Thursday 17 March 2016

MATOKEO UEFA:BARCA 3 ARSENAL 1

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Barcelona imetinga hatua ya robo fainali ya michuano ya klabu bingwa ulaya baada ya kuifumua Arsenal 3-1 usiku wa Jumatano.

Mabao ya Barcelona yalifungwa na wachezaji Neymar da Silva Santos, Luis Suarez na Lionel Messi akahitimisha idadi ya mabao hayo dakika ya 88.

Na goli pekee la kufutia machozi la Arsenal limefungwa na Mohamed Elneny dakika ya 51 kipindi cha pili.

Barcelona imeifunga Arsenal jumla ya mabao 5-1 kufuatia ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa dimba la Emirates.

Katika mwingine Bayern Munich imechomoza na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Juventus ya Italia.

Mabao ya Bayern yamefungwa na Lewandowski, Thomas Muller, Thiago Alcantara na Kingsley Coman, huku magoli ya Juventus ya kifungwa na Paul Pogba, na Juan Cuadrado.

Kwa matokeo hayo Bayern imeshinda jumla ya bao 6-4 kufuatia sare ya mabao 2-2 katika mchezo wa awali.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger