Thursday, 17 January 2019

SERIKALI YATOA MSAMAHA KWA WAVUVU WASIO NA LESENI

Serikali imeagiza wavuvi waliokamatwa kwa kosa la kutohuisha leseni zao na vyombo vyao kwa mwaka 2019, waachiwe na makosa yao yafutwe mara moja.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, alitoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma.

Ulega alisema wizara juzi ilipata taarifa kutoka vyombo vya habari kwamba wavuvi katika ukanda wa pwani ya Bahari ya Hindi hususani soko la Feri, Dar es Saalam, hawakwenda kuvua samaki kwa sababu ya kutokuwa na leseni za vyombo vyao na za uvuvi kwa mwaka 2019.

Kutokana na hali hiyo, Ulega aliagiza wavuvi wote waliokamatwa kwa kosa hilo kote nchini, kuachiwa mara moja kuendelea na shughuli zao.

Pia aliwataka maofisa uvuvi kutoka katika ofisi zao na kuwafuata katika mialo mbalimbali ili kuwakatia leseni.

"Kwa kuzingatia kuwa hiki ni kipindi cha mwanzo wa mwaka na leseni zinatolewa, wizara inaelekeza kwamba wavuvi wote waendelee kukatiwa leseni hadi Januari 31,” alisema Ulega.

Aidha, aliagiza maofisa wote wa wizara na halmashauri katika kipindi hiki wawafuate wavuvi kwenye mialo ili kuwakatia leseni wenye sifa kulingana na sheria na kanuni za uvuvi.

Aliongeza kuwa katika kutekeleza jukumu hilo wizara imekuwa ikiendesha operesheni dhidi ya uvuvi haramu na biashara haramu ya samaki na mazao yake kwa takribani mwaka mzima.

"Shughuli za uvuvi zinatakiwa kutekelezwa kwa mujibu wa sheria ya uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 pamoja na sheria nyingine za nchi. Kwa kuzingatia hilo, kila mtu anayehusika na uvuvi, anatakiwa kuwa na leseni halali ya uvuvi na leseni ya chombo anachotumia,” alisema Ulega.

Chanzo:Mpekuzi
Share:

Wednesday, 16 January 2019

Video Mpya : BEXY - MSHENGA


Nakualika kutazam video mpya ya msanii Bexy inaitwa Mshenga..Itazame hapa chini
Share:

WAZIRI MKUU: BENKI YA KILIMO IHARAKISHE MALIPO YA KOROSHO HATUJAVUKA HATA NUSU

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Benki ya Kilimo Tanzania (TADB) ihakikishe inabadilisha mfumo wake ili iweze kuharakisha malipo kwa wakulima wa korosho ambao wameshahakikiwa. Ametoa agizo hilo Jumatano, 16 Januari, 2019) wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TADB kwenye kikao alichokiendesha kwa njia ya video (video conferencing) kutokea ofisini kwake Mlimwa, Dodoma. Wakuu wa mikoa hiyo mitatu walikuwa kwenye mikoa yao na Mkurugenzi Mkuu wa TADB, alikuwa Dar es Salaam. “Hakikisha mnaharakisha malipo ya wakulima lakini pia suala la uhakiki…

Source

Share:

Video Mpya : NELLY JAKANO Ft BEST NASSO & CHIEF MAKER - JABER




Msanii wa nyimbo za asili Nelly Jakano ametualika kutazama video yake mpya inaitwa Jaber ambayo amewashirikisha wasanii Best Nasso na Chief Maker ..Itazame hapa chini
Share:

KAMPENI YA JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA KUZINDULIWA SHINYANGA WIKI HII


Kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama kuzinduliwa Januari 18,2019 Shinyanga.
Share:

AFISA ELIMU AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Ofisa elimu maalum wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu,mkoani Arusha Martin Goi amefariki dunia baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Tukio hilo lililothibitishwa na mkuu wa Wilaya ya Karatu, Theresia Mahongo limetokea juzi jioni Jumatatu Januari 14, 2019 katika mgahawa wa Rhotia Garden mjini Karatu.

Goi alipigwa risasi mbili kifuani na kukimbizwa Hospitali ya Selian mjini Arusha kwa matibabu na kufariki dunia jana Jumanne Januari 15, 2019.


Na Mussa Juma, Mwananchi

Share:

WALIOTUHUMIWA KULIPUA BOMU WALIPWA MAMILIONI YA FEDHA


Raia watatu waliotuhumiwa kuhusika na mlipuko wa bomu nchini Uganda mwaka 2010, wamezawadiwa kiasi cha shilingi milioni 8 ambazo ni sawa na milioni 181 na Mahakama Kuu Jijini Nairobi nchini Kenya.

Raia hao waliojulikana kwa majina ya Mohamed Adan Abdow, Mohamed Hamid Suleyman na Yahya Suleyman wamelipwa fedha hizo kwa ajili ya fidia juu ya ukiukwaji wa uhuru na haki zao za msingi waliofanyiwa.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji wa Mahakama Kuu, David Majanja amesema kuwa kukamatwa kwa kukamatwa na kuondolewa kwa raia hao kutoka Kenya hadi nchini Uganda kulikuwa ni kinyume cha sheria.

Mwaka 2010 watuhumiwa hao waliiomba Mahakama kupitia upya suala hilo la kukamatwa kwao na kuhamishiwa nchini Uganda wakisema kuwa halikufuata sheria.
Share:

Picha : RAIS MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS MSTAAFU WA NIGERIA OLUSEGUN OBASANJO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Rais mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Rais mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.
Share:

RADI YAJERUHI WANAFUNZI 14 MKOANI KAGERA

Na Mwandishi wetu,Kagera. Wanafunzi 14 wa shule ya sekondari Rulongo muleba mkoani Kagera, wamelazwa katika hospitali ya Rubya baada ya kujeruhiwa na radi iliyoambatana na mvua leo saa 7:15 mchana kati yao wanafunzi watatu wanatajwa hali zao ni mbaya kiafya. Mganga mkuu wa hospitali ya Rubya wilayani Muleba George Kasibante amesema wanaotajwa kuwa na hali mbaya wameungua sehemu mbalimbali za miili yao na mwingine mmoja amepoteza fahamu na kwamba madaktari wanafanya liwezekanalo kuokoa maisha yao Amesema radi hiyo ilipiga vyumba vya madarasa, kidato cha pili na tatu ambapo baadhi ya…

Source

Share:

CHADEMA YATUMA SALAMU ZA POLE NCHINI KENYA KUFUATIA SHAMBULIZI LILILOFANYWA JANA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA)kupitia kwa mkuu wa idara ya habari na mawasiliano Tumaini Makene kimetuma Salamu za pole kwa Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta na wananchi kwa ujumla kufuatia shambulio lililotokea jana january 15 na watu 14 kufariki. Taarifa iliyotolewa leo kwa waandishi wa habari imesema,CHADEMA imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za tukio la shambulizi linalohusishwa na ugaidi, lililofanyika kwenye eneo lenye shughuli mbalimbali za kijamii, katika Hoteli ya DusitD2, Nairobi, nchini Kenya, siku ya Jumanne, Januari 15, mwaka huu. “Kipekee CHADEMA inatuma salaam za pole kwa watu wote…

Source

Share:

MWANAFUNZI ALIYEBAKA NA KUMPA MIMBA MWANAFUNZI MWENZIE AKANA MAELEZO YA AWALI.

Na,Naomi Milton Serengeti Mathayo Songalaeli (21) mkazi wa kijiji cha Natambiso Wilaya ya Serengeti, amekana maelezo ya awali mara baada ya kusomewa maelezo hayo katika kesi yake ya Jinai namba 94/2018. Kabla ya kusomewa maelezo ya awali Hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya Ismael Ngaile alimtaka mwendesha mashtaka wa Jamhuri Faru Mayengela kumkumbusha mshitakiwa mashtaka yake. Akisoma mashtaka Faru alisema makosa yanayomkabili mshitakiwa ni mawili kosa la kwanza ni kubaka kinyume na kifungu 130(1)(2)(e) na 131(1)cha kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 Kosa la pili ni…

Source

Share:

Picha:SHIRIKA LA REDESO LAONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WILAYA YA KISHAPU


Katika mapambano dhidi ya athari zitokananazo na ukataji miti kiholela ikiwa ni pamoja na hali ya ukame mkoani Shinyanga Shirika lisilokuwa la kiserikali la REDESO linalotekeleza mradi wa kukabiliana athari za maafa katika wilaya ya Kishapu limepanda miti zaidi ya 4000 katika kata ya kiloleli kwa lengo la kukabiliana na hali hiyo
 Akiongea na wadau wa mazingira Jumamosi Januari 13,2019 kutoka kata ya Kiloleli, Meneja miradi wa shirika la REDESO Charles Bulegeya amesema kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi yanachangiwa na shughuli za kibinaadamu ikiwemo kukata miti hovyo.

Bulegeya amesema  wanaendelea kutoa elimu ya madhara ya ukataji miti ili kuiniusuru Wilaya ya Kishapu na hali  ukame  hivyo kwa  kushirikiana na jamii shirika hilo limepanda miti elfu 4000 katika kijiji cha Kiloleli .

“Tumeshirikisha wadau kila kitongoji ili kushiriki zoezi hili la upandaji miti kwenye vyanzo vya maji,maana chanzo hiki cha maji kiloleli kinakabiriwa na kujaa tope kwa hiyo kwa kupanda miti maeneo yanayozunguka vyanzo vya maji itapunguza upoteaji wa maji” ,alisema Bulegeya 

“Tumepanda miti zaidi ya 4000 katika kijiji hiki cha Kiloleli kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ambao walichangangia miti 2000 pia ushirikiano wa mgodi wa mwadui walichangia miti 1000 na taasisi ilipokea miti 1000 kutoka kwa wadau” aliongeza Bulegeya. 

Kwa upande wake kaimu afisa mali asili wilaya ya Kishapu Wilson Bigirwa amesema kuwa Halmashauri hiyo imepanga utaratibu wa kila kaya ihakikishe imepanda miti kumi katika maeneo yao na kuitunza huku akiweka wazi kuwa kufikia mwezi wanne wanatarajia kumaliza zoezi la upandaji miti Wilaya nzima ya Kishapu. 

“Ndugu zangu kwa wale wote tulioshiriki katika kupanda miti tuwe walinzi wa miti yetu itapendeza kabisa kama miti yote tuliyoipanda itakuwa na kuwa mfano kwa watu wengine, na Serikali za kijiji zitunge sheria ndogondogo kuwabana wale ambao hawatakuwa sambamba na sisi”alisema Bigirwa 

Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kiloleli wamelipongeza shirika la REDESO kwa kutekeleza mradi wa upandaji miti katika Kata yao ili kukabilianan na ukame unaochangia kukosekana kwa maji na kudai kuwa wapo tayari kuwa mabalozi katika utunzaji mazingira kwa kupanda miti . 

Shirika la REDESO linatekeleza miradi mbalimbali katika mkoa wa Shinyanga ikiwa ni pamoja na kuwezesha akina mama na vijana, ubunifu na uboreshaji wa mnyororo wa thamani wa zao la Mkonge kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya Nchi na mradi wa tatu ni mradi wa kukabilianaa na athari za maafa.

Meneja miradi wa shirika la REDESO Charles Bulegeya akielezea juu ya umuhimu wa upandaji miti ili kukabiliana na hali ya ukame wilayani Kishapu huku akiweka wazi kuwa shirika la REDESO linatekeleza mradi kukabiliana athari za maafa katika Wilaya ya Kishapu. Picha zote na Steve Kanyefu- Malunde 1 blog
Kaimu afisa Mali Asili Wilaya ya Kishapu Wilson Bigirwa akiwaelekeza wananchi  namna bora kupanda miti .
 wananchi wa  Kijiji cha Kiloleli wakishirikiana katika zoezi la upandaji miti 


 Mtathimini na mfuatiliaji wa mradi wa kupunguza athari za maafa Isack Jonas (kulia) akishirikiana na moja ya mwananchi wa Kata ya Kiloleli katika zoezi la upandaji miti ili kukabiliana na hali ya ukame katika wilaya ya Kishapu.
 Afisa mradi wa kupunguza athari za maafa Vera Cleophas (kulia) akishiriki katika upandaji miti.

 Baadhi ya wadau walioshiriki katika upandaji miti katika kata ya Kiloleli 




Share:

CHINA YAOTESHA PAMBA MWEZINI

Mbegu ambazo zimepelekwa mwezini na chombo cha utafiti wa anga za juu cha Chang'e-4 zimechipua, mamlaka jijini Beijing zimethibitisha.
Hii ni mara ya kwanza kwa mmea wa kibaolojia kuchipuwa mwezini, na ni hatua inayofungua njia ya tafiti zaidi za kisayansi mwezini.

Chang'e 4 pia ndio chombo cha kwanza kutafiti sehemu ya mbali zaidi ya mwezi, ambayo haitazamani na uso wa dunia.

Chombo hicho kilitua mwezini Januari 3 kikiwa kimebeba vifaa vya kuchunguza jiolojia ya eneo hilo.

Mimea imekuwa ikioteshwa kwenye kituo cha kimataifa cha anga za juu lakini haijawahi kujaribiwa mwezini.

Hii inafungua milango ya uwezekano wa wanaanga kuweza kuzalisha chakula chao wenyewe wakiwa anga za mbali na kupunguza uhitaji wa kurudi duniani ili kufuata chakula.

Chanzo:Bbc
Share:

SANAMU LA SHETANI LASHUTUMIWA KUFURAHI SANA

Sanamu la shetani linalopangwa kuwekwa katika mji wa Uhispania Segovia limeshutumiwa kwa kufurahi sana.

Sanamu hilo la shaba bronze liliundwa kwa heshima ya ngano au hadithi ya kale inayosema kuwa shetani alihadaiwa kujenga bomba mashuhuri la maji mjini humo.

Lakini wakaazi wanasema shetani huyo - anayetabasamu na anayeonekana kupiga slefie na simu ya mkononi - anaonekana kuwa na upole na urafiki mwingi.

Msanii huyo ameiambia BBC ameshangazwa na kiwango cha shutuma zilizoelekezwa kwa kazi yake.

Jaji mmoja sasa ameagiza sanamu hilo lisiwekwe kwa sasa wakati anaposhauriana kufahamu iwapo linadhalilisha Wakristo.

Chanzo:Bbc


Share:

RAIS KENYATTA : MAGAIDI WALIOUA RAIA 14 NA KUJERUHI 30, WOTE WAMEUAWA


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema magaidi wote waliofanya shambulio katika hoteli ya kifahari ya DusitD2 na kusababisha vifo vya watu 14, wameuawa.

Kenyatta ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 16, 2019 wakati akihutubia Taifa kuhusu operesheni ya kupambana na magaidi waliovamia hoteli hiyo. Tukio hilo lililotokea jana Januari 15, 2019.

Amebainisha kuwa watu 700 wameokolewa na vyombo vya ulinzi na usalama, kwamba operesheni hiyo imekamilika na magaidi wote wameuawa.

Rais Kenyatta amesema watu 30 waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali mbalimbali za mjini Nairobi.

Share:

DOCUMENTARY YA MAONYESHO YA UTALII WA NDANI - 'UWANDAE EXPRO 2019' YAZINDULIWA DAR


Mwenyekiti wa Chama cha wanawake katika fani ya Utalii Tanzania (AWOTTA) Mary Kalikawe (kushoto) akiongea na wandishi wa habari ( hawapo pichani ) jijini Dar es Salaam, wakati wa mkutano wa kutangaza Maonyesho ya biashara ya Utalii wa Ndani ya Kwanza nchini yatakayofanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa Posta Dar es Salaam, Februari 15 hadi 17 ,2019.

 ” Kauli mbiu ya maonyesho hayo ni Tambua Ushindi wa Kibishara katika Utalii wa Ndani Tanzania” Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa TTB ,Geofrey Tengeneza na Mwenyekiti wa chama cha wanawake Tanzania katika biashara (Tanzania Women Chamber of Commerce) Jacqueline Maleko.

Mwenyekiti wa Chama cha wanawake katika fani ya Utalii Tanzania (AWOTTA) Mary Kalikawe (kushoto) Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania ( TTB) ,Geofrey Tengeneza (katikati) na Mwenyekiti wa chama cha wanawake Tanzania katika biashara (Tanzania Women Chamber of Commerce) Jacqueline Maleko, wakiwa wameshikana mikono kuonyesha ushirikiano wao kwa wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wakati wa mkutano wa kutangaza Maonyesho ya biashara ya Utalii wa Ndani ya Kwanza nchini yatakayofanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa Posta Dar es Salaam, Februari 15 hadi 17 ,2019.” Kauli mbiu ya maonyesho hayo ni Tambua Ushindi wa Kibishara katika Utalii wa Ndani Tanzania.
---
Chama cha Wanawake katika fani ya Utalii Tanzania (AWOTTA) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii (MNRT), Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC), Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) na shirika la maendeleo la Ujerumani GIZ, wameandaa documentary ambayo imeziduliwa leo jijini Dar es Salaam.

Hafla ya uzinduzi wa documentary hiyo ambayo inahusu tukio la maonyesho maonesho ya Utalii wa ndani UWANDAE EXPO 2019 yatakayofanyika mwezi ujao mwezi wa Februari tarehe 15 hadi 17 katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa (National Museum –Posta). ilifanyika katika katika ofisi za Bodi ya Utalii Tanzania na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii na waandishi wa habari.

Akiongea kuhusu maonyesho haya ambayo yanafanyika nchini kwa mara ya kwanza, Mwenyekiti wa AWOTTA, ambayo inaratibu maonyesho hayo, Mary Kalikawe, alisema AWOTTA na washirika wake waamua kutekeleza mpango mkakati wa Bodi ya Utalii wa kuutangaza utalii wa ndani kwa vitendo kupitia UWANDAE EXPO 2019 na kauli mbiu ya maonyesho haya ni “Tambua ushindani wa Kibiashara katika Utalii wa Ndani Tanzania”.

“Kuzindua kwa documentary hii ikisisitiza mchango wa akina mama “Nani kama mama” kunaenda sambamba na kuzindua matangazo kwa umma wa Tanzania juu ya uwepo wa sekta kubwa ya utalii humu nchini ambayo ni muhimu ikatambuliwa kusudi ihudumiwe na kupewa umuhimu wake. Sekta hii inachochea uwekezaji kwa wingi kama tunavyoona mahoteli, usafirishaji tangu wa ndege hadi wa bodaboda, biashara ya chakula kila pembe ya nchi, burudani na utalii wa aina nyingine nyingi. Sambamba na uwekezaji huu, sekta ina uwezo mkubwa wa kutengeneza ajira kwa wakubwa na wadogo pia inabeba uwezo mkubwa wa kutengeneza kipato kwa mtu mmoja mmoja, makundi na kuchangia kipato cha taifa kwa kiasi kikubwa. Kwa sasa utalii wa mbuga za wanyama unachangia asilimia 17 ya pato zima la taifa ambayo ni takribani dola Bilioni 2.1 au shillingi zaidi ya trillion 4.7 kila mwaka”. alisema Kalikawe.

Maonesho haya yanatarajiwa kufunguliwa rasmi na Mhe. Dr. Hamisi Kigwangala, Waziri wa Maliasili na Utalii siku ya Ijumaa tarehe, 15 Februari 2019.

Lengo la Maonyesho haya ni kuanzisha utambuaji wa mapana ya sekta ya Utalii wa ndani na fursa kubwa za uwekezaji na ajira zinazoambatana na kukua kwa sekta hii muhimu. Maonyesho yatawaunganisha wafanyabiashara wa bidhaa na huduma katika maeneo mbali mbali yanayosababisaha safari za watanzania. Wafanya biashara hawa na vyombo vinavyowezesha uwekezaji, watatumia jukwaa hili kukuza uhusiano baina ya washiriki na Watembeleaji wa maonesho. Watu elfu tatu wanategemewa kuhudhuria maonyesho.

Taarifa ya tovuti http://bit.ly/2FDzXer inaonesha takwimu zifuatazo: Kuwa mwaka 2014 jumla ya vitengo rasmi vya chakula vinywaji na malazi wakati huo Tanzania bara vilikuwa 11,136. Kati ya hivi asilimia 51.7 vilikuwa vya chakula na vinywaji wakati asilimia 48.3 vilikuwa ni sehemu za watu kulala.

Kwa upande wa sanaa na burudani, jumla ya vitengo rasmi katika utafiti wa mwaka 2014/15 vilikuwa 239 ambayo ni chini ya asilimia 1 ya vitengo vyote vya biashara vilivyotambuliwa mwaka huo. Kati ya hivi ubunifu na burudani vilikuwa asilimia 35.6, michezo na starehe vilikuwa asilimia 24.3, michezo ya kubahatisha na kubeti ilikuwa asilimia 23.8 na vitengo vya library, kujisomea, makumbusho na burudani za utamaduni ilikuwa asilimia 16.3

Waandaaji wa maonesho wanapenda kutangaza kuwa kupitia uelewa wa upana wa sekta zilizomo katika utalii wa ndani, takwimu hizo hapo juu zimekwishaanza kubadilika na kupanda na mwamko wa watanzania na watoa huduma katika kuboresha utalii wa ndani utapandisha sana ukuaji wa vitengo hivi vya biashara.

Ni muhimu mikoa yote itambue umuhimu wa kuvuta wageni wa ndani kwenda kutembea kwa sababu mbali mbali katika mikoa yao. Kuwasili kwa wageni ndio ukuaji wa sekta ya utalii wa ndani. Takwimu hizo hapo juu zitajidhihirisha katika mikoa mbali mbali ikifanya bidii kuvuta wageni wa ndani na kuwapa huduma nzuri kama vile wanataka wageni wasahau kurudi kwao!

Faida ya kushiriki:

-Kuonyesha bidhaa au huduma wanazozalisha au wanazotoa;

-Kupata fursa ya kujifunza teknonolija mpya na ujuzi kutoka kwa washirikiwengine;

-Kupata fursa ya kushiriki katika kongamano na semina ya bure itakayofanyika sambamba na maonyesho hayo;

-Kukutana na Wafanyabiashara, Wawekezaji, washauri wa kibiashara na Wasambazaji wa huduma mbalimbali;

-Kupata kutangazwa kwenye utandawazi wa kitaifa na kimataifa kwa njia mbalimbali;

-Kupata fursa mbali mbali ambazo ni pamoja na tiketi ya raffle, vocha ya malazi, zawadi za kusafiri n.k.

Aidha, ni fursa ya kimkakati ya kuwahamasisha wananchi wa Tanzania kupenda kutumia huduma zinazotolewa na wadau wa sekta ya utalii hapa nchini.

Maonyesho haya yanatarajiwa kushirikisha, Wizara, Taasisi, Makampuni pamoja na Wafanyabiashara wa sekta mbalimbali. Kongamano litakuwa juu ya "Biashara, Uwekezaji na Ajira katika Utalii wa Ndani ambalo litatolewa bure (idadi ni watu 250 tu kwa siku moja wataruhusiwa, hivyo jiandikishe mapema kabla nafasi hazijaisha).

Kiingilio kwenye maonesho ni bure asubuhi hadi saa 10 jioni. Kisha yanafuata masaa ya burudani ambayo inalipiwa kiasi kidogo.
Share:

HILI NDIO KUNDI LILILOTHIBITISHA KUFANYA SHAMBULIZI RIVERSIDE NAIROBI

Kundi la wapiganaji la al-shabab linakabiliana na serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa nchini Somalia na limefanya misururu ya mshambulizi katika eneo zima.
Kundi hilo linalohusishwa na al-Qaeda limefurushwa katika miji mingi lililodhibiti lakini linasalia kuwa hatari.

Neno al-Shabab linamaanisha vijana kwa lugha ya kiarabu.

Lilijitokeza kutokana na kundi lenye ititakadi kali la Muungano wa mahakama za kiislamu nchini Somali ambalo lilikuwa likidhibiti mji wa Mogadishu 2006, kabla ya kufurushwa na vikosi vya Ethiopia.

Kuna ripoti kadhaa za wapiganaji wa Jihad wa kigeni wanaoelekea Somalia kusaidia al-Shabab, kutoka mataifa jirani pamoja na Marekani na Ulaya.

Limepigwa marufuku kama kundi la kigaidi na Marekani pamoja na Uingereza na linaaminika kuwa na kati ya wapiganaji 7000 na 9000.

Al-Shabab linahubiri Uislamu wa madhahabu ya Wahhabi kutoka Saudia huku raia wengi wa Somali wakiwa wa madhahabu ya Sufi.

Limeweka sheria kali za Kiislamu katika maeneo linayodhibiti , ikiwemo kumpiga mawe hadi kufa mwanamke anayetuhumiwa kuzini mbali na kuwakata mikono wezi.

Chanzo:Bbc
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger