Thursday, 6 February 2025

MALUNDE BLOG YATUNUKIWA CHETI CHA SHUKRANI NA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KANDA YA SHINYANGA

...

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga Frank Mahimbali akimtunuku cheti cha shukrani, Mkurugenzi na Mmiliki wa Mtandao wa Malunde 1 blog kama ishara ya kuthamini mchango wa mtandao huo maarufu wa habari katika kufanikisha Maadhimisho ya Wiki ya Sheria na Siku ya Sheria ya Mwaka 2025.

Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga imeadhimisha Siku ya Sheria nchini Februari 3, 2025 ambapo maadhimisho hayo yalitanguliwa na Wiki ya Sheria iliyofanyika Januari 25,2025 hadi Februari 1,2025 katika viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga.


"Cheti hiki kimetolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga kwa chombo hiki cha habari kutokana na ushirikiano wa karibu na juhudi za Malunde 1 Blog katika kuhamasisha na kuendeleza mahusiano mazuri kati ya Mahakama na jamii. Ushiriki wa Malunde Blog umeleta manufaa makubwa kwa jamii ya Shinyanga na kuimarisha utawala wa sheria katika mkoa wa Shinyanga",amesema Jaji Mahimbali leo Februari 6,2025 wakati wa kikao cha Tathmini ya maadhimisho kilichohudhuriwa na wadau mbalimbali.


Malunde 1 Blog inashukuru kwa kutambuliwa na kuahidi kuendelea kutoa mchango wake katika kukuza elimu ya sheria na haki kwa wananchi.







Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger