Tuesday 11 August 2015

KAMATI KUU YAAGIZA KURA ZA MAONI KURUDIWA KATIKA MAJIMBO MATANO

...
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Nape Nnauye akizungumza kwenye moja ya mikutano na waandishi wa habari

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CC) imeagiza kurudiwa kwa uchaguzi   katika majimbo matano  kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kura ya maoni.
Majimbo hayo ni Makete,Busega,Ukonga,Rufiji na Kilolo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Dodoma Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye amesema mchakato  huo utarudiwa siku ya alhamisi Agosti 13.

Amesema baada ya uchaguzi huo matokeo yatapelekwa katika vikao vinavyoendelea kwa ajili ya uamuzi.
Akizungumzia kuhusu vikao vinavyoendelea Ndugu Nape amesema vikao hivyo vinaendelea vizuri ambapo jana kikao cha kamati ya maadili kiliendelea mpaka usiku.
Amesema leo wanatarajia kumaliza  kikao cha CC ambapo kesho na kesho kutwa watamaliza na kikao cha halmashauri kuu ya chama hicho(NEC) kama ilivyopangwa.
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger