Sunday, 18 August 2019

MEAL Specialist at Save the Children

MEAL Specialist at Save the Children MEAL Specialist   TEAM/PROGRAMME: Programme Development and Quality LOCATION:  Dar-es-Salaam with frequent travel to the field GRADE: POST TYPE: Child Safeguarding: Level 2 – the responsibilities of the post may require the post holder to have regular contact with or access to children or young people ROLE PURPOSE: The MEAL Specialist represents a… Read More »

The post MEAL Specialist at Save the Children appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunities at Oxo Africa Limited, Developers

Overview Oxo Africa Limited is a software Engineering Enterprise focusing on offering software development services. Oxo Africa hiring entry level developers…Oxo Africa Limited is a software Engineering Enterprise focusing on offering software development services to a diverse client base within the East African Region. Our clients range from NGO’s , SME and the public sector. We have a… Read More »

The post Job Opportunities at Oxo Africa Limited, Developers appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali kuuza asilimia 10 ya Mamba nje ya nchi

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Hamis Kigwangala amesema Serikali itaanza kuuza asilimia 10 ya mamba nje ya nchi kwa kile alichokieleza kumekuwa na ongezeko kubwa sana, wanyama wakali kuingia kwenye makazi ya watu.


Waziri amesema Serikali imejhitahidi vya kutosha kuhakikisha suala la ujangiri linaisha na nchini na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa bali changamoto iliyopo, ni wanyama hao kuingia kwenye makazi ya watu.
 
Aidha, Kigwangalla amesema Serikali itauza viboko wote waliopo kwenye maziwa, mabwawa na mito yaliyopo maeneo ya mijini.

Kigwangalla ametaja miongoni mwa maeneo ambayo yana viboko watakaouzwa ni Mpanda, Mafia, Babati na kwamba mauzo hayo yatafanyika kwa  mnada kwa utaratibu ambao utatangazwa wiki ijayo




Share:

Kiswahili Chapitishwa Kuwa Lugha Rasmi ya SADC

Rais Magufuli amesema Wakuu wa Nchi wa SADC kupitisha lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya 4 itakayotumika katika shughuli rasmi za Jumuiya hiyo,ni heshima kubwa kwa Mwl Nyerere ambaye aliongoza Nchi nyingi Afrika katika  Mapambano ya kudai Uhuru akitumia Kiswahili.

Akizungumza leo Jumapili Agosti 18, 2019 katika kilele cha  mkutano wa 39 wa wakuu wa nchi, Rais Magufuli amesema katika kikao kilichofanyika jana Ikulu jijini Dar es Salaam, wakuu hao kwa pamoja wamekubaliana lugha hiyo ianze kutumika.

Lugha zilizokuwa zikitumika katika nchi hizo 16 ni Kiingereza, Kireno na Kifaransa.  Kuanzia sasa Kiswahili kitatumika katika mikutano ya jumuiya hiyo pamoja na machapisho yake mbalimbali.


Share:

CRDB YAWATAKA WANANCHI KUACHA TABIA YA KUWEKEZA PESA KWA WATU BINAFSI WAPELEKE BENKI

Benki ya CRDB tawi la Bukoba mkoani Kagera wamejipanga kutoka elimu kwa makundi mbalimbali ya wajasiriamali hasa akina mama wenye utamaduni kuwekeza fedha zao kwa mtu binafsi jambo ambalo si salama kwa fedha hizo.


 Kauli hiyo imetolewa leo Agosti 18 , 2019 na Meneja Mwandamizi wa Benki ya CRDB Tawi la Bukoba Karlo A. Sendwa wakati akielezea umuhimu wa kutunza fedha katika Benki ili kuondokana na upotevu wa fedha hizo mara zinapotunzwa kwa mtu binafsi.

Sendwa amesema  kuna utamaduni uliojengeka katika jamii hasa kwa baadhi ya wajasiriamali walio katika makundi mbali mbali hasa ya akina mama juu ya kuwekeza fedha za michango ya makundi hayo kwa mtu binafsi huku wengi wao wakiwa na dhana potofu ya kusema kuwa wanaoenda Benki ni matajiri tu jambo linalosababisha upotevu wa fedha hizo na kufanya maendeleo ya vikundi hivyo kurudi nyuma kutokana na mtu binafsi waliomuwekesha fedha hizo kutoweka nazo.

"Bado kuna watu hawajui umuhimu wa kutumia benki hasa akina mama walioko vijijini, utakuta wanasema pesa yetu ya kikundi anayo fulani jambo hili si salama kwani benki ni mahala salama kwa fedha za mtu", alisema.

Aliahidi utoaji elimu kwa makundi sambamba na kushirikiana nao ili wapate kujua njia sahihi ya utunzaji fedha zao.

Katika hatua nyingine amempongeza mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti pamoja na uongozi wake  kwa kubuni wiki ya uwekezaji kagera kwani Benki hiyo ya CRDB imenufaika na wiki hiyo ambapo amewahimiza wafanya biashara na wakulima kuacha woga katika kuzifikia taasisi za kifedha kwani usalama wa kuwekeza pesa kwa mtu ni sawa na sifuri.

Na Lydia Lugakila - Malunde 1 blog
Share:

Idadi Kubwa Ya Hati Za Ardhi Ofisi Ya Msajili Kanda Ya Magharibi Yamshtua Naibu Waziri Mabula

Na Munir Shemweta, WANMM TABORA
Idadi kubwa ya Hati za Ardhi takriban12,000 katika Ofisi ya Msajili wa Hati imemshtua Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alipofanya ziara Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi.

Mwishoni mwa wiki Dkt Mabula akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi sambamba na kukagua masijala ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Tabora alitembelea Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi kujionea utendaji kazi wa kanda inayojumuisha mikoa ya Tabora, Katavi na Kigoma.

Akiwa Ofisi ya Msajili wa Hati, Dkt Mabula alielezwa na Msajili wa Hati wa Kanda ya Magharibi Julian Ngonyani kuwa ofisi yake ina takriban hati 12,000 ambazo ziko tayari kwa ajili ya kukabidhiwa kwa waombaji lakini wahusika hawajajitokeza kuchukua kwa sababu ambazo hazijulikani.

Naibu Waziri Dkt Mabula alishangazwa na idadi kubwa ya Hati hizo na kubainisha kuwa Hati zilizopo Ofisi ya Msajili wa Hati kama zingechukuliwa basi wahusika wangekuwa na nyaraka zinazoonesha umiliki halali wa maeneo yao sambamba na hati hizo kuwasaidia katika shughuli za maendeleo kama vile kukopa pesa katika mabenki mbalimbali.

Alisema, Halmashauri katika mikoa ya Kanda hiyo ya Magharibi zinapaswa kuwajibika kwa kuhakikisha waombaji wanapata hati ambapo alizitaka kuandaa utaratibu maalum utakaowezesha Hati kupelekwa kwenye halmashauri husika na waombaji kuzichukua.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, utaratibu huo utawawezesha wananchi kuchukua hati zao kwa urahisi bila ya usumbufu ambapo hivi sasa waombaji hulazimika kuzifuata Ofisi ya Kamishna wa Kanda jambo alilolieleza kuwa ni usumbufu kwani baadhi ya waombaji hulazimika  kutembea umbali mrefu hasa kwa wale wanaokaa maeneo yaliyo mbali na Ofisi ya Kanda.

‘’Halmashauri inaweza ikandaa utaratibu wa kupelekewa Hati za Ardhi katika maeneo yao na Ofisi ya Kamishna wa Kanda na jukumu la halmashauri litakuwa kugharamia pesa ya kujikimu kwa watumishi wa Kanda watakaopeleka hati na kuzikabidhi kwa waombaji, hiyo itasaidia kuwapunguzia mzigo wananchi’’ alisema Dkt Mabula.

Katika Hatua Nyingine, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameikabidhi Hati ya Kiwanja No 47 Block A Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora kilichopo eneo la Kanyenye Manispaa ya Tabora mkoni Tabora baada ya kiwanja hicho kuwa na mgogoro wa muda mrefu Kati ya ofisi ya CCM na Shirika la Utangazaji (TBC).

Dkt Mabula alimkabidhi hati hiyo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora Mohamed Katete ambapo makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Solomon Kasaba, Katibu UWT mkoa Rehema Mohamed, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharbi Idrissa Kayera na Msajili wa Hati wa Kanda Julian Ngonyani.

Katika Makabidhiano hayo, Dkt Mabula alisema Chama cha Mapinduzi kina maeneo mengi inayomiliki lakini siyo yote yenye hati na kubainisha kuwa kukabidhiwa hati hiyo iwe chachu kwa chama kuhakikisha maeneo yake yote yanakuwa na hati kuepuka migogoro.

Ametoa wito kwa CCM kuhakikisha maeneo ya Kata yanayomilikiwa na chama hicho yasiyopimwa yanapimwa na kupatiwa hati na hata yale yasiyo pimwa basi yawe na mipaka na kubainisha kuwa kwa kufanya hivyo kutaondoa migogoro na kukifanya chama kuwa na miliki halali ya maeneo yake.


Share:

LIVE : MwenyeKiti wa SADC Rais John Magufuli Akihitimisha mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya SADC

LIVE : MwenyeKiti wa SADC Rais John Magufuli Akihitimisha mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya SADC


Share:

Rais wa DRC Felix Tshisekedi Aiomba Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (Sadc) Isaidie Kulidhibiti Kundi la MTN Na Ugonjwa wa Ebola

Nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (Sadc) zimeombwa kuchukua jitihada kukabiliana na matishio ya ugaidi na ugonjwa wa Ebola.

Maombi hayo yaliwasilishwa na rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wakati wa mkutano wa 39 wa jumuiya hiyo unaoendelea nchini.

Rais Tshisekedi alisema nchi yake bado imeendelea kukabiliwa na matishio ya usalama hasa katika eneo la Mashariki kutokana na kuwapo kwa kikundi cha MTN ambacho kinatumia mfumo wa kushambulia kwa mtindo wa ugaidi.

“Ndiyo maana nilitengeneza mkakati wa kuimarisha mamlaka ya serikali ili kuzuia kundi hili kuendelea na tumeweka mfumo wa mapatano kwa makundi yote ili kusaidia kurejesha amani.

“Mtusaidie tuwe na mshikamano ili kupitia kwenu tutoke na tamko litakalosaidia kuimarisha kundi la Monusco (Majeshi ya walinda Amani ya Umoja wa Mataifa) ili liweze kukabiliana na makundi hasimu,” alisema Rais Tshisekedi.

Pia aliziomba nchi wanachama kuunda kundi la kikanda litakalosaidia kutokomeza vikundi vya kigaidi ambavyo vimekuwa tishio kwa baadhi ya nchi.

Kuhusu ugonjwa wa Ebola alisema wanashirikiana na Shirika la Afya duniani  (WHO) na tayari wamechukua hatua mbalimbali kuudhibiti na kutaka nchi wanachama kuendelea kuwasaidia kuudhibiti.

Pia alizihimiza nchi wanachama kuendeleza ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme ili kuwa na nishati ya kutosheleza mahitaji ya Sadc.

“Katika suala la kilimo nchi zetu zina fursa nyingi sana na sisi tuko tayari kwa ajili ya utekelezaji wa mikakati mbalimbali, naamini mkutano huu wa marais na viongozi wa serikali utafikia uamuzi thabiti wa kuhakikisha kunakuwa na mazingira wezeshi ya kuimarisha viwanda ili kuwa na maendeleo jumuishi,” alisema.


Share:

Waasi wa Kihouthi washambulia kiwanda cha mafuta nchini Saudia Arabia

Waasi wa kihouthi nchini Yemen hapo jana walifanya Shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani dhidi ya kisima cha mafuta cha Shaybah nchini Saudi Arabia kinachotoa takriban mapipa milioni moja ya mafuta ghafi kwa siku. 

Hilo ni shambulizi la pili la aina hiyo katika sekta hiyo muhimu ya mafuta nchini humo katika siku za hivi karibuni.

Vyombo vya habari nchini humo viliwanukuu maafisa wa serikali ya Saudi Arabia wakisema kuwa uzalishaji mafuta katika kisima hicho haukuathirika Kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali ya Saudia Aramco, imetoa taarifa inayokiri kutokea moto kiasi katika kituo hicho kinachotoa mafuta huko Shaybah.

Waasi wa kihouthi wamefanya misururu ya mashambulizi ya angani yanayolenga maeneo tofauti tofauti ya Saudi Arabia katika miezi ya hivi karibuni. 

Mzozo huo nchini Yemen kwa kiasi kikubwa unaonekana kuwa ni vita baina ya Saudi Arabia yenye Waislamu wa dhehebu la Kisunni na Iran yenye Waislamu wa madhehebu ya Kishia.


Share:

LIVE -- MWENYEKITI WA SADC RAIS DKT JOHN MAGUFULI AKIHITIMISHA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI WA JUMUIYA YA SADC

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili 18 August




Share:

Saturday, 17 August 2019

MWINYI, MKAPA, KIKWETE, KARUME WAHUDHURIA MKUTANO KUSHUHUDIA RAIS MAGUFULI ATAKAVYOKABIDHIWA UENYEKITI WA JUMUIYA YA NCHI ZA SADC

 Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii

MARAISI wastaafu wa Serikali ya Tanzania wamehudhuria Mkutano Mkuu wa 39 unaofanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam  kushuhudia Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk.John Magufuli akikabidhiwa Uenyekiti wa jumuiya hiyo.

Katika mitandao ya kijamii baadhi ya watu wasiokuwa na njema walikiwa wakizusha kuwa Dk.Magufuli amesusiwa mkutano huo na watangulizi wake.Hata hivyo uzushi wao umekosa mashiko kwani viongozi wa ngazi mbalimbali wakiwamo marais hao wote wastaafu wamehudhuria mkutano huo wa kihistoria.

Marais wastaafu ambao wamehudhuria ni Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ambaye ni Rais ww Serikali ya Awamu ya Pili,Benjamin Mkapa ambaye ni Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu,Jakaka Kikwete aliyekuwa Rais wa Awamu ya Nne na kwa upande wa Zanziabar Rais mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Amani Karume.

Mbali ya wastaafu hao kuwemo kwenye mkutano huo ambao pia wametambulishwa kwa wageni mbalimbali kutoka nchi 15 za jumuiya hiyo,pia viongozi wengine wa Serikali ya Tanzania waliohudhuria ni Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais Mama Samia Suluh Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Wengine ni Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu Balozi John Kijazi,mawaziri, viongozi wa ngazi mbalimbali wastaafu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Poul Makonda.Pia wamehudhuria watu mashuri wa ndani na nje ya Tanzania.

Pamoja na shughuli mbalimbali ambazo zinaendelea kwenye mkutano wa jumuiya hiyo ambao utafanyika kwa siku mbili,tukio ambalo linasubiriwa na Watanzania wengi ni kuona Rais Dk.Magufuli anakabidhiwa Uenyekiti wa SADC.
Nafasi hiyo ya Uenyekiti wa SADC kwa Tanzania mara ya mwisho ilishikiliwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa miaka 16 iliyopita na sasa anakwenda kukabidhiwa Rais mchakazi Dk.Magufuli.

Hata hivyo nchi mbalimbali za jumuiya hiyo zimeonesha matumaini na imani kubwa kwa Rais Magufuli hasa kutokana na utendaji wake tangu akiwa Rais ambaye anaamini katika wananchi kufanya kazi na nchi kujitegemea.

Pia amekuwa na kauli mbiu ya Tanzania ya viwanda ambayo itaipeleka nchi uchumi wa kati.Kwa nchi za SADC moja ya mkakati wao ni kuhamasisha viwanda kwa nchi wanachama kazi ambayo Rais Magufuli ameianza kabla ya kukabidhiwa uenyekiti,hivyo nchi za jumuiya hiyo zinaamini akiwa Rais Magufuli atawafikisha kwenye nchi ambazo uchumi wake utatokana na viwanda.
Share:

Wananchi Bahi Watakiwa Kutowaficha Na Kuwanyanyapaa Walemavu

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Wananchi wa kata ya ibihwa wilayani bahi wametakiwa kutowaficha watoto wao ndani kwa kigezo cha ulemavu ,Kama  sheria ya mtoto kifungu cha 8  inavyotoa katazo la jamii kumnyima mtoto haki ya kusoma kwa kigezo cha ulemavu.
 
Akizungumza katika mkutano wa wanachi uliyoratibiwa na shirika la International Aids service jana mkoani Dodoma meneja wa shirika hilo Alan Kamnde alisema ukosefu wa elimu  kwa wanachi kuhusu umuhimu wa kumthamini mtoto mwenye ulemavu bado ni kikwazo kikubwa katika jamii.
 
“Lengo la shirika hili ni kuhakikisha  jamii inafikiwa na kupewa uwelewa kuweza kuwaruhusu watoto kupata haki ya kielimu na Zaidi kuweza kuwajumisha watoto wenye ulemavu na wasiyo na ulemavu kujumika na kupata elimu pamoja kwasabau watoto  wote ni sawa”Alisema kamnde. 
 
Naye afisa mradi wa shirika hilo Jane Mjidange amesema ni vyema wazazi wakawapenda watoto ,samabmba na kuomba mamlaka zinazohusika kuyashughulikia matukio ya watoto wenye ulemvu kuyachukulia uzito matukio yao.
 
“Jamani mama zangu hakuna mtoto aliyeomba mungu amuumbe akiwa mlemavu hivyo msiwatenge na ni vizuri hata zile mamlaka zinazohusika zikachukulia uzito kesi za watoto”alisema jenipha.
 
 Diwani wa kata ya Ibihwa, Daudi lesaka alisema  katika kata yake kumekuwa na mimba za mara kwa mara kesi zimefikishwa mahakani na zinafanyiwa kazi  kwa mujibu wa sharia
 
Aliongeza  kwenye kata yake atachukua hatua kwa familia zote aambazo zimezuia kuwapeleka watoto shule
 
“Kuhusu swala la mimba tumechukua hatua za kuzipeleka kesi zote mahakamani na zinzshughulikiwa na kwa upande wa familia ambazo zimeshindwa kuwapeleka watoto shule nao tutawachukulia hatua haraka sana” alisema lesaka.


Share:

AFISA UVUVI MULEBA AWAONYA WAVUVI HARAMU



Kaimu Afisa uvuvi wilayani Muleba mkoani Kagera Maengo Nchimani 
Na Lydia Lugakila -Malunde1 blog
Kaimu Afisa Uvuvi wilayani Muleba mkoani Kagera Maengo Nchimani ametoa onyo kali kwa wananchi wanaojihusisha na vitendo vya uvuvi haramu vinavyosababisha kipato cha mkoa wa Kagera kushuka.

Nchimani ametoa onyo hilo wakati akiongea na baadhi ya wafanyabiashara waliojitokeza katika uwanja wa Gymkana katika Manispaa ya Bukoba ambako imefanyika wiki ya uwekezaji Kagera yenye lengo la kutangaza fursa mbalimbali zilizopo mkoani Kagera.

Afisa huyo amesema vitendo vya uvuvi haramu vinavyoendelea katika baadhi ya maeneo wilayani Muleba mkoani hapa vinakwamisha maendeleo na jitihada za mkuu wa mkoa wa kagera Brigedia Jenerali Elisha Marco Gaguti za kuutangaza mkoa wa kagera kama sehemu ya uwekezaji ambapo wahitaji wa mazao hayo ya samaki kutohitaji samaki waliokosa ubora na thamani.

Amesema kuwa sheria kali zitachukuliwa dhidi ya wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo huku akitaja kuanzisha doria za usiku ili kuwabania wale wote wanaofanya vitendo hivyo .

Akielezea wilaya hiyo amesema kuwa wilaya ya Muleba ina zaidi ya mitumbwi zaidi ya 400 na inavua dagaa kwa wingi na uzalishaji wake ni kwa asilimia kubwa hivyo amewataka wananchi hao kuacha tabia hiyo mara moja ili kupata wawekezaji wengi toka nje ya nchi.

Amesema kuwa wilayani hiyo ina changamoto ya kutokuwa na kiwanda cha kuongeza thamani ya zao hilo hivyo kuwataka wawekezaji kujitokeze kwa wingi ili kuinua uchumi wa Kagera .

Amesema juhudi kubwa za utoaji elimu juu ya uvuvi haramu zinafanyika ili kunusuru kizazi cha samaki kwa pato la kagera na taifa zima.


Share:

RAIS MAGUFULI AIOMBA JUMUIYA YA KIMATIAFA KUIONDOLEA VIKWAZO ZIMBABWE


Rais  Magufuli ameiomba Jumuiya ya Kimataifa kuiondolea vikwazo vya kiuchumi nchi ya Zimbabwe ambapo amesema kuwa vikwazo hivyo vimelemaza uchumi wa taifa hilo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumamosi Agosti 17, alipokuwa akihutubia wakuu wa nchi Wanachama Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kukabidhiwa uenyekiti wa jumuiya hiyo na Rais wa Namibia, Dk Hage Geingob ambapo ataingoza kwa kipindi cha mwaka mmoja.

"Zimbabwe wamekuwa kwenye vikwazo kwa muda mrefu, hiki kifungo tunaathirika sisi wote, napenda kupendekeza kupitia mkutano huu kuziomba Jumuiya za Kimataifa ziiondolee vikwazo Zimbabwe, na nawaomba wanachama wote tulisemee hili." amesema Rais Magufuli

Zimbabwe iliwekewa vikwazo na mataifa ya Magharibi kutokana na hatua ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Robert Mugabe, kuchukua kwa lazima ardhi ya wahamiaji wenye asili ya kizungu.


Share:

Rais Magufuli Akabidhiwa Uenyekiti Wa SADC Na Kuitaka Sekretarieti Ya SADC Kuchukua Hatua Kukuza GDP Ndani Ya Jumuiya

Na Mwandishi Wetu,MAELEZO
RAIS Dkt John Magufuli amekabidhiwa rasmi nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) huku akiitaka Sekretarieti ya Jumuiya hiyo kuchukua hatua za makusudi ili kuharakisha ukuaji wa Pato la Uchumi la Taifa ndani ya Jumuiya hiyo ambalo limekuwa likishuka mwaka hadi mwaka.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo leo Jumamosi (Agosti 17, 2019) Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ukuaji wa Pato la Taifa katika jumuiya hiyo umekuwa si wa kuridhisha, pamoja na nchi nyingi za Jumuiya hiyo kuwa na wingi wa utajiri wa raslimali.

Rais Magufuli alisema Sekretarieti ya Jumuiya hiyo haina budi kuweka mikakati na mipango madhubuti kwa Nchi wanachama ndani ya jumuiya hiyo kuhakikisha kuwa zinaweka na kuandaa mazingira bora na wezeshi yenye uwezo wa kutoa fursa za ukuaji wa uchumi ikiwemo ukuzaji wa sekta ya biashara ndani ya jumuiya hiyo.

“Mwaka 2005, 2006 na 2007 ukuaji wa Pato la Taifa ndani ya Jumuiya lilikuwa kwa asilimia 6.6 (2005), 7.3 (2006) na 8.0 (2007) lakini mara baada ya hapo ukuaji wake haukuwa wa kuridhisha ambapo mwaka 2012 ilikuwa (4.4), 2013 (4.3), 2014 (3.4), 2015 (2.2), 2016 (1.4), 2017 (3.0) na 2018 (3.1)” alisema Rais Magufuli.

Alisema ili kuweza kukuza uchumi Nchi za SADC, Viongozi wa Mataifa hayo hayana budi kuwa na viwango, sera, sheria na kanuni za pamoja zinazotoa fursa kwa nchi hizo kuwa na mfumo wa pamoja utakaowezesha jumuiya hiyo kuweza kubadilishana ujuzi, uwezo na kuuziana bidhaa na kuondoa masharti mepesi yatakayorahisha ukuaji wa uchumi.

Akifafanua zaidi, Rais Magufuli alisema pamoja na Jumuiya hiyo kujiwekea malengo kwa kila Nchi za jumuiya hiyo kukuza uchumi wake angalau kufikia kiwango cha asilimia 7 mwaka 2018 kwa kila Nchi, lakini ni nchi chache zilizofanikiwa kufikia kiwango hicho, hivyo juhudi za pamoja zinahitajika katika kuhakikisha kuwa kiwango hicho kinafikiwa kwa nchi zote.

Aliongeza kuwa malengo ya pamoja yanapaswa kuwekwa na Nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa taarifa za biashara ambazo Mataifa mengi ya Asia yamekuwa yakitumia fursa hiyo pamoja na kuimarisha na kujenga viwanda vyenye uwezo wa kuzalisha bidhaa vitavyowezesha kupunguza gharama za ununuzi wa bidhaa kutoka nje ya Jumuiya hiyo.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema pamoja na mafanikio mbalimbali ambayo tayari yamepatikana, zipo baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa zikiikabili jumuiya hiyo ikiwemo majanga ya binadamu, njaa na ukame ambazo zimefanya ukuaji wa uchumi katika baadhi ya nchi wanachama kuweza kuathirika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti aliyemaliza muda ambaye pia ni Rais wa Namibia Dkt. Hage Geingob alisema Jumuiya hiyo ina imani na Uongozi mpya wa Rais Dkt. John Magufuli kutokana na utendaji kazi na msisitizo alionao katika kusimamia malengo ya uanzishaji wa jumuiya hiyo katika kuleta maslahi na maendeleo ya wananchi waliopo ndani ya jumuiya hiyo.

Anaongeza kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Uongozi wake, Jumuiya hiyo imeweza kutekeleza miradi na programu mbalimbali kupitia Mpango kazi wa miaka mitano wa Jumuiya hiyo (2015-2020) ikiwemo kutatua tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana ambalo limekuwa likiongezeka siku hadi siku.

Aidha aliongeza kuwa ili kufikia Malengo mapana ya Jumuiya hiyo, Nchi wanachama hazina budi kuweka mkazo katika  kujenga ushirikiano baina ya sekta binafsi na ile ya umma kwa kutekeleza miradi na programu mbalimbali pamoja na usimamizi wa rasilimali muhimu zilizopo ndani ya jumuiya hiyo ikiwemo nishati, madini na viwanda.

Awali Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo, Dkt. Stegomena Tax aliisifu Tanzania kutokana na kiwango kizuri cha ukuaji wa uchumi wake uliofikia asilimia 7.0 na kuwa Nchi ya mfano katika Jumuiya hiyo, hatua iliyotokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha Dkt. Tax pia aliusifu utekelezaji wa  mradi wa kufua umeme wa maji wa Nyerere katika Maporomoko ya Mto Rufiji kwa kuwa ni miongoni mwa miradi ya kimkakati ambayo inatarajia kumaliza changamoto ya ukosefu wa nishati ya uhakika katika Nchi za SADC.

MWISHO


Share:

Soko La DSE Laendelea Kushika Nafasi Ya Tatu Barani Afrika Kwa Ubora

Na. Peter Haule, WFM, Dar es Salaam
Soko la Hisa la Dar es Salaam- DSE limetakiwa kuendelea kujiimarisha kwa kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kuwekeza zaidi katika soko hilo lengo likiwa kukuza kipato chao na uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Khatibu Kazungu, alipofanya ziara katika Soko hilo ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.

Dkt. Kazungu alisema kuwa, idadi ya watu takribani laki tano ambao wamewekeza katika Soko hilo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 50, hivyo ni vema DSE ikatumia majukwaa mbalimbali kuhamasisha wananchi kushiriki katika Soko hilo ili kukuza kipato chao kutokana na faida zake.

Alisema ushiriki wa watu wengi katika Soko hilo hususani walio katika sekta ya uvuvi, mifugo na kilimo, kutaongeza chachu ya maendeleo yao na Taifa kwa ujumla hasa katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea katika uchumi wa kati uliojikita katika viwanda.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DSE, Bw. Moremi Marwa, amesema kuwa Soko la DSE lipo kwa ajili ya kuwezesha wawekezaji kuwekeza katika maeneneo mbalimbali kulingana na bidhaa zilizopo sokoni.

Alisema ili kuleta bidhaa zaidi katika Soko la Mitaji, DSE imekuwa ikifanya juhudi kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuziwezesha Serikali za Mitaa na Halmashauri za Miji na Majiji kuweza kupata fedha kupitia mifumo ya Masoko ya Mitaji ili kuweza kuwekeza katika miradi ya Maendeleo ya Uchumi na Kijamii.

Alieleza kuwa mifumo ya masoko ya Mitaji katika Halmashauri inataleta wigo mwingine wa upatikaji wa fedha kwa ajili ya kujenga miradi ya miundombinu na viwanda katika miji na majiji nchini.

Bw. Marwa alibainisha kuwa DSE huwapa wajasiriamali, wafanyabiashara, wawekezaji pamoja na Serikali kutumia soko kwa ajili ya masuala ya upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu na wa kati katika kusaidia wafanyabiashara kuboresha biashara zao pia kwa Serikali Kuu kuendesha miradi mbalimbali ya Serikali hasa iliyo katika Bajeti.

“Soko la DSE limekua kutoka Sh. trilioni 16 hadi trilioni 20 katika kipindi cha miaka minne,  hati fungani Sh. trilioni 3.5 hadi trilioni 9.5. na kwa wawekezaji kutoka  220,000 na sasa 550,000; ukwasi na miamala sokoni imeongezeka kutoka wastani wa  takribani Shilingi bilioni 50 kwa mwaka hadi zaidi Shilingi bilioni 500  kwa mwaka na katika miamala na ukwasi wa hati fungani kutoka wastani wa Shilingi bilioni 300 hadi kufikia wastani wa takribani Shilingi bilioni 900 kwa mwaka”, alieleza Bw. Marwa

Bw. Marwa alisema kuwa kumekuwa na maendeleo mazuri katika vigezo hivyo ambavyo hutumika katika kupima maendeleo ya Soko, pia DSE imeongeza tija na ufanisi kwa kuwa kampuni inayojiendesha kwa faida na kulipa faida hiyo kama gawio kwa wanahisa wake, ikiwemo Serikali.

Alisema kuwa DSE ilipata uanachama wa kidumu katika Chombo cha Kimataifa kinachosimamia masoko ya Hisa (World Federation of Exchanges) mwanzoni mwa mwaka huu, ikiwa ni soko la saba kufikia hatua hiyo barani Afrika.

Afisa huyo Mtendaji Mkuu wa DSE alisema Soko hilo limewekwa kwenye uangalizi “Watch-List” na Shirika la Kimataifa la Kupima viwango na ubora vya Uchumi na Masoko ya Mitaji “Country and Market Classification” kwa nia ya kuifanya DSE kuwa “Frontier Market Status” ifikapo Septemba Mwaka huu.

Hatua hiyo inatoa fursa ya kulitangaza zaidi soko kwa wawekezaji wa nje lakini pia kupata mitaji kutoka kwa wawekezaji wanaotoka nje wanaokuja kuwekeza katika kampuni na biashara nchini na kwenye miradi mbalimbali.



Soko la DSE limekuwa la tatu katika masoko 30 yaliyopo barani Afrika kufikia hatua hiyo, masoko mengine ni Soko la Hisa ni Johannesburg la Afrika Kusini ambalo lina miaka zaidi ya 100, na pia Soko la Hisa la Nairobi (Nairobi Securities Exchange) ambalo lina miaka takribani 70 tangu uanzishwaji wake, lakini DSE likiwa na miaka 20 tu na  linafanya vizuri katika medani za kimataifa.

Alisema kuwa DSE ina bidhaa kuu tatu zilizopo Sokoni ambazo mwananchi yeyote anaweza kuwekeza, bidhaa hizo ni Hisa, ambapo kuna Kampuni 28 zilizoorodheshwa Sokoni zenye ukubwa wa thamani ya takribani Shilingi bilioni 19.2. Bidhaa nyingine ni Hati Fungani za Serikali zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 9.5 na pia Hati fungani za makampuni binafsi zenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 250.

Mwisho


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger