Wednesday, 9 March 2016

PROF. NDALICHAKO AZIMA MGOMO WA WANAFUNZI ST. JOSEPH NA KUWASIHI WARUDI MADARASANI WAJIANDAE NA MITIHANI

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi prof. Joyce Ndalichako akieleza jambo wakati akiwa kwa viongozi wa chuo kikuu cha St. Joseph leo asubuhi. (picha na Adrian Mgaya)

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako leo amewapa siku tano wanafunzi wa chuo kikuu cha St. Joseph tawi mama lililoko maeneo ya Mbezi Jijini Dar es salaam ili wafanye mitihani yao ili wafunge chuo na kupisha ukarabati wa baadhi ya maeneo ambayo yatatumika kwa ajili ya mafunzo stadi ya wanafunzi hao.

Mbali na kutoa agizo hilo waziri ndalichako alitumia fursa hiyo kuwaomba wanafunzi wote nchini waache kulalamika bali wasome kwa bidii na kuwa na nidhamu ya kutosha.

katibu mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) Prof. Yunus Mgaya (kushoto) akiwa na katibu mkuu wa wizara ya Elimu. Sayansi Teknolojia, na Mafunzo ya Ufundi wakisikiliza kwa makini maneno ya Waziri wa Elimu Prof Ndalichako, hayupo pichani (picha na Adrian Mgaya)
waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini maelezo aliyokuwa anayazungumza Waziri wa Elimu Prof. Ndalichako

wanafunzi wa chuo cha St. Joseph wakimsikiliza waziri wa Elimu Prof. Ndalichako (hayupo pichani).
waandishi wa Habari wa gazeti la The Hill Observer lichapishwalo na Chuo Kikuu cha Dar es salaam wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha St.Joseph Mwendwa Ramadhani Mwendwa.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger