Tuesday 30 November 2021

Jeshi la Uganda lafanya mashambulio ya anga dhidi ya waasi wa ADF huko DRC


Jeshi la Uganda limeanzisha mashambulizi ya pamoja ya anga na ardhini dhidi ya kundi la waasi la Allied Democratic Forces -ADF, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Msemaji wa Jeshi la Wananchi wa Uganda Brigedia Jenerali Flavia Byekwaso amethibitisha hayo kupitia akaunti yake rasmi ya twitter.

Alisema kuwa operesheni hizo zilifanywa na washirika wa Congo, dhidi ya kambi za ADF, lakini hakutoa maelezo zaidi kuhusu maeneo ambayo mashambulizi hayo yamefanywa.

Mamlaka ya Uganda inalaumu ADF, ambayo inashirikiana na Islamic State (IS) kwa msururu wa mashambulizi ya mabomu nchini humo tangu Oktoba.

Wiki mbili zilizopita, IS ilidai kuhusika na milipuko miwili ya mabomu nje kidogo ya Kituo Kikuu cha Polisi cha Kampala na karibu na Bunge.

Takriban watu watano wameuawa katika milipuko hii ya mabomu, baadhi ya mashambulizi yakiwa ya kujitoa mhanga, kwa mujibu wa Polisi wa Uganda.


Share:

NIC KUDHAMINI MBIO ZA UDSM MARATHON 2021

Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya wakionesha jezi ambayo itatumika katika mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Disemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya wakipongezanawakisaini mkataba wa makubaliano NIC kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Novemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya wakionesha mkataba uliosainiwa NIC kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Novemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya wakipongezana mara baada ya NIC kusaini mkataba wa makubaliano kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Novemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya akizungumza mara baada ya kusaini mkataba wa makubaliano na NIC kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Novemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule akizungumza mara baada ya kusaini mkataba wa makubaliano kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajia kufanyika Novemba 4,2021 Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC) wameingia mkataba wa makubaliano wa kudhamini mbio za UDSM Marathon ambazo zinatarajiwa kutimua vumbi Disemba 04, 2021 kuanzia na kumalizika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja (NIC), Bw.Yessaya Mwakifulefule amesema wamekuwa wakitoa mchango mkubwa katika sekta ya michezo kwa lengo la kukuza vipaji kwa watanzania na pia kujiepusha na magonjwa nyemelezi.

Amesema wanakila sababu ya kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa maana wamekuwa wadau wakubwa kwao katika biashara pia ndio kitivu cha elimu hapa nchini.

"Ni mara yetu ya kwanza kusapoti UDSM Marathon na haitakuwa mara ya mwisho kufanya hivyo, tutaendelea kushirikiana kama  ambavyo wamekuwa wadau wakubwa kwetu kwa muda mrefu". Amesema Bw.Mwakifulefule.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa UDSM Marathon Bi.Lulu Kaaya amesema katika mbio hizo wanatarajia kuwepo kwa mgeni rasmi ambaye atakuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais Mstaafu Dkt.Jakaya Kikwete ambaye pia atashiriki kukimbia Kilomita 5.

Amesema mbio hizo zitakuwa na ruti kubwa tatu ambazo ni ruti ya Kilomita 21.1, ruti ya kilomita 10 na ruti ya kilomita 5 ambayo ruti hiyo mgeni rasmi atashiriki 

'Lengo kuu la mbiu hizi ni kwaajili ya uchangishaji wa fedha kwaajili ya kuboresha maisha ya wanachuo. Kwasasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kipo katika ujenzi wa kituo cha wanafunzi (Student Center) inayojengwa kwenye Campus ya Mwalimu Nyerere Mlimani Jijini Dar es Salaam ambacho ni mahususi kwa kutoa mazingir mazuri ya mapumziko kwa wanafunzi". Amesema

Share:

CHUO CHA UONGOZI WA MAHAKAMA LUSHOTO CHAPONGEZWA KUWA NI KISIMA CHA UTOAJI MAFUNZO KWA WATUMISHI WA MAHAKAMA


Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani akifungua mafunzo elekezi ya siku tano yanayowashirikisha Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama ambayo yanafanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA).
 Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel akisistiza jambo alipokuwa anatoa mada katika mafunzo hayo.
Kaimu Mkuu wa Chuo, Prof. Fatihiya Massawe, ambaye pia ni Naibu Mkuu wa IJA, Mipango, Fedha na Utawala akitoa neno la ukaribisho kabla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku tano yanayowashirikisha Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama ambayo yanafanyika katika Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA). ,Mafunzo hayo yamefunguliwa leo tarehe 29 Novemba, 2021 na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani.
Sehemu ya Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama ya Tanzania wakifuatilia mada iliyokuwa inatolewa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel.
***

Na Faustine Kapama na Rosena Suka, Mahakama-Lushoto

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Siyani leo tarehe 29 Novemba, 2021 amefungua mafunzo elekezi ya siku tano kwa Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama ambapo amekisisifia Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kwa mchango mkubwa kinachofanya na kujenga taaluma bora kwa watumishi wa Mahakama na wananchi wengine kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya siku tano yanayowashirikisha viongozi hao, Mhe. Siyani amebainisha kuwa Chuo kwa kushirikiana na Kitengo cha mafunzo cha Mahakama ya Tanzania wamekuwa wakifanya kazi nzuri kwa kutoa mafunzo mbalimbali elekezi na endelevu kwa watumishi wa Mahakama ya Tanzania.

“Kama ilivyo kwa wengine, mimi nina imani kuwa chuo hiki kweli ni kitovu na kisima cha elimu bora. Kimsingi, chuo hili kina uwezo wa kujenga taaluma na kufanya leo hii tuna Wasajili ambao kesho ni Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Kwa hiyo, mimi niwapongeze sana na nifikishie salamu zangu kwa Mkuu wa Chuo,” Jaji Kiongozi alimweleza Kaimu Mkuu wa Chuo, Prof. Fatihiya Massawe, ambaye pia ni Naibu Mkuu wa IJA, Mipango, Fedha na Utawala.

Amesema kuwa mafanikio katika utoaji wa mafunzo elekezi ya awali na mafunzo endelevu ya kimahakama ni mojawapo ya matunda ya kazi nzuri yanayofanywa na IJA kwa kuzingatia Sera ya Mafunzo ya Mahakama ya mwaka 2019 ambayo inakitambua Chuo hicho kama kitovu au kisima cha utoaji mafunzo kwa watumishi wa Mahakama, lakini vile vile utafiti wenye lengo la kuongeza tija na kuboresha utendaji wa Mahakama ya Tanzania.

Jaji Kiongozi aliwakumbusha washiriki kuwa mafunzo ambayo yameandaliwa kwa ajili yao yamelenga kuwapa mbinu na nyenzo sahihi za kuweza kukabili changamoto mbalimbali za kiutendaji. “Hivyo muwe wazi kuuliza maswali na kuchangia uzoefu kila mmoja kwa namna ambayo mnaona italeta matokeo chanya katika utendaji kazi wenu. Shabaha ya kila mmoja wetu iwe ni utoaji wa haki na kuliletea maendeleo taifa letu na kutekeleza kwa vitendo Mkataba wa Huduma kwa Mteja,” amesema.

Mhe. Siyani alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha washiriki wa mafunzo hayo kuwa wapo katika kipindi cha mapinduzi ya nne ya viwanda na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amekuwa akisisitiza watumishi wa Mahakama kujinoa zaidi kwenye eneo la TEHAMA ili waweze kuendana na kasi ya mabadiliko ya kidunia hivi sasa.

Amebainisha kuwa miongoni mwa mada zitakazotolewa katika mafunzo hayo inahusu TEHAMA, hivyo ni imani yake kupitia mada hiyo washiriki wote watapata nafasi ya kujifunza juu ya nafazi zao katika usimamizi wa mashauri kwa njia za kielektroniki. Aliwaomba kutumia fursa hiyo kupata kitu cha nyongeza katika eneo hilo na kwamba kila mmoja wao awe mfuasi wa karibu wa TEHAMA kama dunia inavyowataka hivi sasa.

“Tambueni kwamba tunakoelekea hakutakuwa na nafasi kwa Msajili au Mtendaji asiye na uelewa wa TEHAMA katika Mahakama yetu. Hiyo ni dhahiri kwa sababu ninyi ni wasimamizi wa mifumo ikiwemo ya TEHEMA na bila shaka msimamizi bora ni yule anayefahamu anachokisimamia,” aliwaambia viongozi hao wa Mahakama ya Tanzania.

Awali akitoa neno la ukaribisho, Kaimu Mkuu wa Chuo, Prof. Fatihiya Massawe alisema kuwa mafunzo yanayotolewa kwa Naibu Wasajili na Watendaji wa Mahakama siyo ya kwanza kutolewa hapo Chuoni, kwani IJA imekuwa ikitoa mafunzo elekezi (Induction) kwa wahesimiwa Majaji wote wapya wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania na mafunzo ya awali na elekezi kwa Majaji wote wapya wa Mahakama Kuu ya Tanzania na Zanzibar wanapoteuliwa kwenye wadhifa huo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani pamoja na Rais wa Zanzibar.

Kwa mujibu wa Prof. Massawe, vilevile IJA imekuwa ikiendesha mafunzo elekezi kwa Mahakimu wote mara wanapoajiriwa kujiunga kwa mara ya kwanza na utumishi wa Mahakama kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutenda haki kwa wote na kwa wakati kwa kuzingatia misingi ya sheria na uadilifu.

“Hii ni mara ya kwanza mafunzo ya namna hii yametolewa kwa Naibu Wasajili na hata kwa Watendaji. Tunapenda kuipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kulisimamia hili. Tunaamini mafunzo haya elekezi ni mwanzo tu wa mafunzo endelevu ambayo washiriki hawa wataendelea kupata kama watumishi wa Mahakama. Chuo kinaahidi kitaendelea kutayarisha programu za mafunzo kulingana na uhitaji kadri watakavyoendelea kutekeleza majukumu yao na kubaini changamoto katika maeneo ya uhitaji wa mafunzo,” alisema.

Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali zitawasilishwa na waezeshaji waliobobea katika maeneo mbalimbali, akiwemo Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Wilbert Chuma, Jaji Mkuu Mstaafu ,Mohamed Chande Othman, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Mhe. January Msoffe, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati na watendaji wengine waandamizi wa Mahakama.

Miongoni mwa mada zitakazowasilishwa kwenye mafunzo hayo zinajumuisha Uongozi wa Kimkakati, Stadi za Uongozi na Uwezo wa Kukabili Mabadiliko, Wajibu wa Mahakama, Utamaduni wake na Uhusiano wake na Mihimili Mingine ya Dola, Sheria ya Uendeshaji wa Mahakama na Uboreshaji unaofanywa na Mahakama, Maadili ya Watumishi wa Umma na Maadili ya Kimahakama, Usimamizi wa fedha na Manunuzi ya Umma pamoja na Usimamizi wa Nyaraka.


Share:

REA YAVUKA MALENGO KUWAFIKIA WANANCHI VIJIJINI

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (katikati) akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Nishati leo Novemba 30,2021 Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Nishati leo Novemba 30,2021 Jijini Dar es Salaam.Kamishna Msaidizi wa umeme, Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Wizara ya Nishati leo Novemba 30,2021 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*************************

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesema imevuka malengo iliyojiwekea ya asilimia 50 katika kuwafikishia wananchi huduma ya umeme viijini ambapo hadi kufikia Juni 2021 asilimia 69.6 ya vijiji vilikuwa vimefikiwa na huduma hiyo.

Akiongea leo Novemba 30, 2021 katika ukumbi wa Wizara ya Nishati Jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu wa REA Mhandisi Hassan Seif Saidy alisema kuwa wakati Taifa linaelekea kuadhimisha miaka 60 ya uhuru, hali ya maisha ya wakazi wa vijijini imebadilika ambapo mwaka 2007 wakati Wakala inaanzishwa asilimia 2 tu ya vijiji walikuwa wamefikiwa na huduma ya umeme.

“ Kuna mafanikio mengi tuliyoyapata kutokana na usanifu, utekelezaji na usimamizi wa miradi inayotekelezwa na wakala tangu kuanziswa kwake ambapo miradi hiyo imewezesha ujenzi wa jumla ya kilomita 38,296.56 za umeme msongo wa kati na kilomita 35,253.43 za umeme msongo mdogo lakini pia kuna jumla ya wateja 716,847 waliounganishiwa umeme kwa gharama ya shilingi bilioni 2,661.93 kwa kipindi cha miaka 14 tangu kuanzishwa kwake”, alisema Mhandisi Saidy.

Mafanikio mengine yaliyopatikana ni pamoja na kutengeneza masoko kwa viwanda vya ndani vinavyozalisha vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miradi ya umeme, kuwezesha uboreshwaji wa kilimo cha umwagiliaji katika mashamba likiwemo shamba la Mtakuja Kilimanjaro na Zuzu Dodoma.

Aidha, kufunga mifumo ya umeme katika nyumba za wafanyakazi takribani 831 kwenye sekta ya afya na elimu katika mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Kagera, Pwani, Lindi, Mtwara, Ruvuma na Tabora, wakati huo huo hali ya kuboresha mazingira ya makazi vijijini ambayo imepelekea kupunguza uhamiaji wa vijana kutoka vijijini kwenda mjini kwa kuwa umeme umewamewezesha kufanya shughuli za kiuchumi kwenye makazi yao.

“ Vijana wengi sasa wanatulia vijijini kwani wameweza kuanzisha viwanda vidogo na vya kati katika juhudi za kujikwamua kiuchumi. Vitu kama vile mashine za kusaga, kuchomelea, viwanda vya uselemara pamoja na saloni za kike na kiume vinapatikana hadi vijijini siku hizi, lakini pia upatikanaji wa taarifa na burudani kwa wepesi kama vile televisheni na redio vimeongeza utulivu kwa vijana wengi hapa nchini”, aliongeza.

Kwa upande wake kamishna Msaidizi wa umeme, Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangila alisema kwamba katika kuhakikisha mtu mmoja mmoja anafaidika na uwepo wa umeme, Serikli inahamasisha wananchi wengi waone umuhimu wa kuunganishiwa umeme kwenye makazi yao ili kufaidi fursa zinazoletwa na nishati hiyo.

“ Tunaondoka kwenye hatua ya kuhakikisha umeme unafika kijijini, na hivi sasa tunawahamiasisha wakazi wa eneo husika kuhamasika kuunganishiwa umeme huo kwenye makazi yao. Mwamko ni mkubwa na tunapokea maombi mengi na hivi sasa tunahamasisha ushiriki wa sekta binafsi, taasisi za fedha katika uwekezaji wa miradi ya Nishati vijijini na tunaendelea kuhamasisha utekelezaji wa miradi ya nishati jadidifu kutoka vyanzo vya asili vinavyopatikana maeneo ya vijijini na kwenye visiwa”, alisema Mhandisi Rwebangila.

Wakala wa Nishati Vijiji ulianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Nishati vijijini Na. 8 ya mwaka 2005 na kuanza rasmi utekelezaji wa majukumu yake mwezi Oktoba, 2007 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa iliyokua Sera ya Taifa ya Nishati ya mwaka 2003.
Share:

Balozi Mulamula Akutana Na Waziri Wa Mambo Ya Nje Wa China


Na mwandishi wetu,  Dakar
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Wang Yi jijini Dakar nchini Senegal.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wameelezea kuridhishwa kwao na ushirikiano na uhusiano imara uliopo kati ya Tanzania na China na kuahidi kuendeleza uhusiano huo kwa faida ya pande zote mbili.

Waziri Mulamula amemuhakikishia Waziri Yi utayari wa Serikali  kuendelea kushirikiana na China katika kuhakikisha Tanzania inafikia maendeleo ya kweli kwa ufanisi mkubwa.

Amemshukuru Waziri huyo kutokana na ahadi iliyotolewa awali na Rais Xi Jinping wa China wakati wa ufunguzi wa mkutano wa FOCAC ya kutoa dozi bilioni moja zaidi za chanjo ya virusi vya Covid 19 kwa bara la Afrika kwani kitendo hicho kitazisaidia nchi za Afrika kutoa chanjo ya ugonjwa huo kwa watu wengi zaidi.

Pia ameishukuru China kwa kuwa soko la bidhaa za Tanzania na amemuhakikishia Waziri huyo kuwa Tanzania iko tayari kutumia fursa ya soko la China la kuuza mazao yake ya mbogamboga na matunda ili kuongeza ujazo wa biashara na hivyo kukuza uchumi.

Pia ameelezea ambavyo Tanzania inafarijika na utayari wa China katika kuisaidia kwenye miradi mbalimbali kama ile ya  ya ujenzi wa mabwawa ya kuzalisha umeme utokanao na maji kama ya Ruhuji, mradi wa uendelezaji wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji , upanuzi wa Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete  na ujenzi wa barabara kuu katika Visiwa vya  Zanzibar miradi ambayo amesema itasaidia kuinua na kukuza uchumi wa nchi.

Naye Waziri Yi kwa upande wake ameishukuru Tanzania kwa kuendelea kuiunga mkono China na kuahidi kuendelea na harakati za kusaidia nchi zinazoendelea na kuongeza kuwa China itaendelea kuisadia Tanzania katika kufanikisha miradi mbalimbali ya kimkakati na kuielezea Reli ya TAZARA kama moja ya kielelezo cha ushirikiano huo.

Amesema China itaendelea kuunga mkono jitihada za Tanzania katika kujikwamua kiuchumi na kuahidi kuendelea kutoa misaada ya fedha na  kitaalamu ili  kukamilisha miradi ya ujenzi, uanzishwaji wa kituo cha mfano kwa ajili ya kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo na kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo wadogo nchini.

Mawaziri hao wako Senegal kuhudhuria  Mkutano wa Nane wa  Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) unaofanyika nchini Senegal ulioanza tarehe 29  hadi 30 Novemba  2021.


Share:

Infinix Kuja na Toleo Jipya lenye ukubwa mara mbili zaidi ya matoleo ya awali.....Bofya Hapa Kujua Zaidi


  Je ni kweli baada ya Infinix Zero X pro sasa kampuni ya simu za mkononi Infinix kuja na simu ya kwanza kwenye toleo la NOTE kuwa na ukubwa mara mbili zaidi ya matoleo ya awali ya NOTE?
 

Hivi punde picha yenye muonekano wa simu ikiwa imeandikwa ‘THE NEXT NOTE PLAY BIG’ imeonekana kuvuja kwenye mitandao ya blog za tech lakini pia kwenye kurasa ya @infinixmobile Infinix imetupia picha inayoashiria ujio wa simu mpya kupitia post inayosema ‘FIRST 11, ARE YOU READ FOR THE FIRST ROUND? Kushabihiana kwa hizi sentensi mbili mashabiki wametafisiri kuwa huenda hii ni simu mpya aina ya NOTE 11.
 

 Simu za toleo la Infinix NOTE hukubalika zaidi kutokana na muonekana mzima wa simu hizi ambao ni imara na wenye kuvutia lakini kivutio kikubwa zaidi kwa simu hizi ni ubora wake wa camera zenye teknolojia ya AI. 

Kamera za simu za toleo la NOTE huimarishwa kwa kila toleo jipya kama ilivyokuwa kwa NOTE 8 ikiwa na camera yenye MP48 na NOTE 10 ikiwa na MP64.

 Tetesi zinadai kuwa simu hii huenda ikaja na kioo cha aina ya AMOLED na hii ni baada ya kampuni hiyo kuonyesha kuwa inawezekana kutumia teknolojia ya hali ya juu na bado simu ikiwa na bei rafiki kama ambavyo tumeliona hili kwa Zero x pro.
 

Je ni sifa gani nyengine ya kipekee kuja katika simu hii  https://bit.ly/3BHedZw?...

Tembelea;  https://www.infinixmobility.com/smartphone/note-11-pro/ kupata majibu kamili ya simu hii mpya ya Infinix NOTE 11.



Share:

DC KIBAHA AIPONGEZA TBS KUTOA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI WA MAZIWA KATIKA MKOA WA PWANI

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mhe. Sara Msafiri akifungua mafunzo kwa wajasiriamali wasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa maziwa na bidhaa za maziwa wilayani Kibaha Mkoani Pwani. 

Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe Sara Msafiri (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo kwa wadau wa maziwa na bidhaa za maziwa. 

Baadhi ya washiriki wa mafunzo kwa wadau wa maziwa na bidhaa za maziwa wilayani kibaha wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo. 

*************** 

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wametoa mafunzo ya Udhibiti ubora kwa wajasiriamali ambao niwasindikaji, wasambazaji na wauzaji wa maziwa na bidhaa za maziwa mkoani Pwani. 

Akizungumza na washiriki wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo hayo Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe. Sarah Msafiri alisema amefurahishwa sana na uamuzi wa TBS kuamua kutoa mafunzo kwa wadau wa maziwa na bidhaa za maziwa na kuichagua wilaya ya Kibaha kuwa sehemu ya kwanza kabisa kupokea mafunzo hayo na nimatarajio yake kuwa wadau hawa watatumia vizuri fursa hii ya mafunzo ambayo itapelekea kuwa na uzalishaji wa maziwa na bidhaa za maziwa zitakazokidhi matakwa ya viwango. 

Alisema anatambua nafasi walionayo wadau wa maziwa na bidhaa za maziwa katika kuchangia uchumi wa taifa hivyo basi kama watakuwa wasikivu katika mafunzo hayo mahususi kwa ajili yao ili kuwajengea uwezo na hatimaye kuwa bidhaa zitakazoweza kuuzwa ndani na nje ya nchi. 

Kwa upande wake Bw. Hamisi S. Mwanasala mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu (TBS) alisema kuwa mafunzo haya yanafanyika katika wilaya Kihaha na Bagamoyo ( Pwani) na Kilosa na Bagamoyo ( Morogoro) na yanatarajia kuwa endelevu kwa Tanzania nzima 

Alifafanua kuwa mafunzo haya yatawanufaisha washiriki kwa kutambua faida na matakwa ya viwango vya maziwa na bidhaa za maziwa, kanuni bora za usindikaji wa maziwa, kanuni bora za afya, teknolojia mbalimbali za usindikaji wa maziwa, utaratibu wa uthibitishaji ubora wa bidhaa, usajili wa majenngo ya kusindikia vyakula na kanuni bora za ufugaji. 

Bw. Mwanasala alisema mafuzo hayo yamejumuisha wakufunzi kutoka taasisi mbalimbali kama vile TBS, SIDO, Bodi ya Maziwa , Afisa Biashara, Afisa Afya na Afisa maendeleo ya jamii. 

Lengo la kutumia wakufunzi kutoka taasisi mbalimbali ni kuhakikisha kuwa mafunzo haya yanaleta tija kwa washiriki kwa kupata elimu juu ya taratibu na kanuni za uzalishaji bora wa maziwa na bidhaa za maziwa.
Share:

Chuo Cha Ardhi Morogoro Chatakiwa Kuweka Mikakati Kukamilisha Urasimishaji Makazi


Na Munir Shemweta, WANMM MOROGORO
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amekitaka Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) kujipanga na kuhakikisha kinamaliza kazi ya urasimishaji makazi katika maeneo waliyopewa kazi hiyo.

Hatua hiyo inafuatia Naibu Waziri Dkt Mabula kuelezwa na Mkuu wa Chuo cha ARIMO   Huruma Lugalla kuwa, moja ya changamoto kubwa katika zoezi zima la urasimishaji makazi maeneo mbalimbali ambayo chuo hicho imechukua kazi hiyo ni kasi ndogo ya uchangiaji gharama kutoka kwa wananchi.

‘’Mhe. Naibu Waziri uchangiaji katika zoezi la urasimishaji makazi katika maeneo mbalimbali nchini tunayoyafanyia kazi hasa hapa Morogoro ni mdogo sana pamoja na gharama ya zoezi hilo kupungua kutoka shilingi 150,000 hadi 130,000/=’’ alisema Lugala

Hata hivyo, pamoja na kuelezwa changamoto, hiyo Dkt Mabula ambaye alikuwa akizungumza na Uongozi wa Chuo cha Ardhi Morogoro tarehe 29 Novemba 2021, alikitaka chuo hicho kuhakikisha kinachukua maeneo machache ya kuyafanyia kazi badala ya kuchukua maeneo mengi aliyoyaeleza kuwa yanaweza kuwashinda kukamilisha kazi kwa wakati.

‘’ Ni vizuri mkajipanga katika zoezi zima la urasimishaji, baada ya kufanyika kosa la awali nyuma sasa msirudie tena kosa maana haitaleta picha nzuri kwa chuo na mnachotakiwa ni kujipanga na kuwa na mkakati wa kukamilisha kazi’’ alisema Dkt Mabula

Mkuu wa koa wa Morogolo Martine Shigela alishangazwa na maelezo kuwa, baadhi ya wananchi katika mkoa wake wanakuwa wazito kuchangia gharama za urasimishaji makazi holela wakati wanaweza kujenga nyumba ya milioni 20 huku akishindwa kuchangia shilingi 130,000/

‘’Yaani wananchi wanashindwa kuchangia gharama za urasimishaji wakati wanajenga nyumba kwa gharama kubwa kama milioni 10 mpaka 20? Hii haina afya kabisa’’alisema Shughela.

Awali Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro Huruma Lugalla alimueleza Naibu Waziri Dkt Mabula kuwa Chuo chake kinaendelea na utekelezaji miradi ya urasimishaji makazi katika mitaa 61 nchini kwa kushirikiana na halamashauri na wananchi wanaomiliki ardhi ya makazi yaliyoendelezwa kiholela.

Kwa mujibu wa Lugalla, jumla ya viwanja 30,188 vimeidhinishwa kufanyiwa kazi ya urasimishaji makazi, iwanja 129, 761 vimetambuliwa huku michoro 218 ikisanifiwa  na takriban Shilingi Bilioni 2.553 ikiwa imetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Aidha, Mkuu huyo wa Chuo cha ARIMO aliwasilisha ombi la chuo chake kutaka kusaidiwa uendelezaji eneo la ekari 33 lililoko Mlimakola Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya kupanua wigo wa mafunzo, miundombinu sambamba na kuongeza udahili wa wanafunzi.

Kufuatia ombi hilo, Mkuu wa mkoa wa Morogoro Martine Shigela alisema, ni vyema taasisi za umma zinapoomba msaada wa uendelezaji maeneo yake zikafikiriwa kusaidiwa na kuongeza kuwa, mkoa wake uko tayari kusaidia pale utakapoona mipango ya chuo kuhusu uendelezaji eneo hilo.

Katika hatua nyingine Mkuu wa mkoa wa Morogoro Martine Shighela alilitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kufikiria namna ya kuwekeza miradi katika mkoa huo ukiwemo ule wa eneo la maduka (MALL) kwa lengo la kurahisisha upatikanani huduma.

Akizungumza na Menijementi ya NHC iliyomtembelea ofisini kwake wakati wa kikao chake na Jukwaa la Wahariri Tanzania mkoani Morogoro kilichofunguliwa na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, Shighela alisema, kwa sasa mkoa huo hauna maduka (Mall) kwa ajili ya kuwaewezesha wananchi wa mkoa huo kupata huduma eneo moja kama ilivyo Dar es Salaam wakati mkoa huo unaendelea unapanuka.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Numba la Taifa Dkt Maulid Banyani alimhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kulifanyia kazi suala hilo na katika kuhakikisha utekelezaji unafanyika haraka Shigela na timu ya NHC walitembelea eneo la Kingo Sabasaba katika manispaa ya  Morogoro kuona namna ya kufanya uwekezaji kwenye eneo hilo.


Share:

Technical Advisor at Good Neighbors

Technical Advisor (TA)    Terms of Reference (ToR) for Technical Advisor of  KOICA – Enhancing Quality of Secondary School Education through a Holistic Approach in Zanzibar, Tanzania (EQSSE-Z) Project Description  Enhancing the Quality of Secondary School Education in Zanzibar (EQSSE-Z) project is a fouryear project (2021-2024), with the expected outcomes of: Better teaching and learning […]

This post Technical Advisor at Good Neighbors has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Business Planning and Analytics Manager at NBC

Business Planning and Analytics Manager   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services.   Job Summary   This role requires the holder to work closely with the Head of CIB & BB […]

This post Business Planning and Analytics Manager at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

SEKTA ZA MIFUGO SMT NA SMZ ZAWAWEKEA MIKAKATI YA MAENDELEO WAFUGAJI WA PANDE ZOTE MBILI



Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Amosy Zephania akifungua rasmi kikao cha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa Sekta za Mifugo kilichofanyika Chakechake Pemba ambapo kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha wataalamu . Kushoto kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bi. Maryam Juma Sadallah. 


Baadhi ya wataalam walioshiriki kikao cha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa Sekta za Mifugo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo (Mifugo) Bw. Amosy Zephania (hayupo pichani) wakati akifungua kikao hicho kilichifanyika Chakechake Pemba 


Baadhi ya wataalam walioshiriki kikao cha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa Sekta za Mifugo wakimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo (Mifugo) Bw. Amosy Zephania (hayupo pichani) wakati akifungua kikao hicho kilichifanyika Chakechake Pemba. 


Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Amosy Zephania (wa pili kulia) akieleza dhamira ya ushirikiano wa Serikali mbili (SMT na SMZ) kuwa ni kutatua changamoto za wafugaji nchini kwa mfugaji bora wa ng’ombe Bwana Ahmed Shabaan Salum (kulia kwake)!walipomtembelea shambani kwake eneo la Kinyasini Wilaya ya Wete Pemba. 


Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw. Amosy Zephania (kulia) akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo wa Zanzibar Bi. Maryam Juma Sadallah wakiongea na mfugaji (hayupo pichani )mara baada ya kukagua banda la kufugia ng’ombe la Bwana Ahmed Shabaan walipomtembelea shambani kwake eneo la Kinyasini Wilaya ya Wete Pemba. 


Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo, na Ugani Dkt. Angello Mwilawa (aliyeshika majani) na baadhi ya wataalam walioshiriki kikao cha ushirikiano kati ya Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kwa Sekta za Mifugo wakikagua malisho kwa mfugaji bora wa ng’ombe Bwana Ahmed Shabaan Salum walipomtembelea shambani kwake eneo la Kinyasini Wilaya ya Wete Pemba. 

.......................................................... 

Sekta za Mifugo za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kupitia makatibu wake wakuu wamekutana na kuweka mikakati ya kuendeleza sekta hizo kwa wafugaji wa pande mbili za Muungano ambapo maazimio saba yameridhiwa ikiwa ni hatua ya kufikia malengo tarajiwa. 

Maazimio hayo yamefikiwa Wilayani Chakechake Pemba, kwenye kikao kilichowakutanisha makatibu wakuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT)wa Sekta ya Mifugo Bw. Amosy Zephania na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) Bi. Maryam Juma Sadallah. Akifungua rasmi kikao hicho Kaimu Katibu Mkuu Sekta ya Mifugo (SMT) Bw. Amosy Zephania, aliishukuru Sekta ya Mifugo (SMZ) kwa maandalizi mazuri ya kikao hicho ambacho kilitanguliwa na kikao cha siku moja cha wataalamu wa sekta hizo kutoka pande mbili za Muungano na kusisitiza umuhimu wa vikao hivyo “vikao hivi tuvipe umuhimu wa kipekee ili tuweze kufanya tahmini ya maendeleo ya sekta zetu”. Alisisitiza Kaimu Katibu Mkuu. 

Kaimu Katibu Mkuu pia aliongeza kuwa kwa kuendelea kushirikiana kupitia vikao na utekelezaji wa maazimio yanayoridhiwa na pande zote mbili, sekta za Mifugo zitapiga hatua na kunufaisha wananchi kiuchumi kulingana na idadi kubwa ya mifugo iliyopo nchini. 

Bw. Zephania alisisitiza kuwa ni vyema wataalam wa sekta za Mifugo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuendelea kushirikiana kwa karibu zaidi kiutendaji kwa ajili ya kubadilishana uzoefu ili kupunguza au kuondoa kabisa kero na changamoto zinazowakabili wafugaji wa Tanzania. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Maryam Juma Sadallah akimkaribisha Kaimu Katibu Mkuu Sekta ya Mifugo (SMT) Bw. Amosy Zephania, alishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) kwa kuendelea kushirikiana nao ikiwa ni pamoja na kutimiza makubaliano ya kukutana kwenye vikao kazi kama walivyokubaliana. 

Aidha Bi. Maryam aliipongeza timu ya wataalamu wa Sekta za Mifugo kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa utekelezaji wa kiwango cha hali ya juu wa maazimio ya kikao kilichofanyika Juni 4, 2021 kwenye ukumbi wa TVLA jijini Dar Es Salaam, “ Nawapongezeni wataalamu wetu kwa kazi nzuri mliyoifanya ingawa sio kwa asilimia mia moja lakini mmejitahidi sana”. Alisema Bi. Maryam. 

Aidha aliwataka wataalamu kushirikishana kwenye mipango kazi yao ili iwe rahisi kusaidiana pia kutumia fursa zinazopatikana kwa faida ya pande mbili za Muungano akitolea mfano wa baadhi ya miradi ya miundombinu ya mifugo inayotarajiwa kujengwa Zanzibar kwa mkopo wa dola mil. 60 kutoka nchi ya Hungary. 

Naye Afisa Mdhamini wa Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Pemba, Bw. Hakim Vuai Shein amepongeza timu ya wataalamu kwa utekelezaji wa maazimio mbalimbali na kusisitiza kuwa matarajio ya wadau wa sekta ni kuona changamoto zao zinafikia mwisho. Baadhi ya maazimio yaliyofikiwa kwenye kikao hicho cha ushirikiano wa Sekta za Mifugo za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni pamoja na kuwepo kwa makubaliano maalum kati ya Taasisi za Utafiti na Mafunzo. 

Azimio lingine ni uzalishaji wa mifugo hususan mitamba ya ng’ombe chotara ambapo SMT itatoa mbegu za mifugo dozi 1,000 kwa ajili ya kiwezesha uhimilishaji kwa wafugaji wa Zanzibar. 

Kufanya uchambuzi wa mnyororo wa gharama za uzalishaji wa mifugo na mazao yake na kuandaa maandiko ya miradi ya pamoja pia ni miongoni mwa maazimio yaliyoridhiwa na makatibu wakuu wa Sekta za Mifugo wa SMT na SMZ.
Share:

IP & VAS Networks at Vodacom

  Specialist: IP & VAS Networks   At Vodacom, we’re working hard to build a better future. A more connected, inclusive and sustainable world. As a dynamic global community, it’s our human spirit, together with technology, that empowers us to achieve this.   We challenge and innovate in order to connect people, businesses, and communities […]

This post IP & VAS Networks at Vodacom has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Key Account Manager-VGE at Vodacom

  Key Account Manager-VGE   At Vodacom, we’re working hard to build a better future. A more connected, inclusive and sustainable world. As a dynamic global community, it’s our human spirit, together with technology, that empowers us to achieve this.   We challenge and innovate in order to connect people, businesses, and communities across the […]

This post Key Account Manager-VGE at Vodacom has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Waziri Mchengerwa Awataka Watumishi Wa Umma Kuacha Kiburi Na Majivuno Wanapotoa Huduma Kwa Wananchi


 Na. Veronica E. Mwafisi-Arusha
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amewataka Watumishi wa Umma nchini kuacha kiburi na majivuno pindi wanapotoa huduma kwa wananchi kwani mishahara wanayolipwa na Serikali inatokana na kodi za wananchi.

Waziri Mchengerwa ametoa wito huo kwa Watumishi wa Umma nchini, wakati akifungua Semina ya Viongozi wa Matawi ya TUGHE na Waajiri inayofanyika jijini Arusha.

Mhe. Mchengerwa amesema, Watumishi wa Umma wanapaswa kuwahudumia wananchi ipasavyo kama ambavyo wao wanatamani kuhudumiwa na Serikali.

“Baadhi yetu, kuna vitendo tunavifanya ambavyo haviwapendezi wananchi tunapowahudumia, hivyo tuhakikishe tunatoa huduma bora kama ambavyo sisi tunavyoitaka Serikali ituhudumie,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Akihimiza Watumishi wa Umma kutekeleza wajibu wao pasipo kushurutishwa, Mhe. Mchengerwa amenukuu maneno ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyowahi kusema kwamba, si jambo jema kwa mtu mzima kuwekewa mnyampara ili aweze kumfunza nidhamu ya utendaji kazi hivyo, Watumishi wanapaswa kutimiza wajibu wao bila kushurutishwa.

Akisisitiza dhana ya kujisimamia kiutendaji, Waziri Mchengerwa amemnukuu Rais wa Awamu wa Sita, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye aliwahi kusema kuwa, hajaumbwa kufokafoka, ataangalia utendaji kazi wa kila mtumishi kwa nafasi aliyonayo kwani wote ni watu wazima ambao wanatambua mazuri na mabaya, na ikitokea wakifanya mabaya basi inakuwa ni kwa makusudi hivyo yeye ataongea kwa kalamu.

Kwa Muktadha huo, Mhe. Mchengerwa amesema kuwa, fikra na maono ya Rais wa Awamu ya Sita, Mhe. Samia Suluhu Hassan ndio fikra na maono ya Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hivyo Watumishi wa Umma tunapaswa kuishi kwa vitendo fikra na maono hayo ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Katika kuunga mkono fikra na maono ya viongozi hao kuhusu uwajibikaji, Mhe. Mchengerwa amewataka Watumishi wote wa Umma nchini kuhakikisha kila mmoja kwa nafasi aliyonayo anafanya kazi kwa bidii na weledi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

Awali, akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mhe. Mchengerwa kufungua Semina ya Viongozi wa Matawi ya TUGHE na Waajiri, Mwenyekiti wa TUGHE taifa Bw. Joel Kaminyoge amempongeza Waziri Mchengerwa kwa utendaji kazi mzuri hususani katika kusimamia masilahi ya Watumishi wa Umma nchini.

Bw. Kaminyoge amesema kuwa, utendaji kazi wa Waziri Mchengerwa unadhihirisha kuwa, katika historia ya Utumishi wa Umma amekuwa ni miongoni mwa Mawaziri bora kabisa waliowahi kutokea kushika wadhifa huo wa kumsaidia Mhe. Rais kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Semina hiyo yenye lengo la kuwajengea uwezo kiutendaji viongozi hao wa TUGHE na Waajiri inafanyika kwa siku tano kuanzia tarehe 29 Novemba, 2021 hadi tarehe 03 Disemba, 2021



Share:

Senior Business Analyst at CRDB

Senior Business Analyst   JOB REPORTING TO:  Senior Manager Business Performance & Revenue Assurance JOB PURPOSE Responsible to ensure that revenue collection mechanisms are reviewed and monitored to help businesses identify system loopholes, errors, transaction errors, process weaknesses that could affect income collected from a transaction.  To put in place systems and processes to minimize […]

This post Senior Business Analyst at CRDB has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Zonal Relationship Manager; Channels Performance at CRDB

Zonal Relationship Manager; Channels Performance   Job Reporting To: Zonal Business Manager (Administratively), Manager Agents Performance (Functionally) Job Purpose: To grow and retain a portfolio of Bank Channel’s Business including management of performance for agents, Merchant and ATMs as part of channel Distribution of the zone through relationships by performing both a pro- and re-active […]

This post Zonal Relationship Manager; Channels Performance at CRDB has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Mashirika Ya Kigeni Yazidi Kuvutiwa Kuwekeza Katika Sekta Ya Nishati Tanzania


 Na Dorina G. Makaya - Dar-es-Salaam.
Idadi ya mashirika ya kigeni yanayovutiwa kuwekeza katika sekta ya Nishati nchini yameendelea kuongezeka ikiwemo katika sekta ndogo ya umeme na nishati Jadidifu.

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba, tarehe 29 Novemba, 2021, amekutana na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mitsubishi iliyopo jijini Dar--es-Salaam, Kenji Nishizaki   na kujadili masuala ya ushirikiano wa kisekta na fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini Tanzania.

Miongoni mwa masuala waliyoyazungumzia katika mkutano huo, uliofanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara ya Nishati, ni pamoja na  kupanua wigo wa  biashara kwa kutazama fursa zilizopo za uwekezaji katika maeneo ya sekta ndogo  ya umeme, mafuta na gesi asilia pamoja na ushirikiano wa kisekta kwa ujumla na Serikali ya Tanzania

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba, amewakaribisha Kampuni ya Mitsubishi kwa ajili ya kuwekeza hapa nchini na ameelekeza mashirika ya TPDC na TANESCO kutazama kwa upana zaidi wigo huo wa uwekezaji ambao Mitsubishi wanataka kuwekeza.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger