Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, ameibuka ndani ya Mkutano Mkuu wa ACT-Wazalendo.
Mkutano huo unafanyika leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020 katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
Lissu aliingia ukumbini wakati Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo akijiandaa kutoa hotuba kwa wajumbe wa mkutano huo.
Kabla hajaanza, Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema-Bara, akaingia ukumbini akiwa ameambatana na mgombea wake mwenza, Salum Mwalimu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu-Zanzibar.
Kabla hajakaa katika nafasi iliyokuwa imeandaliwa, Zitto alimwita Lissu na Bernard Membe, Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo wapande jukwaani hali iliyoibua shangwe zaidi.
Membe anatarajiwa kuteuliwa na mkutano huo kuwa mgombea urais
Kabla hajakaa katika nafasi iliyokuwa imeandaliwa, Zitto alimwita Lissu na Bernard Membe, Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo wapande jukwaani hali iliyoibua shangwe zaidi.
Membe anatarajiwa kuteuliwa na mkutano huo kuwa mgombea urais
0 comments:
Post a Comment