Sunday 13 August 2023

MBUNGE UMMY MWALIMU AFANYA ZIARA KATA YA DUGA JIJINI TANGA

...

 








*Atembelea Kituo Cha Afya Duga 
*Afungua Shina la Wakereketwa 
•Afungua Ofisi ya CCM  kata CCM ya duga .
     
Mbunge wa Tanga Mjini Mhe. Ummy Mwalimu leo tarehe 12/8/2023 amefanya ziara kata ya Duga. Katika ziara hii mbunge ametembelea kituo Cha Afya duga kukagua utoaji wa huduma ambapo amepongeza watumishi kwa kutokuwa na kifo hata kimoja cha mama mjamzito na watoto wachanga. Mhe Ummy amesema kuwa Rais Samia atatoa gari ya kubebea wagonjwa kwa ajili ya Kituo cha Afya Duga. 

Aidha Mh Ummy amemtaka Mganga Mkuu wa Jiji  kusimamia kwa karibu upatikanaji wa Dawa katika Kituo hicho. Mhe Ummy pia ameutaka Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga kufanya ukarabati wa paa la Kituo hicho ili kuepusha madhara kwa wananchi. 
  
Pia Mhe Mbunge  alifungua shina la vijana wa CCM lililopo mtaa wa Magomeni Kirare na  kutoa shilingi milioni 1 kuwaunga mkono vijana hawa na kuahidi kuwatengenezea  turubai moja (tent) .

Pia Mhe Ummy amefungua Ofisi ya CCM kata ya Duga na   kusema ataendelea kujitolea kwa ajili ya Chama. Awali Mhe mbunge amenunua meza 3 na viti 7 kwa ajili ya ofisi hiyo.

Mwisho mbunge Ummy alitembelea makazi ya wazee duga ambayo ni kawaida yake kila mara kuenda eneo hilo au kutuma wasaidizi  wake kuwaona wazee hao na kuwapatia vyakula.

Katika ziara hiyo, Mhe mbunge aliambatana na viongozi wa chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Tanga wakiongozwa na Mwenyekiti Meja  mstaafu Hamisi Bakari Mkoba, Mkuu wa wilaya ya Tanga, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhe Shillow na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Simon
 
Imetolewa na :
Ofisi ya Mbunge Jimbo la Tanga Mjini
12/8/2023
Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger