Tuesday, 6 September 2016

Rais Magufuli atoa siku 7 kwa wapangaji wote Serikalini wanaodaiwa na NHC walipe

...
Rais John Pombe Magufuli ametoa siku saba kwa wapangaji wote serikalini wanaodaiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kulipa madeni yao, pamoja na kutoa agizo kwa viongozi wa shirika hilo kuwatolea vitu nje watakaoshindwa kulipa madeni yao kwa wakati.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota.

“Wapangaji wote lazima walipe madeni yao, natoa agizo leo wapangaji wote serikalini wanaodaiwa na NHC ndani ya siku saba wawe wameshalipa madeni yao, ” amesema.

Ameongeza kuwa “Wasipolipa endeleeni kuwatolea vitu vyao nje kama mlivyotoa vya jamaa, awe wa UKAWA toa nje, wa CCM toa. “

Chanzo: Dewji Blog
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger