Friday 29 July 2022

RAIS DKT. MWINYI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA MTANGAZAJI WA ZBC



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa wa marafiki kufuatia kifo cha mtangazaji mkongwe wa ZBC televisheni, Bi.Sharifa Maulid.


Katika salamu hizo za pole, Rais Dkt. Mwinyi ameeleza kusikitishwa na kifo cha mtangazaji huyo mkongwe na kuisihi familia ya marehemu kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo.


“Natoa mkono wa pole kufuatia kifo cha mtangazaji mkongwe wa ZBC televisheni, marehemu bibi Sharifa Maulid, naukumbuka umahiri wake katika utangazaji kwani alikuwa hodari katika kazi yake hiyo na kazi zake nyingine alizozifanya mbali ya utangazaji,”ilieleza sehemu ya salamu za pole alizozitoa Rais Dkt.Mwinyi.


Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amewasihi watangazaji na wafanyakazi wote wa sekta ya habari nchini kufuata nyayo na uzalendo wa marehemu bibi Sharifa Maulid ambaye hadi anafariki dunia alikuwa Afisa Habari katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto.


Rais Dkt. Mwinyi amemuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amin.
Share:

JITIBU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER

Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;


1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama


Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 au 0754568767  utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

MUME WANGU ALIPANGA KUNIFURUSHA BAADA TU YA KUPATA KIDOSHO MJINI


Kwa jina ni Elizabeth kutoka katika kaunti ya Bungoma. Tulikuwa kwenye ndoa na mume wangu Benson kwa muda wa miaka minne sasa. Tulikuwa na maisha mazuri kwani hakuna lolote lililokuwa na kuvunja uhusiano wetu kuja miogoni mwetu.

 Benson alikuwa ni mwanaume ambaye alijali maslahi yangu nami nilikuwa wa kuzingatia yote aliyonishauri kwenye ndoa kwani sikutaka kukosana naye. Baadaye alipata kazi mjini Nairobi na hapo tukawa na makubaliano baina yetu kwamba angeenda mjini kuifanya kazi ile name ningebaki kijijini. Aliupokelea uamuzi ule kwa mikono yote na hapo akawa mwenye furaha ajabu.

Kila mwezi alikuwa akinitumia hela za kufanya shuguli mbalimbali pale nyumbani kwetu. Nilimwamini kwani hakuna hata wakati mmoja mume wangu alionekana kuwavizia vidosho wengine. Jambo hili lilinipelekea mimi kumwonyesha mapenzi ya dhati. 

Kila baada ya mwezi mmoja alikuwa akitembea nyumbani kunijulia hali na hapo sikuwa na shaka ya uwepo wake mjini Nairobi ilhali hatukuwa naye. Baada ya siku kupita tabia yake ilianza kubadilika. Hakuwa akipiga simu tena kama ilivyokuwa kawaida yake kila siku.

 Nilianza kushuku mienendo hii yake kwani nilishuku alikuwa amepata kidosho mjini. Pesa alizokuwa akituma kila mwisho wa mwezi zilipungua kwani hata wakati mwingine hakuwa akituma hata senti moja.

Wakati mwingine nilipompigia simu sauti ya mwanamke ilisikika kwenye simu yake ishara tu alikuwa keshapata mpenzi mwingine. Nilifunga safari na kwenda Nairobi kujua alipokuwa akiishi. Hakuwa akishika simu yangu nilipofika.


 Nyumbani pake nilipigwa na butwaa baada ya kupata mwanamke mwingine kwenye nyumba ile aliyeniambia kwamba alikuwa mke wake na hakuna lolote ningefanya. Nilienda kulala kwa dada yangu usiku ule kwani sikutaka mapigano baina yangu na mwanamke yule.

Dadangu alinihurumia kwa mambo yaliyonikumba na hata akanipa ushauri kwamba palikuwepo na dakatari tajika wa miti shamba kwa jina Kiwanga ambaye angenisaidia. Alinipa nambari za Daktari Kiwanga na hapo nikampigia simu na kutenga siku ambayo tungekutana kwa ajili ya usaidizi wake.

Baada ya wiki moja nilikuwa kwenye ofisi ya dakatri Kiwanga. Nilimwelezea yote yaliyonikumba. Alifanya shughuli zake za mitishamba na kunipa hakikisho kwamba yote yangekuwa sawa na kwamba mume wangu angerejea nyumbani kwa msamaha. Nilirejea nyumbani na baada ya siku tatu sikuyaamini macho yangu. Mume wangu alikuja nyumbani akiwa mnyonge ajabu. Aliniomba msamaha kwa yote yalikyoukuwa kesha tokea.

 Nilimsamehea kwa kuwa nilikuwa mwenye mapenzi ya dhati kwake. Baadaye tulienda naye mjini. Tangu siku ile mume wangu amekuwa ni mtu mwaminifu ajabu kwenye ndoa. Pongezi sana kwa daktari Kiwanga kwa huduma yako. Mtu yeyote ambaye ana shida kama hii anaweza kumtembelea daktari Kiwanga kwani ndiye daktari tajika wa miti shamba katika eno zima la Afrika ya Mashariki.

Daktari Kiwanga hutibu maradhi kama kifua kikuu, kisukari, msukomo wa damu, kifafa na magonjwa mengineyo. Husuluhisha shida za kifamilia kama kutokouwa na uwezo wa kupata mtoto, kutopata mchumba wako wa maisha, shida za ndoa, kuwa na bahati katika maisha haswa katika michezo ya kamari na mengineyo. 


Ama kwa hakika daktri Kiwanga ni mtu wa kutegemewa katika jamii kwa ajili ya kusuluhisha mambo yanayowakosesha watu mbalimbali usingizi ama maisha bora yenye matamanio. Kwa mahojiano na daktari Kiwanga kwa ajili ya kusuluhisha shida zako, piga simu kwa nambari +254769404965/barua pepe kiwangadoctors@gmail.com ama tembelea wavuti wwww.kiwangadoctors.com kwa mengi zaidi.

Share:

HATUPELEKI UMEME VIJIJINI KUWASHA TAA PEKEE – MAKAMBA


Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba (wa pili kutoka) akizungumza na Meneja wa Kiwanda cha KUZA Afrika, Rob Clowes ambacho kinachakata maparachichi ili kutengeneza mafuta na bidhaa nyingine wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Kiwanda hicho kinafanya uzalishaji kwa kutumia umeme uliunganishwa na TANESCO.
Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akifungua valvu ili kuruhusu majimoto yanayotoka ardhini kupita katika kisima kifupi cha utafiti wa Jotoardhi kilichochorongwa katika eneo la Kiejo-Mbaka wilayani Rungwe mkoani Mbeya

………………………

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba amesema kuwa, Serikali haisambazi umeme vijijini kwa ajili ya kuwasha taa peke yake bali kuchagiza pia shughuli za kiuchumi ikiwemo uanzishaji wa viwanda.

Amesema hayo tarehe 28 Julai, 2022 baada ya kutembelea kiwanda kinachochakata parachichi ili kutengeneza mafuta cha KUZA AFRIKA kilichopo wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya mbacho kimeunganishiwa umeme na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Makamba alisema kuwa, uwepo wa kiwanda hicho ni matokeo ya uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta ya Nishati ambao umezaa matunda kwani kiwanda hicho pamoja na kuongezea thamani mazao ya Wakulima, kimezalisha ajira zaidi ya 200 ndani ya kiwanda na katika mashamba ya parachichi.

Aliongeza kuwa, msingi mzima wa kupeleka umeme vijijini ni kusawazisha maendeleo kati ya watu wa vijijini na mijini kwani shughuli za kiuchumi kama za viwanda zinaboresha pia uchumi wa wananchi wa vijijini.

Meneja wa TANESCO, Wilaya ya Rungwe, Mhandisi Mukhsin Kijemkuu alimweleza Waziri wa Nishati kuwa, kiwanda hicho kabla ya kufungiwa transforma yake kilikuwa kikizalisha lita 2000 kwa siku lakini baada ya kupata Transfoma wiki moja iliyopita kinazalisha lita 4000 kwa siku.

Aliongeza kuwa kwa lita 4000 zinazotarajiwa kuzalishwa kwenye kiwanda hicho mwekezaji angetumia shilingi milioni 50 kununua dizeli ya kuendesha mitambo ila kwa kuwa sasa anatumia takriban shilingi milioni 30 kwa gharama za umeme ambayo ni pungufu ya gharama alizokuwa akiingia awali.

Pamoja na kuishukuru Wizara ya Nishati kwa kutenga fedha za kupeleka umeme kwenye maeneo kama hayo, Mhandisi Kijemkuu amekaribisha wawekezaji wengine kuwekeza kwenye miradi kama hiyo kwani hali ya upatikanaji umeme sasa imeimarika na pia TANESCO itaongeza mapato yake.

Katika hatua nyingine, Waziri wa Nishati alifika kwenye Kijiji cha Iramba Kata ya Ntaba wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya ili kukagua kazi zinazoendelea katika chanzo cha Jotoardhi cha Kiejo-Mbaka ambacho kinatarajiwa kuzalisha umeme utakaoingizwa kwenye gridi ya Taifa.

Waziri Makamba mara baada ya kukagua chanzo hicho, alisema kuwa “Serikali imeamua kuweka nguvu katika kuzalisha umeme kwa njia mbalimbali, tuna umeme wa Maji, Umeme wa Gesi na safari hii tumewekeza kwenye umeme wa Joto ardhi, hapa Kiejo-Mbaka ni moja ya vyanzo vya Jotoardhi ambavyo vina uwezekano wa kuzalisha umeme wa Joto ardhi.”

Alisema kuwa katika bajeti ya Wizara ya Nishati ya mwaka 2022/2023, Serikali imetenga shilingi Bilioni 5 kwa ajili ya kuendeleza miradi hiyo na kwamba Serikali imenunua mtambo maalum wa kuchoronga mpaka Kilometa 3 chini ili kuweza kulifikia joto ambalo litatoa mvuke utakaozungusha mtambo wa kuzalisha umeme.

Aliongeza kuwa, matarajio ni kuzalisha umeme wa kiasi cha megawati 200 ifikapo mwaka 2025 huku akitaja kuwa Tanzania kuna maeneo mengi yanayoweza kutoa nishati ya Jotoardhi ya kiasi cha megawati 5000.

Licha ya kuzalisha umeme, alitaja faida nyingine za Jotoardhi kuwa ni pamoja na ukaushaji wa mazao na kupasha moto nyumba kitalu ili kuongeza thamani ya mazao na ufugaji wa samaki kwani maji yanayotokana na jotoardhi hutumika kuongeza joto katika bwawa la samaki katika mazingira ya baridi na hivyo kupelekea samaki kukua kwa haraka.

Nishati ya Jotoardhi inatokana na joto linalotoka kwenye mwamba wenye joto unaochemsha maji yaliyoingia ardhini
Share:

KANISA KATOLIKI JIMBO LA SHINYANGA LAPATA MAPADRE WAPYA


MASHEMASI Watano ambao wanatarajiwa kupewa daraja la Upadre hapo kesho, na askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, leo wamekiri imani Katoliki mbele ya askofu na Kanisa,ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya utolewaji wa daraja la Upadre.

Mashemasi hao ambao ni Emmanuel Kimambo wa Parokia teule ya Shishiyu, Emmanuel Gembuya wa Parokia ya Buhangija, Paul Mahona wa Parokia ya Wila, Simon Lutamula wa Parokia ya Mwamapalala na Eliasi Vumba wa Shirika la Ndugu wadogo wa Mtakatifu Francisco (Wakapuchini) wamekiri imani na kutia saini viapo vyao kupitia ibada ya masifu ya jioni, ambayo imefanyika katika Kanisa kuu la Mama Mwenye Huruma,Ngokolo mjini Shinyanga.
SAUTI ZA MASHEMASI WAKIKIRI IMANI


Akitoa mafundisho yake katika ibada hiyo, Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu,anewaomba waamini kuendelea kuwaombea Mashemasi hao ili watakapopewa daraja la Upadre ,waweze kutekeleza kwa uaminifu utume watakaokabidhiwa na kanisa.

Askofu Sangu amefafanua kuwa, daraja la Upadre ambalo watapewa hapo kesho, ni njia itakayowashirikisha katika huduma ya kikuhani ya kuokoa roho za watu na kuwatafuta wale waliopotea.
SAUTI YA ASKOFU SANGUMashemasi wakitia saini viapo vyao mbele ya AskofuMashemasi wakirudi katika nafasi zao baada ya kusaini viapo vyaoVicar wa Shirika la Wakapuchini kanda ya Tanzania Pd.Paschal Vincent Dohho (mwenye kanzu ya Ugoro) akiwa katika ibada ya masifu ya jioni Kanisa kuu NgokoloAskofu Sangu akiwa katika picha ya pamoja na Mashemasi mara baada ya Ibada ya Masifu ya jioni(Kushoto ni Katibu wa askofu Pd. Deusdedith Kisumo na Kulia ni Paroko wa Parokia ya Mwadui Pd.Michael Msabila)

Chanzo - http://radiofaraja.com/
Share:

Thursday 28 July 2022

NAIBU WAZIRI MASANJA AKAGUA UJENZI WA NYUMBA MPYA 400 MSOMERA WILAYANI HANDENI


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Mary Masanja (Mb) akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Siriel Mchembe (kushoto) na Askari wa SUMA JKT kukagua ujenzi wa nyumba 400 kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga leo.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Mary Masanja (Mb) (katikati) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Siriel Mchembe (kushoto) wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba 400 kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga leo.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Mary Masanja (Mb) akiwaelekeza Askari wa SUMA JKT kuhakikisha ifikapo tarehe 30 Agosti 2022 kaya zaidi ya 50 ziwe zimeletwa Msomera ,wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba 400 kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga leo.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Mary Masanja (Mb) akiwasisitiza na vijana wanaojenga nyumba 400 katika kijiji cha Msomera kufanya kazi kwa uzalendo,wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba 400 kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga leo.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe, Mary Masanja (Mb) akichota zege wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa nyumba 400 kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga leo.

**************************

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amekagua ujenzi wa nyumba mpya 400 katika kijiji cha Msomera Wilayani Handeni, Mkoani Tanga watakazohamia kwa hiari wananchi kutoka Ngorongoro.

Akizungumza katika ziara hiyo leo, Mhe. Masanja amewapongeza SUMA JKT kwa kufanya kazi vizuri kuhakikisha nyumba hizo zinakamilika kwa wakati.

“Maelekezo yetu ni kwamba hadi kufikia tarehe 30 Agosti 2022 kaya zaidi ya 50 ziwe zimeletwa katika nyumba hizi na hatuna mashaka na kazi mnayoifanya” Mhe. Masanja amesisitiza.

Aidha, Mhe. Masanja ameagiza watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya kwa wakati.

“Kwa kuwa Halmashauri mmepewa jukumu la kujenga kituo cha afya, kinatakiwa kikamilike ndani ya miezi minne, fanyeni kazi usiku na mchana kuhakikisha mnakamilisha. Tusingependa nyumba ziwe zimekamilika, huduma za afya ziwe bado”Mhe. Masanja amefafanua.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Siriel Mchembe amesema kuwa agenda muhimu ni kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya.

Kwa upande wake Operation Commander ,Luteni Kanali Edward Anthony Mwanga amesema kuwa ndani ya miezi miwili watahakikisha wanakamilisha nyumba zote na kumuahidi Naibu Waziri kuwa hadi kufikia terehe 20 Agosti 2022 familia zaidi ya 50 zitakuwa zimehamia Msomera.

Ziara hiyo ina lengo la kuangalia utekelezaji wa majukumu ya Wizara na kuangalia changamoto ili kuzipatia ufumbuzi.
Share:

KAMPUNI YA APS YAGAWA TAULO ZA KIKE 'KIPEPEO PAD' SHULE YA WASICHANA JANGWANI

Kampuni ya Aspire Products & Services Co. Ltd (APS Company) inayojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa Taulo za kike maarufu kwa jina Kipepeo Pad imetoa na kugawa taulo za kike 1700 kwa wanafunzi wote wa shule ya sekondari ya wasichana Jangwani Girls Secondary School Jijini Dar es salaam.

Hafla fupi ya makabidhiano imefanyika shuleni hapo Julai 27,2022 ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wilaya ya Ilala, Charangwa Selemani ambaye ametumia fursa hiyo kuwasihi wanafunzi hao wa kike kusoma kwa bidii na kuepuka vishawishi ili watimize ndoto zao huku akiishuru Kampuni ya APS kwa kutoa msaada huo wa taulo za kike.


Mkurugenzi wa Kampuni ya APS Janeth Dutu Mkurugenzi wa kampuni ya Kipepeo Pad Janeth Dutu aliyeambatana na mwakilishi wa Taasisi ya Girls Chapter amesema uhitaji wa taulo za kike kwa mabinti bado ni mkubwa katika shule mbalimbali huku akiwasihi kuzingatia matumizi sahihi ya taulo za kike na kujitunza ili watimize ndoto zao
Katibu Tawala wilaya ya Ilala, Charangwa Selemani akizungumza wakati Kampuni ya Aspire Products & Services Co. Ltd (APS Company) inayojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa Taulo za kike maarufu kwa jina Kipepeo Pad ikitoa na kugawa taulo za kike 1700 kwa wanafunzi wote wa shule ya sekondari ya wasichana Jangwani Girls Secondary School Jijini Dar es salaam
Kampuni ya  APS , Janeth Dutu akizungumza na wanafunzi wa shule Jangwani Girls Secondary School Jijini Dar es salaam
Kampuni ya  APS , Janeth Dutu akizungumza na wanafunzi wa shule Jangwani Girls Secondary School Jijini Dar es salaam


Kampuni ya Aspire Products & Services Co. Ltd (APS Company) inayojihusisha na utengenezaji na usambazaji wa Taulo za kike maarufu kwa jina Kipepeo Pad, Janeth Dutu akifurahia jambo baada ya kugawa taulo za kike 1700 kwa wanafunzi wote wa shule ya sekondari ya wasichana Jangwani Girls Secondary School Jijini Dar es salaam
Share:

Wednesday 27 July 2022

CWT BAGAMOYO YAENDELEA KUTOA MISAADA KWENYE SHULE MBALIMBALI



Na Elisante Kindulu - Chalinze
CHAMA Cha walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya BAGAMOYO kimeendelea kutoa misaada mbalimbali mashuleni ikiwa ni pamoja na kusaidia vifaa vya ujenzi.

Hatua ya kusaidia vifaa vya ujenzi imekuja baada ya shule ya Sekondari ya Dunda kuezuliwa na upepo kwa choo cha wanafunzi wa kike na hivyo kufanya vijana hao kupata changamoto kupata huduma hiyo muhimu.

Vifaa hivyo vilikadhidhiwa na Mwenyekiti wa CWT Wilaya ya Bagamoyo, Mwl. Hamisi Kimeza pamoja na Katibu wake Mwl. Shaaban Tessua katika viwanja vya shule hiyo hivi karibuni.

Katibu Tessua alisema kwamba vifaa hivyo  vya upauaji ni hatua ya mwanzo tu ya msaada wao huku vifaa vingine vikiwemo mifuko ya saruji kupitia CWT mkoa wa Pwani kitengo cha walimu wanawake nayo itafuata.

Katika hatua nyingine CWT Wilaya ya Bagamoyo imeendelea kutoa majiko ya gesi kwa ajili ya walimu mashuleni ikiwa ni sehemu ya Mchango wake ili walimu waweze kupata huduma ya pamoja ya  chakula wawapo mahala pa kazi.

Akikabidhi majiko hayo akiwa na baadhi ya wajumbe wa CWT wa  kamati ya utendaji ya Wilaya, Mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya ya Bagamoyo Mwl. Hamisi Kimeza alisema, lengo la kutoa majiko hayo ni kuongeza mshikamano na upendo kwa walimu wawapo mahala pa kazi, kwani chakula ni eneo mojawapo la kuwakutanisha wote kwa wakati mmoja.

Lakini Mwenyekiti huyo aliwaeleza walimu kuwa chama Wilaya hakitakuwa na fedha za kujaza gesi baada ya ile ya awali kumalizika , badala yake akawashauri watafute namna ya kupata fedha hata kuchangia fedha zinazorejeshwa mashuleni kwa ajili ya posho ya vikao vya kichama mahala pa kazi.

Naye Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Bagamoyo, alisema kuwa wamefanya zoezi Hilo katika awamu mbili kwa baadhi ya shule ,lakini lengo Ni kuzifikia shule zote za halmashauri ya Chalinze pamoja na Bagamoyo zilizopo wilayani Bagamoyo.
Mwenyekiti wa CWT ,Wilaya ya Bagamoyo Hamisi Kimeza(kushoto) na Katibu wa Chama hicho wa Wilaya, Shaaban Tessua(kulia) wakikadhi mbao kwa walimu wa shule ya Sekondari Dunda ili kusaidia matengenezo ya choo kilizoezuliwa na upepo shuleni hapo.

Share:

RADI YAUA WATU 22



NCHINI India imeripotiwa vifo vya watu 20 waliouawa na radi ikiwa ni ndani ya masaa 24 katika miji nane iliyo Mashariki mwa Jimbo la Bihar nchini humo.

Radi hizo ziliambatana na mwanga mkali ambapo Mkuu wa Jimbo la Bihar Nitish Kumar amewataka wananchi kufuatilia kwa ukaribu ushauri wa Mamlaka inayohusika na majanga nchini humo.


Mamia ya watu hufariki kila mwaka kutokana na radi ambazo mara nyingi hutokea kipindi cha mvua za Monsoon.

Sababu kubwa iliyotolewa ambayo inasababisha idadi kubwa ya vifo kwa raia wa India karibu kila mwaka kutokana na radi ni ule utamaduni wa watu wengi wa India kufanya kazi nje tofauti na mataifa mengine.

India imerekodi idadi ya radi milioni 18 kwa kipindi cha kuanzia Aprili 2020 hadi Machi 2021

Aidha siku ya jumanne Kumar alitangaza kiasi cha Rupee 40,000 ambayo ni sawa na Dola 5,008 kwa kila familia iliyofiwa.


Kwa mujibu wa taarifa ni kwamba India imeripoti jumla ya radi milioni 18 katika kipindi cha Aprili 2020 hadi Machi 2021 na hiyo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Climate Resilient Observing System Promotion Council ambalo pia limebainisha kuwa rekodi hizo ni ongezeko la 34% ukilinganisha na rekodi zilizopita katika kipindi kama hicho.
Share:

TANZANIA YANG’ARA UCHAGUZI MKUU WA UMOJA WA WATOA HUDUMA ZA POSTA KUSINI MWA AFRIKA (SAPOA)

Ujumbe wa Tanzania kwenye picha ya pamoja na Mtendaji Mkuu wa SAPOA Bwana Janras Serame Kotsi (wa pili kulia). Kutoka kushoto ni Mhandisi Kulwa Fifi, Kaimu Meneja wa Biashara mtandao, Bwana Constantine Kasese, Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji wa Biashara, Janras Kotsi (SAPOA) na Elia Madulesi, Mkuu wa Mawasiliano na Mambo ya Posta Kimataifa.
Bwana Constantine Kasese,Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji wa Biashara za Shirika, aliyemwakilisha Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania akimpongeza Bwana Elia Madulesi mara baada ya kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Bodi ya Utawala ya SAPOA na baadae Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo jijini Cape Town,Afrika ya Kusini wakati wa vika vya SAPOA vinavyoendelea.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia za Kidijitali wa Afrika ya Kusini Mheshimiwa Phillemon Mapulane (Mb) katika aliyekaa,akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Utawala ya SAPOA. Waliokaa kulia kwake ni Bwana Festus Hangula, Mwnyekiti wa Bodi na kushoto kwake ni Bwana Elia Madulesi, Makamu Mwenyekiti.Waliosimama kutoka kushoto ni Cornelius Ramatlhakwane, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Botswana (Mjumbe), Bibi Nomkhita Mona, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Afrika Kusini(Mjumbe) na Bwana Janras Kotsi Mtendaji Mkuu wa SAPOA

****
Cape Town, South Africa


Tanzania kupitia Shirika la Posta nchini imechaguliwa kuingia kwenye bodi ya Utawala ya Umoja wa Watoa Huduma za Posta Kusini mwa Afrika (SAPOA) kwenye uchaguzi wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa 20 unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Durbanville, ulioanza tarehe 25-28 Julai, 2022, jijini Cape Town, Afrika ya Kusini. 

Katika mkutano huo Bw. Elia P.K.Madulesi, Mkuu wa Mawasiliano na Mambo ya Posta Kimataifa wa Shirika la Posta Tanzania amepata nafasi hiyo ya kuiwakilisha Tanzania kwa kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Bodi ya Utawala ya Umoja huo, nchini Afrika Kusini.

Uchaguzi huo uliofanyika wakati wa Mkutano Mkuu wa 20 wa Mwaka wa SAPOA, uliohusisha nchi zilizo katika Umoja huo ambao ni wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Vilevile, katika Bodi hiyo Bw. Madulesi, amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti kwenye Bodi hiyo, huku nafasi ya Mwenyekiti Ikienda kwa Ndugu Festus Hangula, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Namibia. 

Wengine waliochaguliwa kuingia kwenye Bodi hiyo ni Cornelius Ramatlhakwane, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Botswana, Bibi Nomkhita Mona, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Afrika Kusini na Bibi Elizabeth Mamosehlela Letsoela, Mkurugenzi Mkuu wa Posta ya Lesotho.

Shirika la Posta Tanzania linahudhuria Mkutano Mkuu wa 20 wa Mwaka wa SAPOA na jukwaa la Posta la SAPOA likifanyika sambamba na Mkutano huo. 

Shirika la Posta limewakilishwa na Bw. Constantine Kasese, Kaimu Meneja Mkuu, Uendeshaji wa Biashara ambaye alimuwakilisha Bwana Macrice Mbodo Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania kwenye Mkutano huo, Bw. Kulwa Fifi, Kaimu Meneja wa Biashara Mtandao na Bw. Elia P.K. Madulesi, Mkuu wa Mawasiliano na Mambo ya Posta Kimataifa.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano
Shirika la Posta Tanzania
27 Julai, 2022

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger