Friday, 4 January 2019

BREAKING NEWS:HAYA HAPA MATOKEO KIDATO CHA PILI 2018

Necta imetangaza matokeo kidato cha pili na darasa la nne 2018
Kama kawaida yetu Maswayetu blog ni kukupa kitu roho inapenda

Tunaangalizia matokeo ya form 2 na darasa la 2 kwa gharama ya tshs 3000 tu kwa kila mwanafunzi
Ili uangaliziwe Fanya yafuatayo;
1.Tuma jina la mwanafunzi mf.Jumanne temba ,taja shule,wilaya,na mkoa kwenda no.0621082183
2.weka mbele MF.form 2 au darasa la NNE
3.tuma pesa yako kwenda namba 0768260834
4.utajibiwa ndani ya dk 1 tu
Kuangalia matokeo hayo
Darasa la NNE >>> http://41.59.85.99/results/2018/sfna/sfna.htm
Share:

MTOTO ANAYEDAIWA KUFUNGIWA KABATINI HATOI SAUTI


 Wakati vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wa hali ya mtoto anayedaiwa kufungiwa kabatini kwa miezi mitano, madaktari wametaja tatizo jingine walilolibaini kwa mtoto huyo kuwa hatoi sauti.

Mtoto huyo aliyelazwa wodi ya watoto wenye utapiamlo katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, amegundulika kuwa na tatizo la kutotoa sauti hata anapolia, hivyo kuwafanya madaktari kuanza kutafuta sababu.

Akizungumza na Mwananchi hospitalini hapo jana, Ofisa Muuguzi, Dina Msesa alisema hali ya mtoto huyo inaendelea kuimarika baada ya kumwanzishia lishe ya vyakula vya kuboresha afya yake, lakini tatizo lipo kwenye utoaji wa sauti.

“Mtoto huyu hatoi sauti yoyote wala halii, ila ametulia jambo linalofanya wataalamu waanze kukuna vichwa kutafuta tatizo,” alisema Msesa.

Kuhusu mama wa mtoto huyo ambaye alikuwa mtumishi wa ndani, alisema afya yake imeimarika na mkono uliokuwa umeumia umepona ambapo sasa anaweza kuunyayua tofauti na awali.

Share:

WAZIRI AMPA SIKU 7 MKUU WA UPELELEZI ,SAKATA LA MWANAMKE KUCHOMEWA NYUMBA

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, ametoa siku saba kwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Kagera (RCO), Obassy Nguvillan, kupeleleza upya kesi ya mama aliyechomewa nyumba katika eneo la Kyakailabwa Kata ya Nyanga, Manispaa ya Bukoba.

Lugola alitoa agizo hilo jana kutokana na watuhumiwa kukamatwa kisha kuachiwa na baadaye jalada kufungwa na Mwanasheria wa Serikali.

Kabla ya agizo hilo, mama huyo, Sauda Amir, alilalamika kwa Waziri Lugola katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Uhuru Manispaa ya Bukoba na baadaye RCO alikiri kuwa inawezekana Jeshi la Polisi lilipeleleza kesi hiyo kwa udhaifu.

Lugola alisema kuwa haiwezekani mwanamke huyo achomewe nyumba, watuhumiwa anawafahamu halafu kesi iishe katika mazingira ambayo yana utata na kulazimika kumwita RCO kujibu.

“RCO natoa muda wa wiki moja ufanye kazi hii wewe mwenyewe, uchunguze kesi hii upya na unipe majibu,” alisema.

Akizungumzia tukio hilo, Sauda anayedai alifiwa na mumewe, alisema kuwa nyumba yake ilichomwa moto Juni 11, mwaka jana na kuwa kutokana na tukio hilo, kwa sasa hana mahala pa kuishi.

“Mheshimiwa Waziri, naomba unisaidie suala langu lipatiwe ufumbuzi, nahangaika na watoto, sina pa kuishi, kwa sasa mimi na watoto wangu saba tumepewa hifadhi na mama mmoja katika eneo la Kyakailabwa,” Alisema mama huyo

Share:

MHE. MABULA AFANYA ZIARA KUKAGUA UJENZI WA BARABARA 9 PAMOJA NA UJENZI WA DAMPO ZINAZOGHARIMU BI 15.9

Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanslaus Mabula ameendelea na ziara yake ukaguzi wa miradi ya maendeleo, ambapo amepata fursa kukagua Miradi 10 yenye thamani ya shingi 15,912,434,395.00 iliyochini ya Mpango Kabambe wa uboreshaji Miji na Majiji, Tanzania Strategic Cities Plan inayohusisha kukarabati na ujenzi wa barabara tisa zilizopo Mitaa ya mjini katika Halmashauri ya Jiji Mwanza sanjari na ujenzi wa dampo la Taka. Mhe. Mabula amempongeza Mhe. Dkt. Magufuli kupitia wizara ya Tamisemi Tawala ya Mikoa na Serikali ya Mitaa kwa ushirikiano wake mwema wa wadau wa maendeleo Bank ya…

Source

Share:

SERIKALI KUMTUMIA SAMATTA KUTANGAZA UTALII UBELGIJI,FLAVIANA MATATA ATEULIWA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla, amebainisha kwamba ili kukuza utalii tayari ameanza mazungumzo na klabu ya KRC Genk anakocheza mtanzania Mbwana Ally Samatta ili kuweza kutangaza utalii nchini Ubelgiji.

Waziri Kigwangalla amesema kwamba wakati huu wapo kwenye kuandaa mkakati mahsusi, kwa ajili ya kujitangaza kwenye nchi hiyo.

"Tayari pia tumeanza mazungumzo na mcheza soka wa kulipwa, Ndg. Mbwana Samatta, ili tutumie jina lake kufungua soko jipya la Utalii nchini Belgium. Tunaandaa mkakati mahsusi kwa ajili ya kujitangaza kwenye nchi hii"!

Mbali na kuweka mipango juu ya Samatta, Waziri huyo amemuomba Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata kukubali uteuzi wake wa kuwa balozi wa hiari wa Utalii nchini.

"Tunakushukuru na kukupongeza Ndg. Flaviana Matata kwa uzalendo wako. Tutakupa hati ya shukrani na pia tunakupa Safari ya siku 5 kwenye maeneo ya vivutio siku yoyote utakayokuwa tayari. Pia tutaomba ukubali uteuzi wangu wa kuwa Balozi wa hiari wa utalii"

Pamoja na hayo Waziri amesema kwamba tayari amekwisha kamilisha kazi ya kubuni kauli mbiu ya #TanzaniaUnforgettable ambayo itaitambulisha nchi kwenye masoko ya utalii.

Share:

YANGA WAMJIBU MANARA SAKATA LA KULIPA KODI TRA

Klabu ya soka ya Yanga imetoa jibu kwa msemaji wa klabu ya Simba Haji Manara, aliyehoji juu ya utaratibu wa kuchangisha fedha kwa wanachama wake kama ni halali na unakatwa malipo ya kodi kwa serikali.


Kupitia ripoti yake ya michango ya fedha za mashabiki kwa miezi miwili ya Novemba na Desemba Yanga imeweka wazi kuingiza kiasi cha shilingi 5,165,009 kwa mwezi Desemba na 563,737 kwa mwezi Novemba.

Katika ripoti hiyo Yanga imeeleza michango hiyo imefanyika kwa njia ya simu kupitia Selcom Wallet hivyo lazima kodi zote sitahiki zitakuwa zimelipwa.


Manara alihoji juu ya suala hilo hivi karibuni baada ya kusambaa video mtandaoni ikiwaonesha wachezaji wa Yanga wakipewa fedha na mashabiki baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbeya City uliopigwa jijini Mbeya.

Chanzo:Eatv
Share:

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA JAN,4 2019, RAMSEY KUTIMKIA JUVENTUS

Ramsey ndiye mchezaji wa sasa aliyekaa muda mrefu zaidi Arsenal, alijiunga nao 2008

Kiungo wa kati wa Arsenal Aaron Ramsey, 28, ametia saini makubaliano ya awali ya mkataba na Juventus na huenda akajiunga na klabu hiyo ya Italia mwezi huu. (Sport Mediaset kupitia Calciomercato)

Mkurugenzi wa michezo wa klabu ya Sevilla Joaquin Caparros anasema klabu hiyo huenda ikawasilisha ofa kumtaka mshambuliaji wa Chelsea ambaye zamani alichezea Real Madrid na Juventus Alvaro Morata, 26. (Football.London)


Morata angependa kurejea Madrid iwapo ataondoka Stamford Bridge lakini anaweza tu kuruhusiwa kuondoka iwapo Chelsea watampata mshambuliaji mwingine wakati wa dirisha la kuhama wachezaji la Januari. (Sun)

Hatima ya Mesut Ozil Arsenal haitaamuliwa hadi mwisho wa msimu baada ya kiungo huyo wa miaka 30 na klabu hiyo kupuuzilia mbali uwezekano wake kuhama mwezi huu. (Evening Standard)

Chelsea watafanya uamuzi kumhusu mshambuliaji Tammy Abraham kufikia 14 Januari. Mchezaji huyo wa miaka 21 yupo Aston Villa kwa mkopo lakini anaweza kuitwa kurejea klabu yake wiki mbili baada ya dirisha la kuhama wachezaji kufunguliwa kutokana na maelezo kwenye mkataba wake. (Telegraph)Tammy Abraham

Chelsea wameamua kutomfuata mshambuliaji wa Argentina Gonzalo Higuain, 31, mwezi huu. Mchezaji huyo kwa sasa yupo AC Milan kwa mkopo kutoka Juventus. (Goal)

Cesc Fabregas hatakubaliwa kukamilisha uhamisho wake kwenda Monaco hadi Chelsea wapate kiungo wa kati wa kujaza nafasi ya Mhispania huyo wa miaka 31. (Calciomercato)Cesc Fabregas

Mlinda lango wa Real Madrid Keylor Navas, 32, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Arsenal wiki za hivi karibuni, ameongeza muda wa mkataba wake katika klabu hiyo kwa mwaka mwingine mmoja, hadi Juni 2021. (Marca)Kipa wa Costa Rica Keylor Navas

Bayern Munich wamewasilisha ofa ya tatu ya zaidi ya £30m wakimtaka kiungo mshambuliaji wa Chelsea Callum Hudson-Odoi, 18. (Sky Sports)Callum Hudson-Odoi alijiunga na Chelsea mwaka 2007

Beki wa Chelsea mzaliwa wa England Gary Cahill, 33, anakaribia kuhamia Fulham kwa mkopo. Klabu hiyo ya London magharibi imemrejesha Timothy Fosu-Mensah kwa Manchester United ili kutoa nafasi ya mchezaji mwingine ndipo waweze kumchukua Cahill. (Love Sport Radio)Gary Cahill

Crystal Palace wamewasilisha ofa ya £6.5m kumtaka mchezaji wa Everton na Senegal Oumar Niasse, 28, baada yao kushindwa kumpata mshambuliaji wa Liverpool Dominic Solanke kwa mkopo. (Sun)


Paris St-Germain wamewasilisha ofa ambayo haiwezi kufikiwa na Barcelona kumtaka kiungo wa kati Frenkie de Jong, 21, na beki wa kati Matthijs de Ligt, 19, kutoka Ajax. (Marca)

Leicester wamepokea ofa kutoka kwa Villarreal ya Uhispania wanaomtaka Vicente Iborra, lakini klabu hizo bado hazijakamilisha mazungumzo kuhusu uhamisho wa Mhispania huyo mwenye miaka 30. (Leicester Mercury)nNathaniel Clyne

Chelsea wanapanga kutoa £36m kumtaka winga wa PSV Hirving Lozano, 23, anayetokea Mexico. (Calciomercato, kupitia Talksport)

Cardiff na Bournemouth wote wanamtaka beki wa Liverpool Nathaniel Clyne. Bournemouth wanamtaka mkabaji huyo wa miaka 27 kwa mkopo kwa kipindi kilichosalia cha msimu. (Mail)

Kiungo wa kati wa Liverpool Adam Lallana, 30, anatafutwa na klabu ya Fenerbahce ya Uturuki mwezi huu. (Caught Offside)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino amekataa kufutilia mbali uwezekano wa kiungo wa kati wa Ubeligji Mousa Dembele, 31, kuihama klabu hiyo mwezi huu. (Football.London)

Pamoja na Dembele, Tottenham wanataka kuwauza pia Fernando Llorente, 33, Vincent Janssen, 24, Georges-Kevin Nkoudou, 23, na Victor Wanyama, 27. (Mirror)Victor Wanyama

Nottingham Forest wamehusishwa na kumnunua winga wa Portsmouth Jamal Lowe, 24. (Nottingham Post)

Meneja wa zamani wa Birmingham na Derby Gary Rowett huenda akalazimika kuzuia kushindwa mechi ya Kombe la FA ugenini Shrewsbury Jumamosi ili kunusuru kazi yake kama meneja wa Stoke. (Telegraph)
Share:

NewAUDIO-SAIDA KAROLI-MAGENYI

Msanii Saida Karoli anakukaribisha kuusikiliza wimbo wake mpya uitwao Magenyi. 
Sikiliza wimbo huo hapa chini
Share:

KATIBU MKUU CCM ATEMBELEA MAKUMBUSHO YA BABA WA TAIFA J.K NYERERE


Katibu Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally amepokelewa Mkoa wa Mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Kagera
Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally atafanya ziara ya siku mbili kuimarisha Chama Mkoa wa Mara ikiwa ni pamoja na kutembelea Wilaya ya Butiama alikozikwa mwasisi wetu Mwl. Julius kambarage Nyerere

Aidha, Ndg. Bashiru Ally amesema katika ziara yake hii ni kukijenga chama nakukiimarisha katika Misingi iliyowekwa na Mwasisi wetu Mwl.Nyerere

Ndg. Bashiru Ally ameyasema hayo Mbele ya wananchi na viongozi wa Chama na serikali wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Mkoa Ndg. Samweli Kiboye wakikagua kituo cha Afya jimbo la Bunda

Katika ziara hiyo ameshiriki kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Butiama.

Katika kikao hicho Dkt.Bashiru Ally ametoa salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mh. John Pombe Magufuli kwa wana Mara na kuwambia anawahakikishia kuwa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Mkoa na Uwanja wa ndege wa kisasa Musoma itatekelezwa.

Katibu Mkuu wa CCM amehitimisha kikao hicho kwa kusisitiza Umoja kwa watumishi wa Chama na Serikali, kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaendeleza misingi iliyo asisiwa na Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Share:

WAZIRI MKUU AFUNGUA SOKO LA MAZAO SONGEA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amefungua mradi wa maghala ya kuhifadhi nafaka na soko la mazao la OTC-Lilambo katika Halmashauri ya Songea uliogharimu sh. bilioni 1.5.

Amesema Rais Dkt. John Magufuli ameazimia kuwawezesha wakulima kuwa na mahala pa uhakika pa kuhifadhia mazao yao na sehemu ya kufanyia biashara ili kuwaongezea tija.

Amefungua soko hilo jana (Alhamisi, Januari 3, 2019) akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne ya kukagua shughuli za maendeleo mkoani Ruvuma.

Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na ujenzi wa soko hilo pamoja na maghala kwani umezingatia viwango. Maghala hayo mawili yana uwezo wa kuhifadhi tani 5,000 za nafaka.

“Licha ya soko hili kuwapa wakulima wetu fursa ya kupata masoko ya kuuzia mazao yao, pia watapata mafunzo ya namna ya kuhifadhi bidhaa zao pamoja na taarifa za masoko.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ameiagiza bodi ya soko hilo kuhakikisha inatoa matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari ili wakulima waweze kupeleka mazao yao sokoni hapo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka wananchi kutumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha nchini kuandaa mashamba, kupanda mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

“Nawaagiza viongozi wa kata na vijiji hakikisheni wananchi katika maeneo yenu wanaandaa mashamba na kupanda kwa wakati, tunataka tuwe na chakula cha kutosha na ziada tuuze.”

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Songea, Martin Mtani ameiomba Serikali iwapatie mashine itakayowawezesha kupanga madaraja ya mazao ya nafaka mbalimbali.

Mkurugenzi huyo ameomba soko hilo liwekwe kwenye mpango wa kujengewa vihenge vyenye uwezo wa kukausha mazao kwa viwango vya kimataifa ili kutatua tatizo la unyaufu.

Pia Mkurugenzi huyo ameiomba Serikali iwasaidie katika kuliunganisha soko hilo na TMX ili waweze kuuza mazao ya nafaka ndani na nje ya nchi .

Ufunguzi huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.

Wengine ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na maafisa wengine wa Serikali.
Share:

VideoMPYA: PATORANKING -EVERYDAY

Msanii kutoka Nigeria Patoranking amefungua Mwaka 2019 kwa kuachia wimbo wake mpya unaitwa “EVERYDAY
tazama hapa chini


Share:

SOMA MAGAZETI YA LEO 04/01/2019.

Share:

WAFANYAKAZI DAR ES SALAAM WAMPONGEZA RAIS KUFUATIA KUFUTWA KWA KIKOKOTOO.

Na.Mwandishi wetu. Wafanyakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam jana wameandamana katika maandamano ya amani ya Kumpongeza Rais Magufuli kuhusiana na kusitisha kanuni mpya ya sheria ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Maandamano hayo yaliandaliwa na Shirikisho La Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA)yalipokelewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva . Akizungumza katika sherehe hizo za Wafanyakazi wa mkoa huo, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva alizitaka Halmashauri za Mkoa Dar es Salaam zote Watumishi watumie Walaka kwa ajili ya kuwahudumia…

Source

Share:

LIVERPOOL YAKUBALI YAISHE,YAGONGWA 2 - 1 NA MAN CITY


Liverpool imekubali kupoteza mchezo uliopigwa usiku huu dhidi ya Manchester City kwa kufungwa bao 2-1.

Mabao ya City yamewekwa kimiani na Sergio Kun Arguero na Leroy Sane huku Liverpool ikifuta machozi kupitia kwa Roberto Firmino.

Ushindi huo wa Liverpool unakuwa wa kwanza baada ya mechi tano mfululizo katika EPL kushindwa kupata matokeo mbele ya Liverpool.

Kupoteza kwa Liverpool kumeifanya ikubali kufungwa mabao mawili msimu huu EPL ndani ya mechi moja na ikipoteza mchezo wa kwanza.

Msimamo unaonesha hivi sasa Liverpool bado ipo kileleni ikiwa na pointi 54 kwa tofauti ya alama 4 na Man City iliyo na 50.
Share:

WAAMUZI WA MCHEZO WA SIMBA NA JS SAOURA WATANGAZWA.

Na. Mwandishi wetu. Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetangaza waamuzi watakaochezesha mechi ya Klabu Bingwa Afrika kati ya Simba na JS Saoura. Waamuzi hao ni Joshua Bondo ambaye atasimama kama mwamuzi wa kati, waamuzi wasaidizi Oamogetse Godisamang, Moemedi Godfrey Monakwane na mwamuzi wa akiba, Kutlwano Leso, wote kutoka nchini Botswana. Kamishna wa mechi ni James Leonard Mwenda kutoka nchini Malawi, msimamizi mkuu wa mchezo huo ni Alexander Sakyi Asante kutoka nchini Ghana. Simba itawakaribisha JS Saoura katika mchezo huo wa kwanza wa hatua ya makundi ambao utapigwa Januari 12 Jijini Dar…

Source

Share:

Thursday, 3 January 2019

WATOTO WAOKOTWA UFUKWENI MTWARA WAKIWA WAMEFARIKI.

  Watoto wawili wakazi wa kijiji cha Mgao, Mkoni Mtwara wameokotwa wakiwa wamefariki Dunia pembezoni mwa mwambao wa Bahari ya Hindi. Uchunguzi wa Daktari imebainisha kuwa vifo hivyo vimetokana na watoto hao kukosa hewa baada ya kuzama kwenye maji. Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara, Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Blasius Chatanda amesema hii leo kuwa, tukio hilo la kuzama majini limetokea Januari Mosi katika kijiji cha Mgao ambapo uchunguzi wa awali unaonesha watoto hao hawakuwa na wasimamizi walipokwenda kuogelea. “Watoto hao tumeweza kuwatambua, wa kwanza alikuwa anaitwa Rajab Athman mwenye…

Source

Share:

MHE. MABULA AFADHILI VIFAA VYA MICHEZO VYENYE THAMANI YA SH. 6 MILIONI KOMBE LA MHANDU.

Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanslaus Mabula hivi leo amekabidhi Vifaa Vya michezo vikiwemo Jezi, Mipira pamoja na Vitini Vya waamuzi vyenye thamani ya shilingi 6,000,000 kwa vikosi 11 kutoa Mitaa 11 ya Kata ya Mhandu vitakavyoshiriki michuano Kombe la Mhandu lililoandaliwa na Diwani Kata ya Mhandu Mhe. Constantine Sima litakalo anza mnamo tarehe 05.01.2019. Mhe. Mabula akikabidhi Vifaa hivyo amewaasa wana Mhandu kutumia michuano hiyo kama fursa ya kufahamiana vyema na kuwa na umoja katika kuijenga Mhandu, sanjari uibuaji wa Vipaji itakayochochea Mpira wa mguu kuwa ajira na msingi…

Source

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger