Thursday 20 February 2020

Iran Yagoma Kukabidhi Kisanduku Cheusi Cha Ndege Ya Ukraine Iliyoipiga Kombora Kwa Bahati Mbaya

...
Kisanduku cheusi cha ndege ya abiria ya Ukraine iliyoangushwa kwa bahati mbaya nchini Iran mwezi uliopita kimeharibika lakini Iran haitakabidhi kisanduku hicho kwa nchi nyingine licha ya shinikizo la kufanya hivyo, mawaziri wa ngazi ya juu wa Iran wamesema , kwa mujibu wa vyombo vya habari vya taifa hilo. 

Waziri mkuu wa canada Justin Trudeau alisema wiki iliyopita kuwa amemshauri waziri wa mambo ya kigeni wa Iran Mohammad Javad Zarif kuwa uchunguzi kamili na huru kuhusiana na kudunguliwa kwa ndege hiyo ni lazima ufanyike. 

Wengi wa abiria 176 waliofariki katika mkasa huo ni Wairani wenye uraia pacha, ambao hautambuliki na Iran. 

Canada ilikuwa na raia 57 katika ndege hiyo. Waziri wa ulinzi wa Iran Amir Hatami alisema kisanduku hicho cha kurekodia data za safari, kimeharibika na kiwanda cha jeshi kimeombwa kusaidia katika kukikarabati.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger