Sunday 29 May 2022

BENARD MEMBE AREJEA CCM , AJITANGAZA MBUNGE WA CHINI CHINI....NAPE NNAUYE AELEZA VILE WANANCHI WALIVYOCHUKIA


ALIYEKUWA Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Bernard Membe amerudi rasmi kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Mheshimiwa Membe amerejea leo na kukabidhiwa kadi ya chama hicho katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Mtama, Nape Nape Nnauye uliofanyika katika Kata ya Chipomda mkoani Lindi.

Membe ameeleza jinsi alivyoumia kutokana na uamuzi wa kumuondolea uwanachama wa CCM na kuahidi kufia ndani ya chama hicho ambacho ndicho kilichomlea siku zote

Mheshimiwa Membe amepokelewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka aliyekuwepo katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Mtama.

Februari, 2020 Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ilimvua uanachama Waziri huyo wa zamani wa Mambo ya Nje.

Akizungumza katika mkutano huo, katika Kijiji cha Rondo, alisema Machi 30 hadi Aprili 1, mwaka huu aliitwa Dodoma, kwenye Mkutano wa Kamati Kuu ya Maadili na Mkutano Mkuu wa Halmashauri Kuu, alipewa nafasi na Mwenyekiti wa CCM Taifa kuzungumza na wana CCM.

“Mama yetu, Rais wetu na Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa alinipa nafasi ya kuzungumza na wajumbe wa kamati kuu ya Chama Taifa. Nashukuru kwa kupewa nafasi ile na wajumbe waliliridhia kwa kauli moja nirejee CCM.

“Nimerejea CCM kwa sababu kuu mbili, sababu ya kwanza nilishauriwa na viongozi wa dini zote, nilishauriwa na viongozi wa CCM ngazi ya Wilaya na Mkoa, nilishauriwa na marafiki zangu wote nirejee CCM, nilishauriwa na wana CCM.

“Kutokana na ushauri wote huo sikuwa na namna nyingine zaidi ya kutii, nimekubaliana na ushauri wa wote waliosema nirudi CCM na sasa nimerudi CCM,” amesema Membe wakati akitangaza kurejea tena kwenye Chama.

Amesema sababu ya pili ya kurudi kwenye Chama hicho inatokana na dhamira yake ya kukitumikia Chama Cha Mapinduzi hadi atakapokwenda kaburini. “Nilipoondolewa CCM nilisikitika sana, nilisonekana sana, na ninyi wananchi msikitika, mlisononekana.

“Sababu ambazo zilinifanya niondoke CCM haziko tena, narudi sababu zilizoniondoa CCM haziko tena. Nimerudi, namshukuru Mwenyekiti wa CCM na wajumbe wa Kamati Kuu kunirudisha. Nimerudi kwenye Chama ambacho nimezaliwa na kukulia, chama ambacho kimenisomesha.

“Hivyo niahidi sitaondoka tena, nitabakia CCM hadi mwisho wa uhai wangu. Kurudi kwangu CCM nitaendelea kukitumikia Chama changu na sasa nitaendelea kushirikiana na Mbunge wangu Nape Nnauye. Mwaka 2015 nilisema nitawaletea Nape na kweli nilimleta, hivyo sasa Mtama mtakuwa na wabunge wawili, Mbunge wetu Nape na mimi mbunge wa chini chini.”

NAPE

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mtama ambaye pia ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye alisema baada ya Membe kuondoka kwenye Chama wananchi wengi walichukia, lakini aliwaomba wasichukie kwani kuna siku moja atarejea.

“Leo mwenyezi Mungu ameturudishia faraja la Londo, ameturejeshea furaha Chiponda. Mtama ni wastaarabu na hatuna shida tena, tuna imani kubwa na Membe, alinikabidhi kijiti na kuvaa viatu vyake, kulikuwa na mambo yaliyokwama huku nyuma kwa sababu za kisiasa, lakini Mama Samia amekuja ameziondoa,” alisema.

Aidha, alitumia nafasi hiyo kuwataka wananchi wa Mtama kushikamana, fitina ambazo ziliingia kati zimekwisha. “Membe amenipigania katika mambo mengi, nilipotaka ubunge Ubungo baada ya kuonekana fitna zimeingia katikati Membe aliamua kuchora ramani.

“Ndio maana safari yangu ya ubunge imekuwa nyepesi. Kaka Membe amenipigania sana na bahati nzuri amerudi CCM. Niseme tu Mungu ameamua ugomvi,” alisema.

SHAKA AMKABIDHI KADI

Akizungumza katika mkutano huo, Shaka alisema Membe amerejeshwa katika Chama baada ya kufuatwa kwa utaratibu ikiwemo kujadiliwa na tawi lake kisha na vikao vya juu.

Shaka alisema Membe na wanachama wengine zaidi ya 1670 waliovuliwa uanachama ambao wamejadiliwa katika vikao na kurejeshewa uanachama, sasa wanaweza kukabidhiwa kadi zao katika matawi yao.

Shaka alisema kurejea kwa Membe ndani ya CCM kuendelee kuwa chachu ya kudumisha umoja na mshikamano hususan kwa wana CCM wa Jimbo la Mtama.

CHANZO - DIRA MAKINI
Share:

ANAYEDAIWA KUFANYA MAPENZI KWA NGUVU NA WANAWAKE 'TELEZA' AUAWA JIJINI ARUSHA


Mtu aliyeuawa na wananchi
**
Mtu mmoja mkazi wa Sojema, Kata ya Murieti Jijini Arusha, ameuawa na wananchi baada ya kukamatwa katika nyumba ya moja ya wakazi wa eneo hilo akijaribu kufanya uhalifu, huku wengi wakimhusisha na mtu ajulikanae kama 'Teleza' anayetuhumiwa kuwaingilia wanawake kinguvu hasa nyakati za usiku.


Mtu huyo ambaye haikuwa rahisi jina lake kujulikana kwa haraka, amekutwa na mauti hayo majira ya saa 10:00 alfajiri baada ya kukurupushwa na baadhi ya wakazi wa Murieti kwa kushirikiana na vijana wa sungusungu ambao kwa muda wamekuwa wakishika doria katika kipindi hiki cha habari za teleza kuzagaa katika eneo lao.

Akizungumza Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo, amethibitisha kushambuliwa kwa mtu huyo na kutoa rai kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi kwani hupunguza wigo wa upelelezi wao.

Chanzo- EATV
Share:

TBS YATOA ELIMU YA UDHIBITI UBORA KWENYE MAONESHO YA TATU YA FAHARI YA GEITA


******************************

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeshiriki katika Maonesho ya Tatu ya Fahari ya Geita yanayoendelea mkoani Geita ambayo yamejumuisha wazalishaji wa bidhaa mbalimbali wanaopatikana mkoani humo pamoja na mikoa ya jilani.

Akizungumza leo Mei 29,2022 katika Maonesho hayo, Afisa Usalama wa Chakula Mkuu TBS Kanda ya Ziwa Bw.Julius Panga amesema lengo la maonesho hayo ni kuona namna gani bidhaa mbalimbali zinavyozalishwa na wajasiriamali wa mkoa huo na kutoa elimu ya udhibiti ubora wa bidhaa hizo.

Amesema kupitia maonesho hayo wameendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na wazalishaji wa bidhaa kufahamu majukumu makubwa yanayifanywa na TBS pamoja kuona ni namna gani wanaweza kuzalisha bidhaa zenye viwango vinavyotakiwa.

"Tumekuwa tukiwajukisha majukumu ya Shirika na kuonana na wajasiriamali ambao wanahitaji huduma ya Shirika pamoja na kufahamu namna ya kupata alama ya ubora kwenye bidhaa". Amesema Bw.Panga.

Aidha amewataka wazalishaji,waandaji wa bidhaa na wananchi kwa ujumla kutembelea kwenye maonesho hayo ili waweze kupata elimu ya kutosha kuhusu majukumu ya TBS.
Share:

Saturday 28 May 2022

WANAWAKE 16 WAKAMATWA DAR TUHUMA ZA KUFANYA NGONO KWA KUTUMIA BIA, MAHINDI YA KUCHOMA



Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Murilo Jumanne Murilo

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Jumanne Sagini

UCHUNGUZI uliofanywa na Vyombo vya Dola umebaini kuibuka kwa baadhi ya wanawake wanaofundishana kufanya matendo ya ngono kwa kutumia vifaa hatarishi kama chupa za bia soda, mahindi ya kuchoma, ndizi na matango.


Baadhi wameunda makundi ya WhatsApp ili kuweka picha zao za utupu na wengine huziweka katika mitandao tofauti ya kijamii. Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wanawake na mabinti wanaoonekana kukubuhu kufanya vitendo hivyo husafirishwa kwenda ughaibuni na kutumikishwa katika biashara ya ukahaba, jambo ambalo ni kinyume cha Sheria za Nchi yetu.

Kufuatia kuendelea kufanyika kwa matendo hayo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika Hotuba yake tarehe 03, Mei 2022 alipokuwa akifungua Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwa Bara la Afrika Jijini Arusha,aliguswa sana na kuporomoka kwa maadili.

Alitumia jukwaa hilo kuelekeza viongozi kusimamia suala la Maadili nchini. Kufuatia Maelekezo hayo ya Mhe, Rais, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa alizielekeza Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wanawake Wazee, na Makundi Maalum kushirikiana kukabiliana na uovu huo.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake Wazee na Makundi Maalum kwa kushirikiana na Vyombo vya Dola, zimefanikiwa kuwanasa jumla ya wanawake na mabinti 16 wa mtandao unaojihusisha na Matendo maovu ya kufanya ngono kwa kutumia vifaa hatarishi kama chupa za soda na bia, mahindi ya kuchoma, ndizi na tango.


Watu hao wamekamatwa kutoka maeneo tofauti ya Mkoa wa Dar es Salaam, yakiwemo Mwananyamala, Kinondoni, Mkwajini, Tandale, Sinza, Buza na Magomeni. Aidha, Vyombo vya dola na Mamlaka husika vinaendelea kukamilisha Taratibu za kisheria ili wafikishwe mahakamani wakati wowote kuanzia sasa.”
Share:

Utafiti : HAKUNA POMBE ISIYOKUWA NA MADHARA....HATA KAMA NI GLASI MOJA TU



Habari mbaya kwa wale ambao huwa wanafurahia na kufikiri kwamba bilauri moja ya mvinyo kwa siku ni nzuri kwa kiafya.


Utafiti mkubwa uliofanywa duniani na kuchapishwa katika jarida la lancet umethibitisha kwamba utafiti uliofanywa awali na kuonyesha kwamba hakuna usalama katika unywaji wa pombe.

Watafiti wamekubali kwamba kunywa kwa kiasi kunaweza kumlinda mtu dhidi ya ugonjwa wa moyo lakini waligundua kwamba kuna hatari ya mtu kupata saratani na kukosa kinga ya magonjwa mengine.


Mwandishi wa utafiti huu alisema matokeo aliyoyapata yalikuwa ya muhimu sana kwa sasa kwa sababu ya mambo mengi yaliyozingatiwa


Je! unywaji wa pombe unasababisha hatari kubwa kwa kiasi gani?


Utafiti uliofanywa na 'Global Burden of Disease'unaangalia kiwango cha pombe na madhara yake kiafya kwa mataifa 195 ikiwemo Uingereza katika miaka ya 1996 mpaka 2016.


Utafiti uliangalia umri kuanzia miaka 15 hadi 95,mtafiti alilinganisha watu ambao wanakunywa pombe hata chupa moja kwa siku na wale ambao hawanywi kabisa.


Na kubaini kwamba watu wasiokunywa kati ya 100,000 ni watu 914 tu ndio wanasumbuliwa na matatizo ya kiafya kama saratani au kusumbuliwa na majeraha yeyote.


Lakini watu wanne zaidi wanapata madhara kama wanakunywa pombe hata chupa au bilauri moja kwa siku.

Maelezo ya picha,

Imethibitishwa kwamba hakuna pombe iliyo na manufaa kiafya


Kwa watu ambao hunywa chupa mbili za pombe kwa siku,Watu 63 kati yao uanza kupata mabadiliko ya kiafya na wale ambao hutumia chupa tano kwa kila siku kuna ongezeko kubwa la watu wapatao 338 ambao hupata madhara ya kiafya.


Kiongozi wa tafiti hiyo Dr Max Griswold kutoka Taasisi ya Health Metrics and Evaluation (IHME) katika chuo cha Washngton alisema kwamba utafiti wa awali ulibaini kwamba kuna hatari kubwa za kiafya ambazo zinahusishwa na uongezekaji wa uywaji wa pombe.


Uhusiano mkubwa wa matumizi ya pombe na hatari ya kupata saratani pamoja na magonjwa ya kuambukiza inaondoa kinga ya ugonjwa wa moyo katika utafiti.


Je, unakunywa pombe kiasi gani?

Ingawa hatari ya matumizi ya pombe huanza polepole hukua kwa haraka kwa watu ambao hunywa pombe kwa kiwango kikubwa.


Mwaka 2016 ,serikali Uingereza iliweka kiwango ambacho watu wnapaswa kutumia kwa wanawake na wanaume ili kupunguza athari ya ongezeko la ugonjwa huo.

Chanzo - BBC SWAHILI

Share:

WAWAKILISHI WA JAMII YA WAFUGAJI NGORONGORO WAIOMBA SERIKALI KUFANYIA KAZI RIPOTI WALIYOIWASILISHA SERIKALINI



Na Rose Jackson - Arusha.

Wawakilishi wa jamii ya Wafugaji wa tarafa ya Loliondo wamewasilisha serikalini ripoti na mapendekezo ya jamii yanayohusu tarafa ya Loliondo ambapo wameomba serikali kuisoma ripoti hiyo kwanza ndipo wakae na kamati hiyo ili waweze kujadiliana waliyokubaliana.


Mwenyekiti wa Baraza la Wafugaji wilayani Ngorongoro ambaYe ni mjumbe wa kamati iliyoandaA ripoti hiyo Edward Maura akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ripoti hiyo amesema kuwa ripoti na mapendekezo waliyoiwasilisha serikalini.


Amesema kuwa wanategemea kuwa mara baada ya kukabidhi ripoti hiyo wanaamini serikali itaisoma kwanza na ndipo wakutane na jamii na kamati hiyo kwa ajili ya makubaliano.


"Waziri mkuu alitoa fursa kwa wananchi wa tarafa ya Loliondo na Ngorongoro kuandika changamoto za ongezeko la watu na Changamoto ya kilomita 1500 iliyoko Loliondo na sisi tulikubali kukaa na kuunda kamati mbili ya tarafa ya Loliondo na tarafa ya Sale na bahati nzuri Wananchi walitoa ushirikiano na tumeweza kuiwasilisha serikalini",aliongeza Maura.


Amemwomba waziri mkuu kuangalia mambo yanayoendelea Ngorongoro ya baadhi ya watu kuhamishwa kwenye mamalaka ya hifadhi ya Ngorongoro ya vijana kumi wanaotoka eneo hilo na kuiomba serikali kuangalia uhamisho huo kama umezingatia kanuni na sheria .


Aidha wamemshukuru waziri mkuu kupokea mapendekezo hayo na kuiomba serikali kusoma kwanza ripoti hiyo na haitafanya Jambo lolote bila kukaa na kuzungumza kwa pamoja.


Naye Mwenyekiti wa kamati ya uandaaji wa ripoti hiyo tarafa ya Ngorongoro , Metui Oleshaudo amesema kuwa kazi waliyoifanya ya kukusanya maoni kwa kata zote za wilaya ya Ngorongoro wameshamaliza na wameifikisha serikalini na wanaiomba serikali ifanyie kazi ripoti hiyo .


Kwa upande wake Magreth Kaisoi kutoka tarafa ya Ngorongoro amesema kuwa waziri mkuu aliagiza kamati kukusanya maoni ya wananchi kutoka nanja tatu ambayo ni ongezeko la watu, ongezeko la mifugo pamoja na ujenzi holela ambapo amedai kuwa ripoti hiyo ikisomwa vizuri serikali itaweza kuelewa uhalisia .


Mapendekezo hayo yaliyokabidhiwa na kamati hiyo serikalini ni maoni ya wananchi ambao hawaami Ngorongoro ambapo waziri mkuu alitoa maelekezo kwa jamii hiyo kuunda kamati ya kuandika maoni na mapendekezo ya changamoto za tarafa ya Sale na Loliondo ili serikali iweze kuyatafutia uvumbuzi.

Share:

Friday 27 May 2022

THPS, SERIKALI WAKUTANA NA WADAU KUPANGA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UVIKO – 19 SHINYANGA….IMANI POTOFU BADO TATIZO, HAMASA YAHITAJIKA ZAIDI


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la THPS, Dkt. Redempta Mbatia akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog

Shirika la Tanzania Health Promotion Support (THPS) kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa kushirikiana na kamati za afya za Mkoa na Wilaya za Shinyanga kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC wameendesha mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga ili kutathmini maendeleo ya utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati mahususi ya kuongeza kasi ya utoaji wa chanjo hiyo katika mkoa wa Shinyanga.


Mkutano huo ambao umefanyika leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama na umefunguliwa na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Edward Mjema ambapo kupitia mkutano huo wadau wa afya wamefanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19.


Akifungua mkutano huo, Johnson ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kutumia vizuri fursa ya kupatiwa chanjo ya UVIKO-19 maana kwa kufanya hivyo wataweza kuokoa maisha yao.


Amesema Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau unaendelea kutoa chanjo ya UVIKO -19 katika halmashauri zake zote sita na kwamba kwa kushirikiana na Shirika la THPS wameendelea kutoa huduma za VVU na UKIMWI.

“Tuendelee kuhamasisha jamii kuchukua tahadhari juu ya UVIKO – 19. Serikali itaendelea kutoa taarifa kuhusu namna ya kukabiliana na ugonjwa huu kadri inavyowezekana kwa kutumia vyombo vya habari na wataalamu wa afya”,amesema Johnson.

“Jamii nzima inalo jukumu la la kuhakikisha kwamba kila mmoja,kila kaya, kila taasisi wanatekeleza na kufuata taratibu zote za kujikinga na ugonjwa huu bila kulazimisha wala kutumia nguvu za ziada lakini itakaposhindikana tutafanya hivyo kwa mujibu wa sheria ya afya ya jamii ya mwaka 2009 inayozuia mtu kuambukiza ugonjwa mtu mwingine kwa maksudi ambapo anafahamu kuna njia za kujikinga”,amesema Johnson.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Daniel Mzee amelishukuru Shirika la THPS kwa ushirikiano wanaoendelea kutoa mkoani Shinyanga hasa katika Huduma za VVU na UKIMWI na mapambano dhidi ya UVIKO – 19 .

Aidha amesema Serikali ya Mkoa wa Shinyanga imejipanga kikamilifu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa COVID -19 na kwamba kinachotakiwa ni hamasa katika jamii wananchi wajitokeze kupata chanjo.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la THPS, Dkt. Redempta Mbatia ameomba washiriki wa mkutano huo kubuni mipango mahususi itakayowashirikisha viongozi wa jamii na kisiasa katika uhamasishaji wa chanjo ya UVIKO- 19 na kupelekea kupata matokeo chanya katika utolewaji wa chanjo ya UVIKO 19 huku akipongeza nchi ya Tanzania kwa jitihada za utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 ambazo zimepokelewa vyema na kupelekea kuungwa mkono na  wadau wengi.

“Tumekutana hapa kwa ajili ya kupanga mikakati ya namna gani tutaweza kudhibiti kwa pamoja kuhakikisha jamii ya Watanzania hapa mkoani Shinyanga inakingwa na ugonjwa wa UVIKO – 19 kwa kuhakikisha kila mtu anafikiwa na chanjo ya UVIKO – 19. Tunashukuru sana kwa ushirikiano na jitihada zinazofanyika kwenye halmashauri zote na tunaishukuru serikali kwa kuhakikisha jamii inafikiwa na chanjo na kuweka msisitizo mkubwa katika kuwalinda Watanzania”,amesema Dkt. Redempta.

“Kadhalika tunawashukuru wafadhili wetu ambao wamehakikisha chanjo zinafika kwenye nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania kwa upande wetu sisi tunaishukuru Serikali ya Marekani, siyo tu kwa kuhakikisha tunapata chanjo lakini pia kuleta rasilimali ambazo zinatusaidia sasa hizo chanjo zimfikie kila mtu kule alipo hata kama ni nyumbani kwake",amesema.

Ameongeza kuwa THPS kwa kushirikiana na mkoa na halmashauri zote mkoani Shinyanga wameyafikia makundi maalumu yaliyokuwa yamelengwa hapo awali, ambapo wamefikia asilimia 79 ya Watu Wanaoishi na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI , asilimia 92 ya watumishi wa Sekta ya Afya (watumishi 1552 mkoani Shinyanga) na kufikia wazee zaidi ya miaka 60 wapatao 9012.

“Pamoja na mafanikio haya safari bado ni ndefu.Mpaka kufikia sasa mkoa wa Shinyanga una idadi ya watu 1,011,085 wenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea ambao wanafaa kupata chanjo ya UVIKO-19. Mkoa huu umeweza kuchanja watu 127,071 tu na hii imepelekea kufanya kikao hiki. Changamoto kubwa mkoani Shinyanga tunayokabiliana nayo ni imani potofu kuhusu chanjo hali inayokwamisha wananchi kujitokeza kupata chanjo”,amesema Dkt. Redempta.

“Kati ya malengo ya Mkutano huu ni kutambulisha rasilimali za ziada tulizozipata kupitia Mpango wa Dunia wa Global Vax, kwa upande wa Shinyanga takwimu rasmi zitakuja lakini ni kiasi cha kama Shilingi Bilioni Moja, sasa hii pesa imekuja na malengo ya ziada ya watu takribani 500,000 , hivyo tuna kazi kubwa mbele yetu, na ni jukumu letu sote wakiwemo viongozi wa siasa kuhamasisha wananchi kupata chanjo ambapo sasa wananchi wanafuatwa hadi nyumbani”, ameongeza Dkt. Redempta.


Kiongozi wa Miradi ya Tiba kutoka CDC -Tanzania Dkt. Eva Matiko ameeleza kuwa PEPFAR na CDC wataendelea kusaidia upatikanaji wa huduma ya chanjo ya UVIKO-19 katika vituo vya kutolea huduma za afya na jamii kwa ujumla na kwamba ili kuweza kutumia rasilimali za chanjo ya UVIKO-19, uhusiano madhubuti kati ya serikali za mitaa na mradi wa Afya Hatua unahitajika sana.

Amesema CDC- Tanzania kupitia wadau wake kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kujumuisha huduma za chanjo ya UVIKO-19 katika utekelezaji wa programu zake.

“Tangu Septemba 2021, kwa kufuata malengo ya PEPFAR, kipaumbele cha kwanza kilikuwa ni kuongeza utoaji wa chanjo kwa watu wanaoishi na VVU, na watoa huduma za afya ngazi ya jamii ambao hutoa huduma kwa WAVIU. CDC- Tanzania kupitia washirika wake, watasaidia serikali ya Tanzania katika kufikia malengo yake ya utoaji wa chanjo ya UVIKO-19, mkoa wa Shinyanga ukiwa miongoni mwao”,amesema Dkt. Eva.


KUHUSU THPS

THPS ni taasisi ya Kitanzania iliyoanzishwa mwaka 2011 kwa kufuata sheria ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002. THPS inatekeleza kazi zake kwa kushirikiana na Wizara ya afya, Wizara ya  maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto pamoja na Ofisi ya Rais- tawala za mikoa na serikali za mitaa (OR- TAMISEMI), Wizara ya mambo ya ndani-hususan Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza, na Wizara ya afya huko Zanzibar. Dira ya THPS ni kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa Tanzania, kupitia uimarishaji wa mifumo ya sekta ya afya ili kutoa huduma bora za afya zikiwemo zile za VVU/UKIMWI, kifua kikuu, kuzuia ukatili wa kijinsia, afya ya uzazi, mama na mtoto na afya ya vijana. THPS pia inatoa huduma za kuimarisha mifumo ya maabara na usimamizi wa taarifa za afya kwa TEHAMA.


Mradi wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA (Oktoba 2021-Septemba 2026) unalenga kutoa huduma bora za afya jumuishi katika vituo vya kutolea  huduma za afya (Kigoma, Pwani na Shinyanga) na huduma ngazi ya jamii(Pwani na Kigoma) Huduma za Kinga, tiba na matunzo za VVU ikiwemo huduma huria za kitatibu za tohara kwa wanaume( Kigoma na Shinyanga) na programu ya DREAMS( Determined, REsilient, Empowere, AIDS-free, Mentored and Safe) mkoani Shinyanga. Programu ya DREAMS inatoa huduma jumuishi na mikakati inayoangalia vichocheo hatarishi vya VVU kwa mabinti wadogo.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson akifungua mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Edward Mjema leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama. Mkutano huo wenye lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19 umeandaliwa na Shirika la THPS kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson akifungua mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Edward Mjema leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa ajili ya kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson akifungua mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Edward Mjema leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa ajili ya kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini kwenye Mkutano wa kujadili tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19 ulioandaliwa na Shirika la THPS kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania Health Promotion Support(THPS), Dkt. Redempta Mbatia akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama. Mkutano huo wenye lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19 umeandaliwa na Shirika la THPS kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania Health Promotion Support(THPS), Dkt. Redempta Mbatia akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania Health Promotion Support(THPS), Dkt. Redempta Mbatia akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Daniel Mzee akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Tanzania Health Promotion Support(THPS), Dkt. Redempta Mbatia, kulia ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Daniel Mzee akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la THPS, Dkt. Redempta Mbatia, Wa kwanza kulia ni Meneja Miradi Shirika la THPS Mkoa wa Shinyanga Dkt. Amos Scot akifuatiwa na Kiongozi wa Miradi ya Tiba kutoka CDC -Tanzania Dkt. Eva Matiko  na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson
Meneja Miradi Shirika la THPS Mkoa wa Shinyanga Dkt. Amos Scot (kulia),  Kiongozi wa Miradi ya Tiba kutoka CDC -Tanzania Dkt. Eva Matiko (katikati) na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson wakiwa kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga.
Kiongozi wa Miradi ya Tiba kutoka CDC -Tanzania Dkt. Eva Matiko
akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama kwa lengo  la kufanya tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19.
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Emmanuel Johnson akiongoza mkutano wa wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Sophia Edward Mjema leo Ijumaa Mei 27,2022 Mjini Kahama. 
Meneja Miradi Shirika la THPS Mkoa wa Shinyanga Dkt. Amos Scot
Mkurugenzi Tiba na Matunzo Mradi wa Afya HATUA kutoka Shirika la THPS, Dkt. Frederick Ndossi akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Msimamizi wa Masuala ya Chanjo Shirika la THPS, Dkt. Hans Maro akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Shinyanga, Timothy Sosoma akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Katibu Tawala wilaya ya Shinyanga, Boniphace Chambi akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu, Linno Pius Mwageni akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Shinyanga, Nice Munissy akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa afya mkoa wa Shinyanga
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini kwenye Mkutano wa kujadili tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19 ulioandaliwa na Shirika la THPS kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC 
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini

Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini kwenye Mkutano wa kujadili tathmini na majadiliano ya hali ya utolewaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupanga mikakati ya kupambana na ugonjwa wa COVID -19 ulioandaliwa na Shirika la THPS kupitia mradi wake wa CDC/ PEPFAR Afya HATUA kwa ufadhili wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa UKIMWI (PEPFAR) kupitia Shirika la CDC 
Wadau wa afya wa mkoa wa Shinyanga wakipiga picha ya pamoja.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

TANZANIA YAKUBALIANA NA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA KUUNDA MFUKO WA KUKABILIANA NA WANYAMA WAKALI NA WAHARIBIFU


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (kulia) na Mawaziri kutoka Botswana, Zimbabwe, Zambia na Namibia, katika Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe.


Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI), Dkt. Eblate Mjingo (kulia) na Afisa Wanyamapori Mkuu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Kay Kagaruki wakifuatilia Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe.


Mke wa Rais wa Zimbabwe, Dkt. Amai Auxillia Mnangagwa akifungua rasmi Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe. Kulia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akifuatilia hotuba.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (kulia) na Mawaziri kutoka Zambia na Botswana wakiagana na Mke wa Rais wa Zimbabwe, Dkt. Amai Auxillia Mnangagwa (kushoto) baada ya kufungua rasmi Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika kwenye Hifadhi ya Hwange nchini Zimbabwe.

**************************

Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeingia makubaliano na Nchi za Kusini mwa Afrika kuunda mfuko maalum kwa kila nchi wa kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu hususan tembo.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja(Mb) katika Kongamano la Tembo wa Afrika lililofanyika leo katika Hifadhi ya Taifa Hwange nchini Zimbabwe.

“Tumekubaliana kwamba kuwepo na mfuko maalum kwa kila nchi ambao utakuwa mahsusi kwa ajili ya kudhibiti wanyama wakali na waharibifu kama tembo na pia kuwezesha wananchi wanufaike na rasilimali wanyama hao” Mhe. Masanja amefafanua.

Ameongeza kuwa mfuko huo utakapoanzishwa utawanufaisha wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi na waathirika wa wanyama hao wanaoumizwa au kuuawa kwa kuwezesha kulipwa fidia .

Mhe. Masanja amesema kuwa sambamba na hilo mkutano huo umelenga kuangalia namna jamii zinazoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi kuangalia namna zinavyoweza kushirikishwa katika kutunza rasilimali za wanyama hususan tembo.

Aidha, amesema nchi hizo zimekubaliana zisiingiliwe katika maamuzi na nchi za Magharibi kwa kuwa zenyewe ndio zinahusika katika kutunza wanyama hao na pia zinazoathirika na changamoto za wanyama hao.

Kongamano hilo limehudhuriwa na Mawaziri na Maafisa Waandamizi kutoka nchi za Botswana, Namibia, Afrika Kusini, Tanzania, Zambia na Zimbabwe.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger