Saturday 31 August 2024

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 1, 2024

Share:

WAANDISHI WA HABARI WATEMBELEA CHEMCHEMI YA AJABU YA KONDOA MJINI.. "KUNA ULINZI MKALI WA NYOKA WATATU"

Waandishi wa Habari kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika chemchemi ya ajabu ya maji iliyopo Kondoa Mjini Mkoani Dodoma - Picha na Malunde Media
Waandishi wa Habari kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika chemchemi ya ajabu ya maji iliyopo Kondoa Mjini Mkoani Dodoma 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Waandishi wa Habari kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania wametembelea chemchemi ya ajabu ya maji iliyopo Kondoa Mjini Mkoani Dodoma ambayo inayozungukwa na madhari nzuri ya misitu na viumbe hai mbalimbali wakiwemo ngedere, nyoka na chui mmoja.

Waandishi wa hao wa habari wameshuhudia maajabu ya Chemchemi hiyo iliyopo msituni yenye maji asili ya chumvi ambayo imejengewa ukuta na kuifanya iwe chanzo kikuu cha maji chenye uwezo wa kusambaza maji kwa wakazi wa eneo hilo.

Mmoja wa walinzi wanaolinda eneo hilo anasema chemchemi hiyo ina ulinzi mkali wa nyoka watatu wakubwa ambao huonekana nyakati za usiku wakizunguka kwenye chemchemi lakini pia endapo katika eneo hilo akaingia mtu mwenye nia ovu/mbaya nyoka hao huonekana hata kama ni mchana ili kuzuia janga.

Waandishi wa habari wameelezwa kuwa wageni kutoka maeneo mbalimbali hufika katika chemchemi hiyo ambayo inalindwa na nyoka nyakati za usiku na kuchukua maji hayo ambayo yanadaiwa huondoa balaa/mikosi na kuponya magonjwa.

Msitu unaozunguka chemchemi hii pia unachangia katika uhifadhi wa mazingira na ni nyumbani kwa mimea na wanyama wa aina mbalimbali.

Chemchemi ya Kondoa Mjini, kama sehemu ya mazingira yenye rasilimali za maji, ina maajabu kadhaa yanayoiweka kuwa ya kipekee, mfano Uwepo wa Maisha ya Wanyama na Mimea: Chemchemi ya Kondoa inatoa maji safi na yenye unyevu kwa mazingira ya karibu, na hivyo kuunda mazingira yenye muktadha mzuri kwa wanyama na mimea. Hii inajumuisha aina mbalimbali za mimea ya msitu, wanyama wa porini na viumbe vidogo vidogo.
Pia Uhifadhi wa Maji, Chemchemi hii ni muhimu kwa uhifadhi wa maji kwa ajili ya wakazi wa Kondoa na maeneo jirani. Inasaidia katika kuhakikisha upatikanaji wa maji ya kunywa, kilimo, na matumizi mengine ya nyumbani, hasa katika nyakati za ukame.

Kuhusu Mchango wa Mazingira, Chemchemi ya Kondoa ni sehemu ya mfumo wa maji wa chini ya ardhi ambayo ina mchango mkubwa katika kudumisha mazingira ya asili.

Kihistoria na Utamaduni, Chemchemi ya Kondoa pia ina umuhimu wa kihistoria na kitamaduni. Chemchemi hii ina hadithi na imani zinazohusishwa nayo, na hivyo kuwa sehemu ya urithi wa kitamaduni wa jamii katika eneo hilo.

Chemchemi ya Kondoa ina umuhimu katika urithi wa kitamaduni wa eneo hilo. Hadithi, hadithi za kienyeji, na simulizi zinazohusiana na chemchemi hii zinatoa mwangaza kuhusu maisha na imani za watu wa eneo hilo.

Kwa upande wa Utafiti wa Kijiolojia na Hidrolojia, Chemchemi hii ni muhimu kwa tafiti za kijiolojia na hidrolojia kwa sababu inatoa maelezo muhimu kuhusu michakato ya mawe na jinsi maji yanavyotiririka chini ya ardhi.
Pia inasemekana kuwa mzungu (mmoja wa wageni au mtafiti wa kigeni) alitumbukia kwenye chemchemi ya Kondoa wakati alikuwa akichunguza au kutembelea eneo hilo.

Hadithi kuhusu mzungu kutumbukia kwenye chemchemi ya Kondoa ni maarufu kama simulizi ya kihistoria au hadithi inayohusishwa na eneo hilo. Hadithi hii inaeleza tukio la zamani ambalo linaweza kuwa na sehemu ya ukweli, lakini mara nyingi ni sehemu ya urithi wa kitamaduni wa eneo hilo.

Ipo Hadithi kuhusu tembo kutumbukia kwenye chemchemi ya Kondoa ni sehemu ya simulizi za kienyeji na hadithi za kitamaduni zinazozunguka eneo hilo. Katika baadhi ya hadithi za watu wa eneo la Kondoa, kuna simulizi kwamba tembo alitumbukia kwenye chemchemi au kwenye eneo la maji na kwamba tukio hili lina umuhimu wa kihistoria au kitamaduni. Hizi ni baadhi ya mambo yanayohusiana na simulizi hiyo:

Kwa kifupi, chemchemi ya Kondoa Mjini ina umuhimu mkubwa katika nyanja mbalimbali, na inachangia kwa kiasi kikubwa katika maisha ya watu wa eneo hilo, uhifadhi wa mazingira, na urithi wa kiutamaduni.
Waandishi wa Habari kutoka Mikoa mbalimbali nchini Tanzania wakiwa katika chemchemi ya ajabu ya maji iliyopo Kondoa Mjini Mkoani Dodoma 

Mkurugenzi wa Malunde 1 blog, Kadama Malunde akijipiga picha za kumbukumbu kwenye  Chemchemi ya Kondoa
Waandishi wa habari wakipiga picha za kumbukumbu kwenye  Chemchemi ya Kondoa

Share:

NDOTO YA RAIS SAMIA NI KUWA NA MASHIRIKA YENYE UFANISI - BALOZI Dkt. KUSILUKA

 

Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka amesema kuwa ndoto ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha nchi inakuwa na mashirika yenye ufanisi mkubwa na wa viwango vya kimataifa.

Hivyo, amewataka Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa taasisi na Mashirika ya Umma kuhakikisha wanatekeleza kwa ukamilifu maagizo yaliyotolewa na Mhe. Rais Samia.

Ametoa kauli hiyo leo Agosti 30, 2024 jijini Arusha wakati akifunga kikao kazi cha viongozi hao kilichofanyika jijini humo tangu Agosti 27 hadi 30, 2024.

"Serikali itayachukua maazimio yote yaliyokubaliwa na nawaahidi yatafanyiwa kazi, tutawasaidia kuhakikisha yanatekelezeka ili kutimiza ndoto ya Mhe. Rais Samia juu ya taasisi na mashirika ya umma", amesema Balozi, Dkt. Kusiluka.

Amewataka viongozi wa taasisi na mashirika ya umma kujenga utamaduni wa kujifunza mbinu na mikakati mipya kutoka kwa mashirika yaliofanikiwa na kuitazama serikali kwa upana wake.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Mbaga Kida amesema kuwa wamewasilisha malengo na wanaamini watayasimamia malengo hayo ili kuweza kuhakikisha yale waliyojiwekea katika kusimamia na kuboresha utendaji kazi wa taasisi na mashirika ya umma yanaweza kufikiwa.

Kwa upande wake Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu amesoma jumla ya maazimio sita yaliyoazimiwa na viongozi hao ikiwemo, Ushiriki katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2050 na uandaaji wa mipango mkakati wa taasisi za umma; Utawala bora na mawasiliano ya umma pamoja na Usimamizi wa rasilimali watu, mafunzo na uendelezaji wa uongozi bora.

Maazimio mengini ni, Mikakati ya taasisi na mashirika ya umma kuwekeza nje ya Tanzania; Kuongeza uchangiaji na kupunguza utegemezi katika Mfuko Mkuu wa Taifa na kutekeleza kikamilifu maazimio yaliyotolewa kwenye kikao kilichopita ambayo hayajatekelezwa.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba, Kamishna wa Bima Tanzania kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware amesema kuwa Wakuu wa Taasisi wamepokea maelekezo yote yaliyotolewa na viongozi na wanaahidi kuyatekeleza kwani wana hamu na mageuzi yanayotarajiwa.

Share:

Friday 30 August 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 31, 2024

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger