Thursday 12 September 2024

TASAC YATOA ELIMU KWA WADAU MBALIMBALI WILAYANI UKEREWE

 











Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) leo tarehe 10.9.2024, limetoa elimu ya ulinzi, usalama na utunzaji wa mzingira ya usafiri majini kwa wadau mbalimbali wa usafiri majini katika kisiwa cha Ukara, wilayani Ukerewe.
 
 Elimu hiyo imehusisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na wasafiri na wasafirishaji, wamiliki wa vyombo vya usafiri majini, viongozi wa serikali za Kijiji na wananchi kwa ujumla. 

Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika katika mwalo wa Bukungu Naho. Michael Rogers amesema ”kila mmoja ni balozi wa usalama wa vyombo vya usafiri majini hivyo hatuna budi kuhakikisha vyombo vinakidhi viwango na kuhakikisha vinakuwa na leseni kwa mujibu wa sheria na kupunguza ajali za mara kwa mara kwa kuvaa vifaa vya kujiokolea kwani kila mmoja wetu ni muhimu kwa jamii na taifa kwa ujumla”

Aidha, wananchi wa Ukerewe katika mialo iliyotembelewa na TASAC wamepongeza na kushukuru juhudi za utoaji elimu na kuomba Shirika kuendelea kufanya hivo mara kwa mara ili kuongeza uelewa mpana kwa wananchi juu ya sekta ya usafiri majini.

Zoezi hili la utoaji elimu limeanza Septemba 9 na litafikia tamati Septemba 13,2024.
Share:

Wednesday 11 September 2024

Video : BHUFUNA SHAGEMBE - NGOMA LIVE KWA MASHIGURU, WANACHEZA NA FISI

 

Share:

AGRIWEZESHA KUGAWA MIZINGA 130 KUHIFADHI MAZINGIRA


Na Christina Cosmas, Morogoro

Mizinga ya nyuki 135 inatarajia kugawiwa kwa wananchi wa eneo la Kibaha na Kisarawe ili kulinda na kuhifadhi mazingira ikiwemo vyanzo vya maji kwenye mto Ruvu na mto Kizinga.

Mkurugenzi waTaasisi ya uhifadhi wa mazingira na kilimo (Agriwezesha) Deogracia Ignas amesema hayo wakati wa kumbukizi ya miaka 5 ya taasisi hiyo ambapo alisema mizinga hiyo itagawiwa kwenye vikundi 9 vyenye wastani wa watu 10 hadi 15 na kuwa sehemu ya shamba darasa la watu kujifunza.

Ignas anasema tayari wameshawapa mafunzo wanufaika ambapo wanalenga kufanya mambo ya uhifadhi katika mto Ruvu na Kizinga ili kukomesha watu kufanya shughuli zisizo rafiki kwenye mito na kuwapa shughuli rafiki ili kupunguza uharibifu wa mazingira.

Amezitaja kazi zinazofanywa na kuharibu mazingira kuwa ni pamoja na ukataji wa mkaa kwa ajili ya kuni za biashara na uchomaji wa mkaa ambapo mizinga hiyo itawasaidia kuwaingizia kipato.

Naye Balozi wa mazingira kutoka ofisi ya makamu wa Rais Muungano na mazingira Chage Alex Chage anasema jamii inapaswa kuona haja ya kuendeleza utunzaji wa mazingira utakaosaidia dunia kuepuka kufikia kwenye ongezeko la juu ya joto la kiasi cha nyuzi joto 1.5 mwaka 2050.

Chage anasema kwa mujibu wa takwimu za kimataifa kwa sasa kiwango cha juu cha joto kimefikia nyuzi joto 1.2 ambayo pia haitakiwi kuzidi jamii inapaswa kuwa macho katika kusimamia shughuli za utunzaji wa mazingira na kujiepusha na kufika kwenye matokeo ya mabadiliko ya tabianchi.


Share:

IJUE MBINU SAHIHI YA KUWAKABILI WEZI

Jina langu ni Ibra kutokea Tabora, Tanzania, ni kijana ambaye nimejikita katika biashara ndogo ndogo hapa jijini kwa miaka zaidi ya 10 sasa.

Katika biashara zangu hizi nimewahi kupitia changamoto nyingi sana kiasi kwamba nilitaka hadi kuachana na kazi yenyewe licha ndio ilikuwa inaniingizia kipato.

Changamoto yangu kubwa ilikuwa ni wizi ambao ulikuwa unafanywa na vijana wasio na kazi ambao pia hawataki kujishughulisha kivyovyote vile.

Kila mara nilikuwa nikija asubuhi katika kibanda changu cha biashara muda wa asubuhi nilikuwa nakuta kimevunjwa na kuibiwa kila kitu.

Hilo lilikuwa linanichanganya sana maana ilikuwa inanibidi nianze kutafuta fedha nyingine kwa ajili ya kuanza upya.

Mwisho wa siku nilichoka hali hiyo na kuanza kutafuta suluhisho ya kudumu, ndipo nilikutana na mtu anayeitwa Dr Bokko kupitia mitandao ya kijamii.

Huyu ni mtu ambaye anaweza kuwadhibiti wezi kwenye biashara yako, ukipata tiba yake hakuna mwizi atajaribu kugusa biashara yako hata kidogo.

Nilipopata dawa ya Dr Bokko, asubuhi moja ninafika katika ofisi yangu na kukuta vijana watatu wameganda karibuni na kibanda changu huku wameshika mbali ambazo walikuwa wameziiba.

Hapo hapo nilichukua simu na kuwasiliana na Dr Bokko ambaye alinipa maelezo ya kufanya kuhusu jambo hilo.

Tangu wakati huo hakuna tena mwizi ambaye amegusa mali yangu kutokana tukio hilo lilifahamika na watu wengi. Mpigie  Dr Bokko kwa namba +255618536050 ili kupata msaada wako.

Mwisho.


Share:

DR LUZILA : MAGONJWA YASIYO YA KUAMBUKIZA SI YA WANANCHI WA KAWAIDA PEKEE, NI KWA KILA MTU

 


Na George Mganga, SHINYANGA RRH

KUTOKANA na ongezeko la watu wenye magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa miaka ya hivi karibuni, elimu ya Afya kuhusiana na Ugonjwa wa Kiharusi (Stroke), imetolewa leo Septemba 11, 2024 kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga.

Akitoa elimu hiyo, Daktari Bingwa Bingwa wa Magonjwa ya ndani na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga, Luzila John, ameeleza lengo mama la elimu hiyo ni kuwasaidia watumishi ili waweze kulinda afya zao.

Dkt. Luzima amesema magonjwa yasiyo ya kuambukiza si ya wananchi wa kawaida pekee, bali ni kwa kila rika na kila mtu, akibainisha kuwa watumishi wana haki ya kukumbushwa ili kulinda afya zao pamoja na kuwasaidia wagonjwa wanaokuja hospitalini.

“Nimetoa elimu hii kwa ajili ya kunusuru afya za watumishi ili waweze kutambua madhara ya Kiharusi.

“Elimu hii si kwa wananchi walio nje ya Hospitali pekee, hata watumishi wenyewe wanapaswa kuwa na desturi ya kupima afya zao mara kwa mara ili kuweza kufahamu maendeleo yao”, amesema.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Luzila amebainisha kuwa watu milioni 15 hupata Kiharusi kila mwaka, akieleza katika idadi hiyo, asilimia 30 hufariki, 30 hupona wakiwa na kilema, zilizobaki hupona na kurudi kwenye hali yao ya kawaida.

Kwa upande wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Shinyanga, Luzila amebainisha Hospitali hulaza wagonjwa 20 kwa kila mwezi, huku akisema kwa takwimu za miezi mitano (Februari hadi Juni) mwaka huu, hospitali ilipata jumla ya wagonjwa 108 baada ya kufanyiwa vipimo vya CT SCAN.

Aidha, Luzila ameyataja magonjwa ya Shinikizo la Juu la Damu, Kisukari na Magonjwa ya Moyo, kuwa ndiyo magonjwa sababishi ya Kiharusi, hii ikichagizwa na mtindo wa maisha ambao watu wanaishi nao kwa sasa.

Vilevile, Luzila ameshauri watu wawe na desturi ya kufika kwenye vituo vya afya mara kwa mara kwa ajili ya kupata vipimo, pamoja na kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuulinda mwili na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Kwa upande mwingine, Luzila ameshauri watu kuacha matumizi holela ya pombe, uvutaji wa sigara na tumbaku sababu ndiyo visababishi vikubwa vinavyopelekea mtu kupata magonjwa hayo ikiwemo kiharusi.

Share:

Tuesday 10 September 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 11,2024

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger