Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akizungumza wakati akizindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Kamishina wa Elimu Tanzania Dkt.Lyabwene Mtahabwa,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Elimu Maalum na Jumuishi kutoka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknlojia Dkt.Magreth Matonya,akielezea lengo la mkakati huo wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Mwakilishi Mkazi wa Mashirika ya Kimataifa Dkt.Daniel Baheta,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma Pili Mbaga,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Wanafunzi walioshiriki uzinduzi wakifatilia Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka (hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Wadau mbalimba wakifatilia Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka (hayupo pichani), wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Elimu Maalum na Jumuishi kutoka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknlojia Dkt.Magreth Matonya kabla ya kuzindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akizindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akiwa na wadau pamoja na wanafunzi wakionyesha vitabu vya muongozo mara baada ya kuzindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akiwa katika picha ya pamoja na wadau mara baada ya kuzindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Eliamani Sedoyeka,akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi mara baada ya kuzindua Mkakati wa Kitaifa wa Elimu Jumuishi wa mwaka 2021/22-2025/26 uliofanyika leo Januari 28,2022 jijini Dodoma.
............................................................
Na.Alex Sonna,Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezindua mpango mkakati wa kitaifa wa elimu jumuishi wa miaka mitanto (5) unaolenga kutoa fulsa sawa ya elimu kwa makundi yote bila kujali kikwazo cha aina yotote au mazingira.
Akizindua mpango huo leo Januari 28,2022 jijini Dodoma Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Eliamini Sedoyeka amesema mpango huo ni wa tatu na umelenga kwenda kuboresha utoaji wa elimu katika ngazi zote bila kujali kikwazo cha aina yoyote katika fulsa ya upataji wa elimu kwa watoto.
"Kama Serikali tulikuwa na mipango mbalimbali na huu tunaozindua ni wa tatu ambao unakwenda kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu kwa usawa bila kujali hali ya mtoto toka ngazi ya awali, msingi, sekondari, ualimu, vyuo vya ufundi, maendeleo ya wananchi, elimu ya nje ya mfumo, na elimu ya juu” amesema. Prof. Sedoyeka.
Amesema mkakati huo unalenga kuwa na mfumo wa elimu unaotoa fulsa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu kupata elimu bila vikwazo kimtazamo, mazingira, kiuchumi na kitaasisi katika ngazi zote.
“Mkakati huu unatoa fulsa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu kusoma masomo ya ufundi tangu wakiwa darasa la awali lengo kuwajengea uwezo wa kujitegemea kiuchumi kwa kuwa na uchuzi” amesema.
Ameongeza kuwa “mkakati huu pia utatekelezwa katika ngazi za vyuo vya ufundi, vyuo vya maendeleo ya wananchi ambako wananchi watapata umahiri katika fani mbalimbali zikiwamo za ujasiliamali na TEHAMA kuwaimarisha kiuchumi” Amesema.
Amesema mkakati huo umechapishwa kwa kuzingatia ujumuishi kwa kuwa na nakala za maandishi ya kawaida, maandishi yaliyokuzwa na maandishi Braille kwa ajili ya watu wenye uoni hafifu na wasioona.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Elimu Maalumu Dkt Magreth Matonya amesema mpango mkakati huo umeboreshwa na wanaamini utaendana na mahitaji ya sasa na ili kuhakikisha unafanya vyema mpango huo utakuwa ukifanyiwa tathmini kila baada ya miezi sita ili kuona utendaji kazi wake na matokeo.
“Mkakati huu utatupa dira ya wapi tuelekee katika utekelezaji wa elimu jumuishi, utasaidia upatikanaji wa taarifa za upatikanaji wa taarifa za utelelezaji wa elimu jumuishi ili kurahisisha ufanyikaji wa tathmini” amesema Dkt. Magreth.
Amesema mkakati huo umelenga kurekebisha sera ya elimu iendane na elimu jumuishi, kuimarisha upatikanaji wa elimu bora na kwa usawa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika ngazi zote, kuongeza uandikishwaji na ushiriki wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika ngazi zote za elimu.
Nae Kamishna wa elimu hapa nchini Dkt. Lyabwene Mtahabwa amesema kuzinduliwa kwa mkakati huo ni lengo la kumfanya kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bora na kwa usawa kwa maendeleo ya taifa na jamii kwa ujumla.

























Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa akipiga ngoma kuashiria Uzinduzi Rasmi wa Tuzo za Muziki Tanzania kwenye Hafla iliyofanyika usiku wa Januari 28, 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam. 
Wadau wa Muziki nchini wakiwa wamefurika kwaajili ya kufuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamduni,Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi (wa kwanza kushoto) akifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Utamaduni. sanaa na Michezo Mhe. Mohamed Mchengerwa (katikati) akiwa na Naibu Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Pauline Gekul (wa kwanza kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Mhe.Said Yakubu wakifuatilia buruduni katika uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mheshimiwa Niki wa Pili akifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Wadau wa Muziki Diwani wa Kilungure Mkubwa Fella (Katikati) akiwa pamoja na Mbunge wa Morogoro Kusini Mheshimiwa Hamisi Taletale maarufu Babu Tale wakifuatilia uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa ngoma kutoka wilayani Bagamoyo wakitoa burudani katika katika uzinduzi wa tuzo za muziki pamoja na ugawaji wa mirabaha kwa wasanii uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Banda la kituo cha elimu ushauri na msaada wa kisaikolojia cha Taasisi ya Ustawi wa Jamii lililopo katika uwanja wa ukumbi wa Jiji ilala ambapo huduma ya ushauri na elimu inatolewa bure kwa wafanyabiashara wahanga wa moto uliotokea soko la mchikichini karume Ilala Jijini Dar es Salaam.
Kutoka Kushoto mwenyekiti wa wafanyabiashara walemavu soko la mchikichini Mzee Juma Hamis akisikilizwa kwa umakani mkubwa na maafisa ustawi wa jamii Rukia Mwinyi kutoka kituo cha elimu, ushauri, na msaada wa kisaikolojia (Taasisi ya Ustawi wa Jamii) pamoja na Bi. Lilian Chilo afisa Ustawi wa jamii kutoka Ofisi ya Jiji la Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanya biashara waliofika kwenye uwanja wa ukumbi wa jiji Ilala soko la mchikichini kupata huduma ya ushauri na elimu kutoka kwa maafisa Ustawi wa jamii wa kituo cha elimu na ushari cha Taasisi ya Ustawi wa Jamii na Jiji la Dar es salaam.
Msaikolojia kutoka kituo cha elimu na ushauri Taasisi ya Ustawi wa Jamii Dkt. Zainab Rashid akitoa huduma kwa mfanya baishara mlemavu Bw. Jamal Nassoro Lemu wa soko la mchikichini Ilala ambapo huduma ya elimu na ushauri inatolewa kwa wafanyabiashara wahanga wa moto sokoni hapo hasa wale wenye mahitaji maalum.
Mratibu wa kituo cha elimu, ushauri na msaada wa kisaikolojia Bi Rufina Khumbe akimhudumia mfanyabiashara wa bajaj eneo la soko la mchikichini Bi Ashura Sadiki katika uwanja wa ukumbi wa jiji ilala Dar es Salaam.