Wednesday, 18 August 2021

MWANDISHI WA AYO TV AFARIKI KWA AJALI YA GARI

...

 



Mwandishi wa Habari wa Ayo TV, Nellyson Grigery amefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea leo Agosti 18, 2021 katika eneo la Kibaha mkoani Pwani.

Taarifa ya Kifo cha mwandishi huyo imethibitishwa na mmiliki wa televisheni hiyo ya mtandaoni, Millard Ayo kupitia ukurasa wake wa Instagram.

“Leo imekua siku ngumu sana kwangu na AyoTV Team tumeondokewa na marafiki zetu wawili na mmoja ni mfanyakazi mwenzetu, mpigapicha wa AyoTV Kanda ya Ziwa, Nellyson Grigery,”ameandika Ayo.

“Mwingine ni rafiki yetu Mujitaba Yusuf waliekuwa wakisafiri pamoja kutoka Mwanza kuja Dar. Wamepata ajali Kibaha wakiwa watatu tunamshukuru Mungu mtu wa tatu ambaye ni Khamis Abdallah Mwandishi wa AyoTV Kanda ya Ziwa amejeruhiwa na sasa anaendelea vizuri,"ameongeza
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger