Monday 29 November 2021

RAIS SAMIA NA RAIS MUSEVEN WAZINDUA SHULE YA 'MUSEVENI PRE & PRIMARY SCHOOL' CHATO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwa pamoja wakikata utepe kuzindua rasmi Shule ya Awali na Msingi Museveni Pre & Primary School iliyojengwa kwa msaada wa Rais Yoweri Museveni Wilayani Chato Mkoani Geita leo tarehe 29 Novemba 2021. Picha na Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwa pamoja wakiondoa kitambaa kuzindua rasmi Shule ya Awali na Msingi Museveni Pre & Primary School iliyojengwa kwa msaada wa Rais Yoweri Museveni Wilayani Chato Mkoani Geita leo tarehe 29 Novemba 2021.
Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akimkabidhi mfano wa funguo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kama ishara ya makabidhiano ya Shule hiyo ya Awali mara baada ya uzinduzi uliofanyika katika Shule hiyo ya Museveni Pre & Primary School Chato mkoani Geita leo tarehe 29
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakikagua baadhi ya majengo ya Shule hiyo ya Awali na Msingi iliyojengwa kwa msaada wa Rais Yoweri Museveni Chato mkoani Geita leo tarehe 29 Novemba 2021 mara baada ya kuizindua rasmi Shule hiyo.
Share:

Ngoma Mpya kali kinoma : NG'WANA SAMAKA - MCHEPUKO


Nakualika kusikiliza wimbo mpya wa Ng'wana Samaka unaitwa.. Mchepuko..
Share:

Head of Risk at KCB Bank Tanzania Limited

Head of Risk Reference Number: IRC11770 Job Summary: To provide overall strategic leadership for the Risk Function for KCBT. In addition, the role will be responsible for developing and implementing risk management initiatives and activities to ensure efficiencies in bank operations. Key Responsibilities:   Establish & Maintain risk management strategies, principles, framework and policies and […]

This post Head of Risk at KCB Bank Tanzania Limited has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

WATU SABA WAFARIKI , 24 HOI KWA KULA KASA ZANZIBAR


Watu saba wamefariki dunia na wengine 24 wakipigania maisha yao katika hospitali moja kisiwani Pemba baada ya kula nyama ya kasa.

Kimsingi,kasa wa baharini huliwa na watu wengi katika ufukwe wa bahari lakini inasadikiwa kuwa ule ambao wakazi wa Msuka Taponi Wilaya ya Micheweni Pemba walikula ulikuwa na sumu.

Kamanda wa Polisi Pemba Kaskazini, Juma Sadi amepiga marufuku ulaji wa kasa baada ya kubainika kuwa nyama yake ina sumu,The Citizen imeripoti.

Alisema watatu walikufa Ijumaa , wawili walikufa Jumamosi na vifo vingine viwili vilithibitishwa Jumapili,Novemba 28.

Haikuwa wazi ikiwa wote saba walikuwa wa familia moja au vinginevyo.

Katika ujumbe wake wa Twitter, Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi alituma salamu za rambirambi kwa familia za wafiwa na kuwataka wawe na subra.

Social embed from twitter


Share:

WATU 6 WA FAMILIA MOJA WAPOFUKA GHAFLA KATIKA MAZINGIRA TATANISHI


Wakazi wa kijiji cha Thim Jope, Uriri, kaunti ya Migori nchini Kenya wamepigwa na bumbuwazi baada ya watu wa familia moja kupofuka katika hali tatanishi.

Katika kisa kisichokuwa cha kawaida, Hellen Achieng' na wanawe wanne wenye umri wa kati ya miaka saba na 24 walipofuka ghafla kabla ya kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Migori kwa matibabu.

George Omondi aliambia Nation kuwa mpwa wake mwenye umri wa miaka 12, ambaye alikuwa anaishi na familia hiyo, alianza kutetemeka baada ya kupoteza uwezo wa kuona na kisha baadaye alizirai na kufariki dunia.

Omondi aliongezea kuwa mnamo Ijumaa, Novemba 26,2021 mke wake na wanae watano walikwenda kulala wakiwa buheri wa siha.

 Hata hivyo, asubuhi ya siku iliyofuata, walianza kulalamika kuwa wamepoteza uwezo wa kuona.

Akithibitisha kisa hicho, Chifu Msaidizi wa kata ya Thim Jope, Kerry Otieno alisema mwili wa mvulana huyo ulipelekwa katika makafani ya Hospitali ya Misheni ya Ombo.

Aliongeza kuwa bado hawajapata chanzo cha masaibu yanayokumba familia yake. Kabla ya kukimbizwa hospitalini, familia hiyo ilikuwa imewaalika viongozi wa kidini.

 Madaktari nao hospitalini wanajaribu kutafuta chanzo cha upofu wa familia hiyo.

Chanzo - Tuko News
Share:

ROSE MANUMBA TRUST YAWAPA NEEMA VIJANA 11 KUTOKA VETA


TAASISI ya Rose Manumba Trust kwa kushirikiana na Give A Future Foundation kupitia program ya 'Jiajiri' wamekabidhi vifaa vya ufundi kwa wanafunzi kumi na moja waliopata mafunzo kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafuzo ya Ufundi stadi VETA Chang'mbe, Donbosco na St. Gasper ikiwa ni sehemu ya kuwasaidia kujikwamua kiuchumi, kujiajiri pamoja na kushirikiana na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kutatua changamoto ya ajira nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo kwa vijana hao wanaosomea fani za ufundi cherehani, ufundi umeme, mapishi na urembo Katibu tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala Charangwa Seleman amesema Serikali inatambua juhudi za wadau katika kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto ya ajira hasa kwa kundi la vijana.

''Mkatumie vifaa hivi vya msingi kwa kufanya kazi na kutengeneza ajira, epukeni makundi Serikali na wadau kama Rose Manumba Trust tupo pamoja katika kuhakikisha tunapambana kutatua changamoto ya ajira...Pia mtumie mafunzo ya ujasiriamali mliyopewa kwa ufanisi ili kuwapa moyo wadau hawa na ninaamini mtawainua vijana wengi zaidi kupitia fursa hii mliyoipata.'' Amesema.
Aidha amewataka vijana hao kutumia fursa za mkopo zinazotolewa katika Halmashauri zote nchini kwa makundi ya wanawake ambao hupata asilimia nne, wanaume asilimia nne na wenye ulemavu asilimia mbili.

''Vijana tumieni fursa hii mmepata vifaa msibweteke, pia kuna fursa za mkopo unaotolewa bila riba katika Halmashauri, kwa vifaa mlivyopata mnaweza kuwa na kikundi mkaandika mpango mkakati wa biashara na kuuwasilisha katika Halmashauri zenu,,,kwa wale wanaotoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilala nitawasaidia, jitihada za Rose Manumba Trust na Give A Future Foundation tuziendeleza kwa kuwapa moyo ili waweze kuwafikia vijana wengi zaidi.'' Amesema.

Pia amewataka wadau na mashirika mengine ya kitaifa na kimataifa kuunga mkono juhudi hizo kwa kusaidia kundi la vijana hasa katika changamoto ya ajira inayowakabili.
Awali Mkurugenzi wa taasisi ya Rose Manumba Trust, Veronica Mwamunyange amesema taasisi hiyo imelenga kusaidia vijana, wanawake na wenye ulemavu katika kujikwamua kiuchumi na katika sekta za elimu na afya kwa wanawake na vijana.

Amesema wamekuwa na miradi mbalimbali ikiwemo Msichana Club maalum kwa vijana wa kike na programu ya 'Jiajiri' ambayo imewalenga vijana wanaosoma VETA kwa kupatiwa vifaa vitakavyowasaidia mara baada ya kuhitimu masomo yao.

''Taasisi hii iliona changamoto kwa vijana wanaosoma Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kukosa vifaa vya kazi pindi wanapomaliza masomo yao, tukaona ni vyema kufanya mchakato wa kuwasaidia vijana hawa kupitia shindano ambalo lilishirikisha vijana 150 wanasoma kozi zenye uhitaji ambao walijaza fomu na vijana 11 pekee waliingia katika kinyang'anyiro na walipewa mafunzo ya ujasriamali na wapo tayari kuanza biashara mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo.''
Veronica amesema, wataangalia maendeleo ya vjana hao mara baada ya kukabidhiiwa vifaa hivyo na kuwataka vijana hao kuendeleza ujuzi waliupata katika kujikwamua kiuchumi na kuwasaidia wengine.

''Muasis ya taasisi hii Rose Manumba alitamani kuwa nanyi hapa leo lakini amebanwa naa majukumu ya kiserikali ila amefurahi kuwa sehemu ya mafanikio ya vijana hawa, anawatakia kila la heri katika ujenzi wa taifa ambao kasi yake katika kupambana na changamoto ya ajira inayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan inadhihirika wazi.'' Amesema.

Vilevile mshauri wa taasisi hiyo Jestina Kimesa amesema changamoto kubwa inayokwamisha programu za aina hiyo ni utekeleezaji wa miradi husika na kuwataka vijana hao kubadilisha dhana hiyo na kuwapa moyo wanaowasaidia kwa kufaanya kazi kwa bidii na kuwasaidia vijana wengine.

Mwakilishi wa wanufaika hao Issa Mohammed anayesomea mapishi VETA Chang'ombe ameishukuru taasisi ya Rose Manumba Trust kwa kuwapa nyenzo muhimu ambazo zitawasaidia katika kujikwamua kiuchumi na baadaye kuweza kuwasaidia vijana wengine.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Charangwa Seleman (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Ayenda Ezekiel (kushoto) ambaye ni mmoja wa wanafunzi wa Mamlaka ya Elimu na Mafuzo ya Ufundi stadi (VETA) ya Chang'mbe walionufaika na vifaa vya ufundi kupitia mradi Jiajiri wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Rose Manumba Trust kwa kushirikiana na Give A Future Foundation, katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya ufundi kwa wanafunzi kumi na moja waliopata mafunzo kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafuzo ya Ufundi stadi (VETA) ya Chang'mbe, Donbosco na St. Gasper za Dar es salaam, ikiwa ni sehemu ya kuwasaidia kujikwamua kiuchumi na kujiajiri, iliyofanyika jana kwenye Hoteli ya Kebbs, Dar es salaam. Wengine pichani ni Mkurugenzi wa taasisi ya Rose Manumba Trust, Veronica Mwamunyange (wa pili kulia) pamoja na Mlezi wa taasisi ya Rose Manumba Trust, Jestina Kimbesa.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Charangwa Seleman akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi kumi na moja waliopata vifaa vya ufundi kupitia mradi Jiajiri wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Rose Manumba Trust kwa kushirikiana na Give A Future Foundation, katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya ufundi kwa wanafunzi kumi na moja waliopata mafunzo kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafuzo ya Ufundi stadi (VETA) ya Chang'mbe, Donbosco na St. Gasper za Dar es Salaam.

Share:

HR Business Partner at KCB Bank Tanzania Limited

HR Business Partner Reference Number: IRC11668 Job Summary: Leads and manages the organization’s HR strategies and agenda in partnership with line management. Leads the change management projects and manages the HR related internal and external communication. Shares the responsibility for the delivery of the organization’s strategies and plans. Identifies key, high performing and high potential […]

This post HR Business Partner at KCB Bank Tanzania Limited has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Regional Programme Managers 6 Job Opportunities at Deloitte

Regional Program Managers (Ref: C3HP/RPM/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government of Tanzania’s (GOT) […]

This post Regional Programme Managers 6 Job Opportunities at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Monitoring, Evaluation & Learning Officers 18 Job Opportunities at Deloitte

Monitoring, Evaluation & Learning Officers 18 Posts (Ref: C3HP/MELO/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the […]

This post Monitoring, Evaluation & Learning Officers 18 Job Opportunities at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Assistant Accountants 8 Job Opportunities at Deloitte

Assistant Accountants   Assistant Accountant (Ref: C3HP/AA/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government […]

This post Assistant Accountants 8 Job Opportunities at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Drivers 28 Job Opportunities at Deloitte

Drivers 28 positions   Driver (Ref: C3HP/DRV/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government of […]

This post Drivers 28 Job Opportunities at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Tamko Kuhusu Hatua Ya Kujikinga Dhidi Ya Tishio La Wimbi La Nne La Maambukizi Ya Ugonjwa Wa Uviko-19 Nchini

Serikali ya Tanzania imesema kuna tishio la kutokea wimbi la nne la ugonjwa wa Uviko-19 kutokana na viashiria vitatu vilivyotajwa kuwa ni pamoja na ongezeko la visa vipya na aina mpya ya virusi  katika baadhi ya nchi duniani.

Hayo yamesemwa Jumamosi, Novemba 27, 2021 na Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Aifelo Sichwale wakati akitoa tamko kuhusu hatua za kujikinga dhidi ya wimbi la nne la maambukizi ya ugonjwa wa huo.

Kiashiria kingine kilichotajwa ni pamoja na kuwepo kwa wasafiri wengi ndani na nje ya nchi katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka pamoja na asilimia ndogo ya watu waliochanja nchini.

“Kutokana na hali hii hatuna budi kuendelea kuchukua hatua sahihi za kujikinga dhidi ya ugonjwa huu, Wizara inasisitiza kuendelea kuchukua tahadhari ili kujikinga ikiwemo kuendelea kujitokeza kupata chanjo,” amesema.

Dk Sichwale amesema chanjo zimeonyesha ufanisi mkubwa dhidi ya madhara ya Uviko- 19. Amewataka wananchi kuendelea na uvaaji wa barakoa, kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni au kutumia vipukusi, kufanya mazoezi na kutumia tiba asili zinazoshauriwa na wataalamu.

Kuendelea kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, kila sekta kuendelea kutekeleza miongozo ya kujikinga, kuimarisha uchunguzi wa wasafiri katika viwanja vya ndege, bandari na mipaka ya nchi kavu na kufanya ufuatiliaji wa nchi zenye ongezeko la wagonjwa na kuchukua hatua stahiki



Share:

Rais Samia na Rais Museven wa Uganda washiriki kufunga Kongamano la Wafanyabiashara kati ya Tanzania na Uganda Ikulu jijini Dar


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, wameshiriki Kongamano la Wafanyabishara wa Tanzania na Uganda, lililofanyika jana tarehe 28 Novemba, 2021 katika viwanja vya Ikulu                Jijini Dar es Salaam.

Kongamano hilo lililojikita katika kuzungumzia fursa za biashara ya mafuta na gesi hususan maendeleo ya mradi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga nchini Tanzania.

Aidha, Mhe. Rais Samia amemshukuru Rais wa Uganda Mhe. Museveni kwa jitihada zake zilizowezesha kupatikana kwa mafanikio kuelekea utekelezaji wa mradi huo wa ushirikiano tangu alipofanya ziara ya mwisho Jijini Dar es Salaam tarehe 20 Mei, 2020.

Mhe. Rais amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Tanzania na Uganda umezidi kuimarika hata katika kipindi hiki cha changamoto ya UVIKO 19 hivyo ni ishara nzuri katika kutatua changamoto zinazojitokeza kwenye utekelezaji wa miradi ya ushirikiano.

Mhe. Rais Samia amesema kuwa Serikali ya Uganda imeiunga mkono Serikali ya Tanzania katika mambo muhimu ambayo yamesaidia katika maendeleo ya mradi wa Bomba la kusafirisha mafuta. Kufuatia hatua hiyo, Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa wataalamu wa Tanzania na Uganda kuangalia masuala muhimu yatakayowezesha kuleta ushirikiano katika sekta ya mradi huo.

Kwa upande mwingine, Mhe. Rais Samia amewataka wadau kutoka Sekta binafsi kutumia fursa zinazopatikana kutokana na utekelezaji wa mradi huo kwa kuwa Serikali za nchi hizo mbili zinafanya jitihada kuhakikisha Sekta hiyo na jamii za nchi zote mbili zinanufaika na mradi huo.

Mhe.Rais Samia amewaeleza wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Uganda kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Taasisi yake ya Utafiti na Maendeleo ya Viwanda (TIRDO) ina uwezo wa kutoa huduma za kibobezi ikiwemo kufanya ukaguzi katika mabomba ya kuhifadhi na kusafisha mafuta na gesi.

Mhe. Rais Samia amehimiza nchi zote mbili kuendelea kuvutia uwekezaji katika nyanja mbalimbali ikiwemo viwanda vinavyotumia malighafi za ndani hususan katika sekta za kilimo na maliasili. Hivyo, Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa wawekezaji wa Tanzania kuwekeza Uganda na Uganda kuwekeza nchini Tanzania.

Kwa upande wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Museveni pamoja na mambo mengine,  amesema kuwa mradi wa Bomba la Mafuta ghafi utakuwa na manufaa kwa pande zote mbili  na kusaidia kutoa  ajira kwa wananchi wa nchi hizo.

  

Jaffar Haniu

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.



Share:

Tanzania Yashiriki Mkutano Jukwaa La Ushirikiano Kati Ya China Na Afrika


Na mwandishi wetu, Dakar

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashiriki Mkutano wa Nane wa Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) ulioanza tarehe 28 hadi 30 Novemba 2021 jijini Dakar nchini Senegal.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) ataongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo.

Katika Ufunguzi wa Mkutano wa Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika, Marais wa Nchi Wenyeviti Wenza wa Mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Senegal Mhe. Macky Sall na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Xi Jinping watahutubia Mkutano huo.

Mkutano huo wa Mawaziri wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika unatanguliwa na Mkutano wa Maafisa Waandamizi unaoanza leo tarehe 28 Novemba 2021 hapa Jijini Dakar, Senegal ambapo Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mpango Zanzibar Dkt. Juma Akil na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bibi Amina Shaaban watashiriki.

Mkutano huo utakaowashirikisha viongozi na wawakilishi kutoka nchi za Bara la Afrika na Jamhuri ya Watu wa China pamoja na mambo mengine utajikita katika majadiliano ya maeneo yafuatayo:- Ushirikiano wa Kisiasa, Ushirikiano wa Kiuchumi, Ushirikiano wa Maendeleo ya Kijamii, Utamaduni na Ushirikiano kati ya Watu na Watu, Ushirikiano wa Ulinzi na Usalama, Mapinduzi ya Kijani, Ubadilishanaji Uzoefu katika masuala ya Uongozi Bora pamoja na Maendeleo ya Kitaasisi ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika.


Share:

Administrative Officer at Deloitte

Administrative Officer (Ref: C3HP/AO/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government of Tanzania’s (GOT) Ministry […]

This post Administrative Officer at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Database Manager at Deloitte

Database Manager (Ref: C3HP/DBM/12-21)   Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government of Tanzania’s (GOT) […]

This post Database Manager at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Executive Assistant at Deloitte

Executive Assistant (Ref: C3HP/EA/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the Government of Tanzania’s (GOT) Ministry […]

This post Executive Assistant at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger