Thursday, 4 June 2020

Picha : KAMPUNI YA VINYWAJI VIKALI EAST AFRICAN SPIRITS (T) LTD YATOA MSAADA WA VIFAA VYA KISASA KUJIKINGA NA CORONA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA SHINYANGA


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga inayotengeneza vinywaji vya Diamond Rock na Hansons Choice imekabidhi msaada wa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona vyenye thamani vya shilingi Milioni 8 katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.


Vifaa vilivyotolewa na Kampuni hiyo ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga ni pamoja na kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki chenye thamani ya shilingi Milioni 6.8 kikiwa na masinki matano na tenki la maji lenye ujazo wa lita 1000 na vifaa vingine vya kujikinga na COVID-19 ikiwemo Vitakasa mikono,barakoa,gloves, pamba, sabuni za maji, cord clamp na pulse Oximeter vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2.

Msaada huo umekabidhiwa leo Alhamis Juni 4,2020 na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.

Akikabidhi vifaa hivyo, Gasper Kileo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) amesema vifaa hivyo vitatumika katika kuiongezea nguvu serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.

“Ninaishukuru sana serikali  ya awamu ya tano inayoongozwa na Amiri Jeshi wetu Mkuu, Rais wetu Mpendwa, Dkt. John Pombe Magufuli namna ilivyopambana na ugonjwa wa COVID – 19. Tumepambana na COVID-19 tofauti na nchi zote duniani na sasa wote ni mashahidi kwenye vyombo mbalimbali vya habari na Mitandao ya Kijamii kwamba dunia sasa inaangalia Tanzania imefanya nini kuiondoa Corona. wenzetu ndiyo wanafuta kile tunachofanya Tanzania”,amesema Kileo.

“Nimpongeze pia Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack kwa namna mnavyopambana dhidi ya Corona. Lakini pia niwapongeze Madaktari wetu wote nchi nzima mmepambana kwa kushirikiana na serikali na Mungu ametusaidia tumeweza. Naomba tuendelee kupambana mpaka pale Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli atakaposema silaha zetu tuziweke chini”,ameongeza Kileo.

Mkurugenzi huyo pia amewashauri wananchi kuendelea kunawa mikono na kwamba zoezi hilo liwe endelevu hata siku watakapotangaziwa kuwa Corona imefutika nchini Tanzania.

Akipokea vifaa hivyo, Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack ameishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango huo kwa ajili ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali katika mapambano dhidi ya Corona.

“Mheshimiwa MNEC uliniambia utaleta vifaa kwa ajili ya kupambana na Corona lakini sikujua kama utaleta vikubwa namna hii. Umetuwekea masinki ya kunawia mikono na tenki kubwa la maji na umeweka hadi kivuli ili watu wetu wanaponawa mikono wawe kivulini. Mwenyezi Mungu akubariki sana na abariki Biashara yako na shughuli unazofanya ziendelee na kukua ili uweze kutupa misaada mingine zaidi”,amesema Telack.

“Kimsingi mimi nimepokea vifaa hivi kwa niaba ya wananchi lakini hawa wananchi wanaonawa hapa wataendelea kukuombea kwa Mungu. Umetengeneza kitu kikubwa sana na pengine ndiyo maana walikuchagua kuwa MNEC wao hata wale wasiokuwa wa CCM sasa wanaona jinsi viongozi wa CCM na serikali ya CCM inavyojali wananchi. Huu ni mfano wa kutosha,niombe na viongozi wengine waige mfano wako”,amesema Mkuu huyo wa mkoa.

“Umeenda kisasa zaidi,umetuletea vifaa vya kisasa,na naomba uongozi wa hospitali hii uweke mtu wa kuwaelekeza wananchi namna ya kutumia kifaa hiki, wasianze kugusa gusa wakavunja hapa,wajue kwamba akisogeza mikono yake maji yanatoka. Na pengine hapa patakuwa mahali pa kujifunzia masuala ya teknolojia ya kisasa.

Yaani MNEC unafundisha watu teknolojia ambazo zipo,wataambiana ukienda hospitali,ukisogeza tu mkono maji yanatoka,yaani hiyo nayo ni sehemu ya kujifunzia. Ninategemea tutapata wageni wengi zaidi,wengine watakuja kunawa tu mikono ili waone jinsi maji yanavyoka bila kugusa,wananchi watakuja kujifunza. RMO naomba vifaa hivi vitunzwe ili visiharibike”,amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Katika hatua nyingine,Mkuu huyo wa mkoa amewataka wananchi kuendelea kunawa mikono mara kwa mara ili kupunguza maradhi mengine yanayotokana na kutozingatia taratibu za afya

“Kunawa mikono ni ustaarabu. Sasa hivi siyo COVID -19 peke yake tumegundua kwamba kunawa mikono kunatupunguzia maradhi mengine kama vile tumbo na kuharisha,huko wodini sasa hivi watu waliokuwa wanakuja kwa matatizo ya tumbo na kuhara wamepungua kwa kiasi kikubwa sana”,amesema.

“Niwaombe wananchi wa Shinyanga hii tabia ya kunawa mikono iwe endelevu siyo kwa sababu ya Corona tu,hata baada ya Corona unaingia hospitali nawa mikono yako,unaingia sokoni nawa mikono yako ili pia tuweze kupunguza maradhi mengine yanayotokana na kutozingatia taratibu za afya”,ameongeza Telack.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Timoth Sosoma ameishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa msaada huo na kueleza kuwa vifaa hivyo vitasaidia katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona huku akiwataka wananchi wasiwe wagumu kunawa mikono.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Muonekano wa Masinki ya kunawia mikono bila kugusa koki ambayo ni sehemu ya kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga inayotengeneza vinywaji vya Diamond Rock na Hansons Choice  kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga leo Alhamis Juni 4,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (katikati) akikata utepe wakati akipokea kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona kutoka Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (aliyevaa kilemba cha bluu) namna ya kunawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa cha kunawia mikono.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela akinawa mikono kwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akiishukuru Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango wa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu wa tanki la maji ambalo ni sehemu ya kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kilichotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu palipowekwa kifaa cha kisasa cha kunawia mikono iliyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya vifaa kwa ajili ya kujikinga na COVID-19 ikiwemo Vitakasa mikono,barakoa,gloves, pamba,cord clamp na pulse Oximeter vyenye thamani ya shilingi milioni 1.2 vilivyotolewa na Kampuni ya Uzalishaji Vinywaji Vikali ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akizungumza wakati akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (aliyevaa kilemba cha bluu kushoto) kifaa cha kisasa cha kunawia mikono bila kugusa koki na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona  katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akiipongeza serikali inayoongozwa na  Rais Dkt. John Pombe Magufuli namna ilivyopambana na ugonjwa wa COVID – 19. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (wa tatu kulia) akiishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa mchango wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack sabuni ya kunawia mikono ili kukabiliana na COVID - 19 katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga, Gasper Kileo akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack Vitakasa mikono ili kukabiliana na COVID - 19 katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Timoth Sosoma akiishukuru Kampuni ya East African Spirits (T) Limited Shinyanga kwa msaada wa vifaa vya kujikinga na COVID- 19 ambavyo vitasaidia katika kukabiliana na ugonjwa wa Corona katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis Amtuhumu Trump Kwa Kutaka Kuwagawa Wamarekani Kwa Matabaka

Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis  ametangaza kuwaunga mkono wananchi wa Marekani wanaondamana kulaani ubaguzi wa rangi na mienendo ya polisi ya Marekani hususan dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika.

Mattis alitangaza msimamo huo katika taarifa iliyochapishwa jana Jumatano na gazeti la The Atlantic, ambapo amemtuhumu Trump kuwa anajaribu kuwagawanya Wamarekani kimatabaka.

Ameeleza bayana kuwa, "Donald Trump ni rais wa kwanza katika uhai wangu ambaye hawaunganishi Wamarekani, bali hata hajifanyi kana kwamba anajaribu kuwaunganisha." 

Amesema taifa hili linashuhudia matokeo ya jitihada za makusudi za miaka mitatu za Trump za kuwagawa wananchi wa Marekani.

James Mattis amesema ;, "tunaweza kuungana bila yeye (Trump), hili si jambo jepesi, lakini linawezekana kwa ushirikiano."

Kadhalika amekosoa hatua ya rais huyo kutumia jeshi la taifa kuzima maandamano ya kiraia, ambayo ni haki ya msingi iliyoanishwa kwenye katiba ya nchi hiyo. 

 Mattis ambaye ni jenerali mstaafu aliachia ngazi mwishoni mwa mwezi Februari mwaka 2018, baada ya kuhitalifiana na Trump

 Kama jibu lake kuhusu ukosoaji huo, Trump alituma mfululizo wa ujumbe kwenye Twitter ambapo alisema..."Sikupenda mtindo wake( James Mattis  )  wa uongozi au yeye mwenyewe sikumpenda na wengine wengi wanakubaliana na hilo, "Afadhali  aliondoka mapema"


Wananchi wa Marekani wamekuwa wakiandamana kwa zaidi ya wiki moja sasa, tangu alipouawa kikatili na polisi mweupe, George Floyd, Mmarekani mweusi katika mji wa Minneapolis jimboni Minnesota.


Share:

Vigogo Wanne Wizara ya Maliasili na Utalii Wasimamishwa Kazi

Katibu Mkuu  Wizara ya Maliasili na Utalii ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Utalii, Deogratius Mdamu na kumsimamisha kazi Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa wizara, Flora Masami kutokana na mapungufu na ubadhirifu mkubwa kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Utalii (TDL).



Share:

Watatu Watiwa Mbaroni Dar es Salaam kwa tuhuma za mauaji ya dereva tax (UBER)

Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya dereva tax (UBER) aliyefahamika kwa jina la Joseph Tillya Mpokala,(51),Mkazi wa Mbezi kwa Msuguli .

Watuhumiwa hao :-

1. Godson Laurent Mzaura,(29),Mkazi wa Mbezi Beach,Mpiga picha.

2. Said Mohamed Mahadhi (38),Mkazi wa Afrikana,Fundi simu na

3. Denis Urassa @ Pasua,(45),Mkazi wa Makongo Juu,Fundi simu.

Mnamo tarehe 26.05.2020 Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dsm lilipata taarifa kutoka kwa mke wa marehemu kuwa Mume wake ametoweka tangu tarehe 21.05.2020 na simu zake zote hazipatikani.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM kupitia kikosi chake cha kupambana na uhalifu kilianza ufuatiliaji mara mmoja.

Mnamo tarehe 27.05.2020 alikamatwa mtuhumiwa Godson Laurent Mzaura na kuhojiwa kisha kukiri kufanya mawasiliano na marehemu ambapo alieleza kuwa Mnamo tarehe 21.05.2020 majira ya saa saba mchana walimkodi marehemu ili awapeleke maeneo ya Mbezi na walipofika Mbezi Juu watuhumiwa hao walimuua Joseph Tillya na kumfukia kwenye shimo katika eneo la wazi lenye uzio wa ukuta ambao hujamalizika kujengwa(pagale).

Mnamo tarehe 02.06.2020 watuhumiwa Wote watatu walihojiwa kwa kina na kukiri kuwa walifanya mauaji hayo na kuchukua gari la marehemu lenye T 139 DST Toyota IST na kwenda kulificha huko Kimara Baruti katika nyumba ya wageni ya Api Forest logde.

Jeshi la Polisi kanda Maalum DSM linakamilisha taratibu za kupeleka jalada kwa mwasheria wa serikali na watuhumiwa watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Imetolewa na Kamanda wa Polisi,
Kanda Maalum ya Dar es Salaam,
SACP-Lazaro Mambosasa,
03/06/2020


Share:

JNHPP MW 2115, uchimbaji kina cha lango la kuingilia maji kwenye mitambo wakamilika.

Ujenzi wa eneo la lango (Water Intake) la kuingilia maji kwenda kwenye mitambo ya kufua umeme katika Mradi wa Julius Nyerere (Mw 2115) unatarajiwa kukamilika Februari 2022.

Mhandisi Dismas Mbote, Mhandisi wa ujenzi njia za maji pamoja na Bwawa kwenye Mradi wa Julius Nyerere amesema utekelezaji wa njia hiyo ulianza Mwezi Oktoba 2019.

Aliongeza kuwa kazi ya uchimbaji wa lango imekamilika kwa kuchimbwa kina cha mita 53 ambapo hivi sasa kazi inayoendelea ni uondoaji wa kifusi na uchimbaji wa mahandaki matatu yatakayotumika kupitisha maji.

“Vifusi ambavyo vinachimbwa katika mradi huu wa Julius Nyerere havitupwi, mawe yanasagwa na kuwa mchanga, kokoto na mawe mbalimbali ambayo hutumika kwenye ujenzi”, alisema Mhandisi Mbote.

Aidha, zitafanyika kazi za kuchoronga miamba pamoja na kuimarisha kuta kwa zege.

Maji yatakayo fua umeme kabla ya kwenda kwenye mitambo ya kufua umeme yataingia kwanza kwenye lango.

Pia kwa hivi sasa imeletwa mashine ya kuchoronga miamba ambayo ni ya kwanza kwa Tanzania na inayotarajiwa kuongeza kasi katika uchimbaji wa mahandaki ya kupeleka maji kwenye mitambo.

Handaki la kwanza litakuwa na urefu wa mita 350, la pili mita 410 na la tano mita 570 hadi kwenye mitambo ya kufua umeme.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis June 4



















Share:

Wednesday, 3 June 2020

DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)

DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST  Employer: Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) POST DETAILS POST DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST POST CATEGORY(S) PHYSICAL & NATURAL SCIENCES STATISTICS AND MATHEMATICS EMPLOYER Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) APPLICATION TIMELINE: 2020-05-20 2020-06-04 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Advise the Director… Read More »

The post DOCUMENTATION AND PUBLICATION MANAGER- RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)

DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST Employer: Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH)   POST DETAILS POST DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST POST CATEGORY(S) PHYSICAL & NATURAL SCIENCES STATISTICS AND MATHEMATICS EMPLOYER Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) APPLICATION TIMELINE: 2020-05-20 2020-06-04 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i.   … Read More »

The post DIRECTOR OF KNOWLEDGE MANAGEMENT – RE-ADVERTISED – 1 POST at Tanzania Commission for Science and Technology (COSTECH) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TAKUKURU YAWASHIKILIA KWA RSUHWA VIGOGO WANNE WA BARAZA LA TAIFA NA UHIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA - NEMC





Share:

Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Kesi ya Spika Ndugai na Cecil Mwambe

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na wakili Paul Kaunda dhidi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai akiomba mahakama hiyo kutengua amri ya Spika kumtambua Cecil Mwambe kama mbunge halali wa Ndada ikisema amekosea kufungua shauri hilo.

Mbali na Ndugai, walalamikiwa wengine ni Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika kesi hiyo Wakili Kaunda anaiomba Mahakama Kuu kutengua amri ya Spika Ndugai ya kumtambua  Mwambe kama Mbunge halali wa Ndanda.

Katika uamuzi mdogo uliosomwa leo Juni 3, 2020 na Jaji Issa Maige aliyekuwa akisaidiana na Jaji Stephen Magoiga na Jaji Seif Kulita amesema mlalamikaji alikosea namna ya kufungua kesi ya kikatiba badala yake alipaswa kufungua kesi kwa utaratibu wa kawaida.

Amesema,  kauli ya Spika Ndugai aliyoitoa haikuwa imevunja katiba bali ni ya kiutaratibu katika shughuli zake za kiutendaji hivyo mlalamikaji angekuwa sahihi kama angefungua kesi hiyo kwa utaratibu wa kawaida kwa kutumia Ibara ya 83 (1) badala ya ile ya 26 (2) aliyoitumia.

Jaji Maige amesema Ibara hiyo inaenda sambamba na kifungu cha 37 cha Sheria ya Uchaguzi ambacho kinaeleza kuhusu utaratibu wa kutangaza kiti cha Mbunge ambacho kiko wazi.

Wakili Kaunda alifungua  kesi mahakamani hapo dhidi ya  Ndugai, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  Cecil  Mwambe  na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Katika kesi hiyo Wakili Kaunda anadai Mwambe alitangaza kujivua uanachama wa Chadema na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) kauli ambayo iliungwa mkono na katibu mkuu wa CCM Dk  Bashiru Ally  aliyempokea rasmi  Mwambe mbele ya hadhira kwa kumkabidhi kadi ya CCM, na  Mwambe naye alimkabidhi Katibu Mkuu huyo  kadi yake ya Chadema.

Wakili Kaunda anadai  kitendo cha Spika kumtambua  Mwambe kama mbunge halali wakati  ameshajivua uanachama wa chama kilichomdhamini kama Mbunge wa  Ndanda (2015-2020), ni ukiukwaji wa ibara ya 71(1)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na hakuna mamlaka yoyote nchini, achilia mbali Spika, yenye uwezo wa ku mrudisha bungeni Mbunge ambaye kwa hiari yake mwenyewe ameamua kujivua uanachama wa chama cha siasa kilichomdhamini kupata ubunge.


Share:

Rais Magufuli Ampandisha Cheo Mkuu Wa JKT Meja Jenerali Charles Mbuge

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance Mabeyo, kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. John Pombe Magufuli akimvalisha cheo kipya, Meja Jenerali Charles Mbuge, baada ya kupandishwa cheo leo tarehe 3 Jun 2020 Makao Makuu ya JWTZ ya Muda yaliyopo Msalato Jijini Dodoma.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance akimpongeza Meja Jenerali Charles Mbuge muda mfupi baada ya kumvalisha cheo kipya cha Meja Jenerali, leo tarehe 3 Jun 2020 Makao Makuu ya JWTZ ya Muda yaliyopo Msalato Jijini Dodoma.


Share:

AGAPE YAWAKUMBUKA WATU WENYE ULEMAVU MAPAMBANO DHIDI YA CORONA SHINYANGA




Shirika la AGAPE ACP linalotetea haki za wanawake na watoto mkoani Shinyanga, limewataka wananchi mkoani humo kuwakinga watu wenye ulemavu  dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona , pale wanapokuwa wakihitaji msaada wa kuwashika mkono na kuwavusha kwenye vivuko vya barabara.

Hayo yamebainishwa leo Juni 3,2020, na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP John Myola, wakati akikabidhi kifaa cha kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka kwenye ofisi ya Chama Cha Watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA), pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Myola amesema watu wenye ulemavu hasa wasioona wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya virusi vya Corona,kwa  sababu mara nyingi huwa wanahitaji msaada wa watu kuwavusha barabara na ni lazima washikwe mikono, hivyo endapo mtu huyo hakunawa mikono ama kujipaka Vitakasa atakuwa katika hatari ya kuambukizwa.

“Natoa wito kwa wananchi mkoani Shinyanga na maeneo mengine hapa nchini, tuwalinde watu hawa wenye ulemavu hasa wasiiona, pale tunapokuwa tukiwapatia msaada mbalimbali ikiwamo kuwavusha barabarani, tuzingatie unawaji mikono ama kujipaka Sanitizer, ili kuwahakikishia usalama wao wasipate maambukizi ya virusi vya Corona,”amesema Myola.

“Sisi AGAPE tumeguswa na kundi hili maalum, na ndiyo maana tumeamua kuwapatia kifaa hiki cha kunawia mikono kwa sabuni na maji tiririka kwenye ofisi yao, pamoja na kuwapatia elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona ili waendelee kubaki salama,” ameongeza.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richard Mpongo, amepongeza Shirika hilo kwa kuwajali na kuwapatia kifaa hicho pamoja na elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona, jambo ambalo limewafanya kufarijika na wataendelea kujilinda.

Aidha amewataka wananchi mkoani humo kutowanyanyapaa watu hao wenye ulemavu hasa katika kipindi hiki cha Janga la maambukizi ya virusi vya Corona, bali pale wanapokuwa wakihitaji msaada wao wahakikishe wananawa mikono au kujipaka vitakasa mikono (Sanitizer) ndipo wawashike mikono ili wote wabaki kuwa salama.



TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Shirika la Agape mkoani Shinyanga , akitoa elimu ya kujikinga na Maambukizi ya virusi vya Corona kwa watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA).

Mkurugenzi wa Shirika la Agape ACP mkoani Shinyanga John Myola akitoa elimu wa watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) namna ya uvaaji wa barakoa na kuzivua ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Afisa mradi wa utu wa msichana kutoka Shirika la Agape Sophia Rwazo akitoa elimu ya kujikinga na virusi vya Corona kwa watu wenye ulemavu.

Mkurugenzi wa Shirika la Agape ACP mkoani Shinyanga John Myola, akitoa elimu namna ya kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Mwenyekiti wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richad Mpongo (kushoto), akinawa mikono kwa sabuni na maji tiririka mara baada ya kupewa mafunzo namna ya kutumia kifaa hicho ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Katibu wa Chama cha Watu Wenye Ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Uel Nyange, akinawa mikono kwa sabuni na maji tirika mara baada ya kupewa mafunzo namna ya kutumia kifaa hicho ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona.

Mwenyekiti wa Chama Cha Watu Wenye Ualbino mkoani Shinyanga Yunisi Zabron Manumbu, akinawa mikono kwa sabuni na maji tiririka.

Zoezi la unawaji mikono kwa sabuni na maji tiririka likiendelea .

Zoezi la unawaji mikono  kwa sabuni na maji tiririka likiendelea.

Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (Shivyawata) Richard Mpongo akiishukuru AGAPE kwa kuwapa elimu namna ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona , pamoja msaada wa kifaa cha kujikinga na Maambukizi ya virusi hivyo.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger