Wednesday 19 February 2020

Katibu UVCCM Muleba Akutwa Amekufa

...
Jeshi la polisi mkoani Kagera limeanza uchunguzi wa kifo cha aliyekuwa katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi CCM katika Kata ya Katoke wilayani Muleba.

Mwili wa Jaspar Jasson mwenye umri wa miaka 41, umekutwa kando kando ya barabara Asubuhi ya, Februari 17 huku ukiwa na michubuko ya kamba shingoni.

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Revocatus Malimi amesema kuwa mwili huo umekutwa na dalili zote za kunyongwa au kujinyonga lakini kinacholeta utata ni eneo ulipokutwa, kwakuwa hakuna mti wala alama zinazoonyesha kuwa tukio limetokea katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa kamanda Malimi, Jasson alionekana hadharani kwa mara ya mwisho Februari 16, Saa kumi na moja jioni katika kijiji cha Bisore alikohamia baada ya kutelekeza familia yake na kwenda kuishi na mwanamke mwingine na kwamba upelelezi kuhusiana na tukio hilo umeanza, huku akiwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger