Sunday 2 October 2022

MJUMBE WA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM RAIS DKT. MWINYI ASHIRIKI UCHAGUZI WA CCM WA VIONGOZI WA NGAZI YA WILAYA

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini Kichama Ndg. Talib Ali Talib na Viongozi wengine alipowasili katika viwanja vya Afisi ya CCM Amani Mkoa wa Mjini, kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Uchaguzi CCM Ngazi ya Wilaya ya Amani uliofanyika katika ukumbi huo leo 2-10-2022.(Picha na Ikulu) MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi mbalimbali alipowasili katika viwanja vya Afisi ya CCM Amani Mkoa wa Mjini, kuhudhuria Mkutano Mkuu wa wa Uchaguzi wa CCM Ngazi ya Wilaya ya Amani, uliofanyika katika ukumbi huo leo 2-10-2022.(Picha na Ikulu) MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Husseinn Ali Mwinyi akipiga kura kumchagua Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani na Viongozi wa ngazi ya Wilaya wa CCM, uliofanyika katika ukumbi wa Afisi CCM Amani Mkoa wa Mjini Kichama.(Picha Ikulu) WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi Ngazi ya Wilaya ya Amani wakishangilia wakati Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, akihutubia na kuzungumza na Wajumbe baada ya kumaliza kupiga Kura kumchagua Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani na Wajumbe wengizi wa ngazi ya Wilaya, uliofanyika katika ukumbi wa CCM Amani Mkoa leo 2-10-2022.(Picha na Ikulu)

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini Kichama Ndg.Talib Ali Talib, wakiwa katika ukumbi wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi CCM Ngazi Wilaya ya Amani Kichama, uliofanyika katika ukumbi wa Afisi ya CCM Amani Mkoa wa Mjini leo 2-10-2022.(Picha na Ikulu)
Share:

TANESCO DODOMA YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA WATEJA KUHUSU UTARATIBU WA KUPATA HUDUMA ZA UMEME


Afisa Uhusiano Tanesco Mkoa Dodoma Sarah Libogoma ,akizungumza na wananchi wa Kata ya Nala Mtaa wa Seguchini Mkoani Dodoma wakati wa kampeni ya uelimishaji juu ya huduma za TANESCO zilizofika mitaa hiyo kupitia mradi wa umeme wa REA.


WANANCHI wa Mtaa wa Seguchini wakimsikiliza Afisa Uhusiano Tanesco Mkoa Dodoma Sarah Libogoma wakati akitoa kampeni ya uelimishaji juu ya huduma za TANESCO zilizofika mitaa hiyo kupitia mradi wa umeme wa REA Kata ya Nala Mtaa wa Seguchini Mkoani Dodoma wakati wa


Diwani Kata ya Nala Julius Chimombo akizungumza na Wananchi Mtaa wa Seguchini Kata ya Nala Baada ya Shirika la umeme Mkoa wa Dodoma kwenda kutoa elimu juu ya huduma za TANESCO zilizofika mitaa hiyo kupitia mradi wa umeme wa REA.

...........................................

Na Alex Sonna-DODOMA

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linaendelea na kampeni ya uelimishaji kata za Dodoma juu ya taratibu za upatikanaji huduma kwa Wateja maeneo yote ya Jiji na usalama wa umeme ikiwemo ulinzi shirikishi wa miundo mbinu ya umeme na umuhimu wake katika shughuli za uzalishaji mali na matumizi ya kawaida ya nyumbani.

Afisa Uhusiano Tanesco Mkoa Dodoma Sarah Libogoma akizungumza na wananchi wa Kata ya Nala Mtaa wa Seguchini Mkoani Dodoma katika kampeni ya uelimishaji juu ya huduma za TANESCO zilizofika mitaa hiyo miezi ya karibuni kupitia mradi wa umeme wa REA.

Amesema wiki hii wamekuwa katika mitaa yote ya Kata ya Nala na kukamilisha kampeni hiyo ya elimu katika mtaa wa Seguchini huku lengo likiwa ni Wananchi kutambua taratibu za huduma, tahadhari juu ya vishoka na Uhujumu miundombinu.

"Ni vyema kila Mtu aelewe na kutambua taratibu zetu za huduma ikiwemo maombi ya umeme na utoaji taarifa, pia kuwapa angalizo na tahadhari juu ya vishoka na wale wanao hujumu miundombinu, jambo ambalo linajitokeza sana kwenye kata yetu hii", amesema

"Tumeona tuendelee kuwakumbusha Wananchi kuwa wanawajibu wa kulinda miundo mbinu na ulinzi ni wa kwetu wote sio wa viongozi tu au wa TANESCO peke yao kwasababu bila hivyo wanaoathirika zaidi ni Wateja na Wananchi kwa ujumla watumiaji umeme eneo husika". Amesema Libogoma

Hata hivyo Afisa usalama Tanesco Mkoa wa Dodoma Ndugu Madega dudu amesema wamekuwa katika kipindi kigumu na Watu wanaohujumu miundo mbinu ya Umeme.

"Uharibifu mkubwa unaofanywa wanaenda kwenye maeneo yanayofungwa mashine umba (Transformer ) na kukata nyaya za mfumo wa kulinda mashine hizo na kusababisha kukosekana huduma ya umeme maeneo mengi vitendo hivi vinaongezeka na hivyo pamoja na kukamata inabidi kuendelea kutoa elimu hii ya tahadhari kwani hili ni la Uhujumu", amesema Dudu

Katika mikutano hiyo ameongezea kwa kutoa rai kwa Wananchi waliofikiwa na wale ambao bado kwa pamoja wawe walinzi katika maeneo yao kwa kutoa taarifa kwa uongozi mtaa husika, polisi kata au kwa shirika la umeme Mkoa wa Dodoma pale wanaposhuhudia vitendo hivyo vya uharibifu wa miundombinu ya umeme inapotokea ikiwemo uchomaji nguzo na hivyo kuepuka athari kubwa kutokea katika mitaa yao kutokana uhujumu huo.

Mtendaji wa Mtaa wa Seguchini Stanley Obedi Msaga amesema wamefurahia kupokea elimu hiyo kutoka kwa Shirika la Umeme Mkoa wa Dodoma na Wananchi sasa wanaendelea na taratibu za uombaji pamoja na Ofisi kuwasilisha taarifa na majina ya wahitaji walio mbali na miundombinu kuweza kufikiwa pia.

"Kimsingi Tumewaelewa vizuri TANESCO na tunawashukuru kwa kuturahisishia upatikanaji huduma kupitia Mfumo wao wa Nikonekt ambao umeshatatua changamoto nyingi zilizokuwepo awali hivyo nasi tutaendeleza kutoa ushirikiano kwao ili kuweza kutokomeza hujuma zinazoweza kujitokeza kwenye miundombinu ya maeneo yetu kwani umeme huu serikali imelenga uwe ni wa maendeleo zaidi kwenye mitaa yetu", amesema Msaga.

Mkutano huo ulihusisha mitaa ya Segu Juu, Bwawani na wenyeji wa kikao mtaa wa Seguchini ambapo pia ulihudhuriwa na Mstahiki Meya Prof. Davis G Mwamfupa pamoja na Diwani wa kata hiyo ambapo uhamasishaji uchangiaji jitihada za maendeleo ya Kata ulifanyika pia.
Share:

WAZIRI DKT MABULA AWATAKA WAKURUGENZI HALMASHAURI KWENDA NA KASI YA RAIS SAMIA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza wakati wa kuhitimisha Kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Dkt Allan Kijazi na kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe.

Sehemu ya washiriki wa kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022.

******************************

Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo yaMakazi Dkt Angeline Mabula amezitaka halmashauri nchini kwenda na kasi ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga ardhi kwa ajili ya uwekezaji.

Dkt Mabula alitoa kauli hiyo oktoba 1, 2022 wakati akihitimisha kikao kazi baina ya wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wa sekta ya ardhi kikichofanyika jijini Dodoma.

Huku akimshukuru Mhe Rais Samia kwa kuipa kipaumbele sekta ya ardhi, Dkt Mabula aliwaeleza washiriki wa kikao kazi kuwa, kinachohitajika kwa sasa ni kwenda na kasi ya mhe Rais hasa kwa kuzitaka halmashauri kujiandaa katika zoezi zima la uwekezaji.

"Hata kama mmetenga maeneo je meyatwaa na ni ya kwenu au mkipata muwekezaji ndiyo mnaanza kuhangaika, hapa kinachohitajika ni kwenda na kasi ya mhe rais na wakurugenzi ndiyo ninyi na maafisa ardhi ndiyo ninyi". Alisema Dkt Mabula

Aliongeza kwa kusema kuwa, ardhi zilizotengwa kwa ajili ya uwekezaji katika halmashauri, wakurugenzi wake wahakikishe wanazitwaa na kuwa mali ya serikali ili iwe rahisi kumpatia Muwekezaji pale anapotokea.

Aidha, Waziri wa Ardhi alizungunzia suala la halmashauri kushililia ardhi kwa muda mrefu bila kulipa fidia kwa wamiliki wake ambapo alisema pale halmashauri inaposhindwa kulipa fidia eneo ililotwaa basi eneo hilo lirudishwe kwa mhusika na pale litakapohitajika ufanyike tena uthamini.

" Kuna ardhi mmezihold kwa miaka nenda rudi fidia hailipwi lakini mgogoro unakuja ardhi sasa tuseme ukishindwa kulipa fidia maana hiyo ardhi umrudishie mwenyewe ukitaka tena utafanya uthamini" alisema Dkt Mabula

Aliwaambia washiriki wa mkutano huo kuwa, serikali haitaki uonevu kwa wananchi kwa kuwa siyo maelekezo ya rais na kusisitiza kuwa serikali inathamini wawekezaji hata wa ndani na pale wanapokuja wawekezaji wa nje wale wa ndani wasionekani siyo lolote.

Kikao kazi kati ya wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wa sekta ya ardhi mbali na mambo mengine kilijadili changamoto na kutoa maoni na ushauri kuhusu namna bora ya kusimamia watumishi wa sekta ya ardhi nchini kwa lengo la kuwa na ufanisi na kwa maskahi mapana ya nchi.
Share:

SERIKALI YAONYA UBADILISHAJI MATUMIZI YA ARDHI BILA SABABU ZA MSINGI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika Kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Sehemu ya washiriki wa kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi akizungumza katika kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (wa tatu waliokaa mbele ) na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa halmashauri walioshiriki Kikao kazi kati ya wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022.

****************************

Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline Mabula amezionya halmashauri nchini kuacha utaratibu wa kubadilisha matumizi ya ardhi bila sababu za msingi.

Dkt Mabula alitoa onyo hilo Oktoba 1, 2022 jijini Dodoma wakati wa kuhitimisha kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na wataalamu wa sekta ya ardhi kilichofanyika jijini Dodoma.

" Sasa hivi kila mmoja anaondoa open space anataka kupima viwanja anafuta mashamba anataka kupima viwanja hata kama bado yako katika sura ya kijijini ya kimashamba na anataka kila sehemu kuwe fremu"

Akitolea mfano wa jiji la Dodoma, Dkt Mabula alisema, jiji hilo limeanza kusheni fremu wakati ni Makao makuu ya nchi na kusema haiwezekani kuwa na miji ya aina hiyo ambayo haipangwi kwenye sura ya makao makuu kwa kujaza fremu na vituo vya mafuta na kusisitiza kuwa hiyo si sahihi kitaaluma.

Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi, wapo wataalamu wengi katika sekta ya mipango miji na mabadiliko ya matumizi yasiyo na sababu za msingi hayakubaliki kwa kuwa yanawakosesa hata watoto maeneo ya kucheza sambamba na miji kupumua.

"Mipango iliyopangwa awali inatakiwa kubaki siyo kuendekeza mabadiliko ya matumizi kwa kujaza fremu au vituo vya mafuta na kuharibu miji, tunahitaji pia maeneo ya matumizi ya umma". Alisema Dkt Mabula

Kupitia kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Tumushi wa Umma na Utawala Bora Laurean Ndumbaro, Dkt Mabula aliwataka Wakurugenzi ambao halmashauri zao tayari zina mipango kabambe kutoruhusu ujenzi kuendelea kwenye maeneo yao bila kuzingatia mipango hiyo na kusisitiza umuhimu wa maeneo kutunzwa kwa kuzingatia mipango kabambe badala ya kufuata mkumbo wa kutaka kubadili matumizi ya ardhi na kuharibu sura ya miji.

Kikao Kazi kati ya wakurugenzi wa halmashauri na wataalamu wa sekta ya ardhi kimefanyika kwa lengo la kupata maoni juu ya muundo mpya wa utendaji kazi wa wataalam wa ardhi katika ngazi ya Halmashauri.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 2,2022








Share:

Saturday 1 October 2022

KARIBU BUILDING SOLUTION DESIGNING KWA HUDUMA ZA UCHORAJI RAMANI ZA NYUMBA

 


Share:

SAUTI PROGRAMU KUZALISHA MIFUGO BORA KWA MAHITAJI YA SOKO LA NDANI NA NJE YA NCHI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kushoto) akizungumza na vijana waliochaguliwa kujiunga kwenye vituo atamizi (hawapo pichani) wakati alipotembelea Chuo cha Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Mabuki mkoani Mwanza ambapo amewaeleza vijana hao malengo na matarajio ya serikali ya kuanzisha vituo hivyo, hasa kwa kuhakikisha wanapata ujuzi na uzoefu wa kuweza kufuga mifugo kisasa na kibiashara.


Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene (wa pili kulia) akitoa taarifa ya uendeshaji wa vituo atamizi katika Chuo cha Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Mabuki na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) - Mabuki mkoani Mwanza kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa tatu kutoka kulia) ambapo amesema tayari baadhi ya vijana wameshafika na wanaendelea na maandalizi.


Mkurugenzi wa Utafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Daniel Komwihangilo (wa pili kutoka kushoto) akiwasihi vijana waliochaguliwa kujiunga na vituo atamizi kuhakikisha wanafanya kazi za ufugaji kwa vitendo kwa bidii ili malengo yaliyokusudiwa na serikali dhidi yao yaweze kutimia.


Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya ufugaji mifugo kisasa na kibiashara wakimsikiliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (hayupo pichani) wakati alipotembelea Chuo cha Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Mabuki mkoani Mwanza kukagua kazi zinazoendelea kwa ajili ya uanzishaji vituo atamizi.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene (kulia waliokaa), Mkurugenzi wa Utafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Daniel Komwihangilo (kushoto waliokaa) pamoja na watumishi wa LITA na TALIRI Mabuki na vijana waliochaguliwa kujiunga kwenye vituo atamizi mara baada ya Waziri Ndaki kumaliza kuzungumza na vijana hao kwenye Kampasi ya Mabuki mkoani Mwanza.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (wa nne kutoka kulia) akizungumza na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene (wa pili kutoka kushoto) wakati alipofika kwenye Chuo cha Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Mabuki Mkoani Mwanza kukagua kazi zinazoendelea kufanyika kwenye eneo litakalotumika kwa ajili ya vituo atamizi ambapo amewataka viongozi wa LITA kuhakikisha kazi hizo zinakamilika kwa wakati.

.....................................

Programu ya Samia Ufugaji kwa Tija inakwenda kumaliza changamoto ya upatikanaji wa mifugo bora inayohitajika kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki wakati anazungumza na vijana waliochaguliwa kujiunga na vituo atamizi kwa ajili ya kupata mafunzo ya ufugaji kwa vitengo katika Chuo cha Mafunzo ya Mifugo Kampasi ya Mabuki mkoani Mwanza ili waweze kufuga kisasa na kibiashara.

Waziri Ndaki amesema kuwa prograu hii kwanza imelenga kuwabadilisha vijana kifikra kwa kuwapatia mbinu mbalimbali za ufugaji wa kisasa na kibiashara ikiwa ni pamoja na kuwaonyesha fursa zilizopo kupitia Sekta ya Mifugo na namna ya kuzitumia kwa tija.

Programu hii imeanzishwa kwa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa wakati wa kuhitimisha sherehe za Wakulima – Nanenane zilizohitimishwa mkoani Mbeya ambapo aliagiza Sekta ya Mifugo kuanzisha vituo kwa ajili ya kuwajengea uwezo vijana ili waweze kujiajiri kupitia ufugaji.

Waziri Ndaki amesema kuwa lengo la SAUTI Programu ni kuwawezesha vijana kuanzisha na kuendesha miradi ya ufugaji wa mifugo kibiashara, kuwapatia vijana stadi rahisi kwa vitendo za namna bora ya kuanzisha na kuwekeza katika miradi ya ufugaji wa mifugo, kuwawezesha vijana kupata ujuzi, uzoefu na ujasiri wa kuanzisha miradi ya ufugaji kibiashara, pia kuwaunganisha vijana kwenye mnyororo wa thamani wa uzalishaji wa mazao ya mifugo kibiashara.

Kutokana na malengo hayo, SAUTI Programu inakwenda kuongeza ajira kwa vijana kupitia Sekta ya Mifugo na hivyo kuifanya Sekta hiyo kuongeza kipato kwa wafugaji wenyewe lakini pia mchango wa Sekta kwenye pato la Taifa.

Hivyo amewataka vijana hao kutumia fursa hiyo vizuri kwa kuwa Wizara imeshawaandalia maeneo ambayo watapatiwa mara baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo ili waweze kuanza kufuga kutokana na elimu watakayokuwa wameipata. Pia amewataka vijana ambao wamechaguliwa lakini hawajafika kufika, kwani wasipofanya hivyo watachukuliwa vijana wa akiba kuja kuziba nafasi zilizo wazi.

Aidha, Waziri Ndaki ameendelea kuwasihi viongozi wa mikoa na wilaya kuendelea kusimamia zoezi la uwekaji alama za utambuzi kwenye mifugo katika maeneo yao kwani serikali imeongeza mwezi mmoja ambapo baada ya Oktoba 30, 2022 hatua za kisheria zitaanza kuchukuliwa kwa wafugaji ambao mifugo yao haina alama za utambuzi.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene amesema kuwa tayari umeshaandaliwa mwongozo utakaotumika kufuga kisasa ambao utawasaidia vijana kama rejea yao hasa pale kutakapokuwa na kitu kinachotaka kuwakwamisha.

Dkt. Mwambene amasema kuwa vijana hao wataanza kujifunza kwa vitendo kuanzia kwenye ujenzi wa mabanda, manunuzi ya chakula na ng’ombe na katika kufanya biashara ili shughuli zote wazielewe.

Mkurugenzi wa Utafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Dkt. Daniel Komwihangilo akiwasihi vijana waliochaguliwa kujiunga na vituo atamizi kuhakikisha wanafanya kazi za ufugaji kwa vitendo kwa bidii ili malengo yaliyokusudiwa na serikali dhidi yao yaweze kutimia.

Akizungumza kwa niaba ya vijana hao, Adelina Bilembo amesema ameishukuru serikali kwa kuanzisha vituo hivyo vyenye lengo la kuwajengea kuwe wa ufugaji kwa vitendo na kuona vijana katika sekta ya mifugo wanahitaji kuwezeshwa. Naye Baraka Ezekiel ameahidi kuwa wataweka juhudi kubwa katika kujifunza ili malengo yaliyowekwa na serikali ya kuwajengea uwezo vijana kupitia ufugaji ifanikiwe na matunda yake yaonekane.
Share:

TAMISEMI NA WATAALAMU SEKTA YA ARDHI WATAKIWA KUJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA ARDHI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika Kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Dkt Allan Kijazi na kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe. Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi akizungumza katika kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Wa pili kushoto ni Waziri wa Ardhi Dkt Angeline Mabula. Wa pili kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe na kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Laurean Ndumbaro. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais –TAMISEMI Prof Riziki Shemdoe akizungumza katika kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Kushoto ni Waziri wa Ardhi Dkt Angeline Mabula na kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Laurean Ndumbaro. Sehemu ya washiriki wa kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. Baadhi ya Wakurugenzi wa Halamashauri wakiwa katika Kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika Kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 1, 2022. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

********************

Na Anthony Ishengoma na Munir Shemweta, WANMM DODOMA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula amewataka wakurugenzi wa Halmashauri nchini kujipanga na kufanya kazi kwa pamoja na wataalamu wa ardhi ili kuondoa changamoto zinazojitokeza katika utendaji kazi na usimamizi wa sekta ya ardhi katika Halmashauri.

Dkt. Mabula alisema hayo leo Oktoba 1, 2022 wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kilichowaunganisha wakurugenzi wa Halmashauri na watalaam wa Sekta ya Ardhi nchini kilichofanyika jijini Dodoma. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kupata maoni juu ya muundo mpya wa utendaji kazi wa wataalam wa ardhi katika ngazi ya Halmashauri.

Dkt.Mabula alisema, zimeanza kujitokeza changamoto katika utendaji kazi kati ya watendaji wa sekta ya ardhi na wakurugenzi wa Halmashauri hasa katika eneo la usimamizi wa sekta hiyo baada ya kuanza utekelezaji wa rejesho la Waraka wa Utumishi Na 1 wa Mwaka 1998 kuhusu usimamizi wa watumishi wa sekta ya ardhi na maji kutokana na sababu mbalimbali.

Rejesho hilo pamoja na mambo mengine liliwahamisha wataalamu wa sekta ya ardhi kutoka kwenye usimamizi wa Mamlaka za serikali za mitaa Kiajira na kinidhamu na kuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Ardhi.

‘’Watumishi hawa kiajira na kinidhamu wako Wizara ya ardhi mamlaka za upangaji ardhi ziko Halmashauri lakini baadhi ya wakurugenzi wamekuwa wakijiweka mbali na wataalam ardhi na kushindwa kufuatilia utekelezaji wa sekta ya ardhi au kukosa ufahamu katika sekta ya ardhi.’’ Alisisitiza Dkt. Mabula

Kwa mujibu wa Dkt Mabula changamoto hiyo imeleta mkanganyiko kwa kuwa baadhi ya watendaji hasa wakurugenzi hawaoni kama wanawajibu wa kusimamia sekta ya ardhi wakati wao ni mamlaka za upangaji ardhi.

‘’Baadhi ya wakurugenzi hawajui taratibu za ardhi na kutojihusisha zaidi na uelewa wa masuala ya ardhi kwani unakuta Mkurugenzi wa Halmashauri ukimtaka hakupe taarifa anakimbilia kupata ufafanuzi kutoka kwa mtaalamu wa ardhi’’Aliongeza Dkt. Angeline Mabula.

Changamoto nyingine iliyoainishwa Dkt Mabula ni kitendo cha baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri kushindwa kurejesha fedha za mkopo ya program ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha ardhi na kutumia fedha hizo kwenye mipango mengine badala ya kurejesha fedha hizo ili ziweze kutumika katika maeneo mengine.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Allan Kijazi alieleza kupitia kikao hicho kuwa ipo haja ya kuboresha mawasiliano kati ya watendaji wa sekta ya radhi na mamlaka za serikali za mitaa ili kuweka mkakati mzuri wa utendaji kazi kwani wote ni watumishi wa Serikali.

Dr. Kijazi aliongeza kuwa, kumekuwa na changamoto ya kiutendaji kati ya serikali za mitaa na uongozi wa kisiasa ikiwemo madiwani na kusisitiza kuwa, la msingi ni kufanya kazi kwa pamoja kwa kuwa wote ni watendaji wa serikali.

‘’Lengo la kikao chetu ni namna ya kuboresha mawasiliano ili tuweze kujiweka sawa kuboresha utendaji kazi kwani kumekuwepo lugha zinazoleta sintofahamu kuwa baadhi ya wakurugenzi wa halmashauri wamekuwa wakitoa kauli kuwa watendaji wa sekta ya ardhi wako chini ya katibu Mkuu na wao hawahusiki’’. Alisema Dkt Kijazi

Madhumuni ya kikao kazi ni kujadili changamoto, kuibua changamoto zingine zinazojitokeza na kutoa maoni na ushauri kuhusu namna bora ya kusimamia watumishi wa sekta ya ardhi nchini kuwa na ufanisi na kwa maskahi mapana ya nchi.
Share:

SAMAF NA ITEL ZAUNGANA KURUDISHA TABASAMU KWA KITUO CHA WATOTO WENYE ULEMAVU CHA AMANI NA MIHAYO




Na Mwandishi wetu,Morogoro 

UMOJA wa waandishi wa habari wanawake Dar es Salaam chini ya asasi ya sauti ya matumaini Foundation SAMAF kwa kushirikiana na Kampuni ya Simu ya Itel  wametembelea Kituo cha kulelea watoto yatima wenye ulemavu na wanaoishi katika mazingira magumu cha Amani na Mihayo vilivyopo  kata ya Chamwino Mkoani  Morogoro na kutoa misaada mbalimbali ikiwemo taulo za kike pamoja na chakula kwa lengo la kurudisha  tabasamu kwa watoto hao.


Akizungumza wakati wa kutoa msaada huo,Mwanzilishi wa Umoja wa umoja huo,Penina Malundo alisema taasisi yao inaendelea kuhakikisha inarudisha tabasamu kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wale wenye ulemavu kwa kuwasaidia vitu mbalimbali ikiwemo kuwapa elimu ya Afya,Kujitambua pamoja na masuala ya ukatili wa kijinsia ili kuweza kuwasaidia katika makuzi yao.


Alisema mbali na elimu hiyo pia wamekuwa wakitoa taulo za kike kwa mabinti hao za kipindi cha miezi sita  ili ziweze kuwasaidia mabinti hao kuweza kupata hedhi salama ambayo itawafanya kutokuwa wanyonge kwa kuendelea na shughuli zao kama masomo.


"Hii sasa ni awamu ya tatu kwa mwezi huu wa tisa kutoa elimu ya afya ya uzazi,kujitambua na ukatili wa kijinsia tumeweza kufikia shule tatu ikiwemo shule ya msingi Buguruni Viziwi,Maweni,Kigamboni,Vijibweni na Kituo cha Amani na Mihayo mkoani Morogoro jumla ya mabinti 200 tumeweza kuwafikia na kampeni yetu ya ithamini na ilinde kesho yangu,"alisema na kuongeza


"Mkoani Morogoro tumeweza kushirikiana na Kampuni ya Simu ya Itel katika kufanikisha shughuli hii na wadau wengine  ikiwemo Shree Jalalam  katika kuwasaidia mahitaji mbalimbali na kuwarudisha katika furaha makundi hayo,"alisema.


Akitaja vitu walivyowakabidhi watoto hao ni pamoja na Mchele,Unga ,Mafuta ya Kula,Maharage,Taulo za Kike Sabuni ya Unga,Maji,Juice na Biscuits ambazo zimetolewa na wadau hao ikiwa na lengo la kuisaidia Samaf kufikia watoto waliokatika mazingira magumu.


Alisema Jamii inatakiwa kuendelea kuwatunza watoto hao na kuwaona nao wanahaki kama wengine ili kuweza kurudisha tabasamu kwao.


Kwa Upande wake Meneja uhusiano wa Kampuni ya Itel,Fernando Mfuole alisema kampuni yao ya Itel inaendesha kampeni ya kurudisha fadhira kwa jamii  katika kila kila faida wanayopata katika Shule mbalimbali au katika vituo vya watoto vya kulelea yatima,wanaoishi mazingira magumu au venye watoto wenye ulemavu.


"Tunafanya hivi katika mikoa yote  mahali popote nchini, tunarudisha fadhila kwa jamii hii ni kuhakikisha tunawasaidia watoto waliopo katika makundi haya leo tumeweza kutoa mahitaji mbalimbali yanayohitajika  ili kuweza kurudisha furaha za watoto hawa wa kituo cha Amani na Mihayo mkoani Morogoro,"alisema 


Alisema Itel imeweza kuguswa na kuhakikisha inawafikia katika kuwapatia kile kitu walichobarikiwa katika faida wanayoipata kwenye bidhaa zake.


Naye Msimamizi wa kituo Amani  ,Padri Beatus Msewando aliishukuru Kampuni ya Itel na Samaf kwa msaada huo na kuiomba jamii kujitokeza kusaidia kituo hicho kwani wanakabiliwa na Changamoto mbalimbali kutokana na wingi wa watoto wanaowapokea.


"Katika huduma zetu hizi tunaona wengine wanaletwa hawana ndugu wala pakukaa,kwahiyo tunawasaidia kuishi nao huku tukiwafundisha mambo mbalimbali kama kazi za mikono,ikiwemo kilimo na Uvuvi ili kuwapa nyenzo za kuja kujitegemea,"alisema.
Share:

MGODI WA BUCKREEF WASHIRIKI MAONESHO YA MADINI GEITA -2022


Afisa Usalama wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu Buckreef Charles Kafuku (wa kwanza kushoto) akitoa maelezo kwa mgeni aliyetembelea Banda la Kampuni hiyo Bw. Roy Mwinga (wa pili kulia) aliyemuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara wa Zambia katika Maonesho ya Madini yanayofanyika Mkoani Geita.
(PICHA ZOTE NA: HUGHES DUGILO) GEITA
Mwakilishi wa Waziri wa Viwanda na Biashara wa Zambia katika Maonesho ya Madini yanayofanyika Mkoani Geita Bw. Roy Mwinga (wa tatu kulia) akitia saini katika kitabu cha wageni katika Banda la Buckreef katika maonesho hayo.
Mjiolojia wa Kampuni ya Buckreef Francis Kiyumbi (wa pili kushoto) akionesha sampuli za aina ya miamba inayopatikana kwenye Mgodi wa Buckreef.
Watumishi wa Mgodi wa Buckreef wakiwa katika picha ya pamoja katika Banda lao katika Maonesho ya Teknolojia katika Sekta ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Bombambili Mkoani Geita. (kutoka kushoto) ni, Afisa Usalama wa Mgodi huo Charles Kafuku, Afisa Rasirimali watu wa Buckreef, Domitilla Mang'ondi, (anayefuata), Mjiolojia Francis Kiyumbi, na Mtaalamu wa masuala ya umeme Mgodini Nahom Mramba. Muonekano wa Banda la Buckreef katika Maonesho ya Madini Mkoani Geita.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger