
Kada maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira, ameteuliwa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa unaoendelea jijini Dodoma leo, Januari 18, 2025.
Jina la Wasira limewasilishwa mbele ya Mkutano Mkuu na limepata baraka za Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho, kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Abdulrahman Kinana, ambaye alitangaza kupumzika miezi mitano iliyopita.
Wasira, ambaye ni miongoni mwa viongozi wazoefu na wenye ushawishi mkubwa ndani ya chama, anapigiwa kura na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa.
Uteuzi huu unalenga kuimarisha uongozi wa chama na kuendeleza mipango ya chama hicho katika kipindi kijacho.
0 comments:
Post a Comment