwanda and Kiswahili as lingua franca.  She further joined the Commonwealth in 2009, to enhance Rwanda’s participation in regional and global economic development on own terms.

Geographical proximity and historical ties 

Tanzania, a SADC pioneer and EAC powerhouse, is renowned for its stabilizing role in the East African great lakes and Southern Africa, thanks to her active role in liberating, rebuilding, brokering peace deals and solving conflicts as well as resettling refugees and asylum seekers from conflict-prone neighbours. 

For the Comorians (alias ‘ngazidjas’ in Tanzania), a shared historical heritage with East Africa has proved to be of socio-economic, political and strategic importance. Besides Tanzanians making up one of the ethnic groups in the Comoros, the Comorian lingua franca is a cocktail of Kiswahili, Arabic, Comorien and French.

Comoros’ bilateral cooperation with Tanzania is symbiotic – Most of foodstuff, livestock and basic goods to the Comoros are imported from the East African country, 1096 km (681 milles) off the Eastern coast of Africa. With the Air-Tanzania flying to the Comoros three times a week, an average of 600 Comorians reportedly visit Tanzania for business and medical tourism per month.

Through “operation restore democracy”, Tanzania once led an AU military intervention to restore civilian rule and stabilize the Indian Ocean islands in 2006.

A legend in the Comoros suggests the archipelago was eager to join Zanzibar’s union with Tanganyika in the 1970s to form what would have been Tanzacom – The hope for this union is still alive in many ngazidjas today.

Mayotte - An incomplete independence?

The continued occupation of Mayotte by the French, is perhaps the most unreported burning questions missing from mainstream media headlines inside and outside the continent. To date, Mayotte, a sister island of the Union of the Comoros, is still under French occupation and has remained a bone of contention between the Union of the Comoros and France since independence of the former in 1975.

With the three remaining constituent islands of the Union of Comoros archipelago now joining the Southern African Development Community (SADC) to become its 16th member, it is natural that material and moral support in stabilizing the coup-prone archipelago but also liberating Mayotte, the ‘French-dominated’ sister island, may be expected. 

The Comorian Foreign minister Souef Mohamed El Amine once said the decision to join SADC is not related to Mayotte, but its membership could certainly bring it stronger allies and more influence in its dispute with France.

Initially formed by frontline states, SADC evolved into a regional economic bloc in 1980 with the Pan-Africanist zeal to liberate and rebuild the economies of southern Africa nations.

Famous for exporting cloves; ylang ylang, the most coveted flower in perfumery; vanilla; essential oils and scrap aluminum, the Comoros will now have a direct free access of its produce into the European Union market, should they wish to join the EU-SADC Economic Partnership Agreement which came into effect in 2016.

However, to realize genuine economic pan-Africanism, regional blocs should not be used as mere instruments for regime protection, rather member countries will have to revitalize their commitment to democracy and enhance economic integration by removing trade and non-trade barriers; integrating markets; allowing free movement of labour, goods and services and moving towards currency union(s), to counter global monetary and economic hegemony. 

END.

By Victor Mlunde

The author is a Dar es salaam-based independent political analyst with experience in international development and governance work.

He can be reached for comments through vicmlunde007@gmail.com
Share:

Naibu Waziri wa Afya Dkt Ndugulile Aagiza Utekelezaji Majukumu Kamati Za Ulinzi Wa Wanawake Na Watoto

Na Mwandishi Wetu WAMJW
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza watendaji wa Wilaya ya Kigamboni kuhakikisha Kamati za ulinzi wa Wanawake na watoto zinatekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kuisadia jamii ya wanakigamboni kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia .

Dkt. Ndugulile amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa akizindua Kamati ya ulinzi ya wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja inayolenga kushirikisha wanaume na wanawake kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii kupitia mbinu anwai.

Aidha Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa Kamati hizo ikisimamiwa vizuri itakuwa nuzo bora katika mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili vinavyozidi kushamiri kila siku nchini katika jamii na familia zetu.

Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu bure nchini kwa kiasi kikubwa kumepunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake ikiwemo mimba na ndoa za utotoni pamoja na uwepo wa Sheria inayotoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa anayebainika kufanya vitendo hivyo.

”Ni matarajio yangu kwamba kampeni hii ya Kupinga Ukatilili wa Kijinsia Kitaifa italeta mabadiliko makubwa kupitia jumbe mbalimbali zilizoandaliwa kupitia muziki, machapisho, nyimbo, shuhuda na Semina zitakazokuwa zinaendelea kutolewa kwenye majukwaa mbalimbali kipindi cha kampeni’’ alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile pia ameagiza kutafutwa kwa wale waonafanya vitendo vya kikatili katika wilaya ya Kigamboni na Tanzania kwa ujumla na vyombo husika kusimamia na kuhakikisha wanawake na watoto wanapata haki zao.

Akizungumzia hali ya ukatili wa kijinsia nchini Dkt. Ndugulile amesema taarifa ya hali ya Uhalifu nchini ya Mwaka 2017 inaonesha kuwa jumla ya watu 41,416 waliofanyiwa ukatili wa kijinsia walitoa taarifa kwenye vituo vya polisi ikilinganishwa na watu 31,996 waliofanya hivyo mwaka 2016.

Dkt. Ndugulile ameyataja baadhi ya matukio ya ukatili yaliyotolewa taarifa kuwa ni ubakaji, vipigo, matusi, ulawiti, kutupa watoto, ukeketaji na kuwapa mimba wanafunzi na kuongeza kuwa kati ya mataukio hayo 41,416 yaliyotolewa taarifa mwaka 2017 matukio 27,703 sawa na asilimia 67 yalifanywa dhidi ya wanawake na watoto.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa asilimia 40 ya wanawake wa umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili au kingono mara moja au zaidi katika kipindi hicho cha maisha wakati wanawake asilimia 20 wenye umri miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili katika kipindi cha miezi 12 iliyopita.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri amesema kuwa Serikali ya Wilaya itahakikisha wanapambana na vitendo vya kikatili na amewaomba wanawake kutoa taarifa ya vitendo hivyo na kuwataka kutofumbia macho vitendo hivyo na kuacha vipite kwa mwavuli wa ndoa.

“Sisi Serikali tunaheshimu ndoa na dini zote ila tunaangalia uhai wa mwananchi hivyo wanawake wenzangu nawaomba ndoa zisiwe sababu ya kuendelea kufanyiwa vitendo vya kikatili na kuachana inawezekana” alisema Mhe. Sarah

Naye mmoja wa wnawake aliyefanyiwa vitendo vya kikatili Bi. Lucy Sanga ameishukuru Serikali ya Wilaya ya Kigamboni kwa kumsaidia kupambana na vitendo vya manyanyaso ambavyo anafanyiwa na mume wake.

“Mume wangu amekuwa akininyanyasa sasa kwa muda mrefu na imefikia hatua ya kuficha vyombo vya kupikia na kunihamisha chumba chetu cha kukaka na kumleta mama yake mzazi kutoka Musoma na yeye analala humo na me nalala kwenye chumba cha watoto” alilalama Bi. Lucy


Share:

Jumla Ya Mashauri 14 Yafunguliwa Na Kusikilizwa Na Mahakama Inayotembea ‘Mobile Court’

 Na Mary Gwera, Mahakama
Jumla ya Mashauri 14 yamefunguliwa na kusikilizwa na Mahakama inayotembea ‘mobile court’ mkoani Mwanza.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Menejimenti ya Usimamizi wa Mashauri-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya amesema kuwa mashauri hayo yamefunguliwa na kutolewa maamuzi katika kipindi cha mwezi Julai, 2019.

Mhe. Nkya alieleza kuwa Mahakama hiyo inayotembea inaendelea kutoa huduma katika maeneo mbalimbali mkoani Mwanza huku Mahakama nyingine inayotembea iliyopo jijini Dar es Salaam inaendelea kutoa elimu kwa Wadau juu ya uendeshaji wa Mahakama hiyo.

Kwa mkoa wa Mwanza, Mahakama hiyo inafanya kazi katika maeneo ya Igoma, Buswelu na Buhongwa na kwa upande wa Dar es Salaam Mahakama hiyo inatoa huduma katika maeneo ya Bunju ‘ A’, Kibamba, Buza na Chanika.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa Mahakama inayotembea inasikiliza mashauri yote yanayosikilizwa na Mahakama za Mwanzo kama vile migogoro ya ndoa, madai, mirathi na jinai, pamoja na rufaa kutoka Mabaraza ya kata, yakiwemo mashauri yanayojitokeza katika operesheni maalmu zinazofanywa na taasisi/vyombo mbalimbali vya serikali.

Huduma nyingine zitolewazo na Mahakama hiyo ni kutoa taarifa za mashauri, kutoa fomu za viapo na kuthibitisha nyaraka mbalimbali, kufanya usuluhishi kwa wadawa na kutoa elimu kuhusiana na masuala ya Mahakama.

Mnamo Februari 06, 2019, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli alizindua rasmi Mahakama inayotembea lengo likiwa ni kusogeza huduma kwa wananchi na kutoa haki kwa wakati.

Aidha; lengo jingine ni kuwapunguzia wananchi gharama za kufuata huduma za Mahakama mbali na maeneo wanayoishi.

Mahakama ya Tanzania ina mpango wa kutanua wigo wa utoaji huduma hii kwa kuanzisha vituo vingine katika mikoa iliyosalia kwa awamu tofauti


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger