Friday 30 July 2021

TANZANIA U-23 MABINGWA CECAFA 2021

...


Timu ya Taifa ya Tanzania imtwaa Ubingwa wa Michuano ya Kombe la Chalenji ya Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) kwa vijana chini ya umri wa miaka 23 kwa mwaka 2021.

Tanzania ilikuwa ikipepetana na Burundi ambapo matokeo yalikuwa suluhu ya bilabial katika dakika 90 hivyo kwenda kwenye matuta ya penalty ndipo Tanzania ikabuka na ushindi wa penalti 6 kwa 5 za Burundi.

Mara ya mwisho Tanzania kuchukua kombe hilo ni mwaka 2010 huku Burundi ikiwa haijawahi kuchukua zaidi ya kuishia nafasi ya pili mwaka 2013.

Timu tisa zilishiriki michuano hiyo ambazo ni Tanzania, Burundi, Kenya, Uganda, Ethiopia, Eritrea, DR Congo, Sudan Kusini na Djibouti zilizogawanywa kwenye makundi matatu yenye timu tatu tatu kila moja.

Stori na Sifael Paul


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger