Thursday 20 February 2020

MKANDARASI AFUNGWA JELA MIAKA 7 KWA UDANGANYIFU WA FEDHA

...

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu mkandarasi wa majengo, Alfred Ndeka (60) kifungo cha miaka saba jela baada ya kukutwa na hatia ya kujipatia Sh116 milioni kwa njia ya udanganyifu.

Hukumu hiyo imetolewa jana Jumatano na Hakimu mwandamizi, Vicky Mwaikambo baada ya kuridhishwa na ushahidi wa mashahidi watano wa upande wa mashtaka pamoja na vielelezo 11 vilivyowasilishwa mahakamani hapo.

Mwaikambo amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo na anahukumiwa kifungo cha miaka saba jela ili iwe fundisho kwa wengine.

“Kutokana na ushahidi pamoja na vielelezo vilivyotolewa unadhibitisha ulipokea Sh116 milioni kwa njia ya udanganyifu huku ukijua kufanya hivyo ni kosa la kisheria hivyo mahakama hii inakuhukumu kwenda miaka saba jela,” amesema Mwaikambo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger