Thursday, 16 April 2020

Barack Obama amuunga mkono Biden kuwania katika uchaguzi wa urais Marekani

 Aliyekuwa rais wa Marekani Barack Obama, ametangaza kumuunga mkono aliyekuwa Makamu wake Joe Biden kupeperusha bendera ya chama cha Democratic kumenyana na rais Donald Trump wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Novemba.

Mpinzani mkuu wa Biden, Bernie Sanders alijondoa katika kinyanyanyiro cha kutafuta bendera ya chama hicho katika dakika za lala salama.

Jumanne wiki hii Makamu wa zamani wa rais wa Marekani Joe Biden, mgombea wa uchaguzi wa Novemba, alipokea rasmi uungwaji mkono kutoka kwa mpinzani wake mkuu katika chama cha Democratic, Bernie Sanders.

Hii ni hatua inampa nafasi ya moja kwa moja Joe Biden kuchuana dhidi ya rais Donald Trump anayemaliza muda wake katika uchaguzi wa Novemba mwaka huu.


Share:

VIBAKA WATUMIA FURSA YA CORONA KUIBA KOKI ZA NDOO STENDI YA MABASI


Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza na wapiga debe wa stendi ya mabasi na abiria wakati alipokwenda kuangalia utekelezaji wa maagizo ya wataalamu wa afya namna ya kuchukua hatua za kukabiliana na tahadhari za ugonjwa wa Corona.
 Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kushoto akiwa na Mganga Mkuu wa Jiji la Tanga (CMO) kulia wakiwa stendi za mabasi Jijini Tanga wakiangalia namna ya
utekelezaji wa maagizo ya wataalamu wa afya namna ya kuchukua hatua za kukabiliana na tahadhari za ugonjwa wa Corona.

MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia akiteta jambo na Afisa Mtendaji wa Kata ya Ngamiani Kati wakati wa ziara yake

VIBAKA wametumia fursa ya uwepo wa ugonjwa wa Corona kuiba Koki zilizowekwa kwenye ndoo za maji kwenye stendi ya mabasi madogo ya ngamiani Jijini Tanga na hivyo kusababisha kukosekana kwake na hivyo kuleta usumbufu mkubwa kwa watumiaji.

Hayo yalibainishwa na Msimamizi wa magari madogo maarufu Daladala kwenye stendi hiyo Ally Kibaya wakati wa ziara ya Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa wakati alipokwenda kuangalia utekelezaji wa maagizo ya wataalamu wa afya namna ya kuchukua hatua za kukabiliana na tahadhari za ugonjwa wa Corona.

Koki hizo na ndoo zilitolewa na chama cha wamiliki wa mabasi madogo (Taremia) na Chama cha Wamiliki wa Mabasi Makubwa (Taboa) kuona namna ya kuweza kupambana na ugonjwa wa Corona walipotoka hapo Taremea wakanunua ndooo za kutosha na kutafuta fundi wa kuweka koki na kufanya uzinduzi ambapo kila stendi waliweka ndoo sita kwa ajili ya kuwekwa kwenye maeneo ya stendi hiyo ya mabasi ili kuwawezesha wananchi kuweza kunawa na vitakasa mikono.

Alisema kwamba hali hiyo imewapa wakati mgumu kwani kuibiwa kwa koki hizo kumepelekea maji kushindwa kukaa kwenye ndoo na hivyo abiria kukosa eneo la kunawia mikono ili kuweza kujikinga na ugonjwa huo.

“Uibaji wa koki hizo umesababisha ndoo kushindwa kukaa na maji na hivyo kuwaweka kwenye wakati mgumu huku wakimuomba mkuu wa wilaya kulishughulikia tatizo hilo ambalo linaweza kuleta athari”Alisema Msimamizi huyo.

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alisema wizi huo ni hujuma dhidi ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona ambapo alionya tabia hiyo na kiwataka wanaohusika kutokurudia na vitendo vya namna hiyo.

Aliita mkutano wa mabasi na Alisema kwamba mtu anayekwamisha mapambano hayo dhidi ya Corona hatutawanyamazia watakaobainika wataendelea kuchukuliwa hatua kali kwani wanadhoofisha juhudi za kupambana na ugonjwa huo ambao kwa sasa unatikisha dunia.

Mkuu huyo wa wilaya alisema katika vita dhidi ya mapambano ya ugonjwa huo tusifanya hujuma hasa kwa vile vitu ambavyo vinatolewa na watu kwa ajili ya kukabiliana na janga hili ambapo alisema kitendo hicho hakina tofauti na laana

“Watu wamechangishana kutusaidia kwa lengo la kuweka usafi hasa kwenye maeneo ya stendi lakini unakuja kuhujumu koki hilo sio suala nzuri hivyo niwatake muacha mara moja tabia hiyo kwani tutakaowabaini watachukuliwa hatua”Alisema
Share:

Taarifa Ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza

Tarehe 14.04.2020 majira ya 06:30hrs huko eneo la gereza kuu butimba watuhumiwa Yusuph s/o Benard, miaka 34, mnyamwezi mahabusu no 3444/2016 na Seleman s/o Seif, miaka 28, muha, mahabusu no 1177/2017 wa kesi za mauaji walijaribu kutoroka kwenye gereza hilo ndipo askari magereza wakishirikiana na wananchi waliwakimbiza na kufanikiwa kuwakamata ambapo wananchi waliwashambulia kwa kipigo katika sehemu za miili yao nakupelekea hali zao kuwa mbaya, baadae walipelekwa hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-Toure kwa ajili ya Matibabu, lakini majira ya saa 18:30hrs walifariki dunia wakati wakiendelea na matibabu.

Aidha mtuhumiwa wa tatu katika utoro huo aitwaye George s/o Aloyce, mnyambo, miaka 34, mfungwa no 200/2019 aliyekuwa amefungwa kwa kosa la uhujumu uchumi miaka 15 lakini pia akiwa na kifungo kingine cha kutoroka chini ya ulinzi miezi 6, baada ya kukamatwa katika jaribio hilo la kutoroka tena kwenye gereza hilo la butimba alihojiwa na askari polisi na akawaeleza kuwa kama wangefanikiwa wangechukua tax eneo la mabatini – nyamagana na akiwa njiani kuwapeleka polisi kuwaonesha huyo dereva tax ambaye angewasafirisha kuwapeleka eneo la katoro mkoani geita walivyoshuka kutoka kwenye gari na kuanza kutembea huku akijidai anataka kuwaonesha muhusika ghafla alianza kukimbia ndipo askari polisi waliokuanae walimwamuru kusimama huku wakipiga risasi juu lakini hakutii amri ndipo walimrushia risasi zilizomjeruhi miguuni na kufanikiwa kumkamata na kumpeleka hospitali ya Seko – toure ambapo baadae naye alifariki dunia.

Wito wa jeshi la polisi ni wananchi kuendelea kutoa ushirikiano wa taarifa zinazohusu wahalifu ili wahusika wakamatwe.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi April 16





















Share:

Wednesday, 15 April 2020

Quality Assessor at Steel Masters Ltd

Quality Assessor  Steel Masters Ltd is seeking a young, talented and passionate individual for the position of Quality Assessor. Applicants must have a minimum of 3 years experience. Job Responsibility: Checking and assessing the quality of mild steel ferrous scrap. Analysis of molten metal elements using a high-tech Spectrometer Electronic Understanding the usage of Argon gas to achieve… Read More »

The post Quality Assessor at Steel Masters Ltd appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Workshop Foreman at Frankfurt zoological Society – Tanzania

Workshop Foreman Description Location: Matambwe, Nyerere National Park Reports to: Deputy Project Leader, Selous Conservation Project FZS Vision in Tanzania: FZS is committed to maintaining biodiversity and conserving wildlife and ecosystems in protected areas and outstanding wild places of the Serengeti, the Selous and the Mahale ecosystems in partnership with the Government of the United Republic of Tanzania… Read More »

The post Workshop Foreman at Frankfurt zoological Society – Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Picha : MWILI WA MWANAHARAKATI JOSEPHAT TORNER KUZIKWA KESHO IMALAMATE BUSEGA SIMIYU



Waombolezaji wakibeba Jeneza lililobeba mwili wa Josephat Torner
Josephat Torner enzi za uhai wake
Mazishi ya Mwili wa Mwahaharakati wa kutetea Haki za watu wenye ualbino Josephat Torner Nkwabi (42) yanatarajiwa kufanyika kesho Alhamis Aprili 16,2020 katika kijiji cha Mwamwenge kata ya Imalamate wilaya ya Busega mkoani Simiyu alikozaliwa.

Josephat Torner Nkwabi amefariki dunia Siku ya Sikukuu ya Pasaka Aprili 12,2020 majira ya saa mbili usiku baada ya kugongwa na Hiace 'Daladala' akivuka barabara jijini Mwanza .

Mwili wa marehemu Josephat ulikuwa unahifadhiwa katika Hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza ambapo leo Jumatano Aprili 15,2020 umesafarishwa kwenda wilayani Busega kwa ajili ya mazishi kesho Alhamis.

Alikuwa Mkurugenzi wa Idara ya Ushawishi na Utetezi wa Taasisi ya Kimataifa inayojihusisha na Utetezi wa haki za Watu wenye Ualbino iitwayo Foundation of Josephat Torner Europe Aid (FOJOTEA) awali ikijulikana Josephat Torner Foundation Europe lakini pia amewahi kuwa Afisa Mahusiano na Habari wa Chama cha watu wenye Ualbino nchini Tanzania (TAS).

Josephat Torner Nkwabi alizaliwa tarehe 15.04.1978 na kufariki dunia tarehe 12.04.2020 siku tatu kabla ya Kutimiza miaka 42 ya kuzaliwa kwake.

Mwili wa Marehemu Josephat Torner ukiwa katika Hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza leo Jumatano Aprili 15,2020

Mwili wa Marehemu Josephat Torner ukitolewa katika Hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza leo Jumatano Aprili 15,2020 kwa ajili ya kusafarishwa kwenda wilayani Busega kwa ajili ya mazishi kesho Alhamis.

Mwili wa Marehemu Josephat Torner ukitolewa katika Hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza leo Jumatano Aprili 15,2020 kwa ajili ya kusafarishwa kwenda wilayani Busega kwa ajili ya mazishi kesho Alhamis
Share:

Dar es Salaam yatenga vituo 25 vya kukusanya sampuli za vipimo vya Corona....Tazama Hapa

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  Paul Makonda ametanagza vituo 25 katika jiji la Dar vitakavyotumika kukusanya sampuli za vipimo vya ugonjwa wa Covid-19 kwa wagonjwa watakaohisiwa kuwa na maambukizi. 


Vituo hivyo ni pamoja na hospitali za rufaa za mikoa, vituo vya afya na hospitali binafsi.

Taarifa hiyo imesema kuwa manispaa ya Kinondoni itatumia vituo sita vikiwemo hospitali za Mwananyamala, Magomeni, Mikoroshini, IST, TMJ na Rabininsia.

Manispaa ya Ilala vituo vitakavyotumika ni Amana, Buguruni, Mnazi mmoja, Muhimbili, Hindu Mandal, Aga Khan na Regency.

Vituo vingine vilivyoteuliwa katika manispaa ya Temeke ni hospitali ya Temeke, Mbagala Rangi Tatu, Yombo na TOHS.

Vituo vitakavyotoa huduma hiyo katika manispaa ya Ubungo ni pamoja na Sinza, Kimara, Mloganzila na Bochi na manispaa ya Kigamboni vitatumika vituo vitatu vya  Vijibweni, Kigamboni na Agha Khan.

==>>Msikilize hapo chini


Share:

WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAONGEZEKA NA KUFIKA 225, MMOJA KAFARIKI LEO


Watu tisa zaidi wameambukizwa Virusi hatari vya Corona  Nchini Kenya  chini ya saa 24 zilizopita na hivyo kufanya idadi ya waliombukizwa virusi hivyo sasa kufika 225. 

Saba kati yao ni wakenya, wengine ni raia toka mataifa mengine

Waziri wa Afya nchini humo Mutahi Kagwe, leo Jumatano Aprili 15, amesema mtu mmoja pia amefariki kutokana na virusi vya ugonjwa huo  na kufanya idadi ya waliofariki kufika 10.

Amesema wagonjwa wengine  12   wamepona na hivyo kufanya idadi ya waliopona hadi sasa kufika 53


Share:

Simba wamshtaki Mwakalebela TFF Sakata la Clatous Chama




Share:

Mwandishi wa habari na mtunzi wa vitabu maarufu Ken Walibora Afariki Dunia

Mwandishi wa habari na mtunzi wa vitabu maarufu nchini Kenya, Profesa Ken Walibora amefariki dunia.

Prof Walibora aligongwa na gari katika barabara ya Landhies, jijini Nairobi Ijumaa na mwili wake umekuwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa ya Kenyatta (KNH).

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, Walibora hakuonekana tangu Ijumaa na familia yake ilikuwa ikimtafuta kwa siku kadhaa kabla ya kubaini kwamba alikuwa amegongwa na gari.

Walibora ni mmoja wa watunzi mashuhuri wa vitabu nchini Kenya akiwa ameandika takribani vitabu 40.

Baadhi ya vitabu vyake maarufu ni pamoja na Siku Njema ambacho kilitumika kama kitabu cha kiada katika elimu ya sekondari nchini Kenya, na kitabu cha Ndoto ya Amerika.

Kifo chake ni pigo kubwa kwa tasnia ya uandishi na kwa watetezi wa lugha ya Kiswahili. Ingawa anakumbukwa sana kama mwandishi wa vitabu, amekuwa pia mtangazaji, mwandishi na msomi wa lugha ya Kiswahili.

Rais Kenyatta ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu.

Amemsifu Prof Walibora kama mtangazaji na mwandishi vitabu aliyebobea na ambaye kazi zake za fasihi zitaendelea kuhamasisha vizazi na vizazi.


Share:

TCRA YAWATAKA WANANCHI 'KU - SCREEN SHOT' TAARIFA ZA HOVYO KUHUSU CORONA MITANDAONI....MAADMIN KUCHUKUA TAHADHARI



Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imewataka wananchi kupiga picha (Screen shot) ujumbe wowote katika mitandao ya kijamii unaopotosha kuhusu corona na kuwatumia.

Tangazo hilo linakuja siku chache baada ya tangazo la awali la kuwaonya wanaosambara taarifa au picha za masuala ya corona kwenye mitandao ya kijamii atachukuliwa hatua.

“Ukipokea au ukiona ujumbe unaochochea, kuzusha au kupotosha taarifa za corona katika group (kundi) lako au lolote lingine mtandaoni, piga picha ujumbe huo na namna ya aliyetuma na utume TCRA kupitia namba  0737 300 300 au Kwa barua pepe :  nocorona@tcra.go.tz” ,linasema tangazo hilo.

"Maadmin wa Magroup ya Mitandao ya Kijamii ambao mitandao yao itabainika kuwa inatuma taarifa za uongo,uchochezi au uzushi kuhusu Ugonjwa Corona watawajibika,"Chukua Tahadhari', Tutumie Mawasiliano Kujiletea Maendeleo ",linaeleza tangazo jingine la TCRA.

"Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inatambua mchango wa watoa huduma za mawasiliano dhidi ya janga hili la mpito la ugonjwa wa Corona (Covid - 19). Taifa linawategemea mtuvushe salama kupitia huduma zenu. Tutumie Mawasiliano Kujiletea Maendeleo", - TCRA


Share:

MWANDISHI MASHUHURI WA RIWAYA PROFESA KEN WALIBORA AFARIKI DUNIA….NI YULE ALIYESIFIKA KWA KITABU YA ‘SIKU NJEMA’


Riwaya ya Siku Njema ilitafsiriwa kwa Kiingereza na kuwa A Good Day
Ken Walibora (kushoto) atakumbukwa na wengi kwa mchango wake katika kuendeleza lugha ya Kiswahili
***
Mwandishi mashuhuri wa riwaya nchini Kenya, Profesa Ken Walibora amefariki dunia.

Prof Walibora aligongwa na gari katika barabara ya Landhies, jijini Nairobi Ijumaa na mwili wake umekuwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Taifa ya Kenyatta (KNH).

Alikuwa na miaka 55.

Kifo chake ni pigo kubwa kwa tasnia ya uandishi na kwa watetezi wa lugha ya Kiswahili.

Ingawa anakumbukwa sana kama mwandishi wa vitabu, amekuwa pia mtangazaji, mwandishi na msomi wa lugha ya Kiswahili.

Waliofanya kazi naye wanamwelezea kama mtu mnyenyekevu, mpenda watu na aliyekuwa na hamu sana ya kuwainua wengine na kuiendeleza lugha ya Kiswahili.

Rais Kenyatta ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehemu.

Amemsifu Prof Walibora kama mtangazaji na mwandishi vitabu aliyebobea na ambaye kazi zake za fasihi zitaendelea kuhamasisha vizazi na vizazi.

Siku Njema

Prof Walibora anafahamika sana kutokana na kitabu chake Siku Njema kilichochapishwa mwaka 1996. Ni kitabu ambacho Wakenya wengi walikisoma katika shule za upili kati ya 1997 na 2003. Kitabu hicho baadaye kilitafsiriwa kwa Kiingereza na kuwa A Good Day.

Kidagaa Kimemwozea pia ni kitabu kilichosomwa katika shule za upili.

Kwa jumla ameandika au kuchangia katika vitabu zaidi ya 40 kikiwemo Ndoto ya Almasi.

Prof Walibora alihariri au kuchangia katika vitabu vingi vya hadithi fupi na diwani za mashairi.

Aliandika pia vitabu vya watoto kama vile Ndoto ya Amerika kitabu ambacho kilishinda Tuzo ya Fasihi ya Jomo Kenyatta mwaka 2003.

Prof Walibora alisimulia kuhusu maisha yake ya utotoni kwenye tawasifu wake ya Nasikia Sauti ya Mama ambapo anaonesha maisha yake yalivyokumbwa na changamoto nyinyi zikiwamo maradhi,wivu na uadui kutoka kwa baadhi ya watu wa ukoo pamoja na umasikini miongoni mwa nyingine.

Katika tawasifu hiyo, anaeleza jinsi mamake alivyokuwa kichocheo kikubwa katika maisha yake ya utotoni. Anaeleza kuwa alikuwa ashiki na mchezaji wa kabumbu, mwanariadha na mchoraji.Tawasifu ya Naskia Sauti ya Mama pia ilishinda Tuzo ya Fasihi ya Jomo Kenyatta

Utotoni hadi kuwa msomi

Kennedy Walibora Waliaula alizaliwa mwaka 1964/65 katika eneo la Baraki, Bungoma magharibi mwa Kenya. Baadaye familia yake ilihamia eneo la Kitale na kisha Cherangany bado magharibi mwa Kenya. Baadaye alifupisha Kennedy na kuwa Ken.

Alifanya kazi kama mwalimu wa Kiswahili na Kiingereza katika shule ya upili kati ya 1985-86 kabla ya kuwa afisa wa kufuatilia watu waliofungwa vifungo vya nje katika wizara ya mambo ya ndani kati ya 1988 na 1996.

Alijitosa katika uanahabari baada ya hapo kwa kufanya kazi kama mtangazaji wa redio, mhariri na mtafsiri wa habari katika Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) hadi mwaka 1999 alipohamia shirika la habari la Nation Media Group na kuwa mtangazaji wa runinga na redio hadi 2004.

Wakati huo huo alikuwa akisomea shahada ya kwanza katika Fasihi na Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Nairobi ambapo alifuzu Mei 2004.

Kati ya 2005 na 2007 alikuwa mhariri msaidizi katika Chuo Kikuu cha Ohio nchini Marekani ambapo alisoma shahada mbili za uzamili kwa wakati mmoja.

Alitawazwa profesa msaidizi katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison nchini Marekani mwaka 2009.

Baadaye alirejea katika kampuni ya Nation Media Group na kuwa mkuu wa ubora wa Kiswahili hadi mwaka 2017.

Hata baada ya kuondoka kwenye shirika hilo, amekuwa akichangia makala kwenye gazeti la Taifa Leo kwa jina Kauli ya Walibora.
Mlezi wa vipawa

Douglas Mutua, mwandishi na mwalimu wa Kiswahili Marekani, aliyewahi kufanya kazi na Prof Walibora, anasema atamkumbuka kama "mlezi wa vipawa".

Kishairi, ingawa alikuwa mwanamapokeo, kwa maana ya mshairi anayezingatia kanuni zote za ushairi, aliwatambua na kuwapa moyo walioandika mashairi huru.

Ni msomi asiyekubali usomi umwingie akilini na kumpokonya utangamano kati yake na watu.

"Ni mtu aliyeyachukua mashairi yangu nikiwa sina jina akayachapisha kwenye Diwani ya Karne Mpya. Kisha akafuatisha na mengine kwenye Diwani ya Waja-leo," anasema.

"Pia alikuwa mcheshi, mwadilifu na mnyenyekevu, mara nyingi akipiga gumzo na watu wa tabaka la chini kabisa. Si ajabu upate alikwenda kumzuru rafiki mkuu kwenye sekta ya Jua-Kali karibu na barabara ya Landhies alipogongewa na matatu."

Kutokana na uandishi wake wa kupigiwa mfano, aliwasadikisha wachapishaji wa vitabu kwamba mtu kutoka bara angeandika Kiswahili cha kufundishwa darasani.Kitabu cha Siku Njema kilitumiwa kufundishia fasihi kwa miaka mingi shule za upili Kenya

Ni kupitia uandishi wake mpevu, hasa wa riwaya ya Siku Njema, ambapo alichochea vipawa vya waandishi wengi kutoka bara wakajasiria kuandika.

Bw Mutua anasema marehemu alithamini sana vitu vitatu: Kiswahili, utu na soka.
CHANZO - BBC
Share:

WILFRED LWAKATARE ATANGAZA KUTOGOMBEA TENA UBUNGE

Mbunge wa Bukoba Mjini kupitia CHADEMA Wilfred Lwakatare, jana Aprili 14, 2020, amesema kuwa kwa sasa atapumzika katika siasa ambazo amezitumikia kwa miaka mingi na kwamba hana deni na mtu yeyote hata wale ambao aliwahi kushindana nao walikwishamalizana.

Lwakatare anaungana na Mbunge wa Kuteuliwa, Alhaj Abdallah Bulembo na Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka (CCM) ambao wametangaza kutogombea tena ubunge.

Mbunge huyo anakuwa ameongoza jimbo hilo kwa miaka kumi.

Akichangia jana mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa mwaka 2020-2021, Lwakatare alilishukuru Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Bukoba Mjini kwa kufanya nao kazi vizuri.


Share:

DOWNLOAD - PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG ...TUWE TUNAKUTUMIA HABARI ZOTE BURE MOJA KWA MOJA KWENYE SIMU YAKO

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.


Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa
Share:

ANUSURIKA KUFA KWA KIPIGO AKITUHUMIWA KUIBA NDOO YA KUNAWA MIKONO KUJIKINGA CORONA SHINYANGA MJINI

Mmoja wa wananchi akimdhibiti "kibaka" asikimbie baada ya kudaiwa kuiba ndoo ya maji kwa ajili ya kunawa mikono ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa Corona. (Picha na Suleiman Abeid, Timesmajira, Shinyanga)

Na Suleiman Abeid, Shinyanga

KIJANA mmoja mjini Shinyanga ambaye hakufahamika jina wala makazi yake mara moja amenusurika kufa baada ya kushambuliwa kwa kipigo na wananchi wenye hasira akituhumiwa kuiba ndoo inayotumika kwa ajili ya watu kunawa mikono kujikinga na ugonjwa wa Corona.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo ambalo limetokea maeneo ya mjini kati leo saa 2.20 asubuhi, kijana huyo anadaiwa kuiba ndoo hiyo kwenye moja ya vibanda vya mama Lishe maeneo ya mtaa wa Ikelenge mjini Shinyanga.

Mashuhuda hao wamefafanua kuwa, wakati akielekea maeneo ya Soko Kuu la mjini Shinyanga kwa ajili ya kutafuta mteja wa kumuuzia ndoo hiyo, mmiliki wake alibaini kuibiwa ndoo hiyo na kuanza kumfuatilia huku akiomba msaada kwa baadhi ya wananchi waliokuwa maeneo ya viwanja vya ofisi za CCM ambao walimuona na ili kujihami, alianza kukimbia akiwa na ndoo aliyoiba na kuingia ndani ya eneo la Soko Kuu la mjini Shinyanga.

Akiwa katika harakati za kujinusuru na kipigo, aliamua kukimbilia ndani ya jumba la wauzaji wa nafaka mchanganyiko ambapo alidakwa na wafanyabiashara na kulazimika kuitupa chini ndoo hiyo huku akijitetea kwa bidii kwamba yeye siyo mwizi lakini watu wenye hasira walimuadhibu kwa kipigo lakini alipopata upenyo aliwatoroka na kukimbilia mtaani.

Baada ya kukimbia, watu wenye hasira walimkimbiza huku wakimshambulia kwa kutumia mawe na fimbo lakini baadaye walipomkamata, waliamua kumpeleka kituo cha Polisi ili kunusuru asiuawe na watu hao.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger