Thursday 29 April 2021

Tazama Picha : KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA


Wajumbe Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM, wakiwa wamesimama kwa muda wa Dakika moja kwa ajili ya kumkumbuka aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, wakati wa Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM iliyokuta leo April 29,2021 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Jijini Dodoma, kwa ajili ya kuandaa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM unaotarajiwa kufanyika kesho.



Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM (Bara) Rodrick Mpogolo akizungumza katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM (NEC) kilichofanyika leo tarehe 29 Aprili, 2021 katika Makao Makuu cha Chama, White House Jijini Dodoma. Kikao hicho kimehudhuriwa na Mjumbe wa NEC Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Dkt. Ali Mohamed Shein pamoja na Makamu Mwenyekiti CCM Tanzania Bara Philip Mangula


Mjumbe wa NEC Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa katika kikao hicho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM (NEC) kilichofanyika leo tarehe 29 Aprili, 2021 katika Makao Makuu cha Chama White House Jijini Dodoma.


Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa katika kikao hicho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM (NEC) kilichofanyika leo tarehe 29 Aprili, 2021 katika Makao Makuu cha Chama White House Jijini Dodoma.


Wajumbe mbalimbali wa NEC wakiwa katika Kikao hicho cha NEC kilichofanyika leo tarehe 29 Aprili, 2021 katika Makao Makuu cha Chama White House Jijini Dodoma. PICHA NA IKULU


Wajumbe Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM, wakiwa kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM iliyokuta leo April 29,2021 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Jijini Dodoma, kwa ajili ya kuandaa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM unaotarajiwa kufanyika kesho.


Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid akitii jambo kutoka kwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM iliyokuta leo April 29,2021 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Jijini Dodoma, kwa ajili ya kuandaa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM unaotarajiwa kufanyika kesho.


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, akiagana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman, mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM iliyokuta leo April 29,2021 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Jijini Dodoma, kwa ajili ya kuandaa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM unaotarajiwa kufanyika kesho.
Share:

TAKUKURU MARA YAOKOA MIL. 689 BAADA YA KUDHIBITI MIANYA YA RUSHWA

 

Na Dinna Maningo,Musoma

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU ) mkoani Mara imefuatilia na kudhibiti mianya ya rushwa na kuokoa sh Milioni 689,317,212.00 wakati wa ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya sh.Bilioni 8.188 katika kipindi cha mwezi Januari hadi Machi,2021.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mara Hassan Mossi alisema kuwa kiasi hicho cha fedha kilikuwa kifanyiwe ubadhilifu na kingelipwa kwa wakandarasi na wazabuni mbalimbali ambao walikuwa wakitekeleza kazi ya ujenzi wa miundombinu ya majengo na barabara kinyume na sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11 ya mwaka 2007.

Mossi alisema kuwa katika kipindi cha Januari hadi Machi, 2021 TAKUKURU mkoani humo imefanya uchunguzi wa malalamiko yanayohusiana na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kadhaa iliyotekelezwa kwa kutumia fedha za makusanyo ya ndani yenye jumla ya sh. 891,288,244.00.

"Tulifanya uchunguzi dhidi ya mkopeshaji mmoja aliyemkopesha fedha mama ambaye kwa sasa ni marehemu aliyekuwa akimiliki nyumba, baada ya mkopeshaji kusikia mama mmiliki wa nyumba kufariki, alitengeneza nyaraka kuonyesha kuwa walifanya mauziano,mpaka sasa mkopeshaji huyo anamiliki nyumba hiyo ya marehemu kwa kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu kinyume na sheria,tunaendelea na uchunguzi ukikamilika taratibu za kumfikisha mahakamani zitafanyika",alisema Mossi. 

Alisema kuwa ofisi hiyo imesaidia Kanisa la Mennonite Serengeti kuokoa sh milioni tatu fedha ambazo zilitokana na mauzo ya gari aina ya Toyota Cruiser yaliyofanyika kinyemela na baadhi ya viongozi wa kanisa hilo.

Aliongeza kuwa TAKUKURU imefanya uchunguzi wa makusanyo ya mapato yanayofanyika kwa kwa kutumia mashine ya POS na kubaini mianya ya rushwa iliyosababisha ubadhilifu wa sh.milioni 220,000,000 kinyume na sheria,ubadhilifu uliofanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Serengeti.

"Baada ya kuanza uchunguzi watuhumiwa tayali wamerejesha fedha sh. milioni 13,00,000 ikiwa ni miongoni mwa makusanyo ambayo yalikuwa hayafiki kwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo. 

Alisema kuwa ofisi inaendelea na uchunguzi wa mkopeshaji mwingine ambaye alimkopesha mwalimu mstaafu sh. 1,400,000,baada ya mafao yake kutoka alichukua kiasi cha sh.66,000,000 na tayari mkopeshaji amerejesha sh.30,000,000 baada ya TAKUKURU kuingilia kati na bado anatakiwa kumrudishia mstaafu huyo shilingi 34,600,000.

"Mwalimu mwingine alikuwa amechukuliwa fedha zake shilingi 20,000,000 na bwana mmoja aliyedai kuwa amemsaidia mwalimu huyo kulipwa mafao yake haraka lakini kwa uhalisia hakuna kazi aliyoifanya,baada ya uchunguzi alimrejeshea kiasi chote cha fedha", alisema Mossi. 

Alisema kuwa ofisi hiyo imeokoa fedha milioni 1.474,800 ambazo ni fedha za NSSF ambazo zilichukuliwa na wananchama wa MUSOMA SACCOS walizokopeshwa, nakwamba TAKUKURU imepokea malalamiko 189 yanayohusu vitendo vya rushwa ikilinganishwa na malalamiko ya mwezi Octoba -Desemba, 2020.

"Tumefanikiwa kushinda kesi nne na kufungua kesi tatu mpya na kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, tuna program ya TAKUKURU inayotembea na imeweza kufika katika kijiji cha Bwitego,na Nyinchoka wilayani Serengeti nakuzungumza na wananchi na kutatua migogoro katika vijiji hivyo", alisema Mossi.

Aliongeza kuwa TAKUKURU ina mikakati katika kipindi cha mwezi Aprili -Juni,2021 kuhakikisha inazuia rushwa na kudhibiti mianya ya rushwa kwenye miradi ya maendeleo pamoja na uelimishaji umma juu ya madhara ya rushwa katika jamii na kufanya uchunguzi wa tuhuma mbalimbali za rushwa na kuwafikisha watuhumiwa mahakamani hivyo alitoa rai kwa watumishi wa umma na wananchi kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Share:

ASSISTANT TECHNICIAN II (PLUMBER) – 3 POST at TUWASA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

POST ASSISTANT TECHNICIAN II (PLUMBER) – 3 POST POST CATEGORY(S) ENGINEERING AND CONSTRUCTION EMPLOYER TABORA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY(TUWASA) APPLICATION TIMELINE: 2021-04-28 2021-05-12 JOB SUMMARY NA DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To report all water leakage as assigned; ii. To report water loss, distribution faults and recommend necessary action; iii. To connect water supply […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

WATENDAJI / Executive Officers at MADABA District Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Songea is the capital of Ruvuma Region in southwestern Tanzania. It is located along the A19 road.The city has a population of approximately 203,309, and it is the seat of the Roman Catholic Archdiocese of Songea. Between 1905 and 1907, the city was a centre of African resistance during the Maji Maji Rebellion in German East […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

TAKUKURU YAWAFIKISHA MAHAKAMANI VIGOGO WA SHINYANGA KWA KUGHUSHI NYARAKA, MATUMIZI MABAYA YA MADARAKA


Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga, Francis Luena 
**
Aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi/ugavi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Godfrey Mwangairo na mkuu wa idara ya Kilimo, umwagiliaji na ushirika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Panda International Co Ltd, Edward Maduhu wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa makosa ya kughushi, kutoa nyaraka za uongo na matumizi mabaya ya mamlaka kwa kujaribu kujipatia fedha isivyo halali.

Watuhumiwa wengine katika mashtaka hayo ni Wang Wei raia wa China ambaye ni Mmiliki na Mkurugenzi Mtendaji wa Panda International Co Ltd, Emmanuel Ipandu ambaye ni Mwajiriwa wa kampuni hiyo na Adam Kilimbi ambaye ni Mkurugenzi wa Shinyanga Farm Supplies.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa kazi katika kipindi cha robo tatu ya mwaka wa fedha 2020/2021 (Januari- Machi, 2021) iliyotolewa leo na Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga, Francis Luena katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini hapa, amesema kuwa makosa hayo yalitendwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016 na mwaka 2017.

Ambapo, katika kesi ya kwanza ya uhujumu uchumi inayomkabili Godfrey Mwangairo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi halmashauri ya manispaa ya Shinyanga mwaka 2017, aliwasilisha nyaraka zenye maelezo ya uongo kwenye kamati ya tahmini na kusababisha bodi ya zabuni kutoa kazi kwa kampuni ya EMC System Ltd pasipo kuwa na ushindani na kampuni hiyo kujipatia fedha Sh. 43,249,281.34 kwenye zabuni ya kuweka mfumo wa mtandao kiambo (LAN) katika ukumbi wa mkutano uliopo katika halmashauri ya manispaa ya Shinyanga pasipo kufuata sheria.

Katika Kesi ya pili ya jinai dhidi ya aliyekuwa mkuu wa idara ya kilimo, umwagiliaji na ushirika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ambaye pia ni Mkurugenzi wa Panda International Co Ltd, Edward Maduhu, Mmiliki na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Panda Wang Wei pamoja na Emmanuel Ipandu ambaye ni Mwajiriwa wa Kampuni hiyo, watuhumiwa wanakabiliwa na makosa matatuikiwemo kujaribu kutenda kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu Sh. 3,480,000.

Pia, Edward Maduhu akikabiliwa na kosa la kumdanganya mwajiri kwa kuandika kuwa zoezi la kugawa ruzuku za pembejeo lilifanyika wakati siyo kweli na kutumia madaraka vibaya kama mkuu wa idara ya kilimo. Huku, Wang Wei na Emmauel Ipandu wakishtakiwa kwa kosa la kughushi na kutoa nyaraka ya uongo kuonyesha kuwa pembejeo za ruzuku ziligawanywa kwa wananchi wa Kijiji cha Ibubu walioandikwa katika vocha wakati haikuwa kweli.

Kesi ya tatu inawahusu washtakiwa wanne Edward Maduhu, Adam Kilimbi, Wang Wei na Emmanuel Ipandu ambao wanakabiliwa na makosa ya kujaribu kutenda kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu Sh 3,480,000, huku Adam Kilimbi ambaye ni Mkurugenzi wa Shinyanga Farm Supplies akikabiliwa na kosa la kutoa nyaraka za uongo za vocha za pembejeo alizowasilisha halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa wana Kijiji aliowaandika katika kila vocha kuwa walipata pembejeo za ruzuku wakati siyo kweli.

Via Shinyanga Press Club blog
Share:

TIC YAFANIKIWA KUSAJILI MIRADI MIPYA 51 JANUARI HADI MACHI 2021

 Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho Dkt. Maduhu Kazi

Na Dickson Billikwija 

Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) kimesema katika kipindi cha mwezi Januari hadi Machi mwaka 2021 kimefanikiwa kusajili jumla ya miradi mipya 51 yenye thamani ya dola za Marekani milioni 451 huku kikibainisha sekta ya viwada kuongoza katika miradi hiyo kwa kuwa na miradi 30 sawa na asilimia 59 ya miradi yote.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho Dkt. Maduhu Kazi wakati wa utoaji wa taarifa ya robo tatu mwaka 2020/2021 kwa waandishi wa habari.

Dkt. Kazi amesema miradi hiyo inatarajia kuzalisha ajira mpya 4,272 sawa na ongezeko la asilimia 3.5 ukilinganisha na kipindi kama hicho mwaka jana ambapo miradi 54 ilisajiliwa ambyo ilitarajiwa kuwekeza mtaji wa dola za kimarekani 283 milioni iliyozalisha ajira 4,127.

"Sekta iliyoongoza kwa uzalishaji wa ajira mpya ni utalii ambapo inategemea kuzalisha ajira 572 sawa na asilimia 13.4 ya ajira zote,"amesema Dkt. Kazi.

Amebainisha kuwa kati ya miradi 51 iliyosajiliwa mwaka huu miradi 13 sawa na asilimia 25 ni miradi ya wawekezaji wa ndani,miradi 26 sawa na asilimia 51 ni miradi ya wawekezaji wa kigeni,na kusisitiza miradi 12 sawa na asilimia 24 ni miradi ya ubia kati ya watanzania na wageni.

Aidha amesema TIC kinatunza kumbukumbu za miradi ya uwekezaji iliyosajiliwa hivyo wawekezaji ambao wamewekeza nchini bila kupitia kituo hicho hawako katika takwimu hizo  badala yake wawekezaji wengine husajiliwa na EPZA,Tume ya Madini na wengine huwekeza bila kupitia katika taasisi hizo.

Ameongeza kuwa katika kuendelea kuboresha uwekezaji nchini kituo hicho kimejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo kuendelea kuboresha mfumo wa kusajili miradi unaotumiwa na kituo hicho,kuunganisha Mfumo wa Kusajili Miradi (TIW) unaotumika na TIC na mifumo mingine inayohudumia wawekezaji nchini.

Mikakati mingine ni kuhamasisha zaidi uwekezaji kwa wazawa na ubia,kufuatilia kwa karibu wawekezaji kwa lengo la kung'amua changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi yao,pamoja na kuboresha zaidi matumizi ya tehama katika shughuli zote za kunadi na kuhumia wawekezaji.

Aidha ameongeza kuwa kituo hicho  miongoni mwa miradi iliyosajiliwa mwezi Aprili mwaka 2020 ni Mradi wa Kiwanda Kikubwa cha Mbolea cha Kampuni ya Itracom Fertilizers unaojengwa Dodoma utakaowekeza dola za Marekani milioni 180 na kuzalisha ajira za moja kwa moja milioni 3000 ambapo tani za mbolea 500,000.

Dkt.  Kazi alisema kituo hicho kinaendelea kuwakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza nchini kwani mazingira ya uwekezaji yameboreshwa.

Share:

MWENYEKITI WA HALMASHAURI TARIME AZUIA SARUJI 1,800 ZILIZOGANDA KWA FEDHA ZA CSR


Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Simion Samweli akikagua tofari zinazodaiwa kutokuwa na ubora

Na Dinna Maningo, Tarime
MWENYEKITI wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Simion Samwel ambaye pia ni Diwani kata ya Nyakonga amezuia saruji zaidi ya 1,800 zilizonunuliwa kwa fedha ya uwajibikaji wa makampuni kwa jamii (CSR) zinazotolewa na mgodi wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya uchimbaji wa dhahabu ya Barrick baada ya kuganda kutokana na kukaa mwaka mzima bila kutumika.

Samwel aliyasema hayo wakati wa ukaguzi wa baadhi ya miradi inayotekelezwa kwa fedha za CSR akiwa ameongozana na Mwenyekiti wa kamati ya uchumi na ujenzi ambaye ni Diwani wa kata ya Matongo Godfrey Kegoye, Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii  Steven Gibai ambaye ni Diwani wa kata ya Manga na Kaimu Muhandisi ujenzi halmashauri ya wilaya ya Tarime  ambaye pia ni fundi sanifu ujenzi John Phabian.

Aliongeza kuwa mbali na saruji hizo zilizoganda amebaini uwepo wa matumizi mabaya ya fedha baada ya kukuta vifaa vingi vikiwa vimezidi mahitaji yaliyokusudiwa zikiwemo saruji huku miradi hiyo ikishindwa kukamilika kwa wakati,gharama kubwa za manunuzi na matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ikilinganishwa na uhalisia.

Samwel alisema kuwa amezuia saruji hizo kutotumika kwakuwa zimekwisha ubora na endapo zikitumika majengo hayatakuwa imara hali ambayo inaweza kuisababishia hasara halmashauri kutoa fedha zingine kukarabati majengo. 

"Mimi na Wenyeviti wa kamati tuliamua kuzunguka kutembela ujenzi wa miradi ya elimu na afya kwa fedha za CSR tulipofika kijiji cha Nyakunguru tulikuta saruji mifuko 334 ikiwa imeganda na vifaa vingine vikiwa vimehifadhiwa kwa muda mrefu zaidi ya mwaka bila kutumika, vingine vimebaki,hii ni hasara na matumizi mabaya ya fedha haiwezekani saruji zimeganda alafu ziendelee kutumika huu ni uzembe wa halmashauri ambao ndiyo wasimamizi wa miradi inayojengwa kwa fedha za CSR.

"Kama mwenyekiti wa halmashauri na wenyeviti wa kamati tumezuia isitumike kwanza tukalijadili hili kwenye vikao vyetu ikiwezekana halmashauri ipeleke saruji zingine pesa watajua watakakozitoa wenyewe maana ni uzembe wa mkurugenzi na wataalamu wake kwasababu sisi tumeingia halamshauri mwaka huu na miradi hii ni ya mwaka 2018 na hadi sasa haijakamilika",alisema Samwel.

Diwani wa kata ya Kibasuka Thomas Nyagoro alisema kuwa zahanati ya Itandura ilijengwa kwa nguvu za wananchi majengo yake yamechakaa kwakuwa ina zaidi ya miaka 30 haitumiki bila kutoa huduma yoyote na haijasajiliwa.

Akisoma taarifa kwa Mtendaji wa kijiji cha Nyakunguru Zakayo Wangwe alisema kuwa Mgodi wa North Mara ulitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mganga, ukarabati wa zahanati, ujenzi wa kichomea taka na placenta piti, ujenzi wa choo na barabara. 

"Ujenzi wa nyumba 1 pacha ya mtumishi utakao gharimu fedha milioni 88,734,528.17,ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) sh. milioni 32,662,872.00,ujenzi wa choo cha nje matundu 21 sh.Milioni 19,289.617.30,ujenzi wa kichomea taka na placenta piti sh. Milioni 11,091,750.00 na sh. Milioni tatu  kama gharama za usimamizi kwa kamati ya ujenzi na wataalamu, jumla ya fedha zote za mradi wa zahanati ni sh Milioni 154,778,767.47",alisema.

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyakunguru Chacha Makuri alisema kuwa fedha hizo ni za mwaka 2018,hawajapokea fedha za CSR kwa mwaka 2019 -2020 nakwamba walipokea mradi mwingine wa barabara kutoka barabara ya Nyakato -Turuturu km 7,barabara ya Nyakunguru senta -Nyamuma wa sh Milioni 55 lakini mradi huo ujenzi umekuwa ni wakusuasua.

"Hii miradi fedha zinatolewa na mgodi na wasimamizi ni halmashauri wao ndiyo wanaandaa BOQ na kufanya manunuzi sisi ni kupokea vifaa na kuwasimamia mafundi,mafundi wana suasua halmashauri inatuletea fundi ambaye anakuwa na tenda nyingi anashindwa kumaliza kwa wakati ukimuuliza anakwambia hujamwajili yeye mwajili wake ni mkurugenzi ndiye anatakiwa amuhoji,hizi saruji tulizipokea julai, 2020 hadi sasa hazijatumika zimeganda",alisema Makuri.

Mwenyekiti wa kitongoji Cha Itandura Masero Matiko alisema kuwa Mgodi una nia nzuri ya kusaidia jamii lakini usimamizi wa miradi ndiyo unakwamisha ujenzi kutokamilika kwa wakati huku Chacha Chacha yeye akisema tatizo siyo Fundi tatizo ni pesa kutolipwa kwa wakati hali inayosababisha vibarua kukimbia ambapo yeye kama kibarua wa kuchanganya udongo anamdai fundi sh 50,000/= tangu Novemba 2020.

Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi kijiji cha Nyakunguru aliwalalamikia wataalamu wa ujenzi kutoka halmashauri kutofika kwa wakati kukagua ujenzi na kusababisha miradi kujengwa chini ya kiwango,kuwapa kazi mafundi wasio na uwezo wa kifedha kuchukua mafundi wa bei ya chini wasioweza kukamilisha kazi kwa wakati. 

"Halmashauri imetenga fedha za usimamizi kwa kamati ya ujenzi na wataalamu milioni tatu lakini hawafiki kuna huyu fundi sanifu ujenzi anaitwa Isaya huyu ni tatizo ukimpigia simu kuwa kuna sehemu fundi kajenga vibaya au tofari siyo nzuri anakuambia piga picha nitumie kwa whatsapp sasa mimi simu yangu ni ndogo kasimu katochi nitaitumaje huku kijijini wengi tunatumia simu za tochi, mmeshuhudia tofari zinavyopukutika tofari linalouzwa kwa sh 1,500 wao wanasema wamenunua kwa sh 2,500,ukiona jengo la milioni 88 utashangaa wizi mtupu",alisema. 

Bhoke Marwa mkazi wa Nyakunguru alisema kuwa zahanati hiyo ikifanya kazi itawasaidia kwani wanalazimika kutembea umbali km 7 kuifuata huduma ya afya kituo cha afya Nyarwana hali inayosababisha wajawazito kujifungulia njiani na wagonjwa wengine kufia njia wakati wakitembea kwenda kufuata huduma ya afya. 

Mwenyekiti huyo wa halmashuri na wenyevikiti wa kamati walitembelea ujenzi wa shule mpya ya sekondari Matongo nakukuta ujenzi wa madarasa matatu ukiendelea utakaogharimu zaidi ya Milioni 88 huku mifuko ya saruji 570 iliyoganda ikiwa imetunzwa. 

Kaimu Mwenyekiti wa kijiji Cha Matongo Charles Ryoba alisema kuwa mfumo unaotumika katika pesa za CSR ni mbaya nakwamba badala ya halmashauri kuhusika kwenye michakato ya manunuzi serikali za vijiji ndiyo vihusike katika michakato ya manunuzi ,usimamizi na halmashauri hivisimamie vijiji kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na siyo kila kitu kushughulikiwa na halmashauri. 

 Wakiwa katika shule ya msingi Murito walikuta zaidi ya saruji 200 na vifaa vingine vikiwa vimetunzwa ndani ya darasa wanalosomea wanafunzi wa darasa la nne huku katika hospitali ya halmashauri ya wilaya kukiwa kumehifadhiwa saruji mifuko 650 ikiwa imeganda.

Diwani wa kata ya Kemambo Rashid Bogomba alisema kuna madarasa mawili shule ya Murito yanajengwa yatakayo gharimu Milioni 63 nakwamba changamoto ni mbao kupinda baada ya kukaa muda mrefu bila bati kuezekwa na saruji kuganda. 

Mwenyekiti wa kamati ya uchumi na ujenzi Godfrey Kegoye alisema kuwa kuna miradi ya CSR iliyojengwa tangu 2017 lakini hadi sasa haijakamilika licha yakutakiwa kukamilika ndani ya miezi sita,ujenzi kuwa chini ya kiwango,vifaa kununuliwa kwa gharama kubwa Nakwamba yeye kama mwenyekiti wa kamati hajaridhishwa na ujenzi wa miradi ya fedha za CSR licha ya miradi hiyo kugharimu fedha nyingi. 

Mwenyekiti wa kamati ya huduma ya jamii Steven Gibai alisema kuwa usimamizi wa miradi siyo mzuri nakwamba watahakikisha wanasimamia vyema miradi hiyo na itakayokuwa chini ya kiwango hawatokubari kukaa kimya wataisemea ili kuhakikisha inakuwa na ubora.

Kaimu Muhandisi wa halmashauri ya wilaya hiyo John Fabian alisema kuwa idara ya ujenzi haina gari na wakati mwingine analazimika kutumia gharama zake kwa usafiri wa pikipiki au kutumia usafiri wa gari la mgodi wanapokuwa wakiitembelea miradi ya fedha wanazozitoa za CSR. 

 Alisema kuwa saruji ikikaa kwa zaidi ya miezi 6 bila kuhifadhiwa sehemu salama upungua ubora na kuharibika,akashauri saruji hiyo isitumike kwenye ujenzi na upigaji wa ripu badala yake itumike kuweka jamvi sakafuni au kufyatua tofari.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Apoo Tindwa alikiri kuwepo kwa changamoto ya ufujaji wa fedha katika idara ya ujenzi na manunuzi nakwamba ameshachukua hatua kwa kuwaandikia barua baadhi ya watendaji nakwamba wakithibitika kwa ufujaji wa fedha watachukuliwa hatua na kuwa baadhi ya mafundi waliochelewesha kazi wamekamatwa.

Alisema kuwa kitendo cha fundi mmoja kupewa kazi nyingi na kusababisha miradi kuchelewa kukamilika kwa wakati ni uzembe wa idara ya ujenzi wakiwemo wahandisi kutokagua miradi kwa wakati nakusababisha baadhi ya miradi kujengwa chini ya kiwango. 

Hata hivyo baadhi ya mafundi wakuu waliopewa kazi za ujenzi wa miradi ambao hawakutaka kutajwa majina walidai kuwa fedha wanazopewa haziendani na kazi, kwani huambiwa kiasi fulani kutokana na mikataba yao na halmashauri lakini wakifuatilia fedha siyo halisi kwa mujibu wa mikataba.

Walieleza kuwa wakifatilia mgodini fedha zinazotolewa ni zaidi ya kiasi kilichopo kwenye mikataba yao na wakipungukiwa fedha wakiomba kuongezewa hawapewi na wakati mwingine hawalipwi fedha kwa wakati wakifatilia hutishiwa  kutopewa kazi  hali inayosababisha miradi kutokamilika kwa wakati na kujengwa kwa ubora ikilinganishwa na fedha halisi zinazotolewa na mgodi. 
Mifuko ya Saruji ikiwa imehifadhiwa kwenye chumba cha darasa la nne katika shule ya msingi Murito kata ya Kemambo ikiwa imeganda baada ya kukaa muda mrefu bila kutumika.
Saruji zikiwa zimehifadhiwa katika hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Tarime zilizoganda baada ya kukaa muda mrefu zaidi ya miezi 10 bila kutumika
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tarime Simion Samwel akionyesha Saruji zilivyoganda zilizohifadhiwa shule ya msingi Murito
Saruji na vifaa mbalimbali vikiwa vimehifadhiwa kwenye chumba kinachotumiwa na wanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Murito kata ya Kemambo
Saruji na vifaa vilivyohifadhiwa kwenye zahanati tarajiwa ya Itandura kijiji cha Nyakunguru
Mwenyekiti wa kamati ya uchumi na ujenzi halmashauri ya wilaya Tarime ambaye pia ni Diwani kata ya Matongo -Nyamongo akijaribu kuvunja tofari, matofari hayo yanaelezwa kutengenezwa chini ya kiwango ambapo tofari moja linauzwa sh 2500 yanayojenga zahanati ya Itandura
Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi ya kijiji cha Nyakunguru akionyesha tofari zinazodaiwa hazina ubora
Wa kwanza kulia mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tarime Simion Samwel akiwa ameongozana na wenyeviti wa kamati ya uchumi,ujenzi na huduma za jamii pamoja na wajumbe wa kamati ya ujenzi kijiji Cha Nyamwaga wakati wakutembelea ujenzi wa baadhi ya wodi

Share:

Vacancy For Board Members at Mkombozi Commercial bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

VACANCY FOR BOARD MEMBERS INTRODUCTION Our client MKOMBOZI COMMERCIAL BANK PLC (MKCB), is a leading commercial bank in Tanzania established in 2009. The bank provides banking solutions to growing, medium sized and large companies, institutional investors, financial institutions and government entities. The bank attained an important milestone when it was listed on the Dar es […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Demand H&S Specialist – Africa at diageo

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description : From Arthur Guinness to Johnnie Walker, our business was founded on people of great character, and in 250 years, nothing’s changed. We’re the world’s leading premium alcohol company. Our brands are industry icons. And our success is thanks to the strength of our people, in every role. It’s why we trust them […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ITDT Regional Voluntary Workforce Volunteer at VSO

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

VSO is the world’s leading international development charity that works through volunteers to create a fair world for everyone. At VSO we pride ourselves on doing development differently. We fight poverty not by sending aid, but by working through volunteers and partners to create long-lasting change in some of the world’s poorest regions. We bring […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Advisor – Gender and Youth Empowerment at Pact

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

At the heart of Pact is the promise of a better tomorrow. A nonprofit international development organization founded in 1971, Pact works on the ground in nearly 40 countries to improve the lives of those who are challenged by poverty and marginalization. We serve these communities because we envision a world where everyone owns their […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MWENYEKITI MPYA WA CCM KUJULIKANA KESHO IJUMAA


Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unatarajiwa kufanyika kesho Ijumaa jijini Dodoma.Miongoni mwa kazi kubwa za mkutano huo ni kumchagua Mwenyekiti wa CCM Taifa.

CCM inamchagua Mwenyekiti wake mpya kufuatia kifo cha Dkt. John Magufuli aliyekuwa Rais wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, kilichotokea Machi 17 mwaka huu.

Akizungumza leo Alhamisi Aprili 29,2021 kuhusu maandalizi ya mkutano huo katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amesema Wajumbe 1876 wa mkutano mkuu maalumu wa CCM wanatarajiwa kupiga kura jina moja litakalowasilishwa katika mkutano huo kumchagua mwenyekiti mpya wa chama hicho .

Amesema mbali na wajumbe hao ambao watashiriki kupiga kura, wapo wageni 1,000 watakaoshiriki mkutano  wakiwamo kutoka vyama mbalimbali vya siasa nchini, wawakilishi wa vyama rafiki vilivyoshiriki katika ukombozi wa Bara la Afrika na mabalozi.

Amebainisha kuwa  mkutano huo utaongozwa na makamu mwenyekiti wa CCM- Bara, Philip Mangula na makamu mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar,  Dk Ali Mohamed Shein.


Share:

ASKARI WALIOOMBA RUSHWA YA MIL. 100 WAFUKUZWA KAZI


Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha limewafukuza kazi askari wanne na kuwasimamisha kazi wakaguzi wawili wa polisi ambao wanatuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni 100.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha ACP Justine Masejo, na kueleza kuwa tukio hilo la kuomba rushwa walilitekeleza Machi 19, 2021, maeneo ya Arumeru.

Aidha Kamanda Masejo ameongeza kuwa wakaguzi pamoja na askari hao watakabidhiwa kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), mkoani humo kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kiuchunguzi.

Inadaiwa kuwa askari hao waliomba rushwa kwa Profesa Justine Maeda, ambaye amewahi kuwa mshauri wa uchumi wa Rais wa awamu ya kwanza, Hayati Julius Nyerere, baada ya kumpekua nyumbani kwake na kukuta vipande viwili vya meno ya Tembo kwenye mzinga wa Nyuki.


Share:

Senior Advisor – Gender and Youth Empowerment at Pact

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

At the heart of Pact is the promise of a better tomorrow. A nonprofit international development organization founded in 1971, Pact works on the ground in nearly 40 countries to improve the lives of those who are challenged by poverty and marginalization. We serve these communities because we envision a world where everyone owns their […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Director of Operations at Medical Teams International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Description                                                                                 Operations Director (1)                                      Medical Teams International   Department:  Operations Grey Sections to be completed by Human Resources. Team: Operations Job Code:  Reports to (position): Country Director Org. Reporting Line: Country Office Location(s): Dar es Salaam Job Band: 19 Choose an item. Workdays & Number of scheduled hours per week:    Monday-Friday, 40+ hours/week, occasional […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

POLISI SHINYANGA WAKAMATA KONDOMU ZILIZOPIGWA MARUFUKU...MALI ZA WIZI, VIFAA VYA KUFANYIA UHALIFU NA WAHALIFU 231

Share:

Waziri Kalemani Apiga Marufuku Uagizaji Wa Vikombe (Insulators) Kutoka Nje Ya Nchi


Na Teresia Mhagama, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani amepiga marufuku uagizaji wa vikombe (insulators) kutoka nje ya nchi baada ya uzalishaji wa vikombe hivyo sasa kufanyika nchini.

Dkt.Kalemani ametoa agizo hilo tarehe 28 Aprili, 2021 baada ya kukagua shughuli za uzalishaji wa vikombe hivyo katika Kiwanda cha Inhemeter kilichopo wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam.

“Nilikuja hapa mwezi Novemba mwaka jana kukagua uzalishaji wa mita za umeme na nikatoa agizo kuwa vikombe navyo visiagizwe nje ya nchi na viwanda vya uzalishaji wa vikombe vijengwe ndani ya nchi, hivyo nimekuja kufuatilia agizo hilo na kujiridhisha kama vikombe vinazalishwa au havizalishwi.” Amesema Dkt.Kalemani

Baada ya kufanya ukaguzi katika kiwanda hicho, Dkt. Kalemani amesema kuwa, amejiridhisha kuwa kiwanda  kinazalisha vikombe takriban milioni 1.5 kwa mwaka  na pia kiwanda kingine cha Africab kinazalisha vikombe Milioni Moja kwa mwaka huku mahitaji kwa sasa yakiwa ni vikombe Milioni M1.8.

Kutokana na uzalishaji huo, Dkt.Kalemani ameeleza kuwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na wakandarasi wa umeme wanunue vikombe na vifaa vingine vya umeme vinavyozalishwa ndani ya nchi, hali itakayopelekea wananchi kuunganishiwa umeme kwa kasi.

Ameeleza kuwa, kuna faida mbalimbali za kuzalisha vifaa hivyo ndani ya nchi ikiwemo vifaa husika kupatikana kwa bei nafuu kulinganisha na vifaa vinavyoagizwa kutoka nje ya nchi, vifaa hivyo kutengenezwa kwa ubora na kuongeza ajira ndani ya nchi.

Aidha, ameipongeza kampuni hiyo kwa kuzalisha vifaa hivyo na kutoa ajira kwa vijana wa kitanzania takriban 150.

Ametoa wito kwa watendaji wa kiwanda hicho kuongeza uzalishaji wa vikombe hivyo ambavyo hufungwa katika miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme ya uwezo tofauti ikiwemo 11kV, 33kV na 400kV.

Insulators (vikombe) hufungwa kati ya nguzo na nyaya za umeme kwa lengo la kuzuia umeme huo kusafiri kupitia kwenye nguzo na baadaye kuleta madhara mbalimbali ikiwemo ya moto.

Katika ziara yake jijini Dar es Salaam, Waziri wa Nishati aliambatana na watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger